Madhara ya Nape kushindana na TEC yameanza kuonekana

Ni jana tu nimetoka kukuasa kuhusu kupambana na TEC kwa kutumia wadhifa wako wa u-waziri wa habari nchini.

Ukaenda kupiga marufuku ukiwazuia wahariri wa vyombo vya habari ili kutorusha maudhui au kuchapisha maandiko yoyote yanayohusu Waraka wa maaskofu wa "TEC". Kuhusiana na DP-WORLD kuhusu Bandari zetu nchini.

Leo hii inakuja habari ya wewe kukataliwa na machifu na wazee wa kikabila huko Chiponda -Londo.

Kwamba huna asili ya huko bali wewe ni Mnyiramba toka Singida na umekulia Misungwi-Mwanza.

Asiyesikia la mkuu.....
Huu ni mwanzo na ni mfano hai.mengi yatafuata kwa wenzio na kwa njia tofauti.

Pia soma..
Tetesi: - Kimenuka Mtama: Nape akatisha shughuli za Serikali na kuitisha mkutano wa hadhara

Pia ieleweke hivi:


Asili ya mama mzazi wa Nape ni mkoa wa Singida, yeye ni Mnyiramba.
Baba mzazi wa Nape ni Moses Nnauye (marehemu) ambaye alistaafu utumishi wa umma akiwa Brigedia Jenerali wa Jeshi. Asili ya baba yake Nape ni mkoa wa Lindi, yeye ni Mmakonde wa Chiuta, Nyangamara. Mzee Nnauye ni mmoja kati ya wanasiasa mashuhuri wa kizazi kinachoondoka, kazi yake ya kwanza ilikuwa ni “ukuli” wa bandari ya Lindi na Mtwara. Baadaye alisoma kidogo na kushiriki kwenye harakati za kudai uhuru akiwa kijana mdogo na baada ya Uhuru alikuwa kiongozi wa Umoja wa Vijana wa Tanu.
Akiimbisha kwaya za Tanu Youth League, piga mkolonii eh aende zake,TANU yajenga nchii, ehe TANU yajenga nchiiii
 
Mara KKKT mara Nape ..
Watu wanazubaishwa ajenda ya Bandari hata hawaelewi skendo skendo zitazuka nyingiiii ..
 
Mara KKKT mara Nape ..
Watu wanazubaishwa ajenda ya Bandari hata hawaelewi skendo skendo zitazuka nyingiiii ..
Wewe ndie utachanganyikiwa!
Ila sisi tunatembea kwenye mataruma ya Reli husika.
Ni muendelezo wa yaletale ya TEC na bandari zetu.
Ila wewe sio msomaji muelewa.
 
Kwa nini nape asili ni singida wakati baba yake ni wa Lindi?
Kwani Kitila Mkumbo, Askofu Gwajima, John Mnyika, Halima Mdee, Rita Mlaki, marehemu Masumbuko Lamwai orodha ndefu, walipewa ridhaa kuwa wabunge kati ya majimbo ya Dar ni Wazaramo wa wapi vile!
 
Kwani Kitila Mkumbo, Askofu Gwajima, John Mnyika, Halima Mdee, Rita Mlaki, marehemu Masumbuko Lamwai orodha ndefu, walipewa ridhaa kuwa wabunge kati ya majimbo ya Dar ni Wazaramo wa wapi vile!
Tayari umesema walipewa ridhaa.
Sasa Nape yeye anenyimwa ridhaa hiyo na jopo la wazee wa kimila.
Na badala yake wamemteua Stephen Membe kuwa chifu wao,lakini pia wakimtaka huuo huyo kuwa mgombea wa ubumge jimbo la mtama itakapofika 2025!

Soma hiyoooo!
 
Amezaliwa Singida na kukulia Singida na akasoma huko primary kisha akaenda Misungwi Mwanza na kusoma pale Bukumbi na hajawahi kukulia Lindi bali kaenda huko akiwa mbaba na mzee wake akiwa kisha fariki.
Tupo sawa mpaka hapo?
Nape kazaliwa na kukulia wilaya ya Kwimba, sekondari amesoma Nsumba iko nyegezi - Mwanza
 
Nimekuelewa mkuu ila ni wazi Hata huku JF kuna tatizo kubwa!
Leo pekee zimefutwa nyuzi zangu zaidi ya Tatu.
Na sio tu kufuta, hawa moderator pia wana kamchezo wa change title Na kuongezea maudhui. Wakati mwingine wanakulisha maneno kutokana Na heading waliyo ifanyanyia editing bila consent ya mtoa Mada. Ni hatari sana Kwa kweli- kisheria
 
Maaskofu wanajua kila kitu! Nape anajua vizuri, anafahamu matokeo yake kisiasa ila kiroho hajui sawasawa.
 
Wenyeji wa huko Lindi na Mtwara watathibitisha. Wamakonde wanathamini sana nasaba ya ukoo kutoka kwa mama zaidi kuliko kwa baba.

Nakumbuka hata marehemu Bernard Membe katika simulizi zake aliwahi kusema kuwa hata hilo jina la MEMBE lilitokana na ukoo wa mama yake na wala siyo baba yake.
Wamakonde ukoo uko kwa baba na sio kwa mama. Wamwera ukoo uko kwa mama. Membe ni mmwera na sio Mmakonde. Nape ni Mmakonde wa Mtwara na sio Lindi. Wamakonde wanapatikana Both Mtwara and Lindi. Mtwara wamakonde wanapatikana zaidi wilaya 3, Mtwara, Tandahimba na Newala na Lindi wamakonde wanapatikana zaidi wilaya ya Lindi (Mjini + Vijijini). Mtama iko Lindi vijijini na Majority ni wamakonde, na hii ni kwakuwa imepakana zaidi ni Mtwara.
 
Back
Top Bottom