Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,357
- 35,832
Linapokuja suala la mali au madaraka huenda kundi la wanawake ndio kinara wa kuvuna kirahisi sana, iwe kwa haki au kwa hila, wanawake ni wavunaji tu.
Wakati watawala wa CCM walipokuwa wanawapanga wanawake kwenye safu mbalimbali za uongozi kama alama ya ujanja ujanja ya kuwatumia ili kuimarisha mamlaka ya wanaume, sasa ngoma imegeuka vibaya, leo wanaume wa CCM wamebakia kulialia tu baada ya wanawake kuwafyatua vibaya, tena kwa aibu kubwa.
Ilianza kwa Magufuli, alipokufa tu, wanaume wa CCM wakajikuta wanatamani serikali ya mpito (ambayo haikuwa inakubalika kikatiba) ili Samia Suluhu asiwe rais! Lakini ngoma ikagonga mwamba.
Mikakati mbalimbali mizito ya wanawake ndani ya CCM ikapangwa kuhakikisha Ndugai inatoka kwenye kiti, pasipo kujua akaingia mkenge, akapigwa ngwala na kutupwa mbali, leo hii ni hadithi tu sasa mwanamke anayejulikana kama Tulia anakwenda kukalia kiti cha Spika.
Kwa kuwa madaraka huwa ni matamu, na wanawake wa CCM hawanaga mishipa ya aibu au kutosheka, kituo kinachofuata ni kuhakikisha wenyeviti wa kamati za kudumu za bunge wengi wanakuwa wanawake kama inavyoelekea sasa kwenye baraza la mawaziri.
Yote kwa yote, huenda kituo kinachofuata ni nafasi ya waziri mkuu, Majaliwa ajipange, wenye CCM yao (wanawake!?) wameshafika.
Wakati watawala wa CCM walipokuwa wanawapanga wanawake kwenye safu mbalimbali za uongozi kama alama ya ujanja ujanja ya kuwatumia ili kuimarisha mamlaka ya wanaume, sasa ngoma imegeuka vibaya, leo wanaume wa CCM wamebakia kulialia tu baada ya wanawake kuwafyatua vibaya, tena kwa aibu kubwa.
Ilianza kwa Magufuli, alipokufa tu, wanaume wa CCM wakajikuta wanatamani serikali ya mpito (ambayo haikuwa inakubalika kikatiba) ili Samia Suluhu asiwe rais! Lakini ngoma ikagonga mwamba.
Mikakati mbalimbali mizito ya wanawake ndani ya CCM ikapangwa kuhakikisha Ndugai inatoka kwenye kiti, pasipo kujua akaingia mkenge, akapigwa ngwala na kutupwa mbali, leo hii ni hadithi tu sasa mwanamke anayejulikana kama Tulia anakwenda kukalia kiti cha Spika.
Kwa kuwa madaraka huwa ni matamu, na wanawake wa CCM hawanaga mishipa ya aibu au kutosheka, kituo kinachofuata ni kuhakikisha wenyeviti wa kamati za kudumu za bunge wengi wanakuwa wanawake kama inavyoelekea sasa kwenye baraza la mawaziri.
Yote kwa yote, huenda kituo kinachofuata ni nafasi ya waziri mkuu, Majaliwa ajipange, wenye CCM yao (wanawake!?) wameshafika.