Madaktari Waliogoma Kukutana Leo Jumamosi- Tafsiri Yangu

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Mkutano wa Rais na Wazee wa Dar es Salaam haukufanyika jaan Ijumaa saa kumi kama ilivyopangwa. Na hautafanyika leo Jumamosi saa tano. Utafanyika Jumatatu saa kumi jioni.


Tafsiri yangu;

Matukio ya saa 48 zilizopita yamebadilisha mwelekeo wa mambo. Kuna hekima iliyotangulizwa. Inaonekana , kuwa Serikali imeamua kuitafuta suluhu ya mgogoro na madaktari kwa kuzungumza na madaktari moja kwa moja na kwa kujifungia- closed door dialogue.

Na safari hii, Bwana Mkubwa ndiye anayeongea na wawakilishi wa madaktari kwa kuwakaribisha Ikulu ya Magogoni. Na yaliyojadiliwa Ikulu hayajawekwa hadharani hadi ninavyoandika tafsiri hii. Ndivyo inavyotakiwa iwe, kuacha kupambana hadharani wakati fursa ya kukutana na kuongea kwa kujifungia chumbani ingalipo.


TBC1 imeripoti jana usiku kuwa mgomo wa madaktari kwa kiasi kikubwa umekwisha. Hapana, yumkini hiyo ni tafsiri ya TBC1, maana, kwa yanayoendelea sasa, yawezekana kabisa kuwa mgomo umesitishwa 'over a week- end' kupisha mazungumzo.

Kwenye ukuta wa facebook wa chama cha madaktari wametangaziwa kuwa leo Jumamosi kunako saa tatu kuna mkutano pale Don Bosco. Bila shaka kutakuwa na kupeana feed-back. Na kesho Jumapili wawakilishi wa madaktari wanakwenda tena Ikulu kuzungumza na Mkuu wa Nchi. Kuna kila dalili watafikia makubaliano katika mambo ya msingi. Hivyo basi, kumaliza mgogoro wao na Serikali na mgomo pia.


Je, ndio kusema Mponda na Nkya watajiuzuru?

Hapana, hilo halitawezekana , na JK ana uwezo wa kuwaambia madaktari na wakamwelewa kuwa hilo haliwezekani. Hawezi kuwaondoa mawaziri hao kwa sasa na ikatafsiriwa kuwa ni kwa shinikizo la madaktari. Naam, mambo ya uendeshaji wa nchi lazima yaende hata baada ya Nkya na Mponda kuondoka. Na ili mengine yaende, hatma ya Mponda na Nkya itabaki mikononi mwa JK.

Na Jumatatu itafika, ama wataanza madaktari wenyewe kutangaza kumaliza rasmi mgomo baada ya kuwa na mazungumzo na Rais na kukubaliana kwenye mambo ya msingi juu ya madai yao, au watasubiri kwanza Rais akutane na Wazee wa Dar es Salaam pale Diamond Jubilee. Alihutubie Taifa, na mbali ya mambo mengine, atangaze rasmi kumalizika kwa mgomo wa madaktari.


Na tusubiri tuone...


Maggid Mjengwa,
Iringa, Jumamosi, Machi 9, 2012
 
yote ni heri.mwisho wa mgogoro huu kuna mambo mawili muhimu.....maslahi ya wafanyakazi wa kada ya afya kuboreka na waliopelekea mgomo huu kuwajibishwa.
 
Kweli tusubiri tuone tu!

Ila kwa namna yoyote ile bila mawaziri hawa kuondoka tutakuwa hatujafanikiwa katika kujenga utamaduni wa kuwajibika...

Na vyombo vya habari chiriku vitawananga sana madaktari.....

Ila mwisho ni wito wa dhati kwa nyie waandishi wa habari mtende haki na muwaheshimu sana madaktari wetu katika maandiko yenu, sio mnabebwa na hisia tu na kuwashambulia..


Tusubiri tuone.
 
kikwete kishasema kuwa atawaondoa hao mawaziri........hana namna...amekuwa akipewa taarifa za uongo na jana baada ya kukutana a madaktari alikuwa anashangaa tu anayoelezwa na madaktari ni tofauti na taarifa alizonazo......
 
Ni kweli Mjengwa,

Lakini wa TZ imefika wakati tukatae kupotoshwa na baadhi ya misemo ambayo kwa kwa kweli inaleta tafsiri potofu na kuharibu elimu zetu ndogo za uraia. Atakaokutana na Mh RAis Jumatau na kwa kadri tulivyozoea kuwaona kwa maana ya utashi wao, hulka yao,na hata ujihi wao SIO mkusanyiko wa wazee wa Dar! Hapana Tukatae, tukatae na tukatae.Ni wazee wetu tunawaheshimu lakini kamwe hawaendi kwa kofia hiyo inayotajwa sasa.

Ni tofauti kubwa sana ya wakati ule wa Mwalimu maana sote twajua namna itikadi ilivyokuwa imeshika hatam na jinsi issues zenyewe zilivyokuwa zinajitokeza kimatukio.
 
kikwete kishasema kuwa atawaondoa hao mawaziri........hana namna...amekuwa akipewa taarifa za uongo na jana baada ya kukutana a madaktari alikuwa anashangaa tu anayoelezwa na madaktari ni tofauti na taarifa alizonazo......
Kama ni kweli basi kuna hujuma kubwa kwenye huu utawala wa JK, kuna kundi la UWT linampa taarifa zisizo sahihi, Au ni JK mwenyewe ndiyo anafanya hizi sakarasi kwa kujijengea style fulani ya utawala wake.
 
Kama ni kweli basi kuna hujuma kubwa kwenye huu utawala wa JK, kuna kundi la UWT linampa taarifa zisizo sahihi, Au ni JK mwenyewe ndiyo anafanya hizi sakarasi kwa kujijengea style fulani ya utawala wake.
nadhani hata vile vitisho vya kipindi kile lilitokana na kupewa taarifa za uongo.nadhani hizi taarifa hupelekwa na tbc au kina tambwe hiza.
 
kikwete kishasema kuwa atawaondoa hao mawaziri........hana namna...amekuwa akipewa taarifa za uongo na jana baada ya kukutana a madaktari alikuwa anashangaa tu anayoelezwa na madaktari ni tofauti na taarifa alizonazo......

ni kawaida yake kushangaa. I doubt kama huo 'mshangao' wake hauambatani na unafki ndani mwake..
 
nadhani hata vile vitisho vya kipindi kile lilitokana na kupewa taarifa za uongo.nadhani hizi taarifa hupelekwa na tbc au kina tambwe hiza.

umenena, propaganda na uongo hauwezi kusaidia bali kujiangamiza wenyewe. To me all news from TBC are lies unless proved otherwise, kwa hiyo ni miongoni mwa TV..... duniani
 
Goodwork mjengwa ume analyse vizuri sana ila serikali kwa siku mbili inatumia sana propaganda kwenye vyombo vya habari kuepusha kuchukiwa na wananchi ionekane madaktari ndo wana matatizo
 
Kweli tusubiri tuone tu!

Ila kwa namna yoyote ile bila mawaziri hawa kuondoka tutakuwa hatujafanikiwa katika kujenga utamaduni wa kuwajibika...

Na vyombo vya habari chiriku vitawananga sana madaktari.....

Ila mwisho ni wito wa dhati kwa nyie waandishi wa habari mtende haki na muwaheshimu sana madaktari wetu katika maandiko yenu, sio mnabebwa na hisia tu na kuwashambulia..


Tusubiri tuone.
Mkuu JouneGwalu, tunawaheshimu sana madaktari ila kwa wengine wetu mimi nikiwemo, tunathamini zaidi uhai wa binadamu yoyote na uhai wa Mtanzania ndio unatakiwa uthaminiwe na Mtanzania mwingine yoyote achilia mbali yule aliyekula kiapo cha to "save lives" no matter what!.

Wengi wanasupport madakitari na hata mimi binafsi nakiri madai yao ni genuine but there are many routes to Rome, hiyo njia waliotumia kuleta siasa na kutaka kutumia human shield ya innocent Tanzanians kama bakora ya kuichapia serikali, is a wrong way!. Yes wadai haki zao but not at the expence of poor ordinary innocent Tanzanians!.
 
Mkuu Maggid, naiunga mkono hoha yako ya 'kujifungia ndani' kwa asilimia 100%. Hivi sasa ndivyo inatakiwa iwe!. Thanks for this!.
 
Hapa mbona kama vile gvt inaingilia shauri lililokuwa mahakamani? Separation of powers?! mahakama si ilishatoa amri?

nisawa mkuu,mahakama wanatumia nguvu za sheri,ikumbukwe hawa si wabeba zege.wanahitaji kuombwa na kushauriwa ili waweze kurudisha mioyo yao ya huruma na umakini wa kazi,kinyume na hapo vifo vitaongezeka zaidi ya kugoma.
 
Mkuu JouneGwalu, tunawaheshimu sana madaktari ila kwa wengine wetu mimi nikiwemo, tunathamini zaidi uhai wa binadamu yoyote na uhai wa Mtanzania ndio unatakiwa uthaminiwe na Mtanzania mwingine yoyote achilia mbali yule aliyekula kiapo cha to "save lives" no matter what!.

Wengi wanasupport madakitari na hata mimi binafsi nakiri madai yao ni genuine but there are many routes to Rome, hiyo njia waliotumia kuleta siasa na kutaka kutumia human shield ya innocent Tanzanians kama bakora ya kuichapia serikali, is a wrong way!. Yes wadai haki zao but not at the expence of poor ordinary innocent Tanzanians!.
Hivi kwanini tunapenda kujadili madai ya madaktari nusu nusu?ukipitia madai yao utaona kwamba huduma bora kwa wananchi ni dai la kwanza. Kuwaambia hawa mawaziri waondoke ni njia muhimu ya kupata mazingira mazuri ya mazungumzo yenye tija kati ya kamati ya pinda na madaktari.

Madaktari wameapa ku save life,lakini serikali yetu haijawajibika ipasavyo kuhakikisha hilo, isitoshe uongozi wa wizara ya afya hauthamini madaktari hii inapelekea kukosekana kwa ushauri wa kitaalamu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu afya ya mtanzania.
How can u save life if you prescribe oxygen unaambiwa hakuna, if u want to operate unaambiwa hakuna gauze au sterile gloves!
Leo hii mgonjwa wa asthma anaweza kufa kwa kukosa nebulizer!!.....how can u save life in harsh enviroment kama hii?

Tukirudi kwenye maslahi sitasema mengi but ni aibu kwa daktari kutiwa roba ya mbao mitaa ya uswazi wakati anatoka
kazini saa tatu usiku hapa akiwa ameteseka kwa usafiri wa daladala.

Maamuzi ya kugoma hayakufikiwa kimzahamzaha au kishabiki. Ukiona profesa wa neurosurgery na urology wanaingia kwenye mgomo ujue kuna tatizo kubwa na unatakiwa ulishughulikie kwa uangalifu na umakini wa hali ya juu sana.

Ukiwa muandishi wa habari wa vibahasha huwezi kutafuta undani wa mambo sana sana utafuata mkumbo tu.
 
Natamani watanganyika mngekua na fikra ya tatu. Binafsi ninaamini mgomo wa madaktari ni moja ya propaganda ya serikali ya CCM kurudisha imani ya wananchi kwa Rais Kikwete.

Tumeshaona uhusikaji wa moja kwa moja wa Waziri mkuu lakini hakukua na matokeo chanya zaidi ni kuendelea kwa awamu ya pili ya mgomo.

Pili tumeona mahakama nayo ikitoa tamko lake baada ya pingamizi toka kwa Mwanasheria mkuu,pia utekelezaji ukawa wa kulegalega.
Sasa hapa ndipo "starring Kikwete" anapoibuka na kuvaa ile role yake yupenda sifa ili aonekane ni masihi wa wanyonge.

This time naamini Kikwete huenda akatoa maamuzi magumu lengo likiwa si kuisafisha serikali bali ni kurudisha imani ya Watanganyika kwa chama tawala CCM.

Kama sio Nkya na Mponda kuumia basi baadhi ya Madaktari lazima watolewe kafara.

Nawasilisha!
 
Back
Top Bottom