Maalim Seif anakagua miradi ya maendeleo Tz bara kama nani?

Halafu aje anapewa na ving'ora na msafara!!! kwa cheo ambacho hata kuingizwa kwake kwenye Katiba ya Zanzibar kilikuwa ni makosa!
Mzee Mwanakijiji, mbona na wewe unaingia kwenye mkumbo! au huna chuki binafsi na Maalim Seif.
Mimi nimeona hiyo habari ITV labda nikuulize wewe ni miradi upi wa Serikali amekagua na kufungua?
 
kama kiongozi wa serikali ndani ya ya jamhuri ya mungano wa Tanzania, chadema njie mnaona mita tano mbele wenzenu cuf wanaona mita 100 mbale ukweli ndio huo. mambo waliofanya cuf mwika ya nyuma ndio nyie mnafanya sasa kama maandamano cuf wamefanya sana nawambia endeleeni hivohivo mtaishia mandamano, ndio maana mnashangaa hili na mtashangaa sana cuf wako makini sana ndio maana hata kwenye midalhao kama mnasema ukweli mtaona chadema hamna chakuwambia wa tanzania cuf wanawaburuza kihoja ukweli ndio huo
 
haya ni majungu yaso mpango na wivu wa kisiasa,au kwa kuwa mbowe na slaa hawakuwahi kufungua miradi hata kule uchagani?
 
rais wa china alipokuja kufungua uwanja wa taifa alifungua kama nani?
Hilary clinton alipotembelea kukagua symbon power na kule kibaha alitembea kukagua kama nani?
Usiwe unaleta mada mfu wewe au ulitaka nawewe uonekane umeanzisha thread?

Rais wa China alifungua uwanja wa Taifa kwa sababu Vhina walitoa fedha za ujenzi wa uwanja na mafundi wa kuujenga.
Hilary Clinton alitembelea Symbion kwa sababu inamilikiwa na wafanyabiashara wa kimarekani na kufadhiliwa na serikali yao.
Labda tuelezwe kama hiyo miradi aliyofungua makamu wa raisi wa nchi ya Zanzibar ilifadhiliwa na kusimamiwa na serikali yao ya umoja wa kitaifa.
 
Hata mama Salma Kikwete huwa anakagua miradi na kusomewa taarifa na maRC wetu. Kwani nchi hii watu wanajali?
 
kufungua mbona hata kiongozi wa nchi za nje anaweza kuja na kufungua miradi.
Hayo ni mambo madogo wala usiwe na jazba.
hayo madodogo ndio yana takiwa kuwekwa sawa umesahau mzee six aliokolewa na ffu kule zenji na mswaada wake kuchwana mbele yake wakisema hawamtambui.....
 
ni kufinyanga katiba kumruhusu seif kufanya shughuli za kiserikali huku bara, hakuna sehemu yeyote ya katiba inayoonyesha kuwa kuna makamu wa kwanza wa rais wa zanzibar, upuuzi mtupu
 
Rais wa china na bi clinton kutembelea miradi yetu sawa wao si wafadhili? Sasa seif sharif amefadhili nini hata apewe heshima ya kukagua miradi ya bara?
 
Ni kawaida tu..... kama vile msaidizi wa mtu kitandani anaposomewa ripoti ya maendeleo ya mkoa..... hii ni tz bana
 
Je halali kwa kiongozi ambaye hatukumchagua kwa kura zetu, wala hana mamlaka yeyote ya kutuongoza kikatiba, kuja kufungua na kukagua miradi ya serikali huku Tz bara? Kwa mujibu wa chanel ten leo, seif ameonekana akifungua madarasa, kukagua mirad na kuhutubia wananchi!

Akafungue madrassa kwao Pemba............
 
Hapa mimi ndipo ninapoona umuhimu wa katiba mpya. Itakayoelekeza serikali tatu (yaani Zanzibar, tanganyika na Muungano) au serikali moja ya Muungano. Kinyume na hapo kiini macho kilichopo cha serikali 2 hakuna ataeweza kutoa jibu kamili hata kama yuko kwenye system maana ni kiini macho tayari.
 
Sio maalim seif tu hata waziri wa zanzibar ana haki hiyo katika tanzania na bado hajavunja katiba , ila waziri wa znz hana haki ya tanganyika !
Bila tanganyika siku zote tutaonekana ni machizi, hatuna hoja na wapinga katiba na hatujui maana ya muungano !
 
kama kiongozi wa serikali ndani ya ya jamhuri ya mungano wa Tanzania, chadema njie mnaona mita tano mbele wenzenu cuf wanaona mita 100 mbale ukweli ndio huo. mambo waliofanya cuf mwika ya nyuma ndio nyie mnafanya sasa kama maandamano cuf wamefanya sana nawambia endeleeni hivohivo mtaishia mandamano, ndio maana mnashangaa hili na mtashangaa sana cuf wako makini sana ndio maana hata kwenye midalhao kama mnasema ukweli mtaona chadema hamna chakuwambia wa tanzania cuf wanawaburuza kihoja ukweli ndio huo
Unaruhusiwa kuwa na maoni yako lakini CUF wanajisiriba mavi hebu angalia Seif anasemaje mbele ya wananchi na wafuasi wa CUF anasema sisi serikali tunasema Polisi wasiwahangaishe wananchi ,hapo ni Urambo ambapo mbunge wao Sakaya na na wana CUF waliwekwa ndani bila dhamana alikuwa wapi kuchukua hilo dege liloandikwa Tanzania kwenda kuwatoa ,CUF wamerikoroga hawjui wajiite wapinzani au serikali hovyo kabisa tamaa ya Seif ishanza kumtokea puani ashukuru anapesa manake Hamadi Rashid alikuwa anamg'oa ati ,
 
je halali kwa kiongozi ambaye hatukumchagua kwa kura zetu, wala hana mamlaka yeyote ya kutuongoza kikatiba, kuja kufungua na kukagua miradi ya serikali huku tz bara? Kwa mujibu wa chanel ten leo, seif ameonekana akifungua madarasa, kukagua mirad na kuhutubia wananchi!

katiba ya jmt 1977 haimtambui maalim seif wala balozi iddi. Juzi niko airport namuona mke wa maalim seif nae ana msafara wenye ving'ora vya polisi. Mambo haya unaweza kuyaona bongo tu. Km ni miradi aende akakague makunduchi na kiembemimba sbb hayo ndio maeneo yake. Huku bara aje kuhutubia mikutano ya cuf tu.
 
Je halali kwa kiongozi ambaye hatukumchagua kwa kura zetu, wala hana mamlaka yeyote ya kutuongoza kikatiba, kuja kufungua na kukagua miradi ya serikali huku Tz bara? Kwa mujibu wa chanel ten leo, seif ameonekana akifungua madarasa, kukagua mirad na kuhutubia wananchi!

Mkuu, ni kweli hilo linatoa maswali mengi yasiyokuwa na majibu. Ila kwa kifupi ni hivi kaka yangu; rais wa Zanzibar ana makamu wake wa Kwanza ambaye ndio huyo kibaraka tunayemuongelea, huyu ndio alikubali kabisa kuacha kutetea maslahi ya watu wake maskini akaishia kukubali utwana hadi sasa kina Mwigulu wanadiriki kumtusi na asiweze kuwajibu kwa kuwa tusi mara nyingi huwa ni lugha ya ukweli. Makamu wa rais wa zanzibar ama mfanya biashara haramu za dowans, ama wauza madawa ya kulevya waliojificha kwenye siasa, ama hata muuza kambale sokoni; wanao uwezo wa kwenda kufungua, kuweka jiwe la msingi, kuhutubia hafla au hata kuwa wageni waalikwa popote Tanzania (Bara na Visiwani) ilimradi tu amealikwa na wahusika na havunji sheria ya nchi. Ukitaka kuhoji sana tutaingia kwenye mjadala mkubwa sana wa Protocol ambao kwa kawaida huwa hauna majibu. Mwisho kaa ukijua hawa CUF sio washindani kwa sasa bali ni serikali hivyo sio wa kuwaamini sana na ndio maana hata seif kaenda kufanya unafki wake huko aliko, jiulize Lipumba anajisikiaje??? Ni aibu sana kaka. Nawasilisha.
 
Je halali kwa kiongozi ambaye hatukumchagua kwa kura zetu, wala hana mamlaka yeyote ya kutuongoza kikatiba, kuja kufungua na kukagua miradi ya serikali huku Tz bara? Kwa mujibu wa chanel ten leo, seif ameonekana akifungua madarasa, kukagua mirad na kuhutubia wananchi!

Kwani Pinda jimboni kwenu mlimchagua? Mbona huwa anakuja kukagua miradi ya maendeleo.
 
Back
Top Bottom