MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Rais kwanza nikupe pole na heshima yako na nikupongeze sana Mama kwa uwajibikaji wako katika kulisaidia Taifa hili kwa kuliponya kutoka katika mazingira magumu miaka 8 iliyopita. Hakika tunaweza kusema ya kwamba mabadiliko ni makubwa sana katika sekta zote ispokua baadhi ya Watendaji wako ndio wanaokuharibia na kuendelea kukuchelewesha kufika kule mbali unakotazama.
Bila hiyana wala unafki kwakweli kongole Mama!👏👏
Rais tunafahamu kwamba falsafa yako kubwa katika utendaji ni kuwaacha watendaji wako wafanye kazi wenyewe kwa kujisimamia bila pressure yeyote ya mamlaka tena kwa ubinifu mkubwa. Hii ndio misingi ya kweli ya kiutawala.
KWANINI WAZIRI UMMY ABADILISHWE?
Rais, nikiwa kama Mtanzania Mzalendo,Mdau katika masuala ya Afya na kada/kiongozi mtiifu katika chama cha Mapinduzi, sipendi tuharibikiwe nitaelezea mambo kadhaa muhimu ambayo pengine Mhe Waziri hakuambii ukweli au watendaji walio chini yake hawamwambii ukweli kwa vile yeye siyo mwanataaluma katika sekta ya Afya.
KUSHINDWA KUSIMAMIA NA KUTATUA KERO NA MALALAMIKO YA MADAKTARI TARAJALI(INTERNS) KUTOTENDEWA HAKI NA BARAZA LA MADAKTARI TANGANYIKA(MCT).
Rais wangu, ikumbukwe kua Madaktari tarajali waliwahi kukuandikia Barua ya wazi kwamba hawatendewi haki na Baraza la Madaktari Tanganyika(MCT) wakilalamikia mambo kadha wakadha ambayo nitayabainisha hapa.Lakini baada ya Barua hiyo Mhe Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alimtuma Naibu waziri wake Dr Godwin Moleli ambaye alikutana na Watarajali hao na kisha kueleza kero na changamoto zao. Baadaye Mhe Waziri Ummy Mwalimu alitoa taarifa kuunda tume ya kiuchunguzi kushughulikia changamoto hizo, lakini cha ajabu mpaka sasa hakuna mrejesho na walalamikiwa wanaendelea na kile kile kinacholalamikiwa.
Rais, katika mambo yanayolalamikiwa na watarajali hawa ni kama ifuatavyo;
(i)Kunzishwa kwa mitihani ya Pre-intetnships ambayo haieleweki msingi wake ingawa baraza lilidai kuwapima watarajali hao kutokana na kutilia shaka vyuo vikuu waliotoka. Lakini swali la kujiuliza ni kwamba, TCU kikiwa kama chombo cha kupima ubora wa vyuo vikuu kina kazi gani? Huyu Mwanafunzi aliyesoma miaka yote 5 chuoni kisha akafuzu mafunzo yote ya nadharia na vitendo hospitalini miaka yote anapimwa kitu gani hasa? Unampimaje kwa maswali 150 ya nadharia ya kuchagua masaa peke yake masaa 3 ambapo kwa vitendo hujui ataenda kufanya kitu gani?
Mhe Rais, Kazi ya baraza ni kupima ubora wa mwanafunzi kabla ya kuanza mafunzo au mpaka amalize mafunzo ya hospitalini kwanza?
Ni taifa gani wana mfuno huu wa Pre and post Internship ikiwa hata mwongozo wa WHO hausemi hivyo?
Kwanini tusihisi kwamba hii ni janja janja ya kujikusanyia pesa wanazolipa watarajali hawa kabla ya kujisajili kufanya mitihani hiyo bila sababu za msingi?
Kusu hili Mhe Waziri hajui kabisa chochote Mhe Rais.
(ii)Watarajali kupewa mitihani ambayo haikutathminiwa wala kufanyiwa utafiti matokeo yake hali hii ilipelekea zaidi ya nusu kufanya vibaya kwenye mitihani hii.
Kulikua na kigezo cha mtarajali kwenda kufanya mafunzo mpaka afaulu mtihani huo kwanza, lakini mhe Waziri alipoona kuna malalamiko makubwa na hali ni mbaya sana mahospitalini hakuna madaktari wa kutosha ampapo kimsingi hawa watarajali ndio nguvu kazi kubwa kwenye mahospitali yote nchini, akaondoa zuio hilo la kwenda mafunzoni hadi mtarajali afaulu mtihani huo, ikawa sasa wafaulu wasifaulu wataenda mafunzoni tu na mtihani lazima ufanyike. Mtu unajiuliza, ni ipi sababu ya kuwapima kabla ya ilikua ikiwa wote wanaofeli na wanaofaulu wanaenda mafunzoni? Mantiki ya kipimo hapa ni ipi? Kwanini tusichukulie kua mitihani hiyo ninkitega uchumi tu cha baraza?
Kwenye hili Mhe Waziri Ummy alisema aneunda tume ya kuchunguza Malalamiko ya Watarajali hao na kutoa majibu ndani ya muda mfupi, lakini Mhe Rais Mpaka naandika hivi sasa ni zaidi ya Mwezi mmoja tume hiyo haijatoa mrejesho wala taarifa yeyote na Mhe Waziri yupo kimya.
Mhe Rais, Mpaka sasa Baraza hili ambalo linalalamikiwa na limeundiwa tume kuchunguzwa linaandaa mitihani mingine ya Preinternship, Watarajali hawa wanajiuliza, kuna usalama na uhalali kiasi gani kwenye mitihani hiyo?
Ni sahihi Baraza kuendelea na uandaaji wa mitihani wakati wanachunguzwa?
(iii)Kwanini ni taaluma ya Udaktari kuna mitihani miwili ya Pre and Post internships tofauti na taaluma ziingine ambazo watarajali huenda kufanya mafunzo ya vitendo kwanza chini ya Wasimamizi ambao ni wanataaluma waandamizi kisha baadaye mitihani ya kumaliza hufuata na kupatiwa leseni zao?
Kama hoja ilikua ni kutilia shaka uwezo wa vyuo vikuu kuandaa wataalam, kada zingine wamesomea vyuo gani? Kwanini baraza la madaktari Tanganyika wanafanya kitu ambacho yumkini hata wao hawajui maana yake?
(iv)Kuhusu watarataji waliofeli mitihani yao ambao kwa rekodi ya mtihani uliopita nibzaidi ya nusu ya waliofanya watahiniwa, wao kuendelea kukaa mtaani huku hawana leseni hadi mwaka mzima wakisubiri hadi wengine wamalize ndio waje wafanye mitihani pamoja, tunajiuliza huu ni utaratibu wa wapi kwa vijana hawa ambao tayari wana mikopo ya HESLEB ina mkataba baada ya muda flani kutakiwa kurejesha pesa walizokopa? kama wataendele kukaa mtaani maana yake hawana leseni hawawezi kufanya yeyote ile, siyo hasara kwa serikali iliyowakopesha?
USHAURI KWAKO MHE RAIS
Ikiwa vijana hawa waliandika barua ya wazi kwako Mhe Rais, Mhe Waziri akawahadaa kwa nia ya kuwapooza kwa kuunda tume ambayo mpaka sasa haijatoa mrejesho wala ripoti yeyote huku walalamikiwa wakiendelea na yale ambayo yalilalamikiwa.Kabla vijana hawa hawajakuangukia kwa njia ambayo pengine leo watahitaji tena kukutana nawe ana kwa ana, Mhe Rais wangu chukua hatua ya kumbadilisha Mhe Waziri kwenda wizara nyingine au uamuzi wowote utakaoona unafaa kwa mamlaka yako.
Hii inatafsiriwa ya kwamba amepuuza malalamiko ya wataalam hawa ambao taifa hili linawahitaji kwa kiasi kikubwa maana wamesomeshwa kwa gharama kubwa sana.
Mbona Wizara ya katiba na sheria walichukua hatua haraka baada ya Shule ya sheria(School of law) kulalamikiwa kutotenda haki kwa watahiniwa wa kada hiyo? Wizara ya Afya kuna nini?
Yangu ni hayo Mhe Rais.
Kazi endelee kwa jina la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Bila hiyana wala unafki kwakweli kongole Mama!👏👏
Rais tunafahamu kwamba falsafa yako kubwa katika utendaji ni kuwaacha watendaji wako wafanye kazi wenyewe kwa kujisimamia bila pressure yeyote ya mamlaka tena kwa ubinifu mkubwa. Hii ndio misingi ya kweli ya kiutawala.
KWANINI WAZIRI UMMY ABADILISHWE?
Rais, nikiwa kama Mtanzania Mzalendo,Mdau katika masuala ya Afya na kada/kiongozi mtiifu katika chama cha Mapinduzi, sipendi tuharibikiwe nitaelezea mambo kadhaa muhimu ambayo pengine Mhe Waziri hakuambii ukweli au watendaji walio chini yake hawamwambii ukweli kwa vile yeye siyo mwanataaluma katika sekta ya Afya.
KUSHINDWA KUSIMAMIA NA KUTATUA KERO NA MALALAMIKO YA MADAKTARI TARAJALI(INTERNS) KUTOTENDEWA HAKI NA BARAZA LA MADAKTARI TANGANYIKA(MCT).
Rais wangu, ikumbukwe kua Madaktari tarajali waliwahi kukuandikia Barua ya wazi kwamba hawatendewi haki na Baraza la Madaktari Tanganyika(MCT) wakilalamikia mambo kadha wakadha ambayo nitayabainisha hapa.Lakini baada ya Barua hiyo Mhe Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alimtuma Naibu waziri wake Dr Godwin Moleli ambaye alikutana na Watarajali hao na kisha kueleza kero na changamoto zao. Baadaye Mhe Waziri Ummy Mwalimu alitoa taarifa kuunda tume ya kiuchunguzi kushughulikia changamoto hizo, lakini cha ajabu mpaka sasa hakuna mrejesho na walalamikiwa wanaendelea na kile kile kinacholalamikiwa.
Rais, katika mambo yanayolalamikiwa na watarajali hawa ni kama ifuatavyo;
(i)Kunzishwa kwa mitihani ya Pre-intetnships ambayo haieleweki msingi wake ingawa baraza lilidai kuwapima watarajali hao kutokana na kutilia shaka vyuo vikuu waliotoka. Lakini swali la kujiuliza ni kwamba, TCU kikiwa kama chombo cha kupima ubora wa vyuo vikuu kina kazi gani? Huyu Mwanafunzi aliyesoma miaka yote 5 chuoni kisha akafuzu mafunzo yote ya nadharia na vitendo hospitalini miaka yote anapimwa kitu gani hasa? Unampimaje kwa maswali 150 ya nadharia ya kuchagua masaa peke yake masaa 3 ambapo kwa vitendo hujui ataenda kufanya kitu gani?
Mhe Rais, Kazi ya baraza ni kupima ubora wa mwanafunzi kabla ya kuanza mafunzo au mpaka amalize mafunzo ya hospitalini kwanza?
Ni taifa gani wana mfuno huu wa Pre and post Internship ikiwa hata mwongozo wa WHO hausemi hivyo?
Kwanini tusihisi kwamba hii ni janja janja ya kujikusanyia pesa wanazolipa watarajali hawa kabla ya kujisajili kufanya mitihani hiyo bila sababu za msingi?
Kusu hili Mhe Waziri hajui kabisa chochote Mhe Rais.
(ii)Watarajali kupewa mitihani ambayo haikutathminiwa wala kufanyiwa utafiti matokeo yake hali hii ilipelekea zaidi ya nusu kufanya vibaya kwenye mitihani hii.
Kulikua na kigezo cha mtarajali kwenda kufanya mafunzo mpaka afaulu mtihani huo kwanza, lakini mhe Waziri alipoona kuna malalamiko makubwa na hali ni mbaya sana mahospitalini hakuna madaktari wa kutosha ampapo kimsingi hawa watarajali ndio nguvu kazi kubwa kwenye mahospitali yote nchini, akaondoa zuio hilo la kwenda mafunzoni hadi mtarajali afaulu mtihani huo, ikawa sasa wafaulu wasifaulu wataenda mafunzoni tu na mtihani lazima ufanyike. Mtu unajiuliza, ni ipi sababu ya kuwapima kabla ya ilikua ikiwa wote wanaofeli na wanaofaulu wanaenda mafunzoni? Mantiki ya kipimo hapa ni ipi? Kwanini tusichukulie kua mitihani hiyo ninkitega uchumi tu cha baraza?
Kwenye hili Mhe Waziri Ummy alisema aneunda tume ya kuchunguza Malalamiko ya Watarajali hao na kutoa majibu ndani ya muda mfupi, lakini Mhe Rais Mpaka naandika hivi sasa ni zaidi ya Mwezi mmoja tume hiyo haijatoa mrejesho wala taarifa yeyote na Mhe Waziri yupo kimya.
Mhe Rais, Mpaka sasa Baraza hili ambalo linalalamikiwa na limeundiwa tume kuchunguzwa linaandaa mitihani mingine ya Preinternship, Watarajali hawa wanajiuliza, kuna usalama na uhalali kiasi gani kwenye mitihani hiyo?
Ni sahihi Baraza kuendelea na uandaaji wa mitihani wakati wanachunguzwa?
(iii)Kwanini ni taaluma ya Udaktari kuna mitihani miwili ya Pre and Post internships tofauti na taaluma ziingine ambazo watarajali huenda kufanya mafunzo ya vitendo kwanza chini ya Wasimamizi ambao ni wanataaluma waandamizi kisha baadaye mitihani ya kumaliza hufuata na kupatiwa leseni zao?
Kama hoja ilikua ni kutilia shaka uwezo wa vyuo vikuu kuandaa wataalam, kada zingine wamesomea vyuo gani? Kwanini baraza la madaktari Tanganyika wanafanya kitu ambacho yumkini hata wao hawajui maana yake?
(iv)Kuhusu watarataji waliofeli mitihani yao ambao kwa rekodi ya mtihani uliopita nibzaidi ya nusu ya waliofanya watahiniwa, wao kuendelea kukaa mtaani huku hawana leseni hadi mwaka mzima wakisubiri hadi wengine wamalize ndio waje wafanye mitihani pamoja, tunajiuliza huu ni utaratibu wa wapi kwa vijana hawa ambao tayari wana mikopo ya HESLEB ina mkataba baada ya muda flani kutakiwa kurejesha pesa walizokopa? kama wataendele kukaa mtaani maana yake hawana leseni hawawezi kufanya yeyote ile, siyo hasara kwa serikali iliyowakopesha?
USHAURI KWAKO MHE RAIS
Ikiwa vijana hawa waliandika barua ya wazi kwako Mhe Rais, Mhe Waziri akawahadaa kwa nia ya kuwapooza kwa kuunda tume ambayo mpaka sasa haijatoa mrejesho wala ripoti yeyote huku walalamikiwa wakiendelea na yale ambayo yalilalamikiwa.Kabla vijana hawa hawajakuangukia kwa njia ambayo pengine leo watahitaji tena kukutana nawe ana kwa ana, Mhe Rais wangu chukua hatua ya kumbadilisha Mhe Waziri kwenda wizara nyingine au uamuzi wowote utakaoona unafaa kwa mamlaka yako.
Hii inatafsiriwa ya kwamba amepuuza malalamiko ya wataalam hawa ambao taifa hili linawahitaji kwa kiasi kikubwa maana wamesomeshwa kwa gharama kubwa sana.
Mbona Wizara ya katiba na sheria walichukua hatua haraka baada ya Shule ya sheria(School of law) kulalamikiwa kutotenda haki kwa watahiniwa wa kada hiyo? Wizara ya Afya kuna nini?
Yangu ni hayo Mhe Rais.
Kazi endelee kwa jina la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.