Mkuu kama una habari ni bora ukatupa hata dondoo kidogo kuliko unavyofanya kama kutupatia kitendawili, tega! Basi chukua mji - Sumbawanga ututegulie kitendawili
Leo watu walivamia mgodi wakiwa wanataka kuchukua mawe na kufunga barabara inayotoka mgodini kwenda mjini.
Polisi walikwenda mgodini na ktk fujo hizo na mtu mmoja kujeruhiwa vibaya kwa risasi na inasemekanakana jamaa kapoteza maisha.
Baadae vurugu hizo zilihamia mjini kwa magari ya GGM kushambuliwa na gari moja limechomwa moto.
Kwa mchana hali ilikuwa tete na mabomu ya machozi kutawala mji wa Geita na jioni hii kidogo hali imetulia lakini MD amezuia magari madogo kutoka na watu wote wanatumia mabasi.
Ni kweli yametokea ila hakuna waliovamia mgodi bali wachimbaji wadogo wamefukuzwa eneo walilokuwa wakichimba dhahabu na eneo hilo kapewa mwekezaji na deadline ilikuwa jana waondoke kwa hiari wakakata na kuanza kundamana kuanzia hukohuko mgodini mpaka mjini kwa DC wakatimuliwa na FFU katika purukushani hizo zilizodumu toka asubuhi hadi mchana wachimbaji wawili wameripotiwa kuuawa kwa risasi na baadhi ya magari kuchomwa moto na kuvunjwa vioo habari zaidi tutaziweka humu kadri tutakavyozipata.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.