Nesi mkunga
JF-Expert Member
- Nov 28, 2022
- 701
- 1,843
TAARIFA KWA UMMA WA KIISLAMU.
Jana Tulipokea Taarifa ya kutekwa kwa Ustaadh Abdulrahmaan Imam mkuu wa msikiti Wa GPB Shell Mtaa wa Nyankumbu Mji wa Geita.
Imam Abdulrahmaan Alitekwa akiwa anatoka msikiti kuswalisha Taraweh akiwa Ameambatana na mtoto wake wakiume.
Akiwa njiani aliitwa na watu wawili waliofunika nyuso zao wakiwa wamevaa kiraia na kuzungumza naye,Inasemekana kwa mashuhuda kuwa kulitokea mzozo baina yake na wao Jambo lililopelekea Wafyatue risasi Moja hewani na kisha wakamchukua wakamuweka kwenye gari na kuondoka naye
Zimefanyika Juhudi jana kutwa nzima za kumtafuta kwenye vituo vyote vya polisi lakini hakupatikana na Hajulikani alipo mpaka mda huu.
Pamekuwepo na Wimbi kubwa sana katika mji wa Geita la vijana walio mstari wa mbele katika harakati za dini kutekwa na kupotezwa, ni wakati sasa wa kupaza sauti zetu kama umma wa kiislamu.
Jana Tulipokea Taarifa ya kutekwa kwa Ustaadh Abdulrahmaan Imam mkuu wa msikiti Wa GPB Shell Mtaa wa Nyankumbu Mji wa Geita.
Imam Abdulrahmaan Alitekwa akiwa anatoka msikiti kuswalisha Taraweh akiwa Ameambatana na mtoto wake wakiume.
Akiwa njiani aliitwa na watu wawili waliofunika nyuso zao wakiwa wamevaa kiraia na kuzungumza naye,Inasemekana kwa mashuhuda kuwa kulitokea mzozo baina yake na wao Jambo lililopelekea Wafyatue risasi Moja hewani na kisha wakamchukua wakamuweka kwenye gari na kuondoka naye
Zimefanyika Juhudi jana kutwa nzima za kumtafuta kwenye vituo vyote vya polisi lakini hakupatikana na Hajulikani alipo mpaka mda huu.
Pamekuwepo na Wimbi kubwa sana katika mji wa Geita la vijana walio mstari wa mbele katika harakati za dini kutekwa na kupotezwa, ni wakati sasa wa kupaza sauti zetu kama umma wa kiislamu.