Dr Willibrod Slaa
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 675
- 1,523
Zumbemkuu,
Wana JF awali nawasalimu. Ni muda kidogo sijapost kwenye jamvi japo nimekuwa nikichungulia ama kama member ama kama guest. Nimeona ombi na nimeielewa.
Pamoja na kuwa sina tatizo kutoa mchango wangu kama mkereketwa wa maendeleo ya Taifa letu, na kuchukizwa sana giza totoro linaloikimba nchi yetu, ni maoni yangu kuwa hoja nyingi zilizoko zinahitaji majibu ya Serikali na Chama Tawala. Kwa vile wako wa Chama tawala humu, ninashauri maswali hayo waelekezewe hao tuliowapa dhamana na wanakusanya kodi zetu.
Niko tayari kuchangia pale yatakapohitajika maoni yangu kuhusu jambo lolote lile kama maoni hayo yanaweza kusaidia tusonge mbele. Swala la Madiwani wa Arusha nimekuwa nikilitolea ufafanuzi wa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari. Kama kuna mtu anahitaji ufafanuzi wowote, nitakuwa tayari kuutoak, alimradi ni ndani ya uwezo na mamlaka yangu kwa mujibu wa Katiba ya Chadema.
Nawashukuru sana na ninawatakia mjadala mwema, nikitegemea wahusika wa chama tawala watajitokeza wazi pia. Taifa ni letu sote na litajengwa na wale tu wenye nia njema na Taifa hili.
Wana JF awali nawasalimu. Ni muda kidogo sijapost kwenye jamvi japo nimekuwa nikichungulia ama kama member ama kama guest. Nimeona ombi na nimeielewa.
Pamoja na kuwa sina tatizo kutoa mchango wangu kama mkereketwa wa maendeleo ya Taifa letu, na kuchukizwa sana giza totoro linaloikimba nchi yetu, ni maoni yangu kuwa hoja nyingi zilizoko zinahitaji majibu ya Serikali na Chama Tawala. Kwa vile wako wa Chama tawala humu, ninashauri maswali hayo waelekezewe hao tuliowapa dhamana na wanakusanya kodi zetu.
Niko tayari kuchangia pale yatakapohitajika maoni yangu kuhusu jambo lolote lile kama maoni hayo yanaweza kusaidia tusonge mbele. Swala la Madiwani wa Arusha nimekuwa nikilitolea ufafanuzi wa mara kwa mara kwenye vyombo vya habari. Kama kuna mtu anahitaji ufafanuzi wowote, nitakuwa tayari kuutoak, alimradi ni ndani ya uwezo na mamlaka yangu kwa mujibu wa Katiba ya Chadema.
Nawashukuru sana na ninawatakia mjadala mwema, nikitegemea wahusika wa chama tawala watajitokeza wazi pia. Taifa ni letu sote na litajengwa na wale tu wenye nia njema na Taifa hili.
tunaomba Dr.Slaa uje tena JF ajibu maswali ya moja kwa moja,yapo mengi ya kukuuliza hasa kipindi hiki mfano:-
- giza totoro na majibu mepesi ya rais na mawaziri,
- bahasha la jairo.
- kujivua gamba kwa RA.
- sakata la madiwani wa arusha.
- umaskini unaozidi kukua na gharama za maisha.