Kyela 2010: Mwakyembe Vs Mwakalinga kupitia CCM

Malafyale

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
13,813
11,126
George Mwakalinga mwana Kyela aliyekuwa anaishi na kufanya kazi kama mtaalaum wa kompyuta nchini UK amewasili Kyela majuzi na tayari ametangaza kuwania ubunge wa wilaya ya Kyela ndani ya CCM!

Mwakalinga ametoka kuongea na wana Kyela sasa hivi kwenye hotel ya kisasa ya Sativa na watu waliokuwepo hapo wanasema hapana shaka Mwakalinga kaletwa Kyela na vigogo ndani ya CCM na serikalini na dhahiri anaungwa mkono na mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mzee Mwakalinga na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Japhet Mwakasumi!

Kwa mujibu wa habari za watu wa Kyela,kama uchaguzi wa kura za maoni ndani ya CCM utafanyila leo kwenye kata 15 zinazounda wilaya hiyo, Mwakalinga na Dr Mwakyembe watashinda kata 6 kila mmoja na kata 3 zikiwa ni "swing states".

Kata ya Kyela mjini,kata ya Matema na kata ya Ngonga sehemu ambapo wana siasa hawa wanapotokea ndiyo kata pekee za"swing states"lkn kata ya Kyela mjini ikianza kuegemea upande wa Mwakalinga na kumpa sasa likely kama anaongoza kwa kata 7 kwa 6 za Dr Mwakyembe!

Bila ubishi kata ya Ikolo,kata ya kajunjumele,kata ya Katumba Songwe,na kata 3 za mashariki ya Kyela hizo zitachukuliwa na Dr Mwakyembe ili hali kata ya Ipinda,kata ya Lusungu,kata ya Makwale na kata 3 kuzunguka upande wa Magharibi hasa kuanzia mpakani mwa Kasumulu na mgodi wa Kiwira zitachukuliwa na Mwakalinga kwa kile wanachosema Dr Mwakyembe kashindwa kazi ya kuwasadia wahanga waliofukuzwa kazi kwenye mgodi huo na vijiji jirani!

Mwakalinga,ambae pia ana vitege uchumi vingi sana wilayani Kyela zikiwemo hotel kubwa za kisasa tayari yupo Kyela,na kaanza kuzunguka kwa kasi vijijini kujinadi kwa wana CCM na kuna kila ukweli kuwa viongozi wa CCM wilayani na mkoani wamebariki kuanza huku kwake kampeni kabla ya muda wake.

Juhudi zinafanywa ili mazungumzo ya Mwakalinga akiwa kyela ambako tayari sasa kafanya ndiyo makazi yake yapatikane na yaletwe hapa ili wana JF wayachambue!
 
Last edited by a moderator:
Habari yako ni nzito Mkuu Malafyale....Tunangoja kwa hamu Taarifa za Ndugu Mwakalinga kuhusu kujitosa kwake katika Kinyang'anyiro cha Ubunge wa Kyela....Bwana Mwakalinga ni Mwanachama Mwandamizi hapa....Licha ya Taarifa yako,nafikiri pia nae atakuja mwenyewe kutoa maelezo kuhusu azma yake hiyo ya kuutaka Ubunge wa Kyela!!

Kazi ni Nzito,Lakini ni wananchi wa Kyela ndio wenye Maamuzi ya mwisho ya Mtu wanayemtaka kuwa Muwakilishi wao Bungeni....Mwakalinga kama Alivyo Dr.Mwakyembe ni wana-kyela wakereketwa na watu wanaojulikana sana katika maeneo hayo....... Joto la Uchaguzi limeshaanza kupanda katika kila kona ya Nchi.Ni wazi kuwa Uchaguzi wa Oktoba 2010 utakuwa una Ushindani Mkubwa,katika Majimbo mengi!
 
What is so big with this UBUNGE!

Will this Mwakalinga be so different mpaka tuanze kumjadili hapa! Angalau Mwakyembe tunamjua (alimtoa Lowasa nk!) Sasa huyo Mwakalinga wako, ni hili la kuwa anatoka UK na kuwa anamiliki hoteli!

Hivi jimbo ni Kyela tu! What is so special with Kyela! Si anaweza kugombea sehemu nyingine ya Tanzania na akashinda tu, kama ubunge ndio maisha!

Please, there are better things to discuss than this!
 
Mwakalinga ameisha shindwa kabla hata ya uchaguzi! Hana sera zaidi ya kuwa na kajihoteli huko, kuweni makini wana Kyela hawa mamluki watakuja na njia nyingi, usiache kusoma ule mwongozo ulotolewa na Kanisa!
 
Mkuu Mwawado unaweza kutupatia dondoo zaidi juu ya wasifu wa Bwana Mwakalinga? Maelezo yako yanaonyesha kwamba unamfahamu vizuri. Japo si vyema kutoa maoni hasa kwa mtu ambaye unamfahamu, lakini siyo vibaya ukatumegea japo kidogo ili tujue mwanachama mwenzetu ambaye ameamua kujitosa kwenda kuomba kazi ya kuwatumikia wananchi.

Mtanzania yuko wapi? Mtanzania ni mtu muhimu sana kwa kuwa yeye huwa ni mwepesi wa kuwakumbusha wanachama ambao wakiwa hapa jukwaani/jamvini huonyesha kukerwa sana na ubovu wa utendaji wa serikali na Bunge, lakini wakishaingia Mjengoni ama wakiteuliwa kuwa watendaji huwa wanabadilika ghafla na kuwa wabovu kuliko hata wale aliokuwa akiwashambulia.

Ujumbe kwa Mtanzania: Kwa kuwa nawe ni mzawa wa Kyela tunaomba utuwakilishe wapiga debe wako wa hapa JF ili ukaongeze ushindani kwenye kinyang'anyiro hicho labda tunaweza kupata viongozi wazuri.
 
Mwakalinga ameisha shindwa kabla hata ya uchaguzi! Hana sera zaidi ya kuwa na kajihoteli huko, kuweni makini wana Kyela hawa mamluki watakuja na njia nyingi, usiache kusoma ulw mwongozo ulotolewa na Kanisa!

Mwakyembe kishachemka aachie damu mbichi. George ni injini muhimu ya maendeleo ya Kyela .
 
Kumbe kampeni za uchaguzi wa ubunge ndani ya ccm zimeshaanza, au nimesoma hiyo habari vibaya vile! Naona huyu keshashindwa hata kabla ya kuingiza mguu katika hatua zake. Nampa pole
 
Mwakyembe kishachemka aachie damu mbichi. George ni njini mhimu ya maendeleo ya kyela .

MkamaP,

Tuongezee basi wasifu wake ili tujue huo u-engine wake wa maendeleo ukoje?

Tatizo linaweza kuwa mfumo wa CCM na serikali yake. Kama hawa wabunge wanaochaguliwa kupitia CCM wangekuwa siyo vigeugeu sasa hivi tungekuwa mbali sana. Wakishaingia huko mjengoni wanakuwa corrupted, mwisho wa siku hata kama mtu alikuwa na mawazo ya kimaendeleo anabaki kuwa mtu wa kulalamika kimya kimya ama kukaa kimya kabisa.

Wakati mwingine kuwa mbunge kupitia CCM haina tofauti na kuwa mwana JF, maana inawezekana ukawa unakerwa na mambo yanavyokwenda huko mjengoni lakini ukawa huna mahali pa kusemea na ukabaki kimya na kuwaachia majukwaa watu kama akina Serukamba.
 
Kumbe kampeni za uchaguzi wa ubunge ndani ya ccm zimeshaanza, au nimesoma hiyo habari vibaya vile! Naona huyu keshashindwa hata kabla ya kuingiza mguu katika hatua zake. Nampa pole

Kwani hujawasikia akina Mama Shelukindo wanalalamika Bungeni kwamba kuna watu wanajipitisha pitisha huko majimboni kwao, wanatafuta nini? Ama mtu kuwa Waziri/Naibu Waziri ni lazima aende Jimbo fulani kila wiki? Ama kwenye hayo majimbo ndiko kuna matatizo ambayo yanamhitaji waziri/naibu waziri awepo kila wiki?

Mbaya zaidi mpaka siku za weekends baadhi ya mawaziri wanaonekana wakijivinjari na magari ya serikali, kwa kutumia posho za serikali, mafuta ya serikali na kila kitu cha serikali. Ikifika wakati rasmi wa kampeni serikali inakuwa ilisha gharimia kampeni yake kwa 90%, yeye anaongezea 10% na anabeba jimbo kilaini. Hii ndiyo Tanzania bana.

Kampeni huwa zinaanza uchaguzi unapoisha, kuna wengine walianza kampeni tangu 2006.
 
MkamaP,

Tuongezee basi wasifu wake ili tujue huo u-engine wake wa maendeleo ukoje?

Tatizo linaweza kuwa mfumo wa CCM na serikali yake. Kama hawa wabunge wanaochaguliwa kupitia CCM wangekuwa siyo vigeugeu sasa hivi tungekuwa mbali sana. Wakishaingia huko mjengoni wanakuwa corrupted, mwisho wa siku hata kama mtu alikuwa na mawazo ya kimaendeleo anabaki kuwa mtu wa kulalamika kimya kimya ama kukaa kimya kabisa.

Wakati mwingine kuwa mbunge kupitia CCM haina tofauti na kuwa mwana JF, maana inawezekana ukawa unakerwa na mambo yanavyokwenda huko mjengoni lakini ukawa huna mahali pa kusemea na ukabaki kimya na kuwaachia majukwaa watu kama akina Serukamba.

Hao wanaosemea chinichini ni hurka yao ,hawafungamani ndivyo walivyo, kwani wakati mwakyembe anamsema Lowasa alikuwa mbunge wa chadema kwa wakati huo.?

Hao wanaoshindwa kuwakilisha jamii yao iliyowatuma ndivyo walivyo ni mafisadi kwa asili yao ila walikuwa hawana mahala pa kufisadi ,wala haitegemi katoka chama gani.

kuna msemo unasema ukitaka kujuwa tabia ya mtu mpe fedha.Hao unaofikiri wanabweka wanapokuwa upinzani ,huwezi juwa wanabweka kwa sababu gani na vigezo vipi.usipate kujiridhisha kwa mbweko huo kuna siku wata kudisapointi mpaka ushangae.

Hivi wewe unafikiri Simba anapokuwa na nyumbu wake/swala akijipatia kitoeo harafu fisi wamemzunguka wakibweka wewe unafikiri wale fisi wanambwekea simba eti ya kwamba simba anamwonea yule nyumbu/swala.?

Mchungaji mwema ni yule anayebeba mkuki na kukutana na simba ktk uwanja wa mapambano ana kwa ana .
 
katumwa huyo na mafisadi yanayomwona Mwakyembe mkuki. Kwa mtu kama Mwakyembe anakubalika sehemu nyingi Tanzania tokana na mchango wake kuonekana kwa Watanzania wengi si wana Kyela tu. Mwakyembe anaweza kugombea popote na kwa chama chochote na akashinda. Na ingekuwa busara Mwakyembe aachane na CCM ajiunge na CUF ama Chadema na agombee hapo hapo Kyela na bado atashinda kwa kura nyingi sana.

Huyu Mwakalinga alikuwa mtaalamu wa computer UK?, sehemu gani?, kampuni gani na lini?. Aliacha biashara zake Kyela (mahoteli) na kwenda UK kufanya kazi za computer?. Hapa kuna utata kidogo.
 
Mkuu Mwawado unaweza kutupatia dondoo zaidi juu ya wasifu wa Bwana Mwakalinga? Maelezo yako yanaonyesha kwamba unamfahamu vizuri. Japo si vyema kutoa maoni hasa kwa mtu ambaye unamfahamu, lakini siyo vibaya ukatumegea japo kidogo ili tujue mwanachama mwenzetu ambaye ameamua kujitosa kwenda kuomba kazi ya kuwatumikia wananchi.

Mtanzania yuko wapi? Mtanzania ni mtu muhimu sana kwa kuwa yeye huwa ni mwepesi wa kuwakumbusha wanachama ambao wakiwa hapa jukwaani/jamvini huonyesha kukerwa sana na ubovu wa utendaji wa serikali na Bunge, lakini wakishaingia Mjengoni ama wakiteuliwa kuwa watendaji huwa wanabadilika ghafla na kuwa wabovu kuliko hata wale aliokuwa akiwashambulia.

Ujumbe kwa Mtanzania: Kwa kuwa nawe ni mzawa wa Kyela tunaomba utuwakilishe wapiga debe wako wa hapa JF ili ukaongeze ushindani kwenye kinyang'anyiro hicho labda tunaweza kupata viongozi wazuri.
Keil,
Hapo umegonga musumari ku kichwa. Tumsubiri Mtanzania aje hapa atupe data.
 
Kwani uko UK alikuwa anasomea ana anafanya kazi zinazoendana na ubunge? Nadhani tanzani ina wanasiasa wa kutosha kabisa. sasa tunahitaji wazalishaji na wato huduma kwa wanachi. Kila msomi anatajifanya anataka kusaidia wanachi.

Na ikiwezekana serikali iangali uwezekano wa ku export watu wanaopenda kuwa wanasiasa nchi jirani. Maana tunaweza kujukuta kwenye vita sababu tu mtu fulani anadhani kiti fulani cha kisiasa ni chake.

Tuliimba kilimo ni uti wa mongo lakini sasa naona uti wa mngongo wa kilimo umeshazeeka na kupinda. Kwa kasi hii inaonyesha sasa tuko kwenye kizazi cha siasa ndio uti wa mgongo wa tanzania. Wazee wa NEC wanataka kufanya watotot wao na wajukuu zao waingie kwenye NEC. Vyama mbadala na vyenyewe hatusikiaa vikionglea sera zao zinazoweza kutekelezeka za teknolojia , sayansi.

Na lile swali Nyerere alilowai kuwahoji watu kuhusu mbio za kwenda ikulu kuna kitu gani inabidi tuaze kuwahoji wabunge.

Zaidi ya hapo kama kweli mtu anahitaji kuwasadiai wanachi kwa nini hatuwasikii hawa wakigomgea udiwani . manake atleat udiwani ndio kwenye grass root wanakoweza kukutana na kero halisi za wananchi na si unbinge amabcho ni kijiwe tu.
 
Huyu alikuwa ni mwenzetu humu na ameamua kufanya alivyokuwa akipreach

kilichobaki ni kuanzisha blog awe ana tupdate


safi sana kamanda
 
katumwa huyo na mafisadi yanayomwona Mwakyembe mkuki. Kwa mtu kama Mwakyembe anakubalika sehemu nyingi Tanzania tokana na mchango wake kuonekana kwa Watanzania wengi si wana Kyela tu. Mwakyembe anaweza kugombea popote na kwa chama chochote na akashinda. Na ingekuwa busara Mwakyembe aachane na CCM ajiunge na CUF ama Chadema na agombee hapo hapo Kyela na bado atashinda kwa kura nyingi sana.

Huyu Mwakalinga alikuwa mtaalamu wa computer UK?, sehemu gani?, kampuni gani na lini?. Aliacha biashara zake Kyela (mahoteli) na kwenda UK kufanya kazi za computer?. Hapa kuna utata kidogo.

teh teh teh
Mwakyembe Cuf sidhani kama watampokea kwa ile recomendesheni yake kuwa Maalim Seif akamatwe na apewe kesi ya uhaini,na hapohapo jamaa akapata ubunge ktk afrika mashariki duuu.

Kifupi huyu jamaa yani mwakyembe ni opotunisti mzuri kipindi hicho alikitumia barbara na aka ukwaa ukwasi na saizi kaona watanzania wameegemea wapi katumia tena staili ile ile ya ufisadi kukonga nyoyo za wadanganyika.

swali ni je huko kyelya kwenye jimbo lake kafanya nini, sana sana alichofanikiwa sana na vurugu kuongozeka jimboni kwake.
 
What is so big with this UBUNGE!

Will this Mwakalinga be so different mpaka tuanze kumjadili hapa! Angalau Mwakyembe tunamjua (alimtoa Lowasa nk!) Sasa huyo Mwakalinga wako, ni hili la kuwa anatoka UK na kuwa anamiliki hoteli!

Hivi jimbo ni Kyela tu! What is so special with Kyela! Si anaweza kugombea sehemu nyingine ya Tanzania na akashinda tu, kama ubunge ndio maisha!

Please, there are better things to discuss than this!

Mwakalinga ni mwenzetu hapa JF kwa muda mrefu,michango yake ni muhimu sana amekuwa hakosi kuwepo hapa kila siku masaa karibu 18 kwa siku.
ana exposure kubwa sana akiingia bungeni hata wabunge wengine watanufaika na Mwakalinga ambaye kwake Utaifa ni mbele kwa kila kitu.
Mwakalinga Utanzania umemjaa kuliko Ukyela.

naomba wote tumuunge mkono kama hapa kijiweni kwake tunaanza kumuombea mabaya nani atamsupport?

Mwalimu Nyerere mwaka 1995 alipiga kampeni nchi nzima isipokuwa Arusha Mjini. alipofika Arusha akasema kuwa pale anagombea mtoto wake-Makongoro Nyerere hata kama wako vyama tofauti hawezi kwenda kumpinga mtoto wake jimboni Arusha mjini.kama kuna mtu anaweza kuniambia tofauti aje hapa.

tufanye uzalendo kama wa Nyerere kwa kumsupport mwenzetu.
Mwakalinga hata michango tutakupa.kwetu sisi wewe ni bora mara elfu kwa Mwakyembe.
 
Mwakalinga ni mwenzetu hapa JF kwa muda mrefu,michango yake ni muhimu sana amekuwa hakosi kuwepo hapa kila siku masaa karibu 18 kwa siku.
Sio sababu ya yeye tumuunge mkono....wekeni ID yake tumsome.....
ana exposure kubwa sana akiingia bungeni hata wabunge wengine watanufaika na Mwakalinga ambaye kwake Utaifa ni mbele kwa kila kitu.
exposure ipi alionayo? nasikia nae ni mtaalam wa kompyuta aliekuwa anaishi UK wale wale........mkuu tuambie ana exposure gani kuliko daktari mwakyembe?
Mwakalinga hata michango tutakupa.kwetu sisi wewe ni bora mara elfu kwa Mwakyembe.
mkuu hueleweki ni nini mapungufu ya mwakyembe ambayo mwakalingazi atayafunika? taja mapungufu ya mwakyembe.......
 
Back
Top Bottom