Mhabarishaji
JF-Expert Member
- Oct 5, 2010
- 1,006
- 598
Siku 28 kabla ya Watanzania kupiga kura ya kuchagua Rais, Wabunge na Madiwani, madhehebu kadhaa ya Kikristo nchini yameungana na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zachary Kakobe, kutofanya Ibada Jumapili ya Oktoba 31, badala yake Ibada zutafanyika Jumamosi Oktoba 30.
Akiongea na Jibu la Maisha, katika mahojiano maalumu kwa njia ya simu Jumatano, mchana, Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (PCT) David Mwasota, alisema kuwa wao walikwisha ijadili katika foramu ya Kikristo iliyofanyika Julai mwaka huu.
"Tumekubaliana na makanisa yote ya Kikristo pasipo kujali itikadi zetu za dini kuwa siku ya Jumamosi ndio itakuwa siku ya ibada badala ya Jumapili, ili watu wetu washiriki bila kipingamizi chochote katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumapili Oktoba 31 mwaka 2010", alisema Katibu Mkuu wa PCT, Askofu David Mwasota.
CHANZO: Gazeti Jibu la Maisha - Oktoba 3-9, 2010
Akiongea na Jibu la Maisha, katika mahojiano maalumu kwa njia ya simu Jumatano, mchana, Katibu Mkuu wa Baraza la Makanisa ya Kipentekoste Tanzania (PCT) David Mwasota, alisema kuwa wao walikwisha ijadili katika foramu ya Kikristo iliyofanyika Julai mwaka huu.
"Tumekubaliana na makanisa yote ya Kikristo pasipo kujali itikadi zetu za dini kuwa siku ya Jumamosi ndio itakuwa siku ya ibada badala ya Jumapili, ili watu wetu washiriki bila kipingamizi chochote katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumapili Oktoba 31 mwaka 2010", alisema Katibu Mkuu wa PCT, Askofu David Mwasota.
CHANZO: Gazeti Jibu la Maisha - Oktoba 3-9, 2010