EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Juni mwaka jana, niliweka hapa jamvini habari na picha za kusikitisha kuhusu hali halisi ilivyo kwa baadhi ya sehemu za Tanzania ambapo kutokana na ukali wa maisha na kupanda kwa bei ya mufuta na vyombo vya usafiri, maiti hupakizwa juu ya pikipiki tayari kusafirishwa kwa ajili ya maziko. Hiyo ilikuwa katika kijiji kimoja mkoani Mbeya (https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/150148-maiti-yasafirishwa-na-pikipiki.html). Safari hii imetokea huko Bukoba ambapo maiti imebebwa kwa pikipiki tayari kusafirishwa kwa ajili ya maziko. Yafuatayo ni picha na maelezo kama yanavyopatikana kwenye blogu ya Bukoka (Bukoba).
Mwanzo kwa kunukuhu:
Kweli nimesikitika sana kuona hali ya kwetu Bukoba bado tuko nyuma mpaka maiti inabebwa kwa pikipiki yaani thamani ya utu inaishia hapo kweli nimesikitika sana. Sasa tufanyeje kwa walio mbali na Bukoba na walioko Bukoba wenyewe tunatakiwa kujikomboa kununua vifaa viwasaidie ndugu zetu walioko vijijini nakumbuka zamani kama unatoka Kyaka pale mlima katoma lazima ukutana na watu wamebeba maiti kwenye baiskeli wanapelekwa vijini kila mtu anaona sioni wakati wa sasa jamani.
Nakumbuka kuna kampuni moja iko Dar es Salaam wanazo Bajaji nzuri zinaweza kubeba maiti, wagonjwa, wamama wajawazito tukiamua tunaweza kufanya harambee kwa ajili ya watu wa Bukoba tukanunua hizo bajiji kama tano tukapeleka kwenye kata ili mwanakijiji anapopatwa na shida kama hii anakodi kijijini na inasaidia hata kwa maendeleo. Kuna kijiji kimoja mtwara wanakijiji baada ya kupata shida walichanga wanakijiji wakainunua kwa 10,000,000/= inawasaidia sana na kijiji ndo kilichagua mtu atakayeindesha na kuitengeneza yaani wako sembuse sisi watu kutoka BK tunashindwa nini? Mwisho wa kunukuhu.
Pikipiki ikiwa mwendo wa kasi inatoka Ndolage Hospitali kuelekea Ichwandimi kupitia Nyakigando maeneo ya Rubale.
Picha na maelezo zaidi: Bukoba: ASEMAVYO MDAU ELEWA SABUNI KUHUSU USAFIRI WA MAITI;Hii ni kutokana na habari tuliotoa kupitia wadau wiki iliopita.
Mwanzo kwa kunukuhu:
Kweli nimesikitika sana kuona hali ya kwetu Bukoba bado tuko nyuma mpaka maiti inabebwa kwa pikipiki yaani thamani ya utu inaishia hapo kweli nimesikitika sana. Sasa tufanyeje kwa walio mbali na Bukoba na walioko Bukoba wenyewe tunatakiwa kujikomboa kununua vifaa viwasaidie ndugu zetu walioko vijijini nakumbuka zamani kama unatoka Kyaka pale mlima katoma lazima ukutana na watu wamebeba maiti kwenye baiskeli wanapelekwa vijini kila mtu anaona sioni wakati wa sasa jamani.
Nakumbuka kuna kampuni moja iko Dar es Salaam wanazo Bajaji nzuri zinaweza kubeba maiti, wagonjwa, wamama wajawazito tukiamua tunaweza kufanya harambee kwa ajili ya watu wa Bukoba tukanunua hizo bajiji kama tano tukapeleka kwenye kata ili mwanakijiji anapopatwa na shida kama hii anakodi kijijini na inasaidia hata kwa maendeleo. Kuna kijiji kimoja mtwara wanakijiji baada ya kupata shida walichanga wanakijiji wakainunua kwa 10,000,000/= inawasaidia sana na kijiji ndo kilichagua mtu atakayeindesha na kuitengeneza yaani wako sembuse sisi watu kutoka BK tunashindwa nini? Mwisho wa kunukuhu.
Pikipiki ikiwa mwendo wa kasi inatoka Ndolage Hospitali kuelekea Ichwandimi kupitia Nyakigando maeneo ya Rubale.
Picha na maelezo zaidi: Bukoba: ASEMAVYO MDAU ELEWA SABUNI KUHUSU USAFIRI WA MAITI;Hii ni kutokana na habari tuliotoa kupitia wadau wiki iliopita.