Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,888
- 2,772
Nimeshayasikia kama matatu hivi. yote ni ya kufikirika tu, hakuna la ukweli hata moja. Eti wakwe wanakuja wataogea nini? lingine jamaa hajaoga siku tatu, anaishi sinza anataka kuomba maji tegeta. lingine mke anamkimbia mumewe kisa hakuna maji. na mtoto nguo zake chafu hadi rangi imebadilika. kifupi DAWASCO hawana watu wa kuwatengenezea matangazo yao-wanabuni tu. hawana watu makini wa masoko. Hivi wanataka tuamini kuwa tunaishi katika ulimwengu ambao hakuna chaguo lingine isipokuwa wao tu? Kwani wakazi wa tabata, ubungo, kimara, etc. wanaishije? wanataka tuamini kuwa kila nyumba tanzania hii inategemea maji yao? Ningeandika mengi sana ila kwa huo muhtasari inatosha. DAWASCO wajipange, na matangazo yao yaendane na mazingira halisi wala si ya kubuni kama wanavyofanya.