Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,386
swali limeulizwa na Albedo
Dr. Slaa
Nimekuwa ni mfatiliaji wa karibu wa Kikao cha Bunge kinachoendelea na namna Kinavyoendeshwa kwa Spika hasa Naibu Spika kuwa kandamiza sana Wapinzani na ( Hata jana kwenye Mdahalo ameonesha kwamba ana Chuki na CHADEMA). Hali hii Dr ikiachwa bila kukemea itapelekea Wabunge wa Upinzani kujiona ni Inferior ambacho naamini ndiyo hasa lengo la CCM ikiwatumia Spika na Naibu Spika.
Tumeona namna Naibu Spika anapovumila Uvunjifu wa kanuni hasa pale inapowahusu CCM na kuwa mkali pale inapowahusu Wapinzani.
Dr. Slaa wanannchi wanakerwa sana na hii Tabia ya Naibu spika ila wanakerwa zaidi na Ukimywa wa CDM katika kulikemea hili ikibidi kutumia Nguvu ya Uma kushinikiza Hatua zichukuliwe dhidi ya Viongozi hawa.
Nakumbuka Mheshiwa Shelukindo aliruhusiwa asome barua inayomhusu Jairo lakini Tundu Lisi alikatazwa na kuambia aandike Ushahidi
Nataka Kufahamu kama kama CDM kinayaona haya? na nini Msimamo wake/
Asante sana