KATIBU Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema kuwa hatua ya Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Zanzibar, Ismail Jussa Ladhu kujiuzulu nafasi hiyo ni pigo kubwa kwake na kwa chama hicho kwani alikuwa ‘jembe'.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Maalim Seif licha ya kueleza kuumizwa na msimamo wa Jussa, alitoa siri kwamba alionesha azma ya kutaka kuachia ngazi tangu Julai mwaka huu kwa madai kuwa ana majukumu mengi.
Mbali ya kuwa Naibu Katibu Mkuu, CUF Zanzibar, Jussa pia ni Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe.
"Hata hivyo baada ya kunipa ujumbe huo nilimwambia kuwa ni vyema suala hilo akamwambie Mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba kwa kuwa yeye ndiye mwenye dhamana ya uteuzi," alisema Maalim Seif.
Alisema baada ya majibu hayo, Jussa alikubali, lakini Profesa Lipumba, kutokana na uzito wa suala hilo, aliamua kulipeleka katika kikao maalumu kinachowahusisha viongozi wa juu wa chama akiwemo mwenyekiti mwenyewe, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu kwa majadiliano zaidi.
"Kikao hicho kiliamua kujadili suala hilo kwa kina na baadaye wakamshauri asifanye maauzi hayo hadi uchaguzi mdogo wa Jimbo la Bububu utakapomalizika kwa kuwa huenda lingeweza kuleta dosari katika kampeni, naye bila kusita alikubali ombi letu," alisema Maalim Seif.
Maalim Seif alisema Jussa, juzi aliwasilisha barua ya kuachia ngazi na kumkubalia kwani alibaini kuwa alidhamiria kuachia nafasi hiyo.
"Tumemkosa mtu muhimu sana asiyekuwa mbinafsi jambo linalopaswa na wengine tufuate nyayo zake kwa kuiga tabia ya kutotaka kujilimbikizia madaraka.
"Jussa hakuhama chama ila ameamua kuwatumikia wananchi wake wa Mji Mkongwe na kutaka kuibana zaidi Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar kupitia Baraza la Wawakilishi," alisema Maalim Seif.
My take: Jembe bila kuingizwa mpini haliwezi kulima!!
Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa jana, Maalim Seif licha ya kueleza kuumizwa na msimamo wa Jussa, alitoa siri kwamba alionesha azma ya kutaka kuachia ngazi tangu Julai mwaka huu kwa madai kuwa ana majukumu mengi.
Mbali ya kuwa Naibu Katibu Mkuu, CUF Zanzibar, Jussa pia ni Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe.
"Hata hivyo baada ya kunipa ujumbe huo nilimwambia kuwa ni vyema suala hilo akamwambie Mwenyekiti Profesa Ibrahim Lipumba kwa kuwa yeye ndiye mwenye dhamana ya uteuzi," alisema Maalim Seif.
Alisema baada ya majibu hayo, Jussa alikubali, lakini Profesa Lipumba, kutokana na uzito wa suala hilo, aliamua kulipeleka katika kikao maalumu kinachowahusisha viongozi wa juu wa chama akiwemo mwenyekiti mwenyewe, Makamu Mwenyekiti na Katibu Mkuu kwa majadiliano zaidi.
"Kikao hicho kiliamua kujadili suala hilo kwa kina na baadaye wakamshauri asifanye maauzi hayo hadi uchaguzi mdogo wa Jimbo la Bububu utakapomalizika kwa kuwa huenda lingeweza kuleta dosari katika kampeni, naye bila kusita alikubali ombi letu," alisema Maalim Seif.
Maalim Seif alisema Jussa, juzi aliwasilisha barua ya kuachia ngazi na kumkubalia kwani alibaini kuwa alidhamiria kuachia nafasi hiyo.
"Tumemkosa mtu muhimu sana asiyekuwa mbinafsi jambo linalopaswa na wengine tufuate nyayo zake kwa kuiga tabia ya kutotaka kujilimbikizia madaraka.
"Jussa hakuhama chama ila ameamua kuwatumikia wananchi wake wa Mji Mkongwe na kutaka kuibana zaidi Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar kupitia Baraza la Wawakilishi," alisema Maalim Seif.
My take: Jembe bila kuingizwa mpini haliwezi kulima!!