Baraza Madaktari Tanzania (MCT) lamgomea Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kuhusu Madaktari Watarajali

Fundi Madirisha

Senior Member
Jun 30, 2020
184
987
Katika hali isiyokuwa ya kawaida Baraza la Madaktari Tanzania (MCT) ambalo kimsingi ndilo lenye mamlaka ya kisheria katika kusimamia taaluma ya Utabibu nchini linalalamikiwa na Wanataaluma wa tiba hasa madaktari tarajali kwa kukiuka makubaliono yaliyotokana na majadiliano ya kikao kati ya wataalam hao tarajali pamoja na Naibu waziri wa Afya Dr Godwin Moleli akimwakilisha Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu aliyefunga mjadala kwa kuunda tume ya kiuchunguzi juu ya malalamiko yao.

Wanauliza ni kwanini MCT wametangaza tarehe ya kufanya mtihani wa Pre-Internships mwaka huu wakati kamati ya Mhe Waziri bado haijatoa ripoti yake? Mwenye uhakika na usalama wa huo mtihani ni nani haliyakua watuhumiwa wanachunguzwa? Siyo ukaidi ni nini?

Ni takribani zaidi ya Mwezi mmoja kupita baada ya Mhe Waziri kutoa taarifa kuundwa kwa tume ya kitaalam itakayochunguza ni kwanini Wataalam hao wamekua wakifeli mitihani zaidi ya nusu ya watahiniwa wote? Hata kabla Kamati au Tume ya Mhe Waziri haijatoa Ripoti yake imekuaje MCT wanatangaza mtihani? Yaani wanachunguzwa halafu wanaendelea kufanya kile kile nicholalamikiwa, hii ni sawa?

OMBI/USHAURI KWA MHE WAZIRI
MCT wasitishe kwanza kusajili watahiniwa kwa ajili ya mtihani ambao watungaji wake wametiliwa mashaka.

Kitu kiingine ni kwamba. Hakuna mantiki au hoja yenye mashiko kwenye kufanya mtihani wa Preinternship wakati kuna mtihani wa Postinternship, kwenye preinternship wanapima kitu gani hasa wakati wanafunzi hawa wamekaa darasani miaka 5 na wakafaulu katika vyuo walikotoka? Kama vyuo vingekuwa na walakini TCU wana kazi gani?

Mhe Waziri ulisema kwamba watakaofanya mitihani ya Preintetnships wataendelea na kazi mahospitalini haijalishi wamefeli au wamefaulu, hii maana yake nini? Nini mantiki,tija na umuhimu wa Preinternship zaidi ya siasa na kikundi cha watu wachache kujitengenezea posho kutoka pesa za umma ambazo zingefanya mambo mengine?

Hivyo basi, Mhe Waziri kwa niaba ya Watoa elimu ya utabibu nchini nikiwa kama mwalimu wa vijana hawa, sioni kama Baraza likiwatendea haki, tutapoteza wataalam wengi bila sababu za msingi. Tuige mifano toka kwenye mataifa ya wenzetu.

MCT wasitishe mara moja usajili wa watahiniwa wa mtihani wa preinternship mpaka tume yako itakapokuja na majibu Mhe Waziri.

KAZI IENDELEE!

===================================

Mitihani.JPG


PIA SOMA:

UPDATE: Wizara ya Afya yaunda Kamati kuchunguza Malalamiko ya Madaktari Watarajali

Madaktari watarajali wamekuwa ombaomba Mtaani kisa leseni, wamuangukia Waziri Ummy Mwalimu na Rais Samia

Sina imani na Kamati Huru iliyoundwa na Ummy Mwalimu kufuatilia sakata la Madaktari Watarajali
 
Baraza la madaktari wapo sahihi, kwanza ni chimbo huru hakiendeshwi kisiasa. Pili madaktari wengi wanaozalishwa uwezo wao ni mdogo lazima Baraza lichukue hatua kulinda taaluma yao.
Lakini twende mbele turudi nyuma, kama watunga mitihani wameundiwa tume, kuna haja gani ya kuendelea kufanya kinschilalamikiwa na kinachunguzwa?
 
Ni vizuri mambo ya kitaalamu yabaki kwa wataalamu...sio busara kuwaleta wanasiasa waamue mambo ya kitaalamu....
Hao wataalam wanasimamiwa na nani maana hata sheria wanayoitumia kutunga hiyo mitihani yao imetungwa na wanasiasa. Wakilalamikiwa watawajibishwa na wasiasa.
 
BARAZA MADAKTARI TANZANIA(MCT) LAMGOMEA WAZIRI WA AFYA UMMY MWALIMU.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida Baraza la Madaktari Tanzania(MCT) ambalo kimsingi ndilo lenye mamlaka ya kisheria katika kusimamia taaluma ya Utabibu nchini linalalamikiwa na Wanataaluma wa tiba hasa madaktari tarajali kwa kukiuka makubaliono yaliyotokana na majadiliano ya kikao kati ya wataalam hao tarajali pamoja na Naibu waziri wa Afya Dr Godwin Moleli akimwakilisha Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu aliyefunga mjadala kwa kuunda tume ya kiuchunguzi juu ya malalamiko yao.

Wanauliza ni kwanini MCT wametangaza tarehe ya kufanya mtihani wa Pre-Internships mwaka huu wakati kamati ya Mhe Waziri bado haijatoa ripoti yake? Mwenye uhakika na usalama wa huo mtihani ni nani haliyakua watuhumiwa wanachunguzwa? Siyo ukaidi ni nini?

Ni takribani zaidi ya Mwezi mmoja kupita baada ya Mhe Waziri kutoa taarifa kuundwa kwa tume ya kitaalam itakayochunguza ni kwanini Wataalam hao wamekua wakifeli mitihani zaidi ya nusu ya watahiniwa wote? Hata kabla Kamati au Tume ya Mhe Waziri haijatoa Ripoti yake imekuaje MCT wanatangaza mtihani? Yaani wanachunguzwa halafu wanaendelea kufanya kile kile nicholalamikiwa, hii ni sawa?

OMBI/USHAURI KWA MHE WAZIRI.
MCT wasitishe kwanza kusajili watahiniwa kwa ajili ya mtihani ambao watungaji wake wametiliwa mashaka.
Kitu kiingine ni kwamba. Hakuna mantiki au hoja yenye mashiko kwenye kufanya mtihani wa Preinternship wakati kuna mtihani wa Postinternship, kwenye preinternship wanapima kitu gani hasa wakati wanafunzi hawa wamekaa darasani miaka 5 na wakafaulu katika vyuo walikotoka? Kama vyuo vingekuwa na walakini TCU wana kazi gani?

Mhe Waziri ulisema kwamba watakaofanya mitihani ya Preintetnships wataendelea na kazi mahospitalini haijalishi wamefeli au wamefaulu, hii maana yake nini? Nini mantiki,tija na umuhimu wa Preinternship zaidi ya siasa na kikundi cha watu wachache kujitengenezea posho kutoka pesa za umma ambazo zingefanya mambo mengine?

Hivyo basi, Mhe Waziri kwa niaba ya Watoa elimu ya utabibu nchini nikiwa kama mwalimu wa vijana hawa, sioni kama Baraza likiwatendea haki, tutapoteza wataalam wengi bila sababu za msingi. Tuige mifano toka kwenye mataifa ya wenzetu.

MCT wasitishe mara moja usajili wa watahiniwa wa mtihani wa preinternship mpaka tume yako itakapokuja na majibu Mhe Waziri.

KAZI IENDELEE!
Huu ni ukaidi wa hali ya juu sana, mhe.waziri hawa watu wachukulie hatua kali, unayo mamlaka ya kuifumua MCT. Kwanza imekuwa janga kubwa kwa madaktari. Nilikutana na daktari mmoja akanieleza hata walio makazini ni shida tu, hivi inakuwaje leseni ya udaktari alinew kila mwaka tena 150k utadhani anakata leseni ya biashara, Mhe.Ummy wasaidie hawa watu wanafanya kazi katika mazingira magumu sana.
 
Ninyi wana jf, msichojua ni kwamba hao MCT wasipokaza ili vijana waive, basi tegemeeni kutibiwa hovyohovyo siku za mbeleni, na msije mkamlalamika huku mitandaoni...

Shida kubwa inaanzia kwenye ufundishaji huko vyuoni, elimu ya huko imechekechwa kiasi kwamba vijana wakipewa mitihani ya critical thinking wanaangukia pua.

Hebu tuacheni kuleta siasa kwenye mambo serious.

Kinachotokea kwa madaktari, kinatokea pia kwa nurses,pharmacysts plus wale wazee wa law school... Wote hao kabla ya kusajiliwa lazima wafanye mitihani na wengi wao huwa wanafeli..
 
Ninyi wana jf, msichojua ni kwamba hao MCT wasipokaza ili vijana waive, basi tegemeeni kutibiwa hovyohovyo siku za mbeleni, na msije mkamlalamika huku mitandaoni...

Shida kubwa inaanzia kwenye ufundishaji huko vyuoni, elimu ya huko imechekechwa kiasi kwamba vijana wakipewa mitihani ya critical thinking wanaangukia pua.

Hebu tuacheni kuleta siasa kwenye mambo serious.

Kinachotokea kwa madaktari, kinatokea pia kwa nurses,pharmacysts plus wale wazee wa law school... Wote hao kabla ya kusajiliwa lazima wafanye mitihani na wengi wao huwa wanafeli..
Hoja ya Kijinga kabisa hii, kwani TCU wana kazi gani ambao ndio wasomamizi wa kozi na vyuo husika?
 
MCT kimekua ni kikundi cha wanasisa wachache kukusanya pesa za Madaktari wanajilia. Tuhuma za rushwa kibao
 
Ifike mahali mnzava atumbuliwe tu hiyo kazi anaifanya kimaslahi binafsi sana kama sio upigaji ni nini sasa hii tutamlaumu sana mama lakini wanaoharibia ni vikundi tu vya watu wachache kama hao MCT,waziri tumbumbua hicho kikundi maana hakijui kazi yao ni nini na nini wanatakiwa kufanya,hao hawana tofauti na wezi
 
Hoja ya Kijinga kabisa hii, kwani TCU wana kazi gani ambao ndio wasomamizi wa kozi na vyuo husika?
Wewe ndo una hoja za kijinga...

TCU iko chini ya wizara ya elimu..

Mabaraza yote ya taaluma yako chini ya wizara husika....

Mfano Baraza la madaktari (MCT),baraza la wauguzi (TNMC), baraza la wafamasia, baraza la wataalamu wa maabara yote yako chini ya wizara ya afya. Na yote utaratibu ni uleule wa kufanya mitihani kabla ya kupata leseni. Ni kiwango cha kufaulu ni kinafanana fanana ivoivo..

Hata Law School iko chini ya wizara ya sheria, haiko wizaranya elimu.

Sasa jiulize hao madaktari wanacholalamika ni nini? Qewe kwa akili zako MCT wanaweza kufanya jambo ambalo waziri hana taarifa nalo?

Mitaala ya Wizara ya Elimu (TCU) kuna mahali inapwaya. Sasa vijana wakija site wanakutana na mambo yasiyo na konakona ndiyo maana wanafeli..

Jiongeze acha uzwazwa..
 
MCT kimekua ni kikundi cha wanasisa wachache kukusanya pesa za Madaktari wanajilia. Tuhuma za rushwa kibao
MCT, TNMC, HLPC, PCT endeleeni kukaza ivoivo, hatutaki mazumbukuku maeneo ya kazi...

Wapikeni vijana vile inavyotakiwa, hizi kelele za mitaani zisiwasumbue...

Kule law school waliunda mpaka tume mwaka juzi. Nenda kafuatilie majibu yalikuwaje ndiyo utajua hawa intern doctors wanatakiwa wakae kwa kutulia..
 
Back
Top Bottom