Mada maalum ya magari: Uzoefu, ushauri na maswali

Chukua kitu BMW kaka

Mtu ambaye siyo mara yake ya kwanza kumiliki gari na uchumi sio mbaya sana thats the right choice. Ila wale wenzangu na mimi huwa nawashauri watatafute magari yenye engine common with low running costs na ambayo vipuri vyake hata saa nane usiku unapata.

Gari yangu ya kwanza ilitaka kunitia wehu. Ni siku nyingi kidogo. Naishi mkoani mostly, subaru legacy ilikuwa almost peke yake hapo kijijini kwangu. Nikifunua bonet labda nataka ioshwe watu wanaitana kushangaa engine nikawa napanic kimoyo moyo.

Cv joints zote mbili nilinunua laki tano hivi nikaanza kutafuta mteja kimya kimya. Luckly niliiuza kwa faida nikaja town kula bata wkend kwa hasira.

Siku zinavyozidi kwenda mambo ya spare watu wasiogope sana kama una fungu, ila ni vizuri zaidi kutafuta gari utakalolimudu mabibi na mabwana.
 
Unajua kila mtu ana uzoefu wake inategemea yeye ana Platz model gani,lakini kwa ninazozifahamu mimi sikushauri

Honda nazo zipo ambazo ni vimeo hasa lakini kwa mfano ukipata RD5 ni gari nzuri mno, hata RD 1 pia kuna mdau kavuta moja hapahapa jukwaani baada ya kushauriana anaweza kuwa shuhuda mzuri

BTW gari yeyote ni matunzo, hata upate gari ngumu vp kama itakosa matunzo tarajia kifo cha mapema tu

RD 1 Ni gari nzuri japo Wishbone ndio ugonjwa mkubwa.
 
kuna jamaa yangu alikuwa na gari rav4 ina engene ya D4 ilimzingua akaamua kubadili na kuweka engene ya 3S, gari imekataa kukaa silance tatizo linaweza kuwa nini na afanyeje manake hiyo gari hata kuuzika imegoma.

Nami nilibadlisha Engine kutoka D4 kwenda 3s, ila sioni tatizo lolote, ka jamma bado anatatizo anipm nimuunganishe na fundi, lakin kama gari lipo Dar
 
Voltz kwa maoni yangu ni hybrid ya SuV na sedan....nimeziona no nzuri kwenye ulaji wa mafuta maana ni cc 1780 kama sikosei. Ningemshauri jamaa ainunue nadhani bei hadi 16M

Niliwahi kusoma uzi mmoja humu kuwa Voltz zilitengenezwa piece 10,000 tu na uzalishaji wake ukasimamishwa. Hivyo spea zake itakuwa ishu.
 
Niliwahi kusoma uzi mmoja humu kuwa Voltz zilitengenezwa piece 10,000 tu na uzalishaji wake ukasimamishwa. Hivyo spea zake itakuwa ishu.

Mmh elfu kumi tu? Hapana labda laki moja kwakuwa kwa kiwanda cha magari kutoa magari machache kiasi hicho basi kuna kasoro kubwa sana
 
Samahani mimi nina hilux surf ina engine ya 2LT yenye turbo ila imenisumbua sana hadi nikaamua kununua engine nyingine ila mkanganyiko uko pale mafundi wanaponipa ushauri tofauti. Wengine wanadai niweke engine ya petrol, wengine eti niweke isiyo na turbo ila ya diesel, naombeni ushauri.
 
Samahani mimi nina hilux surf ina engine ya 2LT yenye turbo ila imenisumbua sana hadi nikaamua kununua engine nyingine ila mkanganyiko uko pale mafundi wanaponipa ushauri tofauti. Wengine wanadai niweke engine ya petrol, wengine eti niweke isiyo na turbo ila ya diesel, naombeni ushauri.

Kwanza pole sana 2LT, ni engine majanga sijapata kuona, Hilux Surf nyingi zilipoteza umaarufu kwasababu ya hii engine
Binafsi naomba nikushauri kitu kimoja achana kabisa na Turbo, funga engine yoyote lakini sio ya Turbo!!! Kwa uhakika zaidi fungal engine ya petrol utaokoka na mengi
 
jamani kuna mdau aliuliza kuhusu Toyota wish hakujibiwa na mimi nilikuwa nasubiri ninufaike hapo, yeyote anayejua mazuri na mabaya yake nahitaji kununua kwa matumizi ya kawaida tu sio rough road. kama kuna mtu anajua consumption ya mafuta na durability yake kwa ujumla msaada.
 
Kwanza pole sana 2LT, ni engine majanga sijapata kuona, Hilux Surf nyingi zilipoteza umaarufu kwasababu ya hii engine
Binafsi naomba nikushauri kitu kimoja achana kabisa na Turbo, funga engine yoyote lakini sio ya Turbo!!! Kwa uhakika zaidi fungal engine ya petrol utaokoka na mengi
Sio kweli kuwa turbocharged engine ni mbovu!!, , ila nakubaliana na wewe kuwa kuna baadhi zinasumbua ,
Tunakosea pale tunapojaribu kutumia engine za turbo Kama engine za petroli au natural aspirated diesel engine ,
Turbo ni moja ya vitu complex na very sensitive , lakini fairly treated , huwa zina last almost forever,kiufupi Turbo zinakadiriwa kuwa na maisha sawa na injector pump, by default injector pump zinakuwa na life span ile ile ya engine.
Fanya haya next time utakapotumia engine zenye turbo
Oil.... Hakikisha unatumia oil yenye ubora wa juu
Usizime gari au engine Mara baada ya kufanya kazi nzito au safari ndefu
Air cleaner safisha Mara nyingi uwezavyo

To the best of my knowledge most economic durable,compact and powerful four stroke engine to date ..ni hizo turbocharged diesel engine

Alamsiki !!!
 
jamani kuna mdau aliuliza kuhusu Toyota wish hakujibiwa na mimi nilikuwa nasubiri ninufaike hapo, yeyote anayejua mazuri na mabaya yake nahitaji kununua kwa matumizi ya kawaida tu sio rough road. kama kuna mtu anajua consumption ya mafuta na durability yake kwa ujumla msaada.

Ni nzuri ila sio imara hasa huko chini kwenye wish-bones , tyrodends ball joints na stabilizer links huyo ndio ugonjwa wake mkubwa
 
Sio kweli kuwa turbocharged engine ni mbovu!!, , ila nakubaliana na wewe kuwa kuna baadhi zinasumbua ,
Tunakosea pale tunapojaribu kutumia engine za turbo Kama engine za petroli au natural aspirated diesel engine ,
Turbo ni moja ya vitu complex na very sensitive , lakini fairly treated , huwa zina last almost forever,kiufupi Turbo zinakadiriwa kuwa na maisha sawa na injector pump, by default injector pump zinakuwa na life span ile ile ya engine.
Fanya haya next time utakapotumia engine zenye turbo
Oil.... Hakikisha unatumia oil yenye ubora wa juu
Usizime gari au engine Mara baada ya kufanya kazi nzito au safari ndefu
Air cleaner safisha Mara nyingi uwezavyo

To the best of my knowledge most economic durable,compact and powerful four stroke engine to date ..ni hizo turbocharged diesel engine

Alamsiki !!!

Nakubaliana nawe kabisa nilichosema mimi ni engine za 2lt, na kuhusu turbo nimemshauri asiweke engine ya hivyo kwakuwa mafundi wengi ni majanga
 
Ni nzuri ila sio imara hasa huko chini kwenye wish-bones , tyrodends ball joints na stabilizer links huyo ndio ugonjwa wake mkubwa

Hebu nieleweshe........Toyota Wish inatumia tie rod end au stab link.......?........
 
Samahani kaka mshana jr bado haujanijib kuhusu toyota vanguard new model, pia ningependa kujua weakness zake. Shukran
 
Last edited by a moderator:
Ushauri Wadau,
naombeni ushauri kuhusiana na spare parts za rav 4 old model,ni wapi hasa naweza kupata vipuri vya uhakika maana kila nikibadili shock Absorber (shock up) ni majanga wiki tu gari kwenye tuta naisikia kiukweli napata kigugumizi sehemu sahihi ya kupata vipuri vya uhakika na ntajuaje kwamba ni uhakika.
 
Hebu nieleweshe........Toyota Wish inatumia tie rod end au stab link.......?........

Duu nafikiri ni tierod ends,mimi nilizungumzia kwa ujumla wake tu, swali lako liko sahihi BTW links na tierod ends ni vitu viwili tofauti kwa ufahamu wangu (I may be corrected)
 
Samahani kaka mshana jr bado haujanijib kuhusu toyota vanguard new model, pia ningependa kujua weakness zake. Shukran
witnessj nilikukumbuka Leo, watu niliiongea nao ambao ni wamiliki wamezisifia sana, wote karibia bado ni mpya hawajazitumia sana hivyo ni ngumu kujua weakness zake, bei zinarange 25-30m, kwa mujibu wao
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom