Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,197
Mzungu mmoja ambaye anadaiwa kuwa ni mfanyakazi wa ofisi ya ubalozi wa Canada nchini hapa, anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kumtemea mate askari wa usalama barabarani (Trafiki) aliyekuwa akiongoza magari, Jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile, amesema tukio hilo la aina yake lilitokea jana saa 8:15 mchana eneo la Ukonga Banana, barabara ya Nyerere Jijini.
Kamanda amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Gean Touchatte, 48, ambaye imeelezwa kuwa ni Katibu Mhitasi wa ubalozi huo.
Akisimulia tukio zima, Kamanda Shilogile amesema kabla ya tukio hilo, trafiki mwenye namba NCO E1653 Koplo Samson, alikuwa kazini akiongoza magari katika barabara ya Nyerere pale Ukonga Banana.
Akasema wakati huo mtuhumiwa huyo alipita akiendesha gari lenye namba za usajili T 17 DC 178 aina ya Toyota Land Cruiser, akitokea Ukonga kwenda Uwanja wa Ndege.
Kamanda Shilogile amefafanua kuwa mtuhumiwa huyo alipomkaribia trafiki, alipunguza mwendo, akashusha kioo cha gari, kisha akamtemea mate askari kabla ya kuongeza mwendo na kuondoka.
Kwa mujibu wa Kamanda Shigolile, trafiki alitoa taarifa za tukio hilo kwa wenzake kupitia `redio call za polisi, juhudi zilizosababisha gari hilo kufuatiliwa.
Amesema gari lilipofika maeneo ya Kamata, lilikamatwa na askari na kupelekwa Makao Makuu ya Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Kamanda amesema wakati mtuhumiwa huyo akiendelea kuhojiwa kituoni hapo, alifika mwandishi wa habari wa TBC, Jerry Muro akiwa na nia ya kumhoji lakini naye inadaiwa aliishia kutemewa mate yaliyompata chini ya kidevu na kuenea upande wa mbele wa fulana aliyokuwa amevaa.
Amefafanua kuwa kutokana na kitendo hicho, mwandishi huyo alifungua jalada la mashtaka ya shambulio kituoni hapo na kufunguliwa jalada namba CD/102/4818/2009.
Kwa mujibu wa Kamanda Shilogile, mtuhumiwa huyo hakuwa tayari kutoa maelezo yoyote, kwa madai kuwa atafanya hivyo pindi akiwepo balozi wa nchi yake.
Aidha, akasema fulana ya mwandishi Jerry Muro iliyotemewa mate, imehifadhiwa katika Kituo cha Polisi Kati kwa ajili ya ushahidi na mtuhumiwa huyo anaendelea kushikiliwa na Polisi.
CHANZO: ALASIRI /ippmedia.com
WanaJF, sasa tumefikia wakati hata idara zetu za usalama zinadharauliwa mbele ya macho yetu. Nafautilia kuona ni vipi serikali yetu inafuatilia hili. Najua nini kingenipata kama ningefanya hilo hilo Canada.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Ilala, Faustine Shilogile, amesema tukio hilo la aina yake lilitokea jana saa 8:15 mchana eneo la Ukonga Banana, barabara ya Nyerere Jijini.
Kamanda amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Gean Touchatte, 48, ambaye imeelezwa kuwa ni Katibu Mhitasi wa ubalozi huo.
Akisimulia tukio zima, Kamanda Shilogile amesema kabla ya tukio hilo, trafiki mwenye namba NCO E1653 Koplo Samson, alikuwa kazini akiongoza magari katika barabara ya Nyerere pale Ukonga Banana.
Akasema wakati huo mtuhumiwa huyo alipita akiendesha gari lenye namba za usajili T 17 DC 178 aina ya Toyota Land Cruiser, akitokea Ukonga kwenda Uwanja wa Ndege.
Kamanda Shilogile amefafanua kuwa mtuhumiwa huyo alipomkaribia trafiki, alipunguza mwendo, akashusha kioo cha gari, kisha akamtemea mate askari kabla ya kuongeza mwendo na kuondoka.
Kwa mujibu wa Kamanda Shigolile, trafiki alitoa taarifa za tukio hilo kwa wenzake kupitia `redio call za polisi, juhudi zilizosababisha gari hilo kufuatiliwa.
Amesema gari lilipofika maeneo ya Kamata, lilikamatwa na askari na kupelekwa Makao Makuu ya Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam.
Kamanda amesema wakati mtuhumiwa huyo akiendelea kuhojiwa kituoni hapo, alifika mwandishi wa habari wa TBC, Jerry Muro akiwa na nia ya kumhoji lakini naye inadaiwa aliishia kutemewa mate yaliyompata chini ya kidevu na kuenea upande wa mbele wa fulana aliyokuwa amevaa.
Amefafanua kuwa kutokana na kitendo hicho, mwandishi huyo alifungua jalada la mashtaka ya shambulio kituoni hapo na kufunguliwa jalada namba CD/102/4818/2009.
Kwa mujibu wa Kamanda Shilogile, mtuhumiwa huyo hakuwa tayari kutoa maelezo yoyote, kwa madai kuwa atafanya hivyo pindi akiwepo balozi wa nchi yake.
Aidha, akasema fulana ya mwandishi Jerry Muro iliyotemewa mate, imehifadhiwa katika Kituo cha Polisi Kati kwa ajili ya ushahidi na mtuhumiwa huyo anaendelea kushikiliwa na Polisi.
CHANZO: ALASIRI /ippmedia.com
WanaJF, sasa tumefikia wakati hata idara zetu za usalama zinadharauliwa mbele ya macho yetu. Nafautilia kuona ni vipi serikali yetu inafuatilia hili. Najua nini kingenipata kama ningefanya hilo hilo Canada.