Elections 2010 Madhehebu yaungana na Kakobe kusali Jumamosi: Ni PCT, TEC na CCT

kule kwa gwajima, siku ya jumamosi wanalala hapohapo wakikesha nakuombea taifa, siku ya jumapili wanaamkia kanisani asubuhi halafu wote kabla hawajaenda kulala kwasababu ya usingizi wa mkesha, wanapitia kupiga kura kwanza kabla ya yote. nilikuwepo pale jumapili hii iliyopita, na tulishatangaziwa kuwa hatutakuwa na ibada siku ya kupiga kura, badala yake jumamosi tutafanya ibada kama kawaida na jumapili tunaamkia kupiga kura hadi kieleweke. ngoma inogile kwa kweli..

majeshi, majeshi
 
Umejiunga leo! umekuja na post hii! umetumwa nini na kakobe..?!

Kujiunga leo wala siyo ISSUE ya maana, cha maana ujumbe alioleta kama una lipa au laa, hata wewe ulianza siku mmoja na ukaendelea kulizoea jukwaa. Usimkatishe tamaa kwa kuwa ni mgeni. Mhabarishaji karibu sana feel free!!!!! fuata sheria tu utatoa mawazo yako.
 
Vipi vatican wenyewe wanasemaje?

Nasikia mchungaji Gwajima naye katangazia washirika wake kuwa ibada ya 31 Oct itafanyika jmosi. Naona CCM wameshikwa pabaya. Walidhani uchaguzi ukiwa jumapili basi wakristo wengi (hasa wa mijini) watashindwa kupiga kura?

Wakuu hamkusoma kwenye thread hii kwamba Papa Pius XII aliruhusu tangu mwaka 1953 kuwa misa za Jumapili zianze saa 10:00 jioni Jumamosi. Hii ni kwa sababu Katekism kifungu 2180 inaruhusu misa za Jumapili kuanza Jumamosi jioni. Mimi naamini Kanisa Katoliki litaitumia ile Jumamosi jioni kabla ya uchaguzi kama misa ya kwanza na asubuhi watu wakaamkia uchaguzini.

Soma hii link tulivyoletewa hii concept:

https://www.jamiiforums.com/uchaguzi-tanzania-2010/74330-kuna-tatizo-gani-uchaguzi-usifanyike-jumapili.html
 
Back
Top Bottom