Mchemsho wa TANESCO? Nchi nzima haina umeme

Leo ni ya pili mgao wa umeme umelikumba jiji La Daresalam na Zenji ni ya tano hakuna umeme , maji yamekatika jeneretor zinanguruma ,mifuko ya plastiki mali kwa wanaokaa magolofani hutumia kujazia haja kubwa ,na kuirusha madilishani kwa hasira.
Je huku si ndio kushindwa kwa serikali au watasingizia mtikisiko wa uchumi huko ulimwengu wa kwanza ? Maana ikiwa mtikisiko ni hivi je ukianguka ?

Labda kuna sehemu tu za Dar zilizokatika umeme, leo ya pili nipo maeneo ya Sinza, umeme kaa kazi, na ushahidi ni post kibao nilizotuma jana na leo. Maeneo mengine ya Dar sina uhakika.
 
Hii ni mbaya sana ,sasa inakuwaje kama umeme unakatika na uzalishaji si unapungua duh,we need uncle Sam.
 
Labda kuna sehemu tu za Dar zilizokatika umeme, leo ya pili nipo maeneo ya Sinza, umeme kaa kazi, na ushahidi ni post kibao nilizotuma jana na leo. Maeneo mengine ya Dar sina uhakika.
Inawezekana wanatumia jenerator ,we hujui umekazania kukandamisa keybode. Hapo Sinza ndio usiseme vibatari kibao.
 
Angalia msiunguze nyumba kwa mishumaa,tulionchi za watu tulishsahau kukatika kwa umeme.Rashid alisema hana mpango wa kulinusuru taifa na mgao wa mwezi wa tisa, sasa cjui kama ana na mpango wa kupeleka nguzo walau moja ya umeme kijijini!! Maana na dar yenyewe kuna maeneo hamana umeme vilevile,waliweka nguzo na nyaya wakatulia kama hawajalipwa vile!!!!!
 
Mimi nina umeme siku nzima leo, na nina uhakika sina Genereta unless Dowans wameamua kuniwekea lile lao!
Jana ilikua noma lakini! Mambo yanazidi kuwa mabaya badala ya kuwa mazuri!
 
Inawezekana wanatumia jenerator ,we hujui umekazania kukandamisa keybode. Hapo Sinza ndio usiseme vibatari kibao.

Hapana, hatuna jenereta wala backup power ya aina yeyote ile lakini umeme tunao na nimeongea na Upanga wanao, sasa sijui maeneo mengine.
 
Mwiba acha propaganda. Huu wakati na aina ya propaganda zako haziendani. Bongo mbona umeme uko fresh tu?
Tafuta gear inayoendana na karne hii.
 
Hivi ni kweli kuwa hata leo eneo kubwa la nchi halina umeme? Nimeshtuliwa na jamaa yangu aliye Dar
 
Hivi ni kweli kuwa hata leo eneo kubwa la nchi halina umeme? Nimeshtuliwa na jamaa yangu aliye Dar


Hivi TZ bado kuna umeme wa Tanesco??? Mimi nifikiri zile kelele za majenereta zinathbitisha watu wanajizalishia umeme wao wenyewe.

Anyway, maisha bora kwa kila mtanzania siyo umeme bali ni "barabara, mashule n.k." (JK, 2009).
 
Nahisi national grid ilipata mshikeli ika-trip, ila sasa mambo shwari kwani umeme umerudishwa!!!
 
TANESCO waache urasimu, Stand by Genset zipo waende pale SCANIA TANZANIA, Kuna generator kubwa za kusaidia upungufu wa umme zaidi ya zile walizokodisha kutoka kampuni ya AGGRECO.
 
poleni ndugu sie tulio jirani na jikoni kidatu,umeme ni 24/7 hatujui hata. huo msamiati...ila mto umejaa maji kibao sijui tatizo ni songgas au....?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom