Mdahalo ITV Bila Profesa Lipumba Na Wengine, Kwanini?

Ndugu zangu, Watanzania wenzangu, hawa kina Maggid ni wengi sana kwa sasa. Wametapakaa kila kona. Ukifuatilia vyombo vya habari vilivyoripoti leo kuhusu ile 'TV Show' ya Dk Slaa unaweza kusikia kichefuchefu na hasa magazeti ya Habari Leo, Jambo Leo na lile la Uhuru. Ameibuka mtu mmoja anayeitwa Ngeleja kujaribu kujibu hoja za Dk Slaa zinazohusu madini. Msomaji wa Magazeti pale TBC Taifa yeye ndiye alienda mbali kwa kusema, "Gazeti la Mtanzania Daima limeandika Slaa aumbuliwa" Sina uhakika kama upotoshaji huu ulikuwa wa makusudi au 'ukanjanja' wa mtangazaji huyo maana toka nizaliwe sijawahi kuliona gazeti la Mtanzania Daima.

Kuhusu Maggid, kama mtakuwa mmefuatilia tangu wiki iliyopita alianza kumtajataja Profesa Lipumba. Kwenye makala yake katika gazeti la Raia Mwema aliandika 'Mbio za Urais: Lipumba anakuja, chupa ya maji mkononi!' Aliandika mengi lakini akionyesha kuwa Watanzania wamemsahau Lipumba na kujikita zaidi kwa wagombea wengine, humo ndani akimpa 'misifa' Prof Lipumba. Maggid anacheza na akili za watu kujifanya yeye si mshabiki wa CCM. Nadhani lengo lake ni kuwa wale ambao hawataki kusikia 'madudu' ya Meneja Miradi wa CCM ambaye pia ni mgombea Urais kupitia chama hicho wamwone mbadala wake ni Profesa Lipumba na kwa kuwa huyu mgombea wa CUF sio 'dili' zaidi ya kupunguza kura za Slaa kutoka kwa wapinzani.

Kwenye Blogu yake Maggid ameshaandika mkataba wake wa kazi anayofanya sasa unaisha mwezi wa 12 mwaka huu. Maggid hata kama unafukuzia 'u DC' ndugu yangu macho yako yawe na aibu! Kuna faida gani kushusha Integrity na credibility yako kwa vivyeo vya 'kipuuzi' Maggid inaonekana Makala hii ya mdahalo wa Slaa ulishaiandika kabla hata Slaa hajaongea na kibaya zaidi hukufuatilia hata ule mjadala kwenye TV. Laiti kama ungefuatilia nina imani usinge post hiyo 'Makala Uchwara' yako. Kinachoendelea hivi sasa ni wewe kung'ang'ania kuwa ule haukuwa mdahalo na unachotaka watu wajadili kuwa ule ulikuwa mdahalo au la! Na kwa hakika umefanikiwa kwa sababu humu ndani tumeacha kujadili mambo ya muhimu aliyoyaongea Dk Slaa juzi.

Maggid kwa kuacha kumsikiliza Dk Slaa umepitwa mengi ikiwemo majibu ya yale maswali aliyoiliza yule 'mpuuzi' kwenye Blogu yako kuhusu Makaratasi Feki ya Kura kule Tunduma. Dk Slaa alijibu kwa ufasaha. Maggid nani asiyejua sasa hivi kuna mbinu chafu zimekuwa zikifanywa ili kuzuia yale anayoyasema DK Slaa kwenye mikutano yake yasiripotiwe?.

Maggid wewe endelea na ushabiki wako kwa CCM lakini ungewaonea huruma wale ndugu zako wa kule Kinyeregete. Ambao umekuwa ukitoa picha zao mara kwa mara kwenye Blogu yako wakiwa wamevaa 'masempele' na vile vijumba vyao ambavyo unajiuliza ni mabanda ya kuku au ni mapango ya kufugia ndezi. Wale wanao machotara uliowapeleka kule Kinyeregete huwezi kuniambia maswali waliyokuuliza lakini nadhani waliona kama vile wako 'Mikumi' ya wanyama wanaoitwa Binadamu! Picha zako zote za kule Kinyeregete sijawahi kuona nyumba yako au hata ya baba yako zaidi ya zile za wale unawaita shangazi zako, wajomba zako. Niambie mara ya mwisho ulimaliza usiku mzima pale Kinyeregete lini kama sio kupita dakika moja na kuwaachia ndoo za vitunguu na nyanya zile unazotuonyesha kila siku! Acha bana! Halafu najiuliza huku kwa JK umekuja lini? Najua mwaka 1995 ulikuwa wapi na mgombea wako unakumbuka alivyochafuliwa jina na hawa 'wahuni' Jamani!

Maggid wanao wanasoma International School na huenda hata maisha yao ya baadaye yanaweza yasiwe pale Kinyeregete au hata Kinondoni Biafra. Sasa mwache Slaa aje asomeshe watoto wa Kinyeregete bure na kuangalia afya zao bure, sio kuwapiga picha na vitambi vyao huku wakiwa na umri mdogo wa miaka sita na kwenda kuziuza Sweden. Acha bana!
 
Bwana Maggid labda tungeanza kwanza kwa kuelewa nini hasa maana ya mdahalo ili tuweze kuhitimisha, kama ambavyo umeshafanya, kuwa wa jana ama ulikuwa au haukuwa mdahalo. Kwa kuwa mdahalo umenzia kwa wazungu ni vyema tukajua wao wanauelewa vipi mdahalo katika mapana yake.

Kwa mujibu wa kamusi ya "Oxford Advanced Learners" toleo la saba, iliyochapishwa na Oxford University Press, mdahalo au "debate" imeelezwa ifuatavyo:


Debate:
  • Noun
(i) a formal discussion of an issue at a public hearing or in a parliament. In a debate two or more speakers express oppossing views and then there is often a vote on the issue. e.g. a debate on abortion, the motion under debate (=being discussed)
(ii) an argument or discussion expessing different opinions

  • Verb
(i) to discuss something especially formally before making a decision or finding a solution e.g. politicians will be debating the bill this week
(ii) to think carefully about something before making a decision e.g. debate with yourself.

Kwa hiyo kwa mujibu wa wenzetu neno mdahalo (debate) linaweza kutumika kama Nomino (Noun) kuongelea majadiliano yanayofanyika ama bungeni ama kwenye mkutano mwingine wowote rasmi ambamo waongeaji ama wawili au zaidi wanaeleza maoni yao katika suala linalojadiliwa kwa lengo la kufikia muafaka ama kukubali kutofautiana. Kwenye bunge wanaishia kupiga kura lakini katika public hearing huwa hakuna kupiga kura. Lakini pia unaweza kutumia neno mdahalo (debate) kama kitenzi kumaanisha majadiliano katika mkutano/kikao rasmi kabla ya watu wanaojadili hawajafikia maamuzi wanayopanga kufanya au kitendo cha mtu binafsi kutafakari jambo kabla ya kufanya uamuzi. Kwa hili la mdahalo binafsi mtu hahitaji kuwa katika mkutano au kikao rasmi.

Kwa hiyo kama tulivyoona matumizi ya neno hili ni mapana sana na maana yake inatofautiana kutegemeana na muktadha (context) shughuli yenyewe inayofanyika. Sasa tunaweza kurudi kwenye mdahalo wetu wa sasa juu ya kama kilichofanyika jana ni mdahalo au siyo mdahalo. Naweza kusema kwa uhakika kabisa kuwa kilichofanyika jana ni mdahalo (debate) kwani unakidhi vigezo vilivyoainishwa na waasisi wa neno hilo kama tulivyoona hapo juu.

Vigezo ninavyovitumia kuhitimisha haya ni kama ifuatavyo:-

Mdahalo ni majadiliano rasmi (formal discussion) - jana kulikuwa na "formal discussion".
Lazima kuwe na suala linalojadiliwa kwenye majadiliano hayo (an issue) - jana kulikuwa na "issue" ya uchaguzi ujao inayojadiliwa.
Lazima majadiliano haya yafanyike kwenye mkutano wa jamii (public hearing) au bungeni (parliament) - jana kulikuwa na "public hearing".
Maranyingi (siyo mara zote) kunakuwa na kupiga kura ili kupata upande ulioshinda - jana hakukuwa na kura ya papo kwa hapo kwani ilikuwa ni "public hearing" na siyo "parliament". Lakini kutakuwa na kupiga kura tarehe 31 october.

Kimsingi mdahalo wa jana ulilenga kuanzisha midahalo binafsi (ambayo kimsingi inatamuliwa) kwa wapiga kura ili wafanye uamuzi wa nani watampigia kura itakapofika siku yenyewe.

Naomba kuwasilisha.
KWA HIYO KUAMUA WA KUMPIGIA KURA BAINA YA DR. SLAA NA MWAKITWANGE? KWANZA NI NANI ALIYEKUOMBA UWASILISHE, AU UNADHANI UNAWASILISHA DOKEZO LA KUFISIDI NCHI. Rudi tena shule haraka! uchambuzi wako non-sense kabisa.
 
Omar,
Ahsante sana. Utafiti mdogo niliofanya umenipa matokeo haya yanayotutaka tufikiri kwa bidii. Chini hapa ni habari katika Tanzania Daima ya Jumapili, Julai 4, 2010;

Nahodha akacha mdahalo Z'bar
• Wagombea kumi kuwekwa kiti moto leo

na Shabani Matutu


amka2.gif
WAKATI taasisi huru ya habari nchini ya Vox Media Centre Ltd imeandaa mdahalo kwa wagombea urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha, amekacha mdahalo huo.
Nahodha ambaye ni mmoja wa wagombea hao 11, wanaowania uteuzi wa nafasi hiyo, amekacha mdahalo huo wa kwanza kufanyika visiwani Zanzibar tangu kuanza kwa harakati za kuwania urais, kwa madai ya kutingwa na shughuli za Baraza la Wawakilishi.
Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana, Nahodha alifafanua kuwa hatoweza kuhudhuria mdahalo huo kutokana na kuendelea kwa shughuli za Baraza la Wawakilishi visiwani Zanzibar.
Taarifa hiyo iliyosainiwa kwa niaba yake na Kaimu Katibu wa Waziri Kiongozi, Mohamed Muombwa, ilisema kuwa Nahodha anaungana na taasisi hiyo kimawazo katika kufanikisha mdahalo huo na yuko tayari kushiriki wakati wowote mwingine.
"Mheshimiwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar amepokea kwa furaha mwaliko wako kushiriki katika mdahalo wa wagombea urais Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi. Hata hivyo kutokana na kuendelea kwa shughuli za Baraza la Wawakilishi hivi sasa, tunasikitika kukuarifu kuwa hataweza kuhudhuria," ilisema taarifa hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Vox Media Centre Ltd, Ansbert Ngurumo, alisema wanaendelea na maandalizi ya mdahalo huo kama ulivyopangwa.
Hata hivyo inawezekana waziri kiongozi huyo hakutaka kuhudhuria mdahalo huo kwa sababu za kisiasa, kwani unafanyika leo, ambapo hakuna shughuli zozote za Baraza la Wawakilishi visiwani humo.
Mdahalo huo utakaorushwa hewani na kituo cha televisheni cha Star TV, ulipangwa kuwashirikisha wagombea 11 wanaoomba uteuzi wa kuwania kiti cha urais Visiwani Zanzibar, kinachoshikiliwa na Rais Amani Abeid Karume.
Kwa mujibu wa Ngurumo, mdahalo huo unatarajiwa kufanyika leo, katika Hoteli ya Ocean View Hotel, Zanzibar kuanzia saa 3:30 asubuhi hadi saa 7:00 mchana.
Alisema mdahalo huo utarekodiwa kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana na unatarajiwa kurushwa na kituo cha Star Tv mwanzoni mwa wiki ijayo katika siku itakayotangazwa baadaye.
Lengo la mdahalo huo ni kuwapatia fursa wagombea hao kujieleza mbele ya wanahabari na umma utakaohudhuria, na utakaotazama kipindi hicho kwenye televisheni ili kuwawezesha wananchi kuwajua wagombea ikiwa ni pamoja na kuwapima nia na uwezo wao kuelekea Uchaguzi Mkuu.
Mdahalo huo unafanyika wakati ambapo CCM inaelekea kufanya vikao vya mwisho vya uteuzi, siku moja baada ya Kamati Kuu Maalumu ya chama hicho kufanya kikao cha kupendekeza majina kwenye Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM vitakavyofanyika mjini Dodoma, wiki ijayo.
Wagombea hawa wataulizwa maswali kuhusu masuala yote muhimu ya siasa, uchumi na ya utawala Zanzibar, na itakuwa fursa adhimu kwao kuwashawishi wanachama na viongozi wenzao kuhusu maono yao katika nchi hiyo.
Mbali ya Nahodha ambaye hatashiriki, wagombea waliothibitisha kushiriki ni pamoja na Waziri Kiongozi mstaafu, Dk. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein, Balozi Ali Karume, Ali Juma Shamuhuna, Hamad Mshindo, Haruna Suleiman, Mohammed Yusuf Mshamba, Omar Sheha Mussa na Mohammed Aboud.

So what about it?.....mbona hao wengine walihudhuria?Ansbert tumeambiwa ni MD haimaanishi kuwa ndiye mmiliki...kwani Kiondo Mshana anamiliki IPP Media Ltd?
 
Omar,
Ahsante sana. Utafiti mdogo niliofanya umenipa matokeo haya yanayotutaka tufikiri kwa bidii. Chini hapa ni habari katika Tanzania Daima ya Jumapili, Julai 4, 2010;

Nahodha akacha mdahalo Z'bar
• Wagombea kumi kuwekwa kiti moto leo

na Shabani Matutu


amka2.gif
WAKATI taasisi huru ya habari nchini ya Vox Media Centre Ltd imeandaa mdahalo kwa wagombea urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Waziri Kiongozi Shamsi Vuai Nahodha, amekacha mdahalo huo.
Nahodha ambaye ni mmoja wa wagombea hao 11, wanaowania uteuzi wa nafasi hiyo, amekacha mdahalo huo wa kwanza kufanyika visiwani Zanzibar tangu kuanza kwa harakati za kuwania urais, kwa madai ya kutingwa na shughuli za Baraza la Wawakilishi.
Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari jana, Nahodha alifafanua kuwa hatoweza kuhudhuria mdahalo huo kutokana na kuendelea kwa shughuli za Baraza la Wawakilishi visiwani Zanzibar.
Taarifa hiyo iliyosainiwa kwa niaba yake na Kaimu Katibu wa Waziri Kiongozi, Mohamed Muombwa, ilisema kuwa Nahodha anaungana na taasisi hiyo kimawazo katika kufanikisha mdahalo huo na yuko tayari kushiriki wakati wowote mwingine.
"Mheshimiwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar amepokea kwa furaha mwaliko wako kushiriki katika mdahalo wa wagombea urais Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi. Hata hivyo kutokana na kuendelea kwa shughuli za Baraza la Wawakilishi hivi sasa, tunasikitika kukuarifu kuwa hataweza kuhudhuria," ilisema taarifa hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili, Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi ya Vox Media Centre Ltd, Ansbert Ngurumo, alisema wanaendelea na maandalizi ya mdahalo huo kama ulivyopangwa.
.

Hii ndiyo ilikuwa nia yako, wewe ni mtu hatari sana watu hawajui tu, tuwekee scan ya pasipoti yako hapa kama unaubavu, Tuache wapiga kura halali tuchague..wewe ni mtalii tu.
 
Nothing can be further from the truth. CCM walikataa tangu mwanzo kuhusu midahalo kwa wangombea wake kuanzia ubunge hadi urais. Inavyoonekana Prof. Lipumba yuko so busy na kampeni kiasi kwamba hata mahojiano kati ya ITV na wagombea Urais yanayoendelea katikati ya wiki hajaonekana ( Kina Dovutwa na Mziray na Dr. Slaaa) tumewaona. Inawezekana kwa vile Lipumba anatumia usafiri wa gari muda wake kwa mahojiano ni finyu sana. Sasa sijui Majjid alitaka Mdahalo Dr. Slaa afanye na nani? Hata mahojioano kati ya Star TV Dr. Slaa alifanya na Col. Kinana kana kwamba Kinana ni mgombea! Watu walimuuliza kwa nini JK hayupo Kinana akagwaya!! Sasa ITV wangefanyaje??
 
Ndugu Zangu,
Jana tumesikiliza mdahalo, au labda mazungumzo au mahojiano kati ya Dr Slaa ( CHADEMA) na Rosemary Mwakitwange. Mahojiano yaliyoruhusu wengine kuchangia kwa njia ya simu pia.
Tunawapongeza walioshiriki kufanya jitihada zile. Ilitoa fursa kwa sisi wapiga kura kumsikiliza Dr Slaa. Hata hivyo, pungufu kubwa kabisa lililoonekana ni namna waandaaji walivyoandaa mdahalo wa upande mmoja bila kuwashirikisha wagombea wengine wa Urais waliopitishwa na NEC. Maana, ni vema pia tukatofautisha maana ya mdahalo na mahojiano. Kama yale ya jana yalikuwa ni mahojiano tu, hakuna tatizo kwa mgombea mmoja tu kuhojiwa. Lakini kama unaitwa mdahalo, basi, tujadili maana ya mdahalo.

Kama ni mdahalo, basi, ingekuwa ni vema na busara kwa wagombea wengine wa Urais kushiriki. Bila shaka, wagombea wengine nao wana haki za msingi za kupewa nafasi ya kuelezea sera zao na kujibu maswali ya wapiga kura. Hata kama chama tawala, CCM kimeweka wazi kuwa mgombea wao hatashiriki mdahalo, lakini hatujasikia vyama vingine vitoa misimamo kama hiyo.

Wengi wetu tungependa kuona wagombea wengine wa Urais nao wakialikwa, hivyo basi, kupewa fursa ya kuelezea sera za vyama vyao na kuulizwa maswali. Kungetoa fursa ya wagombea hao kushindana kwa hoja pia. Labda kama kuna maelezo ya kuwa wagombea hao walialikwa lakini hawakuitikia mwaliko wa kwenda studioni. Au kuwa gharama za muda wa kurusha hewani mdahalo ziligharamiwa na chama cha mgombea aliyefika kwenye mdahalo/mahojiano. Kama sivyo, basi, waandaaji watakuwa hawakuwatendea haki wagombea na wapiga kura kwa ujumla wao.

Maana, tukianza sasa kujenga tabia ya kubagua wagombea itakuwa ni jambo la hatari sana. Ikumbukwe, tangu Uchaguzi Mkuu wa 1995, tulianza kujenga misingi mizuri ya wagombea kupewa fursa sawa. Kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 wagombea wote wa Urais walialikwa kwenye mdahalo uliofanyika kwenye iliyokuwa Kilimanjaro Hotel. Kama inavyoonekana pichani, kulikuwa na Profesa Lipumba, Augustino Mrema, Benjamin Mkapa na Bwana Cheyo. Historia ni mwalimu mzuri. Tujifunze.

Maggid,
Iringa, Jumapili, Oktoba, 24, 2010

Nakubaliana na wewe kabisa....Mdahalo ITV Bila JK kwa nini? Maggid naomba jibu
 
Ndugu Zangu,

Kwanza kabisa , niweke wazi, kwamba kwa staili yangu nilichokoza kwa makusudi mjadala ili kutengeneza mwelekeo wa mjadala ambao ungetusaidia kuyafanya mawili haya;
Mosi, kuumiza vichwa vyetu kujadili nini haswa maana ya mdahalo na hususan mdahalo wenye kuhusu masuala ya msingi ya kitaifa. Kufanya kazi ya kuitafuta tofauti ya kimsingi kati ya mdahalo na mahojiano. Hilo nilijaribu kuliandika kwa msisitizo katika majibu yangu katika baadhi ya posti zenu.
Pili, nilitarajia, baada ya kukaikamilisha kazi hiyo ya kwanza, wengi wetu tungejikita kwenye kujadili issues zilizozungumwa na Dr Slaa usiku ule wa Jumamosi. Nilishangaa, kuwa wengi wakaelekea kwenye kuniachia mimi niifanye kazi hiyo. Sikufanya hivyo, kwa makusudi kabisa. Ningefanya hivyo, mjadala huu ungemalizika jana usiku kwa watu kuandika ' thanks' zao. Tusingejifunza mengi.

Tukija kwenye issues, Dr Slaa alipata fursa nzuri sana ya kujieleza. ( Niligusia hilo kwenye moja ya majibu yangu ya posti ). Hata hivyo, kwa mtazamo wangu, Dr Slaa angefanya vema zaidi kama angepambanishwa na mtu kama Profesa Lipumba. Na hapo, umma ungeweza kumpa alama za ziada. Na laiti JK naye angeingiza timu, basi, tungeshuhudia ' mdahalo wa karne' kati ya Profesa Lipumba, Jakaya Kikwete , Dr Slaa na akina Hashim Rungwe na wenzake. Ni katika hali kama hizo, wapiga kura tunasaidiwa kupeperusha pumba na kubaki na mchele. Niliandika, kuwa ni mkakati wa kimakosa kwa CCM kuamua kutoshiriki midahalo. Maana, huko twendako wataihitaji na kuna watakaowashangaa watakapoonyesha hitaji hilo.
Sababu kubwa ya kuwepo walau wagombea wawili kwenye mdahalo ni ukweli, kuwa wapiga kura tungepata fursa ya kusikia sera mbili tofauti au majibu mawili tofauti kwa swali moja. Hapo, tungeweza kujua nani bora zaidi.

Format ya maswali ingekuwa ni yale maswali magumu yanayohusu most controversial issues of our time. Issues kama uharibifu wa mazingira, ufisadi, mikataba mikubwa ya uwekezaji,. Rasilimali za nchi kama madini, Uongozi bora na maadili ya viongozi( Tuna mfano wa Rais aliyefungua kampuni binafsi na kwa kutumia anwani ya Ikulu)
Tuna issues kama za kuwepo au kutokuwepo kwa wagombea binafsi, Katiba, Uraia wa nchi mbili, upigaji kura kwa Watanzania walio nje, mishahara ya Wafanyakazi, nafasi ya wakulima katika uchumi wan chi (Kilimo kwanza), maradhi (UKIMWI na Malaria). Bila kusahau Kushuka kwa elimu na utitiri wa international schools na academies zilizo chini ya viwango. Na mengineyo mengi.
Kuna pia maswali ambayo hayakuulizwa usiku ule. Moja ni hili la itikadi. Mathalan, Dr Slaa na CHADEMA wanasimama katika itikadi gani kwa sasa katika kutekeleza sera zao? Na kama Jakaya Kikwete, Profesa Lipumba na wengine wangekuwapo, nao wangeulizwa swali hilo.
Mwisho, nasikitika kuwa huenda wagombea wengine wa Urais mbali ya Profesa Lipumba , hawatapata nafasi ya kufanya mahojiano kama wenzao wa CHADEMA, CUF na labda CCM. Nafikiri hawatendewi haki akina Hashim Rungwe , Kuga Mziray na mwenzao Muta wa TLP kama nao hawatapata hata robo saa tu ya mahojiano.
Huko twendako, tuwe na matayarisho ya mapema ya midahalo ya kitaifa inapofikia wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu au masuala mengine makubwa ya kitaifa, kama vile Katiba mpya. Kuwepo na taasisi huru na zenye kuaminika na umma zitakazoratibu midahalo hiyo. Kuwepo na kalenda ya midahalo. Mgombea atakayeshindwa kuhudhuria katika tarehe husika ilihali amepewa mwaliko, basi, huyo itakuwa ' imekula kwake' kama wanavyosema mitaani siku hizi.

Nihitimishe kwa kuwashukuru nyote. Nimesoma kila kilichoingizwa kwenye mjadala huu. Kuna mlionishambulia kwa matusi, nimeyasoma matusi yenu, mengine yamenivunja mbavu. Kuna mliotoka nje ya mada na kunishambulia mimi binafsi badala ya kuikabili hoja iliyowasilishwa. Hilo nalo ni pungufu la kawaida. Na kwa kuchokoza mjadala huu kuna wanaojisikia nimewakwaza, basi, haikuwa dhamira yangu. Sijaufunga mjadala.

Ahsanteni Sana.
Iringa,
Jumatatu, Oktoba, 25, 2010
 
Ndugu Zangu,

Kwanza kabisa , niweke wazi, kwamba kwa staili yangu nilichokoza kwa makusudi mjadala ili kutengeneza mwelekeo wa mjadala ambao ungetusaidia kuyafanya mawili haya;
Mosi, kuumiza vichwa vyetu kujadili nini haswa maana ya mdahalo na hususan mdahalo wenye kuhusu masuala ya msingi ya kitaifa. Kufanya kazi ya kuitafuta tofauti ya kimsingi kati ya mdahalo na mahojiano. Hilo nilijaribu kuliandika kwa msisitizo katika majibu yangu katika baadhi ya posti zenu.
Pili, nilitarajia, baada ya kukaikamilisha kazi hiyo ya kwanza, wengi wetu tungejikita kwenye kujadili issues zilizozungumwa na Dr Slaa usiku ule wa Jumamosi. Nilishangaa, kuwa wengi wakaelekea kwenye kuniachia mimi niifanye kazi hiyo. Sikufanya hivyo, kwa makusudi kabisa. Ningefanya hivyo, mjadala huu ungemalizika jana usiku kwa watu kuandika ' thanks' zao. Tusingejifunza mengi.

Tukija kwenye issues, Dr Slaa alipata fursa nzuri sana ya kujieleza. ( Niligusia hilo kwenye moja ya majibu yangu ya posti ). Hata hivyo, kwa mtazamo wangu, Dr Slaa angefanya vema zaidi kama angepambanishwa na mtu kama Profesa Lipumba. Na hapo, umma ungeweza kumpa alama za ziada. Na laiti JK naye angeingiza timu, basi, tungeshuhudia ' mdahalo wa karne' kati ya Profesa Lipumba, Jakaya Kikwete , Dr Slaa na akina Hashim Rungwe na wenzake. Ni katika hali kama hizo, wapiga kura tunasaidiwa kupeperusha pumba na kubaki na mchele. Niliandika, kuwa ni mkakati wa kimakosa kwa CCM kuamua kutoshiriki midahalo. Maana, huko twendako wataihitaji na kuna watakaowashangaa watakapoonyesha hitaji hilo.
Sababu kubwa ya kuwepo walau wagombea wawili kwenye mdahalo ni ukweli, kuwa wapiga kura tungepata fursa ya kusikia sera mbili tofauti au majibu mawili tofauti kwa swali moja. Hapo, tungeweza kujua nani bora zaidi.

Format ya maswali ingekuwa ni yale maswali magumu yanayohusu most controversial issues of our time. Issues kama uharibifu wa mazingira, ufisadi, mikataba mikubwa ya uwekezaji,. Rasilimali za nchi kama madini, Uongozi bora na maadili ya viongozi( Tuna mfano wa Rais aliyefungua kampuni binafsi na kwa kutumia anwani ya Ikulu)
Tuna issues kama za kuwepo au kutokuwepo kwa wagombea binafsi, Katiba, Uraia wa nchi mbili, upigaji kura kwa Watanzania walio nje, mishahara ya Wafanyakazi, nafasi ya wakulima katika uchumi wan chi (Kilimo kwanza), maradhi (UKIMWI na Malaria). Bila kusahau Kushuka kwa elimu na utitiri wa international schools na academies zilizo chini ya viwango. Na mengineyo mengi.
Kuna pia maswali ambayo hayakuulizwa usiku ule. Moja ni hili la itikadi. Mathalan, Dr Slaa na CHADEMA wanasimama katika itikadi gani kwa sasa katika kutekeleza sera zao? Na kama Jakaya Kikwete, Profesa Lipumba na wengine wangekuwapo, nao wangeulizwa swali hilo.
Mwisho, nasikitika kuwa huenda wagombea wengine wa Urais mbali ya Profesa Lipumba , hawatapata nafasi ya kufanya mahojiano kama wenzao wa CHADEMA, CUF na labda CCM. Nafikiri hawatendewi haki akina Hashim Rungwe , Kuga Mziray na mwenzao Muta wa TLP kama nao hawatapata hata robo saa tu ya mahojiano.
Huko twendako, tuwe na matayarisho ya mapema ya midahalo ya kitaifa inapofikia wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu au masuala mengine makubwa ya kitaifa, kama vile Katiba mpya. Kuwepo na taasisi huru na zenye kuaminika na umma zitakazoratibu midahalo hiyo. Kuwepo na kalenda ya midahalo. Mgombea atakayeshindwa kuhudhuria katika tarehe husika ilihali amepewa mwaliko, basi, huyo itakuwa ' imekula kwake' kama wanavyosema mitaani siku hizi.

Nihitimishe kwa kuwashukuru nyote. Nimesoma kila kilichoingizwa kwenye mjadala huu. Kuna mlionishambulia kwa matusi, nimeyasoma matusi yenu, mengine yamenivunja mbavu. Kuna mliotoka nje ya mada na kunishambulia mimi binafsi badala ya kuikabili hoja iliyowasilishwa. Hilo nalo ni pungufu la kawaida. Na kwa kuchokoza mjadala huu kuna wanaojisikia nimewakwaza, basi, haikuwa dhamira yangu. Sijaufunga mjadala.

Ahsanteni Sana.
Iringa,
Jumatatu, Oktoba, 25, 2010

wewe huna akili hujaona kipindi ila unakijadili ndio maana kuna mtu kasema hapo kwanza uliandika kabla .....shame on u
 
Ndugu Zangu,

Kwanza kabisa , niweke wazi, kwamba kwa staili yangu nilichokoza kwa makusudi mjadala ili kutengeneza mwelekeo wa mjadala ambao ungetusaidia kuyafanya mawili haya;
Mosi, kuumiza vichwa vyetu kujadili nini haswa maana ya mdahalo na hususan mdahalo wenye kuhusu masuala ya msingi ya kitaifa. Kufanya kazi ya kuitafuta tofauti ya kimsingi kati ya mdahalo na mahojiano. Hilo nilijaribu kuliandika kwa msisitizo katika majibu yangu katika baadhi ya posti zenu.
Pili, nilitarajia, baada ya kukaikamilisha kazi hiyo ya kwanza, wengi wetu tungejikita kwenye kujadili issues zilizozungumwa na Dr Slaa usiku ule wa Jumamosi. Nilishangaa, kuwa wengi wakaelekea kwenye kuniachia mimi niifanye kazi hiyo. Sikufanya hivyo, kwa makusudi kabisa. Ningefanya hivyo, mjadala huu ungemalizika jana usiku kwa watu kuandika ' thanks' zao. Tusingejifunza mengi.

Tukija kwenye issues, Dr Slaa alipata fursa nzuri sana ya kujieleza. ( Niligusia hilo kwenye moja ya majibu yangu ya posti ). Hata hivyo, kwa mtazamo wangu, Dr Slaa angefanya vema zaidi kama angepambanishwa na mtu kama Profesa Lipumba. Na hapo, umma ungeweza kumpa alama za ziada. Na laiti JK naye angeingiza timu, basi, tungeshuhudia ' mdahalo wa karne' kati ya Profesa Lipumba, Jakaya Kikwete , Dr Slaa na akina Hashim Rungwe na wenzake. Ni katika hali kama hizo, wapiga kura tunasaidiwa kupeperusha pumba na kubaki na mchele. Niliandika, kuwa ni mkakati wa kimakosa kwa CCM kuamua kutoshiriki midahalo. Maana, huko twendako wataihitaji na kuna watakaowashangaa watakapoonyesha hitaji hilo.
Sababu kubwa ya kuwepo walau wagombea wawili kwenye mdahalo ni ukweli, kuwa wapiga kura tungepata fursa ya kusikia sera mbili tofauti au majibu mawili tofauti kwa swali moja. Hapo, tungeweza kujua nani bora zaidi.

Format ya maswali ingekuwa ni yale maswali magumu yanayohusu most controversial issues of our time. Issues kama uharibifu wa mazingira, ufisadi, mikataba mikubwa ya uwekezaji,. Rasilimali za nchi kama madini, Uongozi bora na maadili ya viongozi( Tuna mfano wa Rais aliyefungua kampuni binafsi na kwa kutumia anwani ya Ikulu)
Tuna issues kama za kuwepo au kutokuwepo kwa wagombea binafsi, Katiba, Uraia wa nchi mbili, upigaji kura kwa Watanzania walio nje, mishahara ya Wafanyakazi, nafasi ya wakulima katika uchumi wan chi (Kilimo kwanza), maradhi (UKIMWI na Malaria). Bila kusahau Kushuka kwa elimu na utitiri wa international schools na academies zilizo chini ya viwango. Na mengineyo mengi.
Kuna pia maswali ambayo hayakuulizwa usiku ule. Moja ni hili la itikadi. Mathalan, Dr Slaa na CHADEMA wanasimama katika itikadi gani kwa sasa katika kutekeleza sera zao? Na kama Jakaya Kikwete, Profesa Lipumba na wengine wangekuwapo, nao wangeulizwa swali hilo.
Mwisho, nasikitika kuwa huenda wagombea wengine wa Urais mbali ya Profesa Lipumba , hawatapata nafasi ya kufanya mahojiano kama wenzao wa CHADEMA, CUF na labda CCM. Nafikiri hawatendewi haki akina Hashim Rungwe , Kuga Mziray na mwenzao Muta wa TLP kama nao hawatapata hata robo saa tu ya mahojiano.
Huko twendako, tuwe na matayarisho ya mapema ya midahalo ya kitaifa inapofikia wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu au masuala mengine makubwa ya kitaifa, kama vile Katiba mpya. Kuwepo na taasisi huru na zenye kuaminika na umma zitakazoratibu midahalo hiyo. Kuwepo na kalenda ya midahalo. Mgombea atakayeshindwa kuhudhuria katika tarehe husika ilihali amepewa mwaliko, basi, huyo itakuwa ' imekula kwake' kama wanavyosema mitaani siku hizi.

Nihitimishe kwa kuwashukuru nyote. Nimesoma kila kilichoingizwa kwenye mjadala huu. Kuna mlionishambulia kwa matusi, nimeyasoma matusi yenu, mengine yamenivunja mbavu. Kuna mliotoka nje ya mada na kunishambulia mimi binafsi badala ya kuikabili hoja iliyowasilishwa. Hilo nalo ni pungufu la kawaida. Na kwa kuchokoza mjadala huu kuna wanaojisikia nimewakwaza, basi, haikuwa dhamira yangu. Sijaufunga mjadala.

Ahsanteni Sana.
Iringa,
Jumatatu, Oktoba, 25, 2010
Next?
 
Baregu hawezi kumruhusu Slaa kukaa jukwaa moja na Lipumba kwenye mdahalo. Anajua kilichompata Mrema Mwaka 1995.
 
Baregu hawezi kumruhusu Slaa kukaa jukwaa moja na Lipumba kwenye mdahalo. Anajua kilichompata Mrema Mwaka 1995.

La hasha....Mrema mwenyewe ndie alijiharibia...vile vitu walivyomwambia wakina Baregu azungumzie akavidaharau na kuweka pembeni..akakazania Chavda..Chavda...nusura nimpopoe mawe.....sasa wewe unataka kusema tafauti ngugu?
 
Baregu hawezi kumruhusu Slaa kukaa jukwaa moja na Lipumba kwenye mdahalo. Anajua kilichompata Mrema Mwaka 1995.

Lipumba is a professor (Dr) na kwa mtazamo wangu he is no where near Dr. Slaa kwenye uwezo wa kujenga hoja.
 
.
Maggid wewe endelea na ushabiki wako kwa CCM lakini ungewaonea huruma wale ndugu zako wa kule Kinyeregete. Ambao umekuwa ukitoa picha zao mara kwa mara kwenye Blogu yako wakiwa wamevaa 'masempele' na vile vijumba vyao ambavyo unajiuliza ni mabanda ya kuku au ni mapango ya kufugia ndezi. Wale wanao machotara uliowapeleka kule Kinyeregete huwezi kuniambia maswali waliyokuuliza lakini nadhani waliona kama vile wako 'Mikumi' ya wanyama wanaoitwa Binadamu! Picha zako zote za kule Kinyeregete sijawahi kuona nyumba yako au hata ya baba yako zaidi ya zile za wale unawaita shangazi zako, wajomba zako. Niambie mara ya mwisho ulimaliza usiku mzima pale Kinyeregete lini kama sio kupita dakika moja na kuwaachia ndoo za vitunguu na nyanya zile unazotuonyesha kila siku! Acha bana! Halafu najiuliza huku kwa JK umekuja lini? Najua mwaka 1995 ulikuwa wapi na mgombea wako unakumbuka alivyochafuliwa jina na hawa 'wahuni' Jamani!

Maggid wanao wanasoma International School na huenda hata maisha yao ya baadaye yanaweza yasiwe pale Kinyeregete au hata Kinondoni Biafra. Sasa mwache Slaa aje asomeshe watoto wa Kinyeregete bure na kuangalia afya zao bure, sio kuwapiga picha na vitambi vyao huku wakiwa na umri mdogo wa miaka sita na kwenda kuziuza Sweden. Acha bana!

Kwa maneno hayo kwenye red, hata kama Magid ni Mchmia tumbo namba moja, atatokwa machozi. Haya maneno ndiyo yaliyomfanya Yuda ajinyonge, baada ya kugundua kuwa, pesa si kila kitu. Baada ya kuona mtu wake aliyekuwa anampenda kweli kweli anasulubiwa kwa vipande thelathini vya fedha.
Maggid Pesa si kila kitu. Wala ufuasi was dini haukufanyi uwe mtakatifu. Ni ukweli tu ndiyo utakufanya uishi huru, kwenye jamii ya watu huru, ambao wanakuona wewe ni mwenzao. Jina la Nyerere litaishi milele, lakini sijui kama jina la Kingunge Ngombare Mwiru litadumu hata mwezi mmoja ndani ya masikio ya Watanzania siku Mungu akimchukua!
Usiuze utu, kwa ushabiki na pesa kwa vile tu umelipwa talanta mia. Maisha ni zaidi ya fedha!
 
Ndugu Zangu,
Jana tumesikiliza mdahalo, au labda mazungumzo au mahojiano kati ya Dr Slaa ( CHADEMA) na Rosemary Mwakitwange. Mahojiano yaliyoruhusu wengine kuchangia kwa njia ya simu pia.
Tunawapongeza walioshiriki kufanya jitihada zile. Ilitoa fursa kwa sisi wapiga kura kumsikiliza Dr Slaa. Hata hivyo, pungufu kubwa kabisa lililoonekana ni namna waandaaji walivyoandaa mdahalo wa upande mmoja bila kuwashirikisha wagombea wengine wa Urais waliopitishwa na NEC. Maana, ni vema pia tukatofautisha maana ya mdahalo na mahojiano. Kama yale ya jana yalikuwa ni mahojiano tu, hakuna tatizo kwa mgombea mmoja tu kuhojiwa. Lakini kama unaitwa mdahalo, basi, tujadili maana ya mdahalo.

Kama ni mdahalo, basi, ingekuwa ni vema na busara kwa wagombea wengine wa Urais kushiriki. Bila shaka, wagombea wengine nao wana haki za msingi za kupewa nafasi ya kuelezea sera zao na kujibu maswali ya wapiga kura. Hata kama chama tawala, CCM kimeweka wazi kuwa mgombea wao hatashiriki mdahalo, lakini hatujasikia vyama vingine vitoa misimamo kama hiyo.

Wengi wetu tungependa kuona wagombea wengine wa Urais nao wakialikwa, hivyo basi, kupewa fursa ya kuelezea sera za vyama vyao na kuulizwa maswali. Kungetoa fursa ya wagombea hao kushindana kwa hoja pia. Labda kama kuna maelezo ya kuwa wagombea hao walialikwa lakini hawakuitikia mwaliko wa kwenda studioni. Au kuwa gharama za muda wa kurusha hewani mdahalo ziligharamiwa na chama cha mgombea aliyefika kwenye mdahalo/mahojiano. Kama sivyo, basi, waandaaji watakuwa hawakuwatendea haki wagombea na wapiga kura kwa ujumla wao.

Maana, tukianza sasa kujenga tabia ya kubagua wagombea itakuwa ni jambo la hatari sana. Ikumbukwe, tangu Uchaguzi Mkuu wa 1995, tulianza kujenga misingi mizuri ya wagombea kupewa fursa sawa. Kwenye uchaguzi wa mwaka 1995 wagombea wote wa Urais walialikwa kwenye mdahalo uliofanyika kwenye iliyokuwa Kilimanjaro Hotel. Kama inavyoonekana pichani, kulikuwa na Profesa Lipumba, Augustino Mrema, Benjamin Mkapa na Bwana Cheyo. Historia ni mwalimu mzuri. Tujifunze.

Maggid,
Iringa, Jumapili, Oktoba, 24, 2010
Mkuu, Wale wasiojiamini, wemegomea mdahalo, wanaogopa maswali ya papo kwa papo. Mfano Mh. makamba alisema ukitaka washiriki wapewe maswali kabla. wampe Kinana awatafutie majibu kwanza ndo watashiriki. Dr. Wakweli Slaa amefikisha ujumbe. Kama una hoja sema kwa yale aliyojibu. Ulikuwa mdahalo, mahojiano, au majibizano haijalishi, Ujumbe umefika.
 
mengi in nature mbaguzi na hakuna sumu mbaya kwa taifa kuliko ubaguzi

Sasa huko ni kuchanganyikiwa! Waliojirani wamnusuru asijejitundika kamba! Hafla ile na nyingine zitakazofuata zimeandaliwa na asasi maalum ikiwemo vox media, kazi ya ITV ni kurusha matangazo... Kutamka ulicho na hakika nacho ndio busara yenyewe!
 
Back
Top Bottom