benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mango akiwa ziarani Mwanza amesema hataki kusikia tena Barabara zikifungwa kwa masaa mengi ili apite, huku akisema dakika 10 zinatosha ili Wananchi waendelee na shughuli zao.

Dr. Mpango amewaomba radhi Wananchi kwa usumbufu walioupata baada ya jana Barabara kufungwa kwa saa nne ili veve apite "Nilishamwambia IGP na nirudie kuwaambia Makamanda wa Polisi wa Mikoa, mambo ya kufunga barabara kwa masaa mengi kisa tu Mtoto wa masikini Philip Mpango anapita hapana"

"Jana naambiwa mmefunga Barabara mpaka masaa manne haiwezekani, kwanini?, sitaki kusikia tena hili linajirudia, muambizane na wanaopokea msafara huko tutakakopita"

"Acheni Wananchi wapite kwani dakika 10 hazitoshi), masaa manne kweli!? Nawaomba radhi ya dhati kabisa Wananchi"

======

Kauli ya Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango inafuatia Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani Jijini Mwanza kufunga Barabara kwa Saa 4 katika ziara yake na kusababisha foleni na adha kwa Watumiaji Barabara wengine.

Kitendo hicho kimefanya Dkt. Mpango kuwaomba radhi Wananchi huku akiwahoji Polisi kama Dakika 10 hazitoshi kupisha Misafara. Pia, amemwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) na Makamanda wa Polisi wa Mikoa yote kutorudia tena utaratibu huo.

Kumekuwa na Malalamiko ya Wananchi ya mara kwa mara kuhusu Misafara ya Viongozi kusababisha Foleni na usumbufu katika maeneo mbalimbali Nchini lakini bado suala hilo halijapatiwa ufumbuzi.

 
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mango akiwa ziarani Mwanza amesema hataki kusikia tena Barabara zikifungwa kwa masaa mengi ili apite, huku akisema dakika 10 zinatosha ili Wananchi waendelee na shughuli zao.

Dr. Mpango amewaomba radhi Wananchi kwa usumbufu walioupata baada ya jana Barabara kufungwa kwa saa nne ili veve apite "Nilishamwambia IGP na nirudie kuwaambia
Makamanda wa Polisi wa Mikoa, mambo ya kufunga barabara kwa masaa mengi kisa tu Mtoto wa masikini Philip Mpango anapita hapana"

"Jana naambiwa mmefunga Barabara mpaka masaa manne haiwezekani, kwanini?, sitaki kusikia tena hili linajirudia, muambizane na wanaopokea msafara huko tutakakopita"

"Acheni Wananchi wapite kwani dakika 10 hazitoshi), masaa manne kweli!?, nawaomba radhi ya dhati kabisa Wananchi"
Naunga mkono hoja
P
 

Kauli ya Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mpango inafuatia Polisi wa Kikosi cha Usalama Barabarani Jijini Mwanza kufunga Barabara kwa Saa 4 katika ziara yake na kusababisha foleni na adha kwa Watumiaji Barabara wengine

Kitendo hicho kimefanya Dkt. Mpango kuwaomba radhi Wananchi huku akiwahoji Polisi kama Dakika 10 hazitoshi kupisha Misafara. Pia, amemwagiza Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) na Makamanda wa Polisi wa Mikoa yote kutorudia tena utaratibu huo

Kumekuwa na Malalamiko ya Wananchi ya mara kwa mara kuhusu Misafara ya Viongozi kusababisha Foleni na usumbufu katika maeneo mbalimbali Nchini lakini bado suala hilo halijapatiwa ufumbuzi.
 
Hayo ni maneno, na ninani anatakiwa afungiwe barabara, katibu mkuu wa CCM, waziri mkuu, trafiki anayewahi kwenda kufunga barabara, mwenyekiti bodi ya trc au anayesindikiza mabehewa ya sgr yaliyochafuliwa na vumbi huko baharini? Inabidi waweke wazi wanaotakiwa barabara ifungwe na wasizidi watatu.
 
Makamu wa Rais, Dkt. Philip Mango akiwa ziarani Mwanza amesema hataki kusikia tena Barabara zikifungwa kwa masaa mengi ili apite, huku akisema dakika 10 zinatosha ili Wananchi waendelee na shughuli zao...
Ameongea jambo la maana sana Mheshimiwa, polisi na wana usalama wanakera sana katika hili. Msafara unaweza kupangiwa utaratibu mzuri na kwa muda mfupi pasipo kuathiri shughuli nyingine za kiuchumi na kijamii.

Ni jukumu la polisi na wana usalama kuratibu, kupanga na kuongoza misafara ya viongozi kwa umakini mkubwa, cha msingi tu ni kuepusha kuuingiza katika msongamano. Na kweli jambo hilo linaweza kufanyika kwa dakika kadhaa na siyo kwa masaa.
 
Back
Top Bottom