sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,033
Na hapa nazungumzia Power endelevu miaka nenda rudi, na angalau idadi iwe inaridhisha sio mtu anakuwa moja tu akiondoka panakuwa kimya.
Mara nyingi utaisikia kanda ya pwani, kanda ya ziwa na kanda ya kaskazini wapo active sana mambo ya power, yani hawapoi.
Ila sasa huku mikoa ya kanda za kusini na kati kwanini kumepoa, sana sana utawakuta viongozi wa msimu na kwenye suala la succession & growth of power wapo nyuma sana.
Yaani hata uje kwa wanyamwezi wa Tabora, wasukuma jamii za mikoa ya kati, wafipa wa sumbawanga, wasafwa wa Mbeya, wangoni wa Ruvuma, Wahehe wa Iringa, Wakinga wa Njombe, Wabena, wagogo wa dodoma, unaona bado pana tatizo.