Nyakijooga
Senior Member
- Dec 9, 2018
- 123
- 202
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (#EWURA) imetangaza bei kikomo za Mafuta ya Petroli zitakazotumika kuanzia Desemba 6, 2023 ambapo Dar es Salaam Petroli ni Tsh. 3,158, Tanga Tsh. 3,204 na Mtwara Tsh. 3,231 kwa Lita moja ya Mafuta
Dizeli Dar es Salaam itauzwa kwa Tsh. 3,226, Tanga Tsh. 3,377 na Mtwara Tsh. 3,546. Mafuta ya Taa yamesalia kwenye bei za Novemba ambazo ni Tsh. 3,423 kwa Dar, Tanga Tsh. 3469 na Mtwara Ths. 3,495 kwa Lita moja ya Mafuta
Bei hiyo imekuja siku chache tokea Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) ilipotangaza mabadiliko ya nauli katika safari za masafa marefu na masafa mafupi ikielezwa kuwa ni baada ya kupitia maoni ya wadau wa usafiri nchini.
Kwa mujibu wa LATRA nauli za safari zisizozidi kilometa 10 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 500 kuwa itakuwa 600. Kwa safari za kilometa 11 hadi 15 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 550 sasa itakuwa shilingi 700.
Kwa kilometa 15 hadi 20 ambapo nauli ilikuwa shilingi 600 sasa itakuwa 800 huku kwa safari za kilometa 21 hadi 25 nauli imetoka 700 hadi shilingi 900. Safari ya kilometa 26 hadi 30 nauli ni shilingi 1100, safari ya kilometa 31 hadi 35 ni shilingi 1300 na kilometa 36 hadi 40 nauli ni 1400.
Mabadiliko ya Bei yaligusa pia safari za umbali mrefu mfano kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza, Morogoro pamoja na mikoa mingine.
Kutokana kushuka kwa bei ya nishati hiyo ambayo imekuwa ikitajwa wazi kuchangia ongezeko la bei za nauli kuna haja ya LATRA kutafakari upya mchakato uamuzi wa bei mpya zilizopangwa kuanza kutumika Desemba 8, 2023, au wananchi waelezwe wazi sababu nyingine za kubakia na bei hiyo.
Kama imetokea unafuu kidog wa bei za nishati ya mafuta kushuka hatuna budi kuwaondolea mzigo wa nauli wananchi kutokana na hali ya maisha ilivyo. Kama Serikali imewai kuweka ruzuku ili kupunguza makali ya bei ya mafuta ili kuepusha athari zaidi ambazo zingewapata wananchi mfano kupanda kwa nauli, basi LATRA nao wakiwa kama taasisi ya Serikali hawana budi kuliona hili kusimama upande wa Wananchi katika usawa.
Pia soma > LATRA yatangaza ongezeko la nauli za Safari za Masafa Marefu na Mafupi kuanzia Desemba 8, 2023
Dizeli Dar es Salaam itauzwa kwa Tsh. 3,226, Tanga Tsh. 3,377 na Mtwara Tsh. 3,546. Mafuta ya Taa yamesalia kwenye bei za Novemba ambazo ni Tsh. 3,423 kwa Dar, Tanga Tsh. 3469 na Mtwara Ths. 3,495 kwa Lita moja ya Mafuta
Bei hiyo imekuja siku chache tokea Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) ilipotangaza mabadiliko ya nauli katika safari za masafa marefu na masafa mafupi ikielezwa kuwa ni baada ya kupitia maoni ya wadau wa usafiri nchini.
Kwa mujibu wa LATRA nauli za safari zisizozidi kilometa 10 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 500 kuwa itakuwa 600. Kwa safari za kilometa 11 hadi 15 ambayo nauli yake ilikuwa shilingi 550 sasa itakuwa shilingi 700.
Kwa kilometa 15 hadi 20 ambapo nauli ilikuwa shilingi 600 sasa itakuwa 800 huku kwa safari za kilometa 21 hadi 25 nauli imetoka 700 hadi shilingi 900. Safari ya kilometa 26 hadi 30 nauli ni shilingi 1100, safari ya kilometa 31 hadi 35 ni shilingi 1300 na kilometa 36 hadi 40 nauli ni 1400.
Mabadiliko ya Bei yaligusa pia safari za umbali mrefu mfano kutoka Dar es salaam kwenda Mwanza, Morogoro pamoja na mikoa mingine.
Kutokana kushuka kwa bei ya nishati hiyo ambayo imekuwa ikitajwa wazi kuchangia ongezeko la bei za nauli kuna haja ya LATRA kutafakari upya mchakato uamuzi wa bei mpya zilizopangwa kuanza kutumika Desemba 8, 2023, au wananchi waelezwe wazi sababu nyingine za kubakia na bei hiyo.
Kama imetokea unafuu kidog wa bei za nishati ya mafuta kushuka hatuna budi kuwaondolea mzigo wa nauli wananchi kutokana na hali ya maisha ilivyo. Kama Serikali imewai kuweka ruzuku ili kupunguza makali ya bei ya mafuta ili kuepusha athari zaidi ambazo zingewapata wananchi mfano kupanda kwa nauli, basi LATRA nao wakiwa kama taasisi ya Serikali hawana budi kuliona hili kusimama upande wa Wananchi katika usawa.
Pia soma > LATRA yatangaza ongezeko la nauli za Safari za Masafa Marefu na Mafupi kuanzia Desemba 8, 2023