Maalim Seif: Tunataka Zanzibar yetu!

Maalimu kashindwa kutmaka neno vunja muungano, kuna mbunge gani atakayethubutu?

Unajua baada ya hoja ya Seif ya serikali 3 kudadavuliwa hapa JF alijiona dhalili, sijui iliishia wapi.
Sasa wanataka mkataba. Nakuhakikishia siyo Maalim, Ahmed, Jusa au awaye atakayeweza kutamka hata jambo moja la huo mkataba.

Siri kubwa ya mkataba ni kutaka kujificha nyuma ya mgongo wa Tanganyika.
Maalimu amesema eti bidhaa za ZNZ zinatozwa ushuru zikiingia bara. Alichotaka ni kuwa ziingie ZNZ, SMZ ichukue kodi halafu ziingie bara kama zimetoka Tabora. Kwamba soko la Waarabu lisiwe na kodi huku bara.

Seif anafahamu kuwa soko la ZNZ ni Tanganyika, nje ya muungano ni maumivu.
Tena soko si la biashara, ni pamoja na ardhi. ajira n.k.

Hakuna taifa lolote duniani lililowabeba WZN wengi kama Tanganyika.
Hakuna taifa linaloajiri WZNZ kwa upendeleo kama Tanganyika
Hakuna taifa linalosemesha WZNZ bure kama Tanganyika
Hakuna taifa linalotoa nishati ya bure ZNZ kama Tanganyika.
Hakuna taifa linalogharamia ulinzi na usalama wa ZNZ kama Tanganyika

Ikifika hapo, wote wananywea in fact wanaufyata kutamka neno vunja muungano kama alivyoufyata Seif.
Tanganyika ni ya ajabu sana, tumewabeba hawa watu halafu tunawapa muda wa kucheza msewe mgongoni.
LET THEM GO! Period.

Tanganyika inanufaika na nini na serikali 3 ua mkataba na ZNZ!

Maalim Seif Sharif Hamad Mshirazi, bado unauma maneno tena sana. Toa neno mkataba katika hotuba zako weka neno vunja muungano! hapo tutakuelewa kinyume chake unakula matapisha yale yale.

Mwisho wa mkataba ni Chumbe, baada ya kuvuka hapo nidhamu na adabu mbele!

Sasa kama wewe ni msemaji wa serikali ya Tanganyika na ccm tunakuomba liambie jeshi lako unaloliita la muungano liondoke hapa ZnZ uone kitakachofata.

Usijinape kwakua unajua kuwa Waznz wamedhibiwa lkn Fanya utajua kama kweli waznz wanaihitaji Tanganyika au la. fyoo..ko ww
 
Kama kuna chama ambacho msajili anapaswa kukifuta haraka basi ni CUF. Haiwezekani mtendaji mkuu wa chama anahubiri waziwazi tena bila kificho utengano wa kitaifa halafu anatazamwa tu!

Tanzania ni moja na mipaka yake lazima ilindwe kwa gharama zote. Hoja zake alipaswa azitolee kama mwananchi wa kawaida kwenye Tume ya Katiba na sio majukwaani. Tendwa upo?

Kweli Tanzania ni Moja, bali imetokana na dola mbili huru zilizo na mipaka yake inayotambulika kimataifa, na kwa Mzanzibar ana hakki ya kujigamba na kujivunia sehemu yoyote ndani ya mipaka yetu adhimu ya Zanzibar, na Maalim anapolingania Zanzibar yenye mamlaka kamili, hajatenda kosa lolote kisheria maana asili ya Muungano ni Zanzibar huru na Tanganyika huru, kuna ubaya gani kuurejesha Uhuru wa Wazanzibar....?
 
Sasa kama wewe ni msemaji wa serikali ya Tanganyika na ccm tunakuomba liambie jeshi lako unaloliita la muungano liondoke hapa ZnZ uone kitakachofata.

Usijinape kwakua unajua kuwa Waznz wamedhibiwa lkn Fanya utajua kama kweli waznz wanaihitaji Tanganyika au la. fyoo..ko ww
Si wamekuja Dodoma? Mwenyekiti wa muda si pandu?
Kama wasingetaka muungano basi na mkataba wangekataa na leo wangekuwa Unguja. Midhali wamekuja Dodoma hakuna mawaa tena, wanautaka tena sana tu!

Subiri bunge lianze uone watakavyodai vyeo, nafasi za ubalozi, madaraka sawa n.k.
Kitu ninachokuhakikishia ni kuwa ukimsikia mznz anaongelea gharama zozote ujue ni mwendawazimu.
Mznz mwenye akili timamu hajui gharama, anajua nafasi za ubalozi, vyeo n.k.

Kwa taarifa yako Jusa ndani ya Dodoma. Ali Salehe alishamaliza katika tume ya Warioba.
Maalim kachukua kitambulisho Karimjee kabla ya mznz mwingine. Nani amebaki tena?
 
Huyu si mswana uamsho? Lazima awawakilishe vyema waarabu wenzake katika kudai koloni lao jipya la zanzibar!

hahee, Watanganyika wenzio wameongea hoja dhaifu, ila wewe umeongea pumba!! Yaan Wazanzibar kudai hakki yao ya kuwa na dola huru ndio Uarabu, sio mbaya maana kwetu sie Waarabu ndio wenzetu maana asili ya dini yetu ,mtume wetu ni Mwarabu kwa hapo wala hamna shida!!! lakini kumbuka hayo hajaanza kusema maalim Seif aliyaanza Karume akafuatia Aboud Jumbe ambao hao ndio viongozi waandamizi wa ASP na mapinduzi yetu pia, nadhani kama ni Uarabu basi wao ndio Waarabu wa mwanzo kutaka kuurejesha utawala wa mtukufu Sultan walio mpindua kwa mikono yako!! ongea kwa hoja madhubuti sio unaleta propaganda!!! kwa sasa hazina nafasi ktk kudai Zanzibar yetu!!
 
Huyu ni Mpemba na wapemba hawatakiwi Unguja na hawapendwi hili liko wazi so wauguja ndio hawataki kuvunja muungano ni wapemba tu... na wamanga..

Kumbe Watanganyika ndio wamezuia uchimbaji wa mafuta Zanzibar duh Sijalijua hili!!!!

hebu tuwekee wazi ni Waunguja gani ulokusudia wewe, maana Zanzibar ilikuwepo tokea dahari zamani na wala hatujawahi kusikia hicho unachokisema wew, mie nadhani Waunguja uliowakusudia wewe ni wale waliokimbia kodi ya kichwa kutoka Tanganyika na kukimbilia Zanzibar kwa kufuata maisha bora ya hao Wapemba na Waunguja, na wengine wale waliopenyezwa 64 kutokea Tanga, na Waunguja wengine wale waliokuja na Mwenge baada ya Mapinduzi wakasahau kurudi makwao hadi leo hii, ila kwa waungwana wa Kizanzibar daima chuki hiyo haipo, maana Zanzibar ni moja na watu wake wamoja tokea dahari za man!!!
 
pia kinachokera yeye ndo chanxo cha ndoa kati ya cuf na ccm zenji
 
Maalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:

"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.

Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.

Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.

Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.

Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.

Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."


Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM
hiko ndiko kujali utaifa sio watanganyika wanapoteza utaifa wao,kwa upande wangu siwalaumu wazanzibari kwa msimamo walionao
 
Hata sisi watanganyika hatuwezi kuipoteza historia ya nchi yetu tukufu Tanganyika kwa ajili ya tamaa ya ma CCm yenye uchu wa madaraka. Mkichakachua Bungeni tutaonana kwenye kura. Bora katiba hii isipite tuendelee na hiyo iliyochoka na isiyomatch na katiba ya Zanzibar kuliko kukubali cover mpya katiba ileile.
 
Hiyo ndiyo CUF iliyopewa kazi ya kudhoofisha Chama makini Tanzania, yaani, Chadema. Sasa wakipata Zanzibar yao hawa akina Lipumba sura zao wataficha wapi? Na wanadhani ni Mtanganyika yupi atakayewaona wamaana tena? Waende zao huko kwanza wapemba tumewachoka na ndio maana siku hizi tumegundua na hata bidhaa zetu tunanunua kwa akina Mangi tu ili wapemba wafunge maduka yao. Ndio maana wanazalisha wake zao kila mwezi ili wajaze Zanzibar na baadaye watasema Wapemba ni wengi kuliko waUnguja so wapemba wapewe Jamhuri yao. Watu wanaangalia mbali bwana. Siyo mnasema tu wapemba wanazaa hovyo, kumbe wenzenu hiyo ni mbinu za kujazana ili wapate nguvu za kuja kudai Jamhuri yao.

Zanzibar ina wenyewe, hata wakijazana wewe Mtanganyika inakuhusu nini, nadhani huku ni kushindwa kwa hoja ya kuongea !! sisi kama Wazanzibar wala hatuna habari nalo ila nashangaa ndugu yang wa Tanganyika muliobarikiwa na ardhi kubwa sana, tena hii yetu mwaitakia nini?
 
mie naenda sana Unguja, manenoi haya utayakuta sana Pemba ila cha AJABU sana Unguja upuuiz huu hawataki kuusikia, hata huko Pemba utakuta kwa wananchi wa kawaida sana ila watu walioenda shule hawakubaliani sana na hoja zao ila hadharani wanaitikia maana wanakuambia la sivyo mtakuwa maadui wa kudumu.

Mie ni muumini wa serikali tatu naamini la sivyo maneno na chokochoko hizi hazitakwisha kabisa

Maalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:

"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.

Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.

Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.

Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.

Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.

Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."


Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM
 
Kama Mtanzania nisingependa kuvunjika kwa Muungano,lakini kama wenzetu wanaona hawafaidiki nao ni vyema kuwapa haki yao.Ila siwaamini wanasiasa kwani wangekuwa wakisemacho kinaukweli nina uhakika Maalim Seif angewakatalia wabunge wa CUF walioko kwenye bunge la muungano kutokuhudhuria bunge hilo sababu anataka Zanzibar yake.

Pili nadhani tujilaumu sisi wenyewe Watanzania (Bara na Visiwani) kwani hatuko makini kuchagua viongozi ambao wataleta maendeleo kwenye nchi yetu.Mara nyingi tumechagua viongozi baada ya either kupokea pesa,Khanga,T-shirt na uwongo mwingine mwingi toka kwa wanasiasa.Tatizo wala si Muungano tatizo viongozi tunaowachagua hawana uzalendo kila mtu anajilimbikizia mali na kuuza nchi yetu kwa wageni.

Tuangalie leo hakuna aliyesalama si Mzanzibari wala Mtanganyika wote hatujui kesho yetu kama nyumba iliyopo kesho haitapewa muwekezaji.Tunachotakiwa kufanya nikukataa ujinga tunaofikirishwa na wanasiasa.Tuamke kwa sasa.Tuachane na Ukanda,ukabila,milengo ya siasa ubara au uvisiwani tuangalie mustakabali wa nchi yetu tukatae ujinga unaoletwa na viongozi wetu wa siasa.

Tusiwaachie wachache watutafutie viongozi twende tukapige kura wakati wa upigaji kura,tujiandikishe kupiga kura kama haujajiandikisha ,vinginevyo tunatwanga maji kwenye kinu.
 
Maalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:

"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.

Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.

Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.

Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.

Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.

Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."


Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM

Hapa huu si muungano ni utengano, baadhi ya mambo kama bank, bendera ya zanzibar kupepea UN, sarafu ya zanzibar na mengineyo, hayawezi kufanyika katika muungano ikiwa hivi bas zanzibar itatakiwa kuwa nchi kamili bila ya muungano. Angalia UK kuna nchi kama scotland, visiwa vya wales na England zote hizi huunda muungano wa great britain au UK, wanaserikali zao lakini huwezi bendera zao UN zikipepea, hawana ubalozi, sarafu zao, benki kuu na nk. Huu ndo muungano wa nchi kuwa taifa, wanapotoka nje hujulikana kama great britain au UK.
 
Mkuu naona unajibu kama vile umetokea chooni kutoa haja kubwa... kama ungekuwa unajua asili ya watu huko visiwani ungenyamaza kimya... kuliko kuita ni mabwana wa Dada zetu.. hata mimi nina Demu wa kizenji na siwezi waita hivyo...

Asili haina uhusiano na bongo.
Na huyo demu labda mzanzinara
 
jana nimesikia habari kuhusu bunge la katiba kuwa wajumbe hawatakuwa(hawatalipwa) na mishahara je hii ndio imesababisha walipwe POSHO kubwa ili kufidia malipo ya mshahara??
 
WAKWENDE TU, mi hata sioni tunawabembelezea nini. Huyo Seif anaongea kinafiki sana akifika ikulu anakunywa gahawa vizuri bila shida.
 
Una uhakika na unachokisema ama ndiyo umejifunzia siasa kwenye Jamiiforums?

Kitu gani ambacho hujaelewa hapo mkuu?

umemsoma Sefu kwa umakini au umekurupuka tu.

Leo mmepata Gesi mmeanza ubinafsi hivi bara tunarasimali asilia ngapi na hatujawai kufikiria kuwatenga.

hao wabunge walio kwenye Bunge la muungano wana kazi gani, na kwa nini wabunge watanganyika hawamo kwenye baraza la wawakilishi.

Nipe mchango wa serikali ya Zanzibar kugharamia serikali ya muungano.

Ni maslai ya ccm ndio yanayowafanya tuwe pamoja mpaka leo.
Kifupi Zanzibar ni Mzigo kwa Tanganyik kupitia ccm.!!
 
Back
Top Bottom