Hapa Korogwe Mkoani Tanga tuna changamoto ambayo naomba leo tuiweke wazi kwa sababu imetufika hapa (shingoni).
Naomba kuripoti kero juu ya misafara ya viongozi wanaopita hapa Korogwe Mjini yaani tunasimamishwa muda mrefu sana kisa msafara wa viongozi au kiongozi.
Mara nyingi tu shughuli zimekuwa zikisimama mpaka tunachelewa kazini na kwenye mambo mengine ya muhimu.
Nimeona msafara unavyokuwa kwa sehemu nyingine ni kweli huwa kuna mchakato wa kuwaweka watu pembeni ili viongozi wetu wapiti lakini lakini hapa Korogwe imezidi ndugu, askari wanasimamisha watu kwa muda mrefu zaidi ya saa kadhaa wakati unakuta kiongozi yuko mbali.
Hivi ni haki kweli shughuli za uchumi za Wananchi wote zisimame kwa zaidi ya saa kadhaa kisa tu kuna kiongozi anapita tena unakuta hana mpango wa kusimama, nashauri mamlaka ziangalie utaratibu mzuri wa kufanya.
Juzi kati nilimsikia Makamu wa Rais anasema hapendi kuona Wananchi wanasimamishwa muda mrefu ili yeye apite, nafikiri hilo lizingatiwe.
Naomba kuripoti kero juu ya misafara ya viongozi wanaopita hapa Korogwe Mjini yaani tunasimamishwa muda mrefu sana kisa msafara wa viongozi au kiongozi.
Mara nyingi tu shughuli zimekuwa zikisimama mpaka tunachelewa kazini na kwenye mambo mengine ya muhimu.
Nimeona msafara unavyokuwa kwa sehemu nyingine ni kweli huwa kuna mchakato wa kuwaweka watu pembeni ili viongozi wetu wapiti lakini lakini hapa Korogwe imezidi ndugu, askari wanasimamisha watu kwa muda mrefu zaidi ya saa kadhaa wakati unakuta kiongozi yuko mbali.
Hivi ni haki kweli shughuli za uchumi za Wananchi wote zisimame kwa zaidi ya saa kadhaa kisa tu kuna kiongozi anapita tena unakuta hana mpango wa kusimama, nashauri mamlaka ziangalie utaratibu mzuri wa kufanya.
Juzi kati nilimsikia Makamu wa Rais anasema hapendi kuona Wananchi wanasimamishwa muda mrefu ili yeye apite, nafikiri hilo lizingatiwe.