Katiba yetu ya leo inakosa MAMLAKA ya kuwajibisha. Katiba inapaswa kuunda Taasisi imara na siyo kinga kwa viongozi wasiowajibika ipasavyo

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,754
Katiba.jpeg
  1. Rais ambaye ndiye mlinzi namba moja wa KATIBA ya nchi anasema ni KIJITABU.... na hakuna uwajibikaji wowote kwenye hilo (Ibara ya 26.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kufuata na kutii Katiba hii nasheria za Jamhuri ya Muungano.)
    katiba katuni 4.jpeg
  2. Bunge letu linapokea na kupitisha kwa mbwembwe miswada yote ambayo ina viashiria vyote vya kugawa maliasili zetu kwa wageni bila kuzingatia umiliki wa umma wa maliasili hizo. Nazungumzia Loliondo na maeneo mengine ambayo yanagawiwa kwa kivuli cha uwindaji na uwekezaji (Ibara ya 27.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuriya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yotei nayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia kuiheshimu maliya mtu mwingine. (2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali yamamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifuna ubadhilifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.)
    katiba katuni 2.jpeg
  3. Tumeshuhudia sakata la MoU kati ya Tanzania na Dubai kugenisha bandari zote za bara huku Bunge likipitisha kwa mbwembe mkataba huo, huku likiwakejeli wananchi wanaoukosoa na kuulalamikia, hali ilifika baadhi ya wakosoaji walibandikwa kesi ya UHAINI. Katiba imevunjwa kwa kiwango cha kutisha (Ibara ya 28.-(1) Kila raia ana wajibu wa kulinda, kuhifadhi nakudumisha uhuru, mamlaka, ardhi na umoja wa taifa.)
    dp-world-katuni-jpeg.2938510
    MoU DPW.jpeg
  4. Sheria mbalimbali zilizotungwa na Kupitishwa na Bunge ambazo zinakizana na Sehemu ya Tatu ya Katiba ya JMT (Haki na Wajibu Muhimu). Sheria za kuwawekea kinga ya kutoshtakiwa mkuu wa mhimili wa Bunge, Sheria ya Kinga ya kutoshtakiwa kwa Wanausalama, Sheria ya Makosa ya mitandao, Sheria ya Hadhi za Viongozi, Kanuni zitokanazo na MAAGIZO ya watawala kwa viongozi kwenda kwa Jeshi la Polisi, Sheria mpya ya Bima ya Afya kwa wote, Sheria ya Uchaguzi, Sheria ya Vyama vya Siasa n.k. (Ibara ya 13.-(1) Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki,bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele yasheria. (2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlakayoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambaloni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake. ).
    katuni katiba.jpeg
  5. Serikali imeshindwa kudhibiti wizi wa mali za umma. tumeshuhudia ripoti ya CAG ikianika uchotwaji mkubwa wa fedha za umma kupitia miradi mbalimbali kwenye ngazi mbalimbali lakini mkuu wa nchi amekuwa akitoa kauli za kuwakemea wahusika bila kuchukua hatua yeyote ya kulinda maadili ya umma.
  6. Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kutumika kisiasa ambapo ushahidi upo wazi kabisa. Katiba inakataza askari wetu wa vikosi VYOTE kutokuwa wanachama wa chama chochote cha siasa. Lakini ukweli upo wa askari wengi kumiliki kadi za uanachama wa Chama tawala. Jambo hili linafanyika kwa wazi bila hofu wala utii kwa Katiba (Ibara ya 147 - (3) Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga nachama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na hakiya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.)
Orodha ya mambo yanayoainisha ukiukwaji mkubwa wa sheria na Katiba ya nchi ni ndefu, lakini Katiba yetu imekosa kabisa Ukuu na Utii kwa sababu hakuna chombo chenye mamlaka ya kumhoji na kumuwajibisha MTU YEYOTE anayevunja ama kufanya makosa ya kikatiba. Katiba ya JMT inapaswa kuainishwa kila jambo muhimu kwa umuhimu wake ili kuweka ukuu, uimara na kujenga utii kwake. Taasisi za Ulinzi, Usalama na Mamala muhimu za nchi zinapaswa kuundwa kwa mujibu wa Katiba nasiyo utashi wa watu fulani ndani ya serikali.

Itapendeza sana iwapo Ofisi ya Mwandishi wa Katiba na sheria itawekwa chini ya Katibu wa Bunge ili kutimiza takwa la Kikatiba la Bunge kutunga sheria. Leo tunashuhudia wajibu wa utungaji wa Katiba na sheria vikifanywa na wale ambao sheria inapaswa kuwasimamia na kuwawajibisha kwenye utendaji wao wa kila siku serikalini.

Mpaka sasa tuna Taasisi tatu pekee nchini ambazo Kikatiba hakuna mwenye mamlaka ya kuzihoji
  1. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
  2. Baraza la Mawaziri
  3. Tume ya Uchaguzi ya Taifa
Taaisi hizi hazihojiwi kwa sababu ni turufu kubwa sana kwa chama kinachotawala bila kuzingatia Utawala Wa sheria. Ingependeza sana iwapo Tukaunda Taasisi ambazo ni imara na zinawajibika kwa Katiba ya Nchi na zinaweza kuhojiwa bila kutishia uhai na maisha ya watu ili kulinda uadilifu na utendaji wake. Haya yote hayawezekaniki kwa kwa Katiba iliyopo. Tunahitaji katiba mpya ya Wananchi.

Rais afahamu kwamba, sisi wananchi ndiyo matokeo ya yeye kuwa mkuu wa nchi, pia akumbuke kwamba yeye ni zao la jamii hiyo hiyo anayoiita kwamba haina uelewa wa Katiba na inafaa kuelimishwa. Sisi wananchi wengi tunapata mashaka sana endapo rubani wetu ana ufahamu stahiki wa Katiba ya nchi. Kauli zake zinatupa mashaka kwenye hilo

Wapo Watanzania wenzetu ambao wameamua kuweka akili na fikra zao kapuni kwa kuamini na KUTULAZIMISHA kuamini kwamba Haki na Wajibu Muhimu ni fadhila ya mkuu wa nchi kwa wananchi sisi. Lakini tunaamini sasa kuwa hazina kubwa ya thinktank wa nchi wameelemewa na upumbavu na kufilisika kwa fikra, mtazamo na hoja.

mwangosi.jpeg
Tunataka Katiba Mpya ili kukomesha matukio kama haya ya askari wetu kujitwalia sheria mkononi bila kuzingatia Katiba na Sheria


Ninaamini kwamba siyo kila mmoja anapaswa kuwa kiongozi ili kuleta mabadiliko bali Watawala wa nchi hii wamefanya eneo la uongozi kuwa DUKA LA FURSA kwa kila anayewania/ kupata nafasi hiyo.

Ni muhimu sana kuelewa kwamba; Ukimya na utulivu wa nchi yetu umejengwa kwenye UTU, UZALENDO, UPENDO na MSHIKAMANO ambavyo ni sehemu ya tunu za taifa letu hususani kwenye kujenga Taifa moja imara lenye malengo chanya. Tumeanza kupoteana kwa sababu walioshika madaraka wamejipa umungu wa nchi hii kwa kutumia vikosi halali vya Serikali kujimilikisha nchi na maamuzi yake yote. Bado nafasi ya kujisahihisha ipo na tukaanza upya. Muda utafika ambapo hizi hoja zetu zitageuka mjukuu wa majuto kwani supu ikishawekwa tui si supu tena

NB
Tuweke viwango vya utungaji wa Katiba ya Nchi yetu ambapo Mtanzania yeyote atakaye shiriki kwenye Bunge la Katiba anakubaliana na sharti la kutoshiriki uchaguzi wowote ngazi ya Ubunge ama kuteuliwa nafasi yeyote kuanzia ngazi ya Wilaya hadi Taifa kwa muda wa miaka 15 au 20. Hii itatupatia waadilifu na wenye nia safi ya kutuletea Katiba inayokidhi viwango vya Taifa letu. Hivyo hata sasa Serikali inaweza kuandaa utaratibu wa kupata Wabunge wa Bunge Maalum la Katiba bila kuathiri taratibu za Bunge la JMT linaloelekea ukingoni.


Msanii
 

Attachments

  • DP World katuni.jpeg
    DP World katuni.jpeg
    146.3 KB · Views: 3
Kwa tume kama ile ya Dr Wilsoni Mahera na Jaji Mwijage hakuna uchaguzi pale uliofanyika.....kiini macho.
Hakujawahi kuwa na TUME YA UCHAGUZI kwa mujibu wa mustakabali wa Demokrasia na Utawala Bora kwa nchi yetu. Tume inayoteuliwa imejaa makada wa chama kinachotawala nchi. Jambo hilo ni sawa na mtu mzima kufanya mambo ya kitoto hadharani mchana kweupee.

Wezi, Wauaji na Wanywa Jasho la Wanyonge ndiyo ambao wanapewa kipaumbele na vyombo vyetu vya kikatiba kuliko wananchi ambao hawajui hata kesho wataishije
 
Hakujawahi kuwa na TUME YA UCHAGUZI kwa mujibu wa mustakabali wa Demokrasia na Utawala Bora kwa nchi yetu. Tume inayoteuliwa imejaa makada wa chama kinachotawala nchi. Jambo hilo ni sawa na mtu mzima kufanya mambo ya kitoto hadharani mchana kweupee.

Wezi, Wauaji na Wanywa Jasho la Wanyonge ndiyo ambao wanapewa kipaumbele na vyombo vyetu vya kikatiba kuliko wananchi ambao hawajui hata kesho wataishije
Mpaka sahivi washindi wa hizo kata wanajulikana wanasubiri kutangazwa
 
Mama kasahau kama sio katiba asingekuwepo hapo leo1
nilifikiri angehakikisha inatungwa katiba imara ya kukidhi matakwa ya sasa ya NCHI .
 
Angalia hii, imagine huyu ni Baba mwenye familia View attachment 2939578
Ni lazima awaze hivyo mkuu.
Unadhani kuwageuza watu milioni 63+ kuwa wajinga na wapumbavu ni kazi nyepesi?

Chama ambacho hata shule zilizo chini ya jumuiya zake zimekufa vibaya, ndo kikaongoze madubwasha makubwa kama US, Urusi, Iran, China n.k?? Kuna kiongozi yeyote nchini ambaye anaamini kwenye ubunifu na uendelezaji wa ubunifu kama msingi wa maendeleo ya kisasa?
 
Mama kasahau kama sio katiba asingekuwepo hapo leo1
nilifikiri angehakikisha inatungwa katiba imara ya kukidhi matakwa ya sasa ya NCHI .
Mama inaonesha wazi anaamni kuwa ALIYEPATA AMESHAPATA HAKUNA WA KUBADILISHA....
 
Back
Top Bottom