Lowassa strikes back!

Wala sishangai Sitta ananguvu kwa sababu ya uspika wa bunge nje ya hapo hana tofauti na wakina Mwakyembe na mama Kilango na kwa sababu bunge limevunjwa inabidi arudishe majeshi nyuma unlike lowassa ambaye ni mwanzo mwisho japokua hayupo kwenye serikali bado ananguvu za ajabu
 
Jamani mbali na yote EL ana akili sana na ni mjanja kupita kiasi.
Hebu chek hiyo slogan.
Jamaa ni mbunifu sana.
 
Analysti......huo wimbo Monduli watauimba...ukitaka kujua jamii ya pale ni Kasuku nenda pale ongelea suala la ufisadi afu umtaje EL....nachelea kusema ndugu zetu wa jamii ya Wafuga Ng'ombe kwa Mtindo wa kuhama hama bado wapo nyuma sana.Samahani kwa wale niliowakwaza lakini ukweli ndo huo
 
Mi nilipata mshutuko mkubwa baada ya kuona anahojiwa na Tido! nikajua kuwa huyu bwana inawezekana anarudi kinyume nyume kwenye uongozi. Ila wa-TZ msishangae akiteuliwa kwenye wizara ya mkulu- kama atapita tena rais. japo mi natabiri maajabu. yaani
Chadema 52%
Thithiemu 39%
CUF 8%
TLP 1%
Jamani Watanzania HONGERA KWA KUBADILISHA MWELEKEO.
 
Analysti......huo wimbo Monduli watauimba...ukitaka kujua jamii ya pale ni Kasuku nenda pale ongelea suala la ufisadi afu umtaje EL....nachelea kusema ndugu zetu wa jamii ya Wafuga Ng'ombe kwa Mtindo wa kuhama hama bado wapo nyuma sana.Samahani kwa wale niliowakwaza lakini ukweli ndo huo[/QUOTE


bila samahani. mi sidhani kama wale ndugu wote ni kasuku, lakini ndo siasa, kuna ujinga na pia kuna suala la kuwa "biased" kwa "mtu" wao EL kwa makusudi, pamoja na kasoro zake..its like washabiki wa mpira na timu zao.....bias..., Tz yetu hii viongozi wasafi ni ndoto kwa sababu system inayowazaa ni chafu. ila sijui una maanisha nyuma sana ya nini kwa ni sitegemei wafugaji waachane na mfumo huo wa maisha kuja "mbele" unayofikiria wewe, its relative {kuwa nyumba -kuwa mbele}, but, well, pastoralist simply is a socio-economic system which will reproduce itself forever.
 
Huyu ndiye waziri mkuu wa 2010, pinda ameonesha kuwa si lolote si chochote na kumchagua mtu mpya ni kuongeza idadi ya mawaziri wakuu wastaafu ambao wanaligharimu Taifa billions kuwahudumia mpaka wanapofikia mwisho wa maisha yao. EL is perfect man for the job kwani hata Six amesema kuwa alishituka na kujiuzulu kwake kwa ghafla kwani ni mchapa kazi mzuri. Hii yote ni kuwaandaa watanzania kumpokea mchapakazi katika nafasi yake. You must train yourselves to let again be under Prime-ministeral of EL.
 
Wala sishangai Sitta ananguvu kwa sababu ya uspika wa bunge nje ya hapo hana tofauti na wakina Mwakyembe na mama Kilango na kwa sababu bunge limevunjwa inabidi arudishe majeshi nyuma unlike lowassa ambaye ni mwanzo mwisho japokua hayupo kwenye serikali bado ananguvu za ajabu

hahaha. umenifurahisha, ana manguvu ya ajabu. bora mchapa kazi kuliko mpole anayetupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, bora croloquine kali itakayoponya kidonda kuliko sukari tamu itakayokuletea magonjwa na kupooza....EL is far better than most of our leaders in government, including mkuu wetu....akirudi nitafurahi tu...na ninajua hatafanya makosa kwasababu ameshaonja makonzi....Naomba Mungu Pinda asifikiriwe hata kwa ndoto za usiku tu....hata karama ya uwaziri mkuu, Mungu amempa kwengine ndo aende huko, lakini hapo kwenye u pm, hayupo....Mohamed shein kule zanzibar, wameshapoteza CCM kwa kumuweka yeye, ni choice mbaya sana na hatashinda...hata kama atashinda watakuwa wameweka chaguo la mtu wa kumshika masikio kwa upande wa visiwani...atatii chochote atakachoambiwa na bara...so nasikitika kwa hilo....Mungu ibariki Tanzania.
 
Jamani naombeni mnieleweshe vizuri juu ya kauli ya Sita. Au anaongea kwa hisani ya watu wa Marekani???
 
...mzee wapinzani wa mtandawo walikuwa wamejipanga kweli kweli....na aina yoyote ya kujitetea asingeeleweka...na rais alishafanywa behind the scene ashindwe au aogope kumtetea ......so Mwanajijiji in general Taarifa za kijasusi alizopewa Lowassa kuhusu hali halisi zilimshtua sana..na zilikuwa za ghafla....ie Plan B ya kina Mwakyembe ilikuwa tishio kwa utawala mzima...

...naamini kabisa Lowassa angepata taarifa mapema ya kinachopangwa ....angekuwa waziri mkuu hadi leo ...kwani hata angepata taarifa ndani ya masaa 24 au 48 kabla ya tukio ...angekuwa na uwezo wa kubadilisha kabisa..hali ile na kuwapanga watu wa kumtetea na namna ya kujitetea au hata lolote lingeweza kutokea ......ni wazi tume ya Mwakyembe ilichomudu ni USIRI mkubwa!!!

Mwisho wa siku haya mambo yanakuwa kama story za vijiweni tu! 'Wapinzani wa Mtandao walikuwa wamejipanga kweli"! wepi hao? hawana majina? Walishindwaje kumzuia asipate Uwaziri mkuu waje kuwa na uwezo wa kumlazimisha astaafu??

Je "wapinzani hawa wa mtandao' wako wapi wakati huu ambapo anaanza kujisafisha? wanachukua hatua gani kuhakikisha kuwa Lowasa hapati kitu kama vile vile walivyoweza kumlazimisha akastaafu miaka mitatu iliyopita?

Kwa maana hiyo tuamini kwamba sababu iliyowafanya 'Wapinzani wa Mtandao' wajipange kweli kweli na hatimaye kumg'oa Lowasa madarakani miaka mitatu iliyopita sasa haina haja tena na kwa maana hiyo mmasai anaruhusiwa kurejea cheo chake na cha juu zaidi saa yoyote na kwa namna yoyote anayotaka?

'Taarifa za kijasusi alizopewa zilimshitua sana Lowasa'! Taarifa gani ambazo zilikuwa na nguvu ya kumfanya ajiuzulu wakati ule lakini leo hazina nguvu ya aogope hata kujaribu tu bahati yake ya kuwa waziri Mkuu na baadae raisi?

Huu 'usiri wa tume ya Mwakyembe', 'Wapinzani wa Mtandao' na 'taarifa za kijasusi' vilivyofanya Lowasa aachie ngazi miaka mitatu iliyopita leo havina nguvu tena kiasi kwamba vinamuangalia tu Lowasa anavyoanza kujipanga kurejesha kile alichopoteza??

Somehow, maelezo ya namna hii yanaanza kuonekana kama vile ni riwaya tu ya kusisimua ya James Hadley Chase>
 
MMMh Hapo mm chichemi kitu wooooote Mafisadi sidhani kama waziri anaweza kufanya kitu bila mkuu wa inchi kujua!wizi mtupuuuuuuuuuuuuu
 
wANA JF, NIMESHINDWA KUMWELEWA HUYU NDUGU KUWA ALIKUWA NA AKILI TIMAMU AU LA, NIMESHINDWA KUELEWA JINSI ANAVYOISIFIA RICHMIOND KAMA NDIYE YEYE KWELI ALISEMA KAONEWA. hABARI KAMILI, TIZAMA TBC1 SAA 2 NA NUSU USIKU HUU MAOJIANAO NA TIDO MUNDA YATARUSHWA LIVE. mLIOKO NYUMBANI TUJUZENI BAADA YA KUTAZAMA
NAJISIKIA UCHUNGU SANA .

mahojiano safi sana yale ..Lowassa hakuwa na kosa na amesema hata leo awe PM atalishugulikia suala la richmond vile vile ...mimi napenda viongozi jasiri wa mtindo ule ..mengine ni chuki binafsi na Lowasaa amesema historia itawahukumu...tuone sasa itakavowahukumu....
 
hahaha. umenifurahisha, ana manguvu ya ajabu. bora mchapa kazi kuliko mpole anayetupaka mafuta kwa mgongo wa chupa, bora croloquine kali itakayoponya kidonda kuliko sukari tamu itakayokuletea magonjwa na kupooza....EL is far better than most of our leaders in government, including mkuu wetu....akirudi nitafurahi tu...na ninajua hatafanya makosa kwasababu ameshaonja makonzi....Naomba Mungu Pinda asifikiriwe hata kwa ndoto za usiku tu....hata karama ya uwaziri mkuu, Mungu amempa kwengine ndo aende huko, lakini hapo kwenye u pm, hayupo....Mohamed shein kule zanzibar, wameshapoteza CCM kwa kumuweka yeye, ni choice mbaya sana na hatashinda...hata kama atashinda watakuwa wameweka chaguo la mtu wa kumshika masikio kwa upande wa visiwani...atatii chochote atakachoambiwa na bara...so nasikitika kwa hilo....Mungu ibariki Tanzania.

Tartiib kiongozi. Ingekuwa ni sifa ya utendaji hapan'shaka sote tungekuwa pamoja na EL, lakini huyu ni mwizi profesheno tena mwenye jeuri ya kidikteta - mtu wa kujisikia hasa. Halafu hapo penye red isije ikawa ni tishio kwamba safari hii hakutakuwa na kujiuzulu bali ni kushusha mikwaju kwa wanaa kulia na kushoto hadi kelele dhidi ya ufisaji zizimike zenyewe.

Sasa uchaguzi ndio hapo; tupate mtendaji wa modeli ya himiza ujenzi wa shule za sekondari za kata huku uchumi wote ukimilikishwa kwa EL na washkaji wake na watendaji wa chini wasiotaka ku-facilitate deals wakifyatishwa au tuendelee kusikiliza hekaya za mtoto wa mkulima ambaye kwake kila kitu ni "... mimi nadhani tufanye hivi... tujirudi kidogo... tuachane na suti... n.k." Kipi bora? :biggrin1:
 
yeye ndo alikuwa mmoja wapo wa watu waliokuwa wanataka jamaa ajiuzulu, sasa sijui wanatuchezea akili baada ya kukaa kikao kwamba wanatakiwa kusafishana?...watz tuna macho, tunaona jamani!
 
Tatizo la misukule wanategemea master wao awapatie ugali na kila kitu.
Hapo ndo penye tatizo.

Watu wapo tayari kuuza utu wao ilhali wamtumikie SHETANI

Hizo ndio gharama za siasa uchwara, mtu anasababisha hasara badala ya kupelekwa mbele kwene vyombo vya sheria eti anaundiwa tume na wanasarakasi wenzake...matokeo yake ndio haya wanakuja na episode 2 wakati walitakiwa wawe Ukonga hadi usawa huu.
 
mahojiano safi sana yale ..Lowassa hakuwa na kosa na amesema hata leo awe PM atalishugulikia suala la richmond vile vile ...mimi napenda viongozi jasiri wa mtindo ule ..mengine ni chuki binafsi na Lowasaa amesema historia itawahukumu...tuone sasa itakavowahukumu....

Labda nyie wafuasi wa 'shujaa Lowassa' mtuambie HASARA aliyoiingizia taifa yeye na troop lake atailipia nani?? Huo umahiri wenu wa siasa uchwara unalisaidia vp taifa??
 
Labda nyie wafuasi wa 'shujaa Lowassa' mtuambie HASARA aliyoiingizia taifa yeye na troop lake atailipia nani?? Huo umahiri wenu wa siasa uchwara unalisaidia vp taifa??

Ukisikia Boss wa MAFIA........basi ndio EL............mtandao wake ni mkubwa.........i mean kuna watu wako kwenye network yake (with big deals) hata bila kujijua.............anyone dealing with issues za EL anatakiwa awe EXTREMELY CAREFUL............FYI
 
Wadau, kwa wale waliosikiliza mahojiano kati ya Lowasa na Tido (ktk television ya taifa - TBC) na kusoma makala ya Lula ktk gazeti la Rai wiki hii wanaweza kukubaliana nami kuwa Tido Mhando anaanza kuidhalilisha hadhi aliyoipata baada ya kufanya kazi ktk shirika kubwa kama BBC. Najiuliza kwa mwanahabari aliyebobea kama Tido inakuwaje leo ashindwe kumhoji Lowasa maswali magumu kama yale aliyokuwa anawahoji viongozi wakubwa alipokuwa TBC? Yaani mahojiano yake na Lowasa huwezi hata kuyalinganisha na mtu wa kijiweni ambavyo angefanya kama angepewa fursa ya kumhoji Lowasa. Jamani, je ni kweli Tido ana njaa kiasi hicho kukubali kujidhalilisha ili awaoshe mafisadi? Si bora angepumzika tu nyumbani kuliko kukubali kuidhalilisha taaluma yake na sifa alizojipatia kwa muda mrefu baada ya kufanya kazi BBC. Ni kama vile alikuwa ameandaliwa maswali ya kumwuliza Lowasa. Na kama hii ndivyo ilivyo, kwa nini asikubali kubwaga manyanga kuliko kuchezewa hivyo??? Watanzania sijui tuna matatizo gani? Jamani Tido na wewe????

Naweka makala ya Lula hapa chini kwa wale ambao hamkufanikiwa kuisoma


Maswali ambayo Tido alishindwa kumuuliza Lowassa

lC.gif
Lula wa Ndali-Mwananzela​
Julai 21, 2010
rC.jpg

MAHOJIANO ya Mkurugenzi wa TBC Tido Mhando na aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa ambayo yalirushwa Ijumaa iliyopita yameniacha na maswali mengi zaidi kuliko majibu.
Ilipodokezwa kuwa Lowassa angefanya mahojiano na TBC nilitarajia kuwa hatimaye baadhi ya maswali ambayo nimekuwa nikijuliza kwa miaka miwili karibu na nusu yatapatiwa majibu yake. Nasikitika kusema kuwa mahojiano yale yamerudisha maswali yangu kwa ari kubwa zaidi, nguvu kubwa zaidi na kasi kubwa zaidi.
Hata hivyo, kabla ya kuangalia maswali hayo ambayo yamenikamata kama sungura alivyonaswa kwenye sanamu iliyokuwa na ulimbo, nimeona niseme mambo machache kuhusu mahojiano yale ambayo nayo pia yamenifanya nijiulize kama TBC ni kampuni tanzu ya Lowassa au vipi?
Kwa nini TBC ilimhoji Lowassa?
Siku ile ya kuvunjwa Bunge nilitarajia watu watatu wangeweza kuhojiwa katika kuonyesha umuhimu wa siku yenyewe. Nilitarajia kuwa wangeweza kumhoji Spika wa Jamhuri ya Muungano, wangeweza kumhoji Waziri Mkuu na wangeweza kumhoji Kiongozi wa Upinzani na kubwa zaidi wangeweza kumhoji Rais. Sijaelewa kwa nini walimhoji Lowassa?
TBC itakuwa ina sababu yake na naweza kuhisi bila kutumia chembe nyingi za ubongo kuwa walimhoji Lowassa kwa sababu mahojiano yake ya kwanza na TVT na Tido huyo huyo yalionekana kama yalikatishwa hewani. Kwa hiyo, uamuzi ulichukuliwa kwa makusudi kabisa wa kuendelea pale walipoachia kwani ukichukua mahojiano hayo na kuyaweka sambamba utaona kuwa mahojiano ya wiki iliyopita yalikuwa ni mwendelezo na ukamilisho tu wa mahojiano yale ya miaka miwili iliyopita.
Lakini, hata hivyo, hili bado halijibu swali la kwa nini walimhoji Lowassa kwa sababu hakuwa na jambo lolote jipya la kusema zaidi ya kurudia utetezi wake ule ule wa 2008.
Serikali imelegalega baada ya Lowassa kuondoka?
Maswali ya awali ya Tido kwa Lowassa yalikuwa yanalenga kuwa Serikali imeyumbayumba na kulegalega baada ya Lowassa kuondoka.
Tido alipomuuliza Lowassa juu ya kupungua kwa msukumo katika masuala ya ujenzi wa shule za sekondari Lowassa akicheka kidogo alisema tu kuwa “sijui msukumo umepungua kwa kiasi gani”.
Kwa maneno mengine Tido na Lowassa walikuwa wanakubaliana kuwa msukumo wa utekelezaji umepungua, walichotofautiana ni kwa kiasi gani, kwani Tido alisema “sana” na Lowassa hakutaka kutumia neno hilo “sana”.
Hili ni muhimu kujua kwa sababu Lowassa alizungumza baada ya Waziri Mkuu wa sasa kuhojiwa. Sijui kwa nini Tido hakutaka kupata maelezo kutoka kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kujua kama msukumo umepungua au la. Kwa nini alimuuliza Lowassa?
Haya niyaache hayo wanajuana wenyewe. Hata hivyo, kuna maswali ambayo Tido alitakiwa kumuuliza Lowassa ili kuonyesha angalau chembe ya weledi. Hili ni muhimu hasa ukizingatia kuwa katika mazungumzo yao hayo Lowassa alituhumu kuwa waandishi hawana weledi na kujaribu kujenga hoja kuwa waandishi wakipata digrii basi kusajiliwa basi watakuwa ni waandishi wazuri. Kana kwamba wahasibu wote wenye CPA na waliosajiliwa ni waaminifu kwenye taaluma zao au mawakili wote ni waaminifu kwa viapo vyao! Kumbe mtu anaweza akawa na kabati la vyeti vya taaluma lakini akawa ni fisadi numero uno!
Sasa nilitarajia kuwa Tido angeweza kumuuliza maswali ambayo tumekuwa tukiyauliza kwa miaka miwili kila Lowassa anapozungumzia suala la kuonewa kwake na Kamati Teule ya Bunge. Nilitarajia Tido angeweza kumuuliza maswali ambayo majibu yake yangetupa mwanga kuelewa mawazo ya Lowassa hadi kujiuzulu yalikuwa ni ni hasa. Baadhi ya maswali hayo ni haya:
Lowassa alipata wapi madaraka ya kuingilia mchakato wa utoaji tenda kwenye taasisi ya Serikali, TANESCO? Na ni sheria gani iliyompa nguvu hiyo? Jibu lake la kuwa “ilikuwa ni dharura” halitoshi kwa sababu kama kweli kulikuwa na dharura ni Rais tu ndiye mwenye uwezo wa kutangaza hali ya dharura. Lowassa alipata wapi haki ya kutangaza hali ya dharura na kuchukua hatua za kusimamisha sheria mbalimbali?
Ni kwa nini hakujiridhisha yeye mwenyewe juu ya uwezo wa kampuni ya Richmond kuleta umeme badala ya kuwategemea watu wengine ukizingatia kuwa ni yeye ndiye aliyeunda kamati nje ya utaratibu wa kisheria wa zabuni?
Kwa nini hakujitetea mbele ya Bunge. Baada ya Lowassa kuomba nafasi ya kuzungumza kufuatia maneno makali ya Bunge siku moja kabla, nilitarajia kuwa hatimaye angeweza kujibu hoja mbalimbali za wabunge. Lakini aliposimama asubuhi ile Lowassa aliamua kubwaga manyanga chini. Hakujaribu hata kidogo kuelezea upande wake kwenye chombo sahihi ambacho kilipitisha uteuzi wake kwa kauli moja. Kwa nini hakujitetea?
Kwa nini hakuomba Bunge liahirishwe ili apate nafasi ya kujipanga kutoa majibu ya tuhuma mbalimbali. Waziri Mkuu ana kipaumbele bungeni. Baada ya madongo mengi kurushwa Lowassa angeweza kuomba Bunge liahirishwe kwa muda ili aandae majibu yake kwa Bunge. Kutokana na uzito wa hoja zile siwezi kuona jinsi gani Spika angeweza kumkatalia kumpa nafasi hiyo. Nina uhakika wa asilimia 100 kuwa endapo Lowassa angeomba muda wa kuandaa majibu angepewa. Kwa nini hakufanya hivyo?
Kwa nini anaamini kuwa hakupewa nafasi ya kujitetea wakati Kamati Teule haikutoa hukumu yoyote kwake? Hili ni muhimu kwangu kutaka kulielewa kwa sababu nina uhakika kuwa Lowassa anajua kuwa “haki ya asili” ya kujitetea inahusiana na hukumu na si tuhuma.
Mtu mtu akikamatwa na Polisi, ukishakusanywa ushahidi na kesi kupelekwa kwa mwendesha mashtaka hawezi kuinuka na kusema kuwa “mbona hamkunihoji”. Watu watamshangaa. Ila kama mahakama itapokea ushahidi huo na tuhuma hizo halafu kutoa hukumu dhidi ya mtu huyo bila ya kumpa nafasi ya kumsikiliza basi itakuwa imemnyima haki yake ya msingi ya asili, ile ya kusikilizwa.
Lakini Lowassa hakuhukumiwa na Kamati Teule kwani Kamati Teule kisheria haiwezi kupitisha hukumu yoyote bali inaweza kutoa mapendekezo kwa Bunge. Na sote tunajua kuwa Kamati Teule ilimpa nafasi Waziri Mkuu kujipima kutokana na uzito wa tuhuma hizo na kuchukua uamuzi unaofaa. Alikuwa na uwezo wa mambo mengi ya kuweza kufanya, kwa nini alichagua la kujiuzulu badala ya kujitetea?
Kama kweli Lowassa anaamini kuwa hakutendewa haki na Bunge kwa nini hakuleta hoja bungeni kama Mbunge anayeelewa wajibu wake na kutaka uchunguzi mpya ufanyike au kuwalazimisha Kamati Teule kuweka ushahidi wao dhidi yake hadharani ili kuona kama kweli alihusika na sakata la Richmond au la? Kinyume chake aliamua kuzungumza baada ya Bunge kuvunjwa? Haoni kwamba kwa kufanya hivyo ni kujionyesha kuwa hakuwa anajiamini mbele ya Bunge?
Pamoja na maswali hayo binafsi ningependa kujua kama TBC ina mpango wa kutoa nafasi kwa Spika au mjumbe yeyote wa iliyokuwa Kamati Teule kuweza na wenyewe kuelezea upande wao kwa mtindo ule ule uliofanywa kwa Lowassa?
Vinginevyo kama vile Lowassa alivyojiuzulu kwa kutumia madaraka yake vibaya (hata kama hakubali) naamin Tido Mhando naye ametumia nafasi yake ya Ukurugenzi wa TBC vibaya na kwa sababu hiyo natoa pendekezo na yeye afuate njia aliyoifuata Lowassa; ajiuzulu ampishe Mtanzania mwingine ambaye hataonekana kama anatumika kubeba viongozi au watendaji ambao wamefunikwa na wingu la tuhuma.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom