Anna Nkya

Member
Oct 21, 2021
69
341
Jana Lema alikuwa Serena Hoteli kwenye mjadala uliohusu uwekezaji kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo bandari. Alikuwa pale na kina Mzee Ulimwengu, Rostam Aziz, Wasira na watu wengu wengine. Kwenye meza yake, Lema alikaa na Zito Kabwe na watu wengine mashuhuri.

Lema alipochangia, alianza kwa kutete kauli ya Mbowe ambayo baadhi ya watu wameitafsiri kama ubaguzi. Lema hakupindisha maneno kusema kwamba watu wanatumia kauli za Mbowe kukwepesha mada.

Kuhusu uwekezaji unaotaka kufanyika bandarini, Lema alionekana wazi kwamba anaunga mkono uamuzi wa kuleta wawekezaji katika bandari ya Dar es Salaam. Baadhi ya kauli za Lema zinazodhibitisha hilo;

1. "Nchi hii inahitaji muwekezaji zaidi Bandarini"

2. "Hakuna mtu anakataa uwekezaji, na hakuna namna Tanzania inaweza ikasurvive bila uwekezaji"

3. "Kukataa uwekezaji ni jambo baya sana"

Kisha Lema alichangia kwamba mkataba unaotarajiwa kuipa DP World kazi, ni vyema ukatazamwa na kuboreshwa.

Alitolea mfano wa vifungu vinavyodaiwa kwamba vitaipa DP World bandari zote za Tanzania, lakini alieleweshwa kwamba haiko hivyo; DP World wanapewa baadhi ya maeneo ya bandari ya Dar es Salaam na hawawezi kwenda kwenye bandari nyingine mpaka pale Mamlaka ya bandari Tanzania itakapojiridhisha na kuchagua maeneo tunayohitaji uwekezaji zaidi.
 
Lema ameishia la saba

Yeye anasimama sehem ambayo watampa pesa

Inawezekana lema alishakula pesa za waarabu siku nyingi
 
Kupitia mjadala kuhusu umuhimu wa wawekezaji na ushirikiano wa kimataifa Godbless Lema alitoa mchango wake ambao umeleta matumaini mapya kwa watanzania waliokuwa hawaamini katika uwekezaji.

Godbless Lema alisema kuwa "Tanzania haiwezi kuendelea bila kushirikiana na makampuni kutoka nje ya nchi. Ila muhimu kuangalia wanaokuja kuwekeza. Marekebisho madogo yafanywe ili kuondoa mashaka kwa wananchi.”

lakini pia aliongeza kuwa “Sio dhambi kuleta mwekezaji kwenye nchi na nchi haiwezi kukwepa suala hilo. Dunia yote inafanya kazi na makampuni makubwa. Nchi hii inahitaji wawekezaji wengi.”

Vilevile alitoa ushauri kuwa “Mimi ushauri wangu, Nchi hii inahitaji muwekezaji zaidi ya bandarini.

Hii inathitisha kuwa kupitia uwekezaji unatarajiwa kufanyika katika Bandari na kampuni ya DP WORD watanzania tutanufaika sana na uwekezaji huu maana ufanisi wa bandari utaongezeka zaidi.
 
Lema naona kakataa hela za wakenya waliofanikisha kumtoroshea Canada.

Safi Lema huo ndo uzalendo
 
Wanaobeza wawekezaji Nchini niwale watu waliokosa EXPOSURE.
 

Attachments

  • VID-20230620-WA0252(1).mp4
    14.5 MB
Back
Top Bottom