Mdau Anataka Kuanzisha TV - Iwe na Vipindi Gani?

Allien

JF-Expert Member
Jul 6, 2008
5,546
1,861
Wana JF,

Kuna mdau anataka ku-invest katika TV Station DSM na sasa anaandaa Mchanganuo kwa ajili hiyo ili kuufikisha katika vyombo husika by January 2010.

Anapenda TV atakayoianzisha iwe na mambo yafuatayo:

  • Iwe na vipindi vya kuvutia sana kiasi kwamba kila anayefungulia asihamie channel nyingine.

  • Iwe inaelimisha katika mambo ya msingi ambao Watazamaji watajifunza na yatawasaidia.

  • Isaidie Kupiga Vita Ufisadi

  • Isaidie kubadilisha Attitude ya Watanzania katika kujiletea maendeleo

  • Isaidie katika kuondoa umasikini kupitia vipindi vyake

  • Isaidie katika suala zima la Ujasiliamali.

  • Pia Entertainment, Michezo, Vipindi vya watoto nk. nk.

Inatakiwa zaidi ya 60% ya vipindi viwe local programs (Local Content) na chini ya 40% vinaweza kuwa vipindi vya nje (Foreign Content).

Je ni nini mawazo yako juu ya vipindi mbalimbali na viendeshwe kwa staili gani ili kufanikisha malengo yake?
 
Wana JF,

Kuna mdau anataka ku-invest katika TV Station DSM na sasa anaandaa Mchanganuo kwa ajili hiyo ili kuufikisha katika vyombo husika by January 2010.

Anapenda TV atakayoianzisha iwe na mambo yafuatayo:


  • Iwe inaelimisha katika mambo ya msingi ambao Watazamaji watajifunza na yatawasaidia.

  • Isaidie Kupiga Vita Ufisadi

  • Isaidie kubadilisha Attitude ya Watanzania katika kujiletea maendeleo

  • Isaidie katika kuondoa umasikini kupitia vipindi vyake

  • Isaidie katika suala zima la Ujasiliamali.


Kuhusiana na hayo hapo juu kipindi kinaweza kuitwa YALIYOJIRI KUTOKA JAMIIFORUMS.

Kipindi hiki chaweza kuwa cha nusu saa, kitarushwa siku za Jumatano na Ijumaa kuanzia saa tatu kamili usiku. Kipindi kitarudiwa kurushwa kwa muda wa saa nzima siku ya Jumapili kuanzia saa tatu usiku hadi saa nne usiku.

Mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi hicho naweza kuwa Uwiano Maalum, kama mdau mwenye TV atanitaka.

Asante.
 
Kama tutapata habari kutoka maeneo ambayo hayasikiki au hayafikiwi na vyombo vyengine...yaani vijijini uko, na mambo mengine ya taaluma na burudani kidogo tu.
 
Kuhusiana na hayo hapo juu kipindi kinaweza kuitwa YALIYOJIRI KUTOKA JAMIIFORUMS.

Kipindi hiki chaweza kuwa cha nusu saa, kitarushwa siku za Jumatano na Ijumaa kuanzia saa tatu kamili usiku. Kipindi kitarudiwa kurushwa kwa muda wa saa nzima siku ya Jumapili kuanzia saa tatu usiku hadi saa nne usiku.

Mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi hicho naweza kuwa Uwiano Maalum, kama mdau mwenye TV atanitaka.

Asante.


Mkuu;

Unataka jamaa yangu afungiwe? Mzee wa Uchagani tu na porojo kidogo, anawakosesha usingizi. Ukileta yaliyojili kutoka JF si ndo watakufungia. ama?

Hata hivyo wazo ni zuri. lakini je Wazungumzaji katika kipindi hicho watakuwa wa namna gani? Wanaweza Ku-Dare To Talk Openly?
 
Kama tutapata habari kutoka maeneo ambayo hayasikiki au hayafikiwi na vyombo vyengine...yaani vijijini uko, na mambo mengine ya taaluma na burudani kidogo tu.

Mkuu Junius;

Sasa hivi bila shaka kuna vipindi kama hivyo katika TV zetu. Je unazungumzia viwe katika mfumo huo huo au mfumo gani? Au kuna ubunifu zaidi unatakiwa?
 
Mkuu;

Unataka jamaa yangu afungiwe? Mzee wa Uchagani tu na porojo kidogo, anawakosesha usingizi. Ukileta yaliyojili kutoka JF si ndo watakufungia. ama?

Hata hivyo wazo ni zuri. lakini je Wazungumzaji katika kipindi hicho watakuwa wa namna gani? Wanaweza Ku-Dare To Talk Openly?

Kama mdau ataogopa, ataniuzia muda then kama kushtakiwa nitashtakiwa mwenye kipindi. Hiyo TV iwe tofauti na ITV, Star TV au TBC. Hawa wako biased kiasi fulani hivi. Hiyo mpya iweze kupresent issues kwa uwazi, zinazolenga maendeleo ya wananchi kwa ujumla, elimu ya uraia na demokrasia kwa ujumla. Nyimbo zile zile za kuogopa kufungiwa zinasababisha kutomkomboa mwananchi wa tabaka la chini, kifikra.

Yaliyomo kwenye kipindi hicho yatakusanya mawazo ya members hapa na kuyachambua kwa mtitiriko maalum. Ikibidi kutakuwa na mgeni maalum ambaye yuko responsible na suala husika litakalozungumziwa .ie waziri Masha na tuhuma za kufoji umri, Masha ataalikwa na kuweka ukweli, Mengi na kuoa...Mengi ataalikwa na kuweka ukweli, Michuzi kutumia safari za kikazi kwenda vekesheni, ataalikwa kuelezea jamii, Zitto na Dowans, naye ataalikwa kuelezea msimamo wake, umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura, m/wahusika wahamasishaji wataalikwa e.t.c, e.tc...
 
Unaongelea freddy macha wa uk ? Yeye ndio anatafuta maoni ya watu au sio huyo unayeongelea njia rahisi ni kwenda katika kampuni za utafiti kama steadman , consumerinsight au research international wale wanadata nyingi sana
 
Kama mdau ataogopa, ataniuzia muda then kama kushtakiwa nitashtakiwa mwenye kipindi. Hiyo TV iwe tofauti na ITV, Star TV au TBC. Hawa wako biased kiasi fulani hivi. Hiyo mpya iweze kupresent issues kwa uwazi, zinazolenga maendeleo ya wananchi kwa ujumla, elimu ya uraia na demokrasia kwa ujumla. Nyimbo zile zile za kuogopa kufungiwa zinasababisha kutomkomboa mwananchi wa tabaka la chini, kifikra.

Yaliyomo kwenye kipindi hicho yatakusanya mawazo ya members hapa na kuyachambua kwa mtitiriko maalum. Ikibidi kutakuwa na mgeni maalum ambaye yuko responsible na suala husika litakalozungumziwa .ie waziri Masha na tuhuma za kufoji umri, Masha ataalikwa na kuweka ukweli, Mengi na kuoa...Mengi ataalikwa na kuweka ukweli, Michuzi kutumia safari za kikazi kwenda vekesheni, ataalikwa kuelezea jamii, Zitto na Dowans, naye ataalikwa kuelezea msimamo wake, umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura, m/wahusika wahamasishaji wataalikwa e.t.c, e.tc...


Mkuu Nakusoma Sana;

Naona unataka kumkoma nyani nje ya JF sasa. Nadhani ni wazo zuri sana. wengi wanapowaalika hawa waheshimiwa au wahusika huwa wanauliza maswali nyoronyoro sana.

Je, kuhusu vipindi vingine, ni yapi mapendekezo yako.
 
Wazo zuri hili na tumpongeze mdau kwa kuthubutu hata kuwaza na kutekeleza wazo.
Kwa kuanzia, mimi binafsi nitamshauri yafuatayo:
1.Sipendi kuona jinsi redio na TV nyingi TZ wanavyoigana.Kuna wakati ungeshindwa kuelewa kama unasikiliza Radio 1 au redio TZ... Hii ilitokana na kule kuiba wafanyakazi kutoka tv/redio moja kwenda nyingine na kuwaruhusu kupeleka " uzoefu" wao wholesale.
Ushauri - Mdau apeleleze TV zingine wana vipindi vya aina gani au mpangilio gani ili ajitofautishe ( differentiation)
2.Mdau atengeneze niche yake kufuatia tathimini hiyo kwenye 1.hapo juu.
Nitakuja na mawazo zaidi...
 
Unaongelea freddy macha wa uk ? Yeye ndio anatafuta maoni ya watu au sio huyo unayeongelea njia rahisi ni kwenda katika kampuni za utafiti kama steadman , consumerinsight au research international wale wanadata nyingi sana


Shy; Asante sana Mkuu.

Huyu Mdau si Fred Macha na wala sikuwa najua kama Fred Macha wa UK ana mpango wa kuanzisha TV.

Wazo ulilotoa ni zuri sana. Je una details zozote za kampuni tajwa za utafiti na gharama zao?

Pamoja na hilo, bado kama kuna mwana JF ana mawazo mazuri ya vipindi yanaweza kusaidia. Inakuwa kama ni utafiti mdogo pia.
 
Wazo zuri hili na tumpongeze mdau kwa kuthubutu hata kuwaza na kutekeleza wazo.
Kwa kuanzia, mimi binafsi nitamshauri yafuatayo:
1.Sipendi kuona jinsi redio na TV nyingi TZ wanavyoigana.Kuna wakati ungeshindwa kuelewa kama unasikiliza Radio 1 au redio TZ... Hii ilitokana na kule kuiba wafanyakazi kutoka tv/redio moja kwenda nyingine na kuwaruhusu kupeleka " uzoefu" wao wholesale.
Ushauri - Mdau apeleleze TV zingine wana vipindi vya aina gani au mpangilio gani ili ajitofautishe ( differentiation)
2.Mdau atengeneze niche yake kufuatia tathimini hiyo kwenye 1.hapo juu.
Nitakuja na mawazo zaidi...


WoS asante sana kwa mawazo bomba. Na hongera sana, naona unaendelea vema katika ile thread ya kumtafuta Superlady na Cerebrity wa JF.

Ni kweli vipindi vingi sana vinajirudia rudia, hata style ya utangazaji pia. maoni yako yatafanyiwa kazi na mdau.

Je, una specifiki choice ya vipindi ambavyo ungependa vibuniwe?
 
WoS asante sana kwa mawazo bomba. Na hongera sana, naona unaendelea vema katika ile thread ya kumtafuta Superlady na Cerebrity wa JF.

Ni kweli vipindi vingi sana vinajirudia rudia, hata style ya utangazaji pia. maoni yako yatafanyiwa kazi na mdau.

Je, una specifiki choice ya vipindi ambavyo ungependa vibuniwe?

Ningependa kipindi cha kujenga viongozi wenye mtizamo wa kileo ( contemporary leadership) ambapo kutakuwa na mijadala moto moto kuibua vijana wenye uwezo wa kupembua mambo - kisiasa, kiuchumi, kijamii...
Pia itakuwa ni fursa kuwatambua viongozi katika jamii - tuelewe viongozi siyo lazima watawala au wanasiasa - wanaweza kuwa watu wa kawaida kabisa waliofanya mambo ya kujivunia katika jamii zetu.Wanaweza kuwa wazee wa ukoo, wazee wa familia ambao hakuna mtu anawatambua kwa vile hawakuwahi kushika nyadhifa serikalini.Hii itakuwa fursa kuwaenzi na pia kuona ni kitu gani tunaweza kujifunza kusafisha uovu au uchafu unaochafua jamii zetu za sasa ( kupitia ufisadi/rushwa, uchu wa madaraka n.k.)
Kipindi hiki kitaendelea kuwalea viongozi watarajiwa wake kwa waume... na TV inaweza kushirikiana na taasisi za mafunzo ili kuhakikisha kweli tunapata matunda na siyo porojo tu kama tulivyozoea waTZ.
IN SHORT IM CRAVING FOR OUTPUT ORIENTED PROGRAMMES!
 
Ningependa kipindi cha kujenga viongozi wenye mtizamo wa kileo ( contemporary leadership) ambapo kutakuwa na mijadala moto moto kuibua vijana wenye uwezo wa kupembua mambo - kisiasa, kiuchumi, kijamii...
Pia itakuwa ni fursa kuwatambua viongozi katika jamii - tuelewe viongozi siyo lazima watawala au wanasiasa - wanaweza kuwa watu wa kawaida kabisa waliofanya mambo ya kujivunia katika jamii zetu.Wanaweza kuwa wazee wa ukoo, wazee wa familia ambao hakuna mtu anawatambua kwa vile hawakuwahi kushika nyadhifa serikalini.Hii itakuwa fursa kuwaenzi na pia kuona ni kitu gani tunaweza kujifunza kusafisha uovu au uchafu unaochafua jamii zetu za sasa ( kupitia ufisadi/rushwa, uchu wa madaraka n.k.)
Kipindi hiki kitaendelea kuwalea viongozi watarajiwa wake kwa waume... na TV inaweza kushirikiana na taasisi za mafunzo ili kuhakikisha kweli tunapata matunda na siyo porojo tu kama tulivyozoea waTZ.
IN SHORT IM CRAVING FOR OUTPUT ORIENTED PROGRAMMES!


Mmmmmmmmmhhhhhhhh!!!

Du, mama upewe hiki kipindi nini. You sound so much sure of the output.

Utapenda kiendeshwe kwa mtindo gani na kiwe vipi hasa. Tell us more . . . It is interesting . . . .
 
Mmmmmmmmmhhhhhhhh!!!

Du, mama upewe hiki kipindi nini. You sound so much sure of the output.

Utapenda kiendeshwe kwa mtindo gani na kiwe vipi hasa. Tell us more . . . It is interesting . . . .


Mdau anaweza kunitafuta kwa mawazo ya kina LOL.
On a serious note kuna namna nyingi ila mimi siyo mtaalamu wa kupanga vipindi vya TV ila maoni yangu ni kama hivi:
guest speakers wenye kujadili mada na kuichambua,makala na majarida,nk.
 
Wana JF,

Kuna mdau anataka ku-invest katika TV Station DSM na sasa anaandaa Mchanganuo kwa ajili hiyo ili kuufikisha katika vyombo husika by January 2010.

Anapenda TV atakayoianzisha iwe na mambo yafuatayo:

  • Iwe na vipindi vya kuvutia sana kiasi kwamba kila anayefungulia asihamie channel nyingine.

  • Iwe inaelimisha katika mambo ya msingi ambao Watazamaji watajifunza na yatawasaidia.

  • Isaidie Kupiga Vita Ufisadi

  • Isaidie kubadilisha Attitude ya Watanzania katika kujiletea maendeleo

  • Isaidie katika kuondoa umasikini kupitia vipindi vyake

  • Isaidie katika suala zima la Ujasiliamali.

  • Pia Entertainment, Michezo, Vipindi vya watoto nk. nk.

Inatakiwa zaidi ya 60% ya vipindi viwe local programs (Local Content) na chini ya 40% vinaweza kuwa vipindi vya nje (Foreign Content).

Je ni nini mawazo yako juu ya vipindi mbalimbali na viendeshwe kwa staili gani ili kufanikisha malengo yake?
Kila la kheri. Pengine tutaomba kibarua huko.
 
Allien..
Asisahau vipindi vya michezo kubalance programme zake ukiacha vya habari, uchambuzi na nakala mbalimbali, vipindi vya elimu( sheria, biashara,uchumi) na tusiwasahau watoto katika jamii(hapa ni tatizo kubwa kwenye uendeshaji wake, ubunifu hamna). Na ajipange na watangazaji wenye ujuzi wa kufikisha ujumbe au kukiendesha kipindi vizuri siyo spoti ya channel ten.
Anaweza kupata idea nyingi za vipindi lakini awe creative kuivuta hadhira kwa matukio katika jamii yetu. Pia aangalie na wenzake(competitors) wanafanya nini katika hiyo taaluma ili kupata mwangaza na kujua wapi pa kurekebisha au kuongeza nguvu kwenye vipindi atakavyoandaa kupitia hiyo tv channel mpya.
Zaidi, atukumbuke wazawa kwenye hizo ajira yaani atafute watu wenye ujuzi wa hiyo taaluma kutoka nchini kwake.
 
fred macha ameshirikiana na mtu mmoja kuanzisha TV huko UK nimesahau jina lake ila kwa sasa anatafuta sana watafiti mbali mbali kuhusu vipindi na mambo mbali mbali kuhusu TV hiyo , ni ya uingereza lakini itakuwa inaonyesha mambo halisi ya kiafrika sio propaganda za magaribi

Hao consumer insight wako Nkurumah kuna mtu anaitwa James ni mkenya ndio Director kwa tanzania nafikiri tovuti yao ni www.ciaafrica.com , Hao research international wako Viktoria Director wao anaitwa Vuri ila kuna manaja mwingine anaitwa Tupelike Subiri nichek kama naweza kupata no zako ntakupa Pm
 
Bila kusahau mimi mwenyewe ninatarajia kuanzia mwaka huu mwishoni hivi kuanza vipindi maalumu kwenye tv mbali mbali vya kuelimisha jamii bado najiweka sawa nafikiri tutaonana na huyo mdau huko mbeleni
 
Allien..
Asisahau vipindi vya michezo kubalance programme zake ukiacha vya habari, uchambuzi na nakala mbalimbali, vipindi vya elimu( sheria, biashara,uchumi) na tusiwasahau watoto katika jamii(hapa ni tatizo kubwa kwenye uendeshaji wake, ubunifu hamna). Na ajipange na watangazaji wenye ujuzi wa kufikisha ujumbe au kukiendesha kipindi vizuri siyo spoti ya channel ten.

Anaweza kupata idea nyingi za vipindi lakini awe creative kuivuta hadhira kwa matukio katika jamii yetu. Pia aangalie na wenzake(competitors) wanafanya nini katika hiyo taaluma ili kupata mwangaza na kujua wapi pa kurekebisha au kuongeza nguvu kwenye vipindi atakavyoandaa kupitia hiyo tv channel mpya.

Zaidi, atukumbuke wazawa kwenye hizo ajira yaani atafute watu wenye ujuzi wa hiyo taaluma kutoka nchini kwake.

Mkuu Belinda, asante sana mama.

Kama ulivyoona kwenye bandiko kuu, nia ni kuwa na kitu tofauti na vilivyozoeleka. Kama utakuwa na ideas juu ya mpangilio wa vipindi na uendeshaji wake, nitaomba pia utoe mchango wake. Na nadhani hapa ndipo panapotaka ubunifu zaidi.
 
Back
Top Bottom