Maiti yasafirishwa kwa pikipiki Bukoba

Sizinga wewe na ----- hamtofautiani, sasa serikali itazika maiti ngapi???? basi serikali isiishie hapo ianze kuoa condoms bure, iwalipie watu kodi za nyumba, hela ya kula daily!!!! acha akili za ujima waambie hao wenzio mfanye kazi bure aghali

Kama ni kweli kwanza wafiwa poleni sana kwa msiba.

Pili narudi kwa mtoa mada, naomba nijue haya
1. hapo walikuwa hospitalini au nyumbani kwa marehem?
2.Huyo dereva ni askari au ni mwana chadema? nauliza hivi kwa sababu naona amevaa gwanda ambazo ni uniform za mgambo na chadema
3.katika mazingira ya kawaida hakuna msiba unaokosa presence ya wanawake hapo kwenye picha mbona kama ni isue ya watu wawili tu na watatu yuko anawashangaa kuonesha hayuko nao?
4. kama uwezo ulikuwa hauruhusu nini mantiki ya kusafirisha maiti? inamaana hapo alipofia ilikosekana sehemu ya kumzika?
Kwa nini maiti asafirishwe wakati ni Tanzania,na ardhi ipo ya kumzika.Huko anakokwenda kuzikwa si pia ni Tanzania.
 
mbona kama marehemu alikufa na mimba je hua hawafanyiwi opresheni kuondoa kiumbe aliepo tumboni au alifia njiani wakati akiwaishwa hospital
 
Kwa kweli imenichukua muda kuamini hili swala....lakini moja kwa moja naitupia serikali ambayo kwa namna moja au nyingine imesababisha hali hii....kwa mfano kama serikali ingeboresha huduma za afya vijijini pengine hiki kifo kingeepukika hiyo moja .....mbili maelezo yanasema kuwa kutokana na kupanda kwa ghalama za usafiri wanashindwa kumudu hizo gharama na hatimaye kufikia hatua hiyo......hapo serikali wangetakiwa waboreshe miundombinu hasa maeneo ya vijijini ili kupunguza gharama za usafirishaji na wangesimamia bei za mafuta ipasavyo kwa kuwa nayo kwa kiasi kikubwa inachangia kuongezeka kwa gharama za usafiri........na vile vile ndugu nzangu nshomile muache sifa huku mjini jengeni mkoa wenu.....huku mjini mnamwaga mahela baa na kwenye maharusi huku kwenu huko dada zenu wanajifungulia njiani..............
 
mbona kama marehemu alikufa na mimba je hua hawafanyiwi opresheni kuondoa kiumbe aliepo tumboni au alifia njiani wakati akiwaishwa hospital

Tanzania inaongoza kwa vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano hasa vijijini
 
Duh!
Nchi ya ajabu sana hii imejaa viongozi wapenda sifa wasiojali kabisa masuala muhimu ya kijamii. Maiti inakalishwa kwenye kiti kwa urahisi wa usafirishaji? Hili linawezekana Tanzania tu, nchi inayoongozwa na sharo presidar jk kutoka ccm! Maisha bora hayawezekani, tuache kudanganyana!

Jamani,kila kitu rais tu! hapo kuna ngazi ngapi za kulaumu mmezivuka? hebu tusiwe wavivu wa kufikiri.
 
Kwa kweli imenichukua muda kuamini hili swala....lakini moja kwa moja naitupia serikali ambayo kwa namna moja au nyingine imesababisha hali hii....kwa mfano kama serikali ingeboresha huduma za afya vijijini pengine hiki kifo kingeepukika hiyo moja .....mbili maelezo yanasema kuwa kutokana na kupanda kwa ghalama za usafiri wanashindwa kumudu hizo gharama na hatimaye kufikia hatua hiyo......hapo serikali wangetakiwa waboreshe miundombinu hasa maeneo ya vijijini ili kupunguza gharama za usafirishaji na wangesimamia bei za mafuta ipasavyo kwa kuwa nayo kwa kiasi kikubwa inachangia kuongezeka kwa gharama za usafiri........na vile vile ndugu nzangu nshomile muache sifa huku mjini jengeni mkoa wenu.....huku mjini mnamwaga mahela baa na kwenye maharusi huku kwenu huko dada zenu wanajifungulia njiani..............
1) serikali haina nia kabisa kuboresha sekta ya afya vijijini mkuu.....unawakumbuka wake madokta walikuwa wanatoa huduma usiku kwa wagonjwa kwa kutumia sim ya nokia tochi

2) dah naona unawachokoza watani wangu nshomilee ila watakuwa wamekuskia
 
inahuzunisha sana bado unamkuta mtu anaisifia serikali ya ccm kwa lipi
 
Inatia simanzi sana,CCM haiko tayari kutoka na wananchi hawako tayari kuitoa.hii nchi ni ovyo sana
 
Ni kwakuwa tuliamua kuchagua ujinga kwa ahadi za pilau wali kanga T-shirt na kofia za kijani na njano

Hakika na zile bajaj za wagonjwa zilizoletwa hadi kwenye maonesho viwanja vya bunge ziko wapi walau zingetusitiri katika hili la kubebea wafu na si wagonjwa!
 
Aisee aliyeweka uzi huu alituainlbisha sana watu wa Kagera. Naomba ufutwe

Kijana mwema/mzuri onesha hilo kwa kutoa suluhisho badala ya kukimbilia kuficha aibu mfano kwa kuonesha hivi inawezekana wakina lugemaria mujwauzi tibaijuka wakajua mahala sahihi fedha za umma zinapohitajika na sio kwenye matumbo yao!
 
Mbona maiti mwenyewe anaonekana kama anaongea na simu, hii picha ina mashaka kidogo. Lakini hata hivyo serikali ina majukumu mengi zaidi ya kusafirisha maiti, hata Yesu aliwaambia '' waacheni wafu wawazike wafu wenzao''.......MATHAYO 6:12

we jamaa umewaza mbali hahahahahahaha mi nacheka kwa huzuni
 
Back
Top Bottom