Geita: Aliyevamia Kanisa la RC Geita na kuharibu mali za Tsh. Milioni 48 ahukumiwa miaka mitatu jela

Excel

JF-Expert Member
Jul 8, 2011
19,745
10,078
Elpidius Edward, mkazi wa Mtaa wa Katundu mjini Geita amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu kwa kosa la uharibifu wa mali zenye thamani ya zaidi shilingi milioni 48.2 za Kanisa Kuu la Kiaskofu Jimbo Katoliki Geita.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Geita imemtia hatiani Elpidius baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka katika shtaka la pili.

Hukumu hiyo imetolewa leo na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Johari Kijuwile.

Kwa mara ya kwanza kesi hiyo ilifikishwa mahakamani Machi 6, 2023, mshtakiwa akidaiwa kutenda kosa la kuvunja na kuingia kwenye Kanisa Kuu la Kiaskofu Jimbo la Geita.

Geita.jpg

Pia soma: Aliyevamia Kanisa la RC Geita na kuharibu mali za Tsh. Milioni 48 alikuwa na akili timamu
 
Taasisi za Kiimani zipo kwa mujibuwa wa Sheria na, ni wajibu kwa taasisi zote kutii na kufuata Sheria zilizopo.
Hivyo basi jambo lolote linalotafsirika Kisheria kama ni uhalifu kikitokea shurti lishughulikiwe kwa kufuata vifungu vya Sheria vilivyopo kuhusiana na Kosa lililotendwa.

Sasa, Uhalifu umefanyika,
Mtuhumiwa kakutwa na hatia,
Jamani, arudishwe kuhukumiwa na Kanisani tena?, kweli?

Nikupe 'Chakula ya Akili' japo kidogo,
Mfano;
Ipo Imani fulani (inasemekana) inaamini kuwa kwao wao Mwizi akipatikana,
Ikiwa ni mara yake ya kwanza kukamatwa kwa kutenda Kosa la Wizi basi, akatwe mkono wake wa kulia,
kisha aachiwe aende zake.

Ikitokea mwizi huyohuyo akaiba na kwa mara ya pili akakamatwa tena basi,
na-akatwe mkono wake wa kushoto.,
Ndipo tena aachwe aende zake tu.

Je,wewe Ingekupendeza kusikia Jamaa hao (Wana Dini hao) wamemkata mshikaji eti kaiba nyumba ya Ibada,

Wewe huyohuyo ungegeuka nakuponda zaidi pengine.

Tusiwahi kuhukumu.

Nawasilisha.
 
Unaelekeza lawama kwa Kanisa umetafakari kweli?

Taasisi za Kiimani zipo kwa mujibuwa wa Sheria na, ni wajibu kwa taasisi hizo kutii na kufuata Sheria.

Hivyo basi jambo lolote linalotafsirika Kisheria kama ni uhalifu linashughulikiwa kwa kufuata Sheria za Nchi.

Sasa Uhalifu umefanyika, Mtuhumiwa kakutwa na hatia, apelekwe ili akahukumiwe na Kanisa tena?, kweli?

Nikupe 'Chakula ya Akili' japo kidogo.
Mfano;
Ipo Imani fulani (inasemekana, inaamini kuwa kwao wao Mwizi akipatikana,
Ikiwa ni mara yake ya kwanza kukamatwa akiwa ameiba basi, akatwe mkono wake wa kulia,
kisha aachwe aende zake.

Ikitokea mwizi huyohuyo akaiba tena kwa mara ya pili akakamatwa tena basi,
na-akatwe mkono wake wa kushoto., kisha tena aachwe aende zake tu.

Je,wewe Ingekupendeza kusikia Jamaa wamemkata mkono kisa kaiba nyumba ya Ibada,
Wewe huyohuyo Ungegeuka nakuponda zaidi pengine.

Tusiwahi kuhukumu.

Nawasilisha.

 
Back
Top Bottom