Fasta fasta
JF-Expert Member
- Feb 15, 2011
- 1,126
- 725
Kama ni kweli huyu RPC amezuia maandamano hajatendea CHADEMA haki. Wao ndio watakaohatarisha amani hapa tanzania kwa ujumla. RPC uwe makini na uchukuwe mfano uliopo hapo kwa jirani yako (Kenya) na ujue juzi waliitwa kwa nani kujibu mashtaka, siku utakapo itwa watakukimbia wote. Sisi tunajua kila mtanzania anauhuru wa kuhudhuria au kuendelea na shughuli zake. Hivyo vyombo vya dola ambavyo vimepata hizo habari za kitelijensia vingekuwa wazi kuwa kuna mbinu hii na hii ili kila mtu awe askari au kuwashauri labda tarehe hii haiwezekani tupeleke tarehe fulani, kwa sababu haya maandamano sio ya siri. Wananchi wa Mbeya tunaomba tushirikiane kutafuta haki yetu inayotumiwa vibaya na wapenda mijisifa. CCM mlituburuza mpaka mitongotongo yetu ikatukaukia machoni kwa ajili ya kutishiwa tishiwa na zidumu fikra za M/kiti. Sasa tumesha nawa matongotongo yamekwisha lazima tudai haki yetu. Na tutadai haki yetu kwa amani kwa kutumia sanduku la kura.
Mungu ibariki Tanzania na viongozi wote wa CHADEMA.:israel:
Mungu ibariki Tanzania na viongozi wote wa CHADEMA.:israel: