GY
JF-Expert Member
- Nov 2, 2009
- 1,279
- 126
unaelewa maana ya neno Disaster? mimi si mshabiki wa misaada ya kijinga. Lakini ni muamini wa utu wa mtu na kwamba utu wa mwanadamu haupunguki kwa sababu serikali yake ni ya kifisadi. Nikiona mtu ana njaa nitampa chakula kwanza kabla ya kumlaumu kwanini ana njaa! Nikimuona watu wameangukiwa na nyumba nitakimbia kuokoa kwanza kabla ya kuuliza kama walifuata kanuni za ujenzi bora!
Ninapoona mafuriko na majanga yanayokuna nayo nitakuwa mstari wa mbele kusaidia badala ya kuuliza "serikali iko wapi".
Utu wa mtu haupotei tu ikiwa kuna majanga. Utu wa mtu unapotea ikiwa kwa sababu yeyote ile atakosa mahitaji muhimu kwa maisha yake. Ni rahisi sana kuhalalisha matendo ikiwa kuna urgency/emergency na mfano mzuri ni majanga. Hapa kila mtu atataka kujifanya mwema. Lakini ninakwambia, wako watu wanaishi maisha yanayolingana hivi sasa na yale ya wakazi wa kilosa na maeneo mengine yaliyokumbwa na mafuriko kama ndio maisha yao ya kawaida. Hawana makazi, hawana chakula na hawana huduma za afya. Sisi wengine tumepata bahati ya kufanya shughuli zinazotupeleka kila siku kwa watu wa aina hiyo. Nobody think of them, kwanini, kwakuwa sio rahisi kuijustfy hiyo hali kama janga, lakini ni janga. Hawa hawawezi kusaidiwa na TPN, na Jamii forums, na Michuzi na red cross na red alert, wala hawawezi kusaidiwa na kina mkulo na lukuvi.
Je wanapaswa kusaidiwa na nani?