Mwendo kasi wamepuuza kwa 100% maelekezo ya Waziri; badala yake hata chenji za wateja wanafukia tena kwa kejeli na kiburi. SGR tutaiweza?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,105
Mdau wa Dar amekuja DM akieleza malalamiko yako na masikitiko makubwa yanayofanya na matajiri wachache wanapotaka kufilisi mali za umma.

Mdau anasema Mradi wa mwendo kazi unaosimamiwa na watanzania umepeleka dharau na fedhea kwa mamlaka zifuatazo

1. Wamedharau kwa kiwango cha juu maelekezo ya Mkuu wa Mkoa.

2. Akaenda Waziri mwenye dhamana akatoa maelekezo lakini hakuna utekelezaji

3. Awali alikwenda Waziri Mkuu naye akaongea mabadiliko yakafanyika kwa muda then kimya.

Pamoja na kukiukwa kwa maelekezo wafanyakazi wamebadili mfumo wa maisha na sasa wanajipatia kipato kwa kutotoa chenji. Asubuhi na jioni hakuna chenchi za wateja, kumbuka muda watu wanaotumia kupanga foleni.

Lakini ukifanya uchambuzi mdogo Mradi huu unaonekana una rasilimali kubwa ya watu wasiofanya kazi. Wanaripoti kazini asubuhi hadi jioni bila kazi yoyote. Mchanganuo wa wafanyakazi kwa kituo cha gerezani

1. Kuna askari kumi na mbili kwa shifti
2. Wakata tiketi 4 per shift
3. Wachanja tiketi 7 per shift
4. Wanaoratibu kupanda magari wapo 8
5. Wanaosimamia matangazo wapo 5

Kwa muktadha huu kuna zaidi ya watu 32 wanaotamatisha huduma ya mteja kupanda gari kwenye kituo kimoja.
Swali
1. Askari 12 wanafanya kazi gani vituoni endapo huduma imeboreshwa? Mbona vituo vya daladala hakuna kampuni za ulinzi? Tunadhani mwenye kampuni ya ulinzi ataruhusu huduma za kielektroniki katika mazingira haya? Akiruhusu waajiriwa wake watapata wapi pakujustfy mikataba?

2. Kituo cha gerezani kina abiria wengi kwanini madirisha ya huduma yawe manne tu?

3. Wanaoajiriwa kukata tiketi walikuwa na ulazima wakuwepo kwenye vituo?

4. Waajiriwa wengi kwenye huu Mradi ni watoto wa vigogo na ndugu zao. Akili zao zinaweza kufanya mabadiliko?

Tukumbuke Hiki ni kituo kimoja, sijachambua madereva wanaolipwa mshahara bila kufanya kazi, mameneja na viongozi waliokaa ofisini, wapo watu wameajiriwa kutafuta chenchi nk...

Kufeli huku na kiburi hiki nani yupo nyuma yake? Magu alitumbua wala deal wa mwanzo, je waliokabidhiwa lini watajifunza kwamba utawala ukibadilika watajikuta jela?
 
Una hoja ya msingi kuhusu matumizi ya mfumo wa kielektroniki. Lakini kuna maswali
a. Kwa nini viongozi waliotoa maagizo hadharani wamekaa kimya wakati maagizo yao hayajatekelezwa?
b. Kwa nini media huwa haziendi ofisini kwao ili kubalance story?
c. Suala la chenji, kwa nini BOT alitoa public announcement kuhusu coins.
d. Kuhusu wafanyakazi wengi, unafahamu separation of duties as internal control in cash management where there is no automation to prevent collusion?
Narudia tena una hoja ya msingi kwenye mfumo wa matumizi ya kadi.
 
Una hoja ya msingi kuhusu matumizi ya mfumo wa kielektroniki. Lakini kuna maswali
a. Kwa nini viongozi waliotoa maagizo hadharani wamekaa kimya wakati maagizo yao hayajatekelezwa?
b. Kwa nini media huwa haziendi ofisini kwao ili kubalance story?
c. Suala la chenji, kwa nini BOT alitoa public announcement kuhusu coins.
d. Kuhusu wafanyakazi wengi, unafahamu separation of duties as internal control in cash management where there is no automation to prevent collusion?
Narudia tena una hoja ya msingi kwenye mfumo wa matumizi ya kadi.
Separation of duties katika sekta ipi? Sekta ya ulinzi? Sekta ya wachana tiketi au watoa tiketi?

If it a matter of control, kwanini waliondoa mfumo uliokuwepo swali? Sasa hivi kuna watu wanachana tiketi kwa mikono wanacontrol nini? Je, ukilinganisha tickets zilizotolewa kwa siku na zilizochanjwa na wachanja tickets unadhani kutakuwepo na reconciliation? If it's a matter of control kusingekuwepo na umuhimu wa wachana tiketi bali wachanja tickets..

Lakini pia ukiangalia aina ya wateja wanaotumia mabasi haya unahitaji kuajiri mabaunsa wakusimamia abiria wapande magari? Tukubaliane kwamba hapa hakuna control bali kuna poor thinking na inachangiwa na kukabidhi Mradi kwa familia za matajiri na wanasiasa.

Hakuna mtu wakugusa top management ya huu Mradi kwa sababu ni watoto wao
 
Mdau wa Dar amekuja DM akieleza malalamiko yako na masikitiko makubwa yanayofanya na matajiri wachache wanapotaka kufilisi mali za umma.

e? Magu alitumbua wala deal wa mwanzo, je waliokabidhiwa lini watajifunza kwamba utawala ukibadilika watajikuta jela?
we uliona wapi watu wanauwa tekinolojia ya kisasa (tickets Scanner) ili watumie manual sasa hadi hapo tujue hakuna watu pale wapo pale kusogeza siku mbele..

Waafrica bado hatujakamilika kuwa binadamu kamili tupo kwenye process tuvumiliane jamani..
 
Separation of duties katika sekta ipi? Sekta ya ulinzi? Sekta ya wachana tiketi au watoa tiketi?

If it a matter of control, kwanini waliondoa mfumo uliokuwepo swali? Sasa hivi kuna watu wanachana tiketi kwa mikono wanacontrol nini? Je, ukilinganisha tickets zilizotolewa kwa siku na zilizochanjwa na wachanja tickets unadhani kutakuwepo na reconciliation? If it's a matter of control kusingekuwepo na umuhimu wa wachana tiketi bali wachanja tickets..

Lakini pia ukiangalia aina ya wateja wanaotumia mabasi haya unahitaji kuajiri mabaunsa wakusimamia abiria wapande magari? Tukubaliane kwamba hapa hakuna control bali kuna poor thinking na inachangiwa na kukabidhi Mradi kwa familia za matajiri na wanasiasa.

Hakuna mtu wakugusa top management ya huu Mradi kwa sababu ni watoto wao
Sekta nyingi sana zina muundo mbovu haijawahi kutokea.
Walianza vuzuri tu ila hapo Kati wakaqnza kubuni mbinu za wizi.
Wakaanza kuharibu vituo entry point.
Wakasitisha electronic tiketi wakiharibu machine.
Shida kuajiri watu wasio na elimu ya uelewa! Ndugu.!

Haikuwa na haja ya kuwa na foleni kwenye hii! Nandi maana ya mwendo kasi.
Basi lilitakiwa kuwa kituoni sio zaidi ya dk. 10 kupakia na kuondoka.
Kila.kitu upigaji tuu!!
 
Back
Top Bottom