Kwanini Nyerere hakumkubali Lowassa?

Mtafute mzee Kisori ndo atakuambia ukweli kama Nyerere alimkubali Edward au la sio unaleta bla bla.Mzee Kisori amefanya kazi na Nyerere kwa muda mrefu.
 
Kweli nimeamini fedha inanguvu ya kubomoa milima Lowassa yupi anaependwa na Mwl Nyerere ni yule alinyimwa fursa ya kugombea urais mwaka 1995 au mwingine.Tafuta watoto wadogo wa kudanganywa.
 
Mwaka 1995 katika kinyanganyirocha urais tz yalijitokeza majina 17 ya wanaccm waliotaka kupitishwa na chamahicho. Mmoja kati ya wagombea hao alikuwa ni ndg edward ngoyai lowassa aka laighwanan wakati huo wakati huo akiwakijana wa miaka 42. Mwalimu alijua fika kwamba lowassa ni fisadi mkubwa na kamailivyokuwa kwa mwalimu daima hakumungunya maneno na mbele ya kamati kuuakatamka kuwa lowassa na malecela wakipitishwa yeye anarudisha kadi yake ya ccmno.

1. Majina hayo yakakatwa fasta!!Mwaka 2005 malecela kwa kujuanyerere kaishafariki hivyo njia kwake ni nyeupe akatia timu tena mbele yakamati kuu bila kujua kuwa minutes za kamati kuu za 1995 bado zipo!! Matokeoyake mzee mzima akaangukia pua mbele ya kamati kuu!!Rais J.m. Kikwete alipuuza usiawa baba wa taifa na kumteua lowassa kuwa waziri mkuu wa tz.

Matokeo yake yakutotii usia wa baba wa taifa, lowassa akaweka rekodi ya kuwa waziri mkuualiyekaa kipindi kifupi kuliko wote.lowassa sasa eti anataka kuwarais wa tz!!! Kamati kuu minutes za 1995 bado zipo na kama kwa kamati kuu kutumiarushwa lo-rushwa kumpitisha lowassa basi laana ya nyerere itawatafuna wajumbewoote wa kamati kuu na nchi nzima italaanika!!



MSOME KATIBU WA MWALIMU NYERERE
MZEE SAMWELI KASORI

AKISIMULIA JUU YA MAHUSIANO YA MWL NYERERE NA LOWASSA....Mfuatilie

Kwa mapenzi mema na nchi yetu na mwana (CCM) napenda niwape mfano hai wa Bwana Lowasa asivyo muadilifu na asivyopenda kuwajibika kichama CCM na kiserikali. Tanzania nzima mtakumbuka kuwa huyu mheshimiwa Edward Lowasa alikuwa ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya Urais mwaka 1995 na akaenguliwa kwa hoja nzito ya kutokuwa muadilifu na marehemu Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere, kwa ukweli (wala sio tuhuma) kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa kipindi kifupi ndani ya CCM na Serikali.Muda mfupi alikuwa ni mtumishi wa CCM, muda mfupi kama Mkurugenzi wa kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha.

Mfano hai wenyewe uko hivi; tufuatane kwa kuusoma tafadhali:-
Mara baada ya kurudi Butiama, 1995, baada ya kuenguliwa kugombea nafasi ya urais, siku moja mapema asubuhi Bwana Lowasa alinipigia simu na kusema yafuatayo:
"Bwana Kasori, naomba uende kumwambia Baba wa taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere, aende Monduli kusaidia kusafisha jina langu ili nisikose ubunge kutokana na yale aliyonisema Dodoma'. Nilishikilia mkono wa simu (TTCL) kwa zaidi ya nusu saa tukiwa tunazungumza na hatimaye mimi nilipata ujasiri wa kumwambia Bwana Lowasa kuwa siwezi kwenda kusema maneno hayo kwa Baba wa taifa na kwamba akitaka aje Butiama na nitamruhusu waongee ana kwa ana. Nikanyamaza na hatimaye yeye akawa wa kwanza kukata simu. Hiyo ikawa itifaki njema kwangu!

Kesho yake tena asubuhi nilipokea simu, safari hii akawa ni mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa maneno yake alisema "Bwana Kasori,jana ulizungumza na Edward Lowasa; naomba ufikishe ombi lake kwa Baba wa taifa tafadhali".
Kutokana na heshima ya Mheshimiwa Mzee Kawawa, nilikubali na nikaenda na kabla ya hapo nilimuomba Mzee Kawawa akae karibu na simu ili nimpe jibu muda si mrefu.

Nilimueleza Baba wa Taifa kuwa "Mheshimiwa Edward Lowasa kupitia kwa Mhe. Mzee Rashidi Mfaume Kawawa anaomba usaidie kusafisha jina lake kule jimboni kwake Monduli ili asikose ubunge kutokana na yale uliyomsema katika Kamati Kuu ya CCM Dodoma". Jibu la Baba wa Taifa alilonipa ni kuwa "Nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa"!
Watanzania wote, leo March19, 2008, nawaomba radhi kuwa jibu hilo kwa uzito wa maneno hayo kuwa "Kawawa asiwe mjinga kama Lowasa" kweli kwa kuzingatia heshima kati ya wazee hao wawili; "Kawawa sikumwambia hivyo"! Badala yake nilimdanganya (nawaomba radhi tena watanzania) jibu nililompa Mzee Kawawa ni kuwa juma lililokuwa linafuata tungekuwa Dar es Salaam na kwamba aje Msasani aongee na Baba wa Taifa. Mhe. Kawawa alikubali.

Nikarudi kwa Baba wa taifa kusema uongo (naomba radhi tena) kuwa "Mzee Kawawa ameomba mzungumze tatizo la Lowasa tutakapofika Dar es Salaam". Baba wa taifa alikubali na akaagiza nimuombe Mhe. mzee Kawawa kuwa Lowasa na Guninita na wapambe wengine wa Lowasa wote wafike Msasani.

Siku ya siku ikafika. Tukawepo Msasani na Mhe.mzee Kawawa akaja. Lowasa hakuwepo! Sababu anazijua mwenyewe.(muulizeni maana nasema ukweli). Mkutano ulipoanza mzungumzaji wa kwanza nikawa mimi, kueleza lengo la mkutano. Mzungumzaji wa pili alikuwa Baba wa Taifa na swali la kwanza ni kuuliza Lowasa yuko wapi?.

Bila kupoteza wakati Mwalimu alisema "Rashidi , huyu Kasori ananiambai eti niende Monduli nikasafishe jina la Mhe. Lowasa eti asikose ubunge kwamba nilimchafulia Dodoma katika Kikao cha Kamati Kuu ya CCM. Kutokana na ombi lako nilimtuma akuambie usiwe mjinga kama Lowasa. Kasori alikuambia eh?"
Oneni , huko nyuma tayari nilishasema uongo kwa kutosema maneno hayo kwa Mhe. mzee Kawawa. Kweli hilo kurudiwa na Baba wa Taifa kwa Mzee Kawawa mbele yangu lilisababisha kalamu yangu kuanguka, nikatetemeka na nikatokwa na jasho jingi mbele ya hao wazee!!! Bila kutegemea na kwa mshangao mkubwa Mhe. mzee Kawawa alikubali kwa kuitikia "NDIO ALINIAMBIA". Mwalimu akacheka sana!!!! Sababu sijui hadi leo kwa nini alicheka sana.

Kwa kuendelea, Mwalimu alimwambia Mzee Kawawa kuwa "Kasori ana umri mkubwa kuliko Lowasa. Kasori alipata taabu sana kufikisha kwangu ombi la Lowasa na aliniambia kuwa jana yake alikuwa amekataa ombi la Lowasa. Sasa nasema kuwa kwa umri wangu mimi mzee, Lowasa ni mtoto wangu tena mdogo sana. Kwa heshima mliyonayo kwangu na kwa chama cha Mapinduzi mtanishangaa sana mkisikia niko Monduli eti nipo kwenye majukwaa nasafisha jina Bwana Lowasa asikose ubunge.

Kweli Lowasa ni jasiri sana kusema maneno hayo. Hayo ningeambiwa na Kasori tu ningesita kumuamini. Lakini kwamba hata wewe Rashidi ulitumiwa kusema maneno hayo! Huyu Lowasa ni jasiri sana!!. Lakini kwa nini hajatuambia ukweli kuhusu mali hizo ambazo ni nyingi kuliko mimi ambaye nimekuwa Rais wenu kwa kipindi kirefu? Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mhe. Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowasa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu. Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda,umesikia eh?"

Mkutano ukaisha hapo Msasani. Hadi uchaguzi 1995, unafanyika na kumalizika Baba wa Taifa hakwenda Monduli. Alichukia sana tabia za Lowasa na alimfahamu kama mtu muongo na mwenye kiburi. Hadi Baba wa Taifa anafariki,sikuwahi na hata niandikapo makala hii sijasikia wala kusoma popote ambapo Lowasa anakanusha alivyolombikiza mali akiwa mtumishi wa CCM na serikali kwa muda mfupi kiasi cha kumzidi Rais wa Kwanza !!!

Sasa anatuhumiwa na vyombo vya habari kununua sehemu ya Ranchi za Taifa kwa kuandika majina ya wanafamilia! Kama hilo nalo ni kweli, ningekuwa mimi nisingeota tena kugombea URAIS n.k Tanzania. Bora kuendelea na biashara kwa uwazi kuliko kupitia mgongo au wa serikali au wa chama ( CCM). Huo ndio ushauri wangu kama mwana CCM kwa Lowassa.

Angalia tunavyofanya "total transgression of CCM regulations and ethics." Kamati kuu 1995 ilimwona Mhe. Lowassa hana uadilifu. Mhe. Mkapa baada ya kuingia madarakani baada ya muda si mrefu sijui ni kwa kikao gain cha CCM na taasisi ipi ya serikali akamwona Lowassa ni safi na akamweka katika safu yake ya baraza la mawaziri.

Huyu bwana akaendelea na huo usafi hadi akaukwaa uwaziri mkuu 2005. Yote haya yanatia shaka kama kweli ndani ya CCM na Serikali tuna benki sahihi za takwimu za mienendo kitabia ya wanachama na watumishi wetu kama si kubebana kwa majina tu! Nilinunua gazeti la mzalendo nikampa Baba wa Taifa na aliposoma kuwa Lowassa ni Waziri alimaka AHH!!

Katika hili nabaki nimeduwaa hasa tunapopeana madaraka makubwa ya kuendesha nchi kimzaha tu. Tukumbuke kuwa kwa kila kitu na kwa dini yoyote Mungu huweka wazi mambo mahali na kwa muda atakao yeye.( Time and space) ya Mwalimu J.K Nyerere juu ya Lowassa tuliyapuuza. Sasa Mungu kayaanika! Basi tuone hizi tuhuma za RICHMOND n.k, Mikataba ya Madini, EPA zitakavyoshughulikiwa.

 
Lowasa ndio rais ajaye, hakuna cha nyerere wala nani. Nyere kisha kufa na usia wake hauna maana yeyote. Hii nchi itakaa sawa kama Lowasa atakua Rais.
 
"hivi ni nani msafi ndani ya ccm"?

Kauli hii ni ya ajabu sana. may be jibu lake ni Mbowe aliyeponda maisha DUBAI au alivyohogwa na MKONO ili asipige kampeni kwenye jimbo lake. wapinzani ni WACHAFU KULIKO CCM
 
Hata Nyerere naye alikuwa hafai kuwa kiongozi,,, alitesa Sana wapinzani wake na wengine kuwaweka vizuizini huku wengine wakipotea bila taarifa hadi leo habari zao hazipo. Kwa mujibu wa Mohammed Babu, alisema Nyerere aliwahi kumzika mtu akiwa hai, tena huyo mtu akitokea Zambia alikuwa mpinzani wa Kaunda....
Lakini Nyerere huyu huyu alitoa elimu bora bure, afya bure, alijenga viwanda, rushwa ilikuwa mwiko Enzi za utawala wake

Nyerere alikuwa na mazuri na mabaya yake kama ilivyo kwa Lowassa
 


mikakati 10 ya lowassa ili kufanikisha safari ya matumaini:



  1. kuhonga wajumbe wa vikao vinavyopitisha majina
  2. kuhonga waandishi wa habari
  3. kuhonga vikaragosi kwenye social media
  4. kugawa fedha makanisani
  5. kugawa fedha misikitini
  6. kugawa fedha vikoba
  7. kugawa fedha saccos
  8. kugawa fedha mashuleni
  9. kugawa fedha vibindo
  10. kugawa fedha bodaboda
 
Naanza kazi rasmi ya kumfuatilia nyendo na mambo yote kuhusu lowasa huyu mzee yawezekana anashida fulani siyo bure kabisa.
 
VIKARAGOSI vya LAIGHWANAN MNALO MWAKA HUU KUMBEBA ASIYEBEBEKA. NJAA ZENU ZITAWAUA
 
Mkuu nakuunga mkono hoja yako, hatuwezi tukampa uongozi wa taifa mwinzi kama yule na fisadi mkubwa.
Mungu kumlaani kwa sasa ni mgojwa kama kuku mwenye ndegua.
 
Back
Top Bottom