Kwanini JK hakubaliki ndani ya EAC?

Rutashubanyuma hatuwezi kuingia kwenye kinyang'anyiro bila kujiandaa toka tupate uhuru mwaka 1961 Tanzania tumepoteza muda mwingi tukisaidi nchi zingine kupigania uhuru na kuzikomboa toka kwa watawala wabovu nchi kama Angola, Msumbiji, Zimbabwe, shelisheli, Uganda na Afrika ya Kusini wakati wenzetu wakenya toka uhuru wanashughulika na biashara wanajua umuhimu wa ardhi na wanaelimu ya masoko ya hisa toka mwaka 63 wakati watanzania tumeanza juzi maana muda mwingi pia tulikuwa kwenye siasa ya ujamaa na kujitegemea

Kawhiyo haitakuwa haki kutuunganisha na watu wenye uzoefu undercover ya kuwa nasi tutapata bidii hakuna kitu kama hicho inabidi watanzania wapate muda wa kujiandaa ili kuingia kwenye shirikisho kitendo cha kulazimisha Tanzania kuingia sasa hivi ni sawasawa na mwanafunzi wa darasa la nne umpeleke kufanya mtihani wa darasa la saba eti atajifunza mbele kwa mbele bila kuandaliwa ili afikie kiwango cha mwanafunzi wa darasa la saba au ni sawaswa na kupeleka timu ya Olyimpic kwenye mashindano kabla haijafikia kiwango eti itajiongeza mbele kwa mbele itaishia kuwa msindikizaji

Wenzetu nchi za ulaya zina jiandaa kwanza kabla ya kuingia European Union haziendi kichwa kichwa halafu katika EU kuna nchi viongozi zimeset standard ili mwanachama aweze kuingia ili wanachama wawe ni member wanaofanana. sasa sisi tutaunganaje na madikteta kama Museveni? Kibaki au Kagame lazima wawe na mifumo yenye kuheshimu katiba bila kubalidi term limit kwa mtu kama Museveni na Kenya waondoe dhana ya kuwa bila wakikuyu nchi haitawaliki pia Kagame kujifanya nabii wa Rwanda kuwa bila yeye hakuna Rwanda

hoja hizi ndizo zinatudanganya kabisa................................maendeleo ni kipimo cha ulinganishi...................unajilinganisha na nchi hii kuanzia mwaka 1961 amabyo GDP zilikuwa zinashahibiana?

Jibu ni South Korea ambayo leo...................GDP yake inaizidi hii ya TZ zaidi ya mara 400...................tafakari haya kwanza kabla ya kuwafuta wanasiasa uchwara wa nchi ambao hujivunia umasikini ili kuhalalaisha kitumbua chao ambacho hata hivyo kina mchanga...........
 
Mkuu, Rejea mfano huu:
Hivi kuna kiongozi yeyote wa Marekani, India au China asiyejua maana ya kutunza mazingira au madhara ya kutotunza mazingira katika ustawi wa viumbe duniani? Jibu ni hakuna. Wote wanajua, lakini unafikiri ni kwa nini viongozi wa nchi hizo hawataki kutekeleze kwa 100% Kyoto protocal (Rejea mkutano Wa South Africa,2011)?

Ukichunguza vizuri mfano huu utagudua kuwa Wawakilishi wetu(Sitta nawenzake huko EAC) walikuwa sahihi kwa uamuzi walio chukua.

kama wako sahihi kwa nini wanawazuia wenzao wasiendelee na shirikisho? kwa nini wanatumia veto kuwakwaza? JK anajua ya kuwa wakiendelea watakuwa na mafanikio nasi tutazidi kurudi nyuma...............sasa hivi tunashida kubwa ya soko la ajira na kila mchumi anaona EAC ndiyo mwanzo wa ufumbuzi wa tatizo tajwa...........................kama kuna maamuzi magumu tunapaswa kuyafanya ni kushinikiza shirikisho la EAC lianzishwe haraka kunusuru uchumi wa nchi hii ambao unahitaji wawekezaji makini ambao wapo hapahapa katika EAC..................................vinginevyo nieleze majibu ya kufufua kwa soko la ajira yako wapi
 
Wewe ndio una bad reasoning, mbona wapo pia wawekezaji wakubwa Kutokea Kenya ambao wanamilikishwa ardhi kwenye baadhi ya strategic investments... Na hao wazungu uliowataja bado hawajachukua hata 1% ya ardhi yetu yote...Ambacho hatutaki ni kufungulia mlango kwa VIBAKA karibia milioni 70 (i.e., akina Njuguna, Nyangau na batabaire) kuja kugombea ardhi kiholela na watanzania wazawa kila sehemu....NO WAY

Mfano wako wa Zanzibar ni mfu kwa maana kule ardhi yenyewe haipo na ile iliyopo ni ya kugombea hata kwa wazawa wa huko, zipo sehemu za Tanzania bara ambazo zina ugumu wa kupata ardhi hata kwa wenyeji, kwa mfano mkoa wa Kilimanjaro...

Mfano wako wa wakoloni ni mfu pia...:lol: Hata Uingereza, Ujerumani, na Ufaransa (wakoloni wakuu) kuna baadhi ya mambo likiwemo la ARDHI hawakubalini nalo kabisa kwenye Jumuiya ya Ulaya (EU)...

Sikubaliani na Vasco kwa mengi ila kwa hili la ARDHI niko naye 100% siasa za kufuata sera zavyama naweka naweka kando utaifa mbele...:poa

ardhi ni ya mwenye pesa na ndiyo maana wakenya wanaendelea kuinunua hapa nchini....................kwa hiyo shirikisho kuwepo au kutokuwepo ardhi inakwenda tu kwa mwenye nacho..........................wewe tetea ardhi lakini ardhi haikusubiri wewe.................leo tunavyoongea nakumatt ya Kenya inafungua super market ya nguvu Moshi..........................ardhi kwani hawakupewa?

Sijui ni ardhi gani ambayo waiongelea ambayo inawazuia wakenya wasiipate.........................kila kitu kina thamani yake kwenye soko....................tutoke kwenye hizi ghiliba za wanansiasa za suala la ardhi kuwa halina uhusiano na shirikisho halafu tuangalie ni jinsi ipi shirikisho la EAC litasaidia kutokomeza umasikini hapa nchini........................huhitaji kumiliki ardhi kuondoakana na umasikini................soko la ajira tukiweza kulipanua na hili haliwezekani kufanikiwa ndani ya TZ pekee...........we have to look beyond the tiny box called TZ...............
 
uchumi wa TZ umo mikononi mwa wasauzi na wakenya..........................amka kutoka kwenye usingizi.........................fuatilia takwimu za uwekezaji hapa nchini na utaelewa kinachoendelea......................................wewe subiri wakuajiri wewe na watoto wako.........................

Hakuna wa kuniajiri mie ninaishi Marekani nina guarantee ya maisha yangu na wanangu pia nina miradi yangu ya kulima mashamba mkoani Rukwa na Morogoro labda wakuajiri wewe, ile wanangu kuzaliwa hapa na kuwa na social security numbe wnaweza kufanikiwa katika maisha sihitaji kuwaibia watanzania ili wafanikiwe kazi ni kwao sky is the limit
 
Rutashubanyuma hatuwezi watanzania kulazimishwa kuingia kwenye jumuiya tukiwa bado hatujajiandaa iwapo European union imeanza mwaka 1957 Hispania na Ureno zimejiunga juzijuzi na Norway na Sweeden bado zinajiandaa kuingia unafikiria wao ni wajinga? lazima uwaandae wananchi wako kwanza sio kuingia kwa kufuata mkumbo ndio maana Congo walikataa na kusema kwa sasa hawako tayari inabidi wajiandae kwanza
 
Nina wasiwasi na uraia wako, Mtanzania halisi hawezi kuponda maamuzi ya Sitta kukataa kusaini mkataba kuhusu Ardhi, eti nilikuja duniani sina kitu na nitaondoka sina kitu, Kibwetere wewe.

Hongera JK na Sitta.
 
Kama JK anatetea maslahi ya mipaka, kwa nini Tanzania wameweka pingamiza kwa S. Sudan kujiunga EAC? They have a bigger land and available kwa wakenya na wanyarwanda kusettle. Na DRC nayo inataka kujiunga. Wawaachie tu wajiunge.
 
Wewe ndio una bad reasoning, mbona wapo pia wawekezaji wakubwa Kutokea Kenya ambao wanamilikishwa ardhi kwenye baadhi ya strategic investments... Na hao wazungu uliowataja bado hawajachukua hata 1% ya ardhi yetu yote...Ambacho hatutaki ni kufungulia mlango kwa VIBAKA karibia milioni 70 (i.e., akina Njuguna, Nyangau na batabaire) kuja kugombea ardhi kiholela na watanzania wazawa kila sehemu....NO WAY

Mfano wako wa Zanzibar ni mfu kwa maana kule ardhi yenyewe haipo na ile iliyopo ni ya kugombea hata kwa wazawa wa huko, zipo sehemu za Tanzania bara ambazo zina ugumu wa kupata ardhi hata kwa wenyeji, kwa mfano mkoa wa Kilimanjaro...

Mfano wako wa wakoloni ni mfu pia...:lol: Hata Uingereza, Ujerumani, na Ufaransa (wakoloni wakuu) kuna baadhi ya mambo likiwemo la ARDHI hawakubalini nalo kabisa kwenye Jumuiya ya Ulaya (EU)...

Sikubaliani na Vasco kwa mengi ila kwa hili la ARDHI niko naye 100% siasa za kufuata sera zavyama naweka naweka kando utaifa mbele...:poa

Ni kweli kwa suala la ardhi na rasilimali nyingine za nchi yetu lazima tuwe makini. Namuunga mkono JK kwa hili. Mkianza kulegalega kwa hili utakuta sisi wote tutahamishwa kwenye nchi yetu. Inabidi tusimamie vizuri umilikaji wa rasilimali zetu. Hata pale tulipokosea tukawamilikisha wageni lasima turudi nyuma kwenye sheria zetu za ardhi na kuhakikisha zinafuatwa na kama mtu yoyote akikiuka achukuliwe hatua. Ardhi ya Tz tuipiganie ili vizazi vijavyo viweze kuiridhi.
 
Ruta hebu tofautisha kudharau na kususia,mara nyingi nimeingia kwenye mikwaruzo na jamaa zangu kiasi kwamba sehemu mimi nikiwepo yeye/wenyewe hawaji and vice-versa lakini sidhani kama nikwamba nawadharau au wananidharau ila ni njia tu ya kuonyesha reaction yako juu ya kupishana kwetu kimtazamo.Wamesusia hawajadharau,JK kama binadamu ana matatizo yake tena mengi tu lakini kwa hili la ardhi kwakweli namuunga mkono.Hebu nipe faida moja tutakayoipata kama watanzania tukikubali ardhi yetu iwe ya shirikisho?
Ndugu kama umetumwa waambie hatudanganyiki,watuache na umasikini wetu lakini kwa hili watusamehe!!
 
Sherehe zetu za uhuru na EAC vina uhusiano gani? Haya mbona ni mambo madogo tu na ndio maana wakatumwa akina Kalonzo.
 
hatutaki kuungana kwa ardhi kama umetumwa na mabwana zako wa kenya, uganda, rwanda na Burundi kudhoofisha hoja yetu ya ardhi potea. Kwa suala la ardhi Jk yuko sahihi na tunamuunga mkono watanzania karibu wote wanaolitakia afya njema taifa letu
 
ardhi ni ya mwenye pesa na ndiyo maana wakenya wanaendelea kuinunua hapa nchini....................kwa hiyo shirikisho kuwepo au kutokuwepo ardhi inakwenda tu kwa mwenye nacho..........................wewe tetea ardhi lakini ardhi haikusubiri wewe.................leo tunavyoongea nakumatt ya Kenya inafungua super market ya nguvu Moshi..........................ardhi kwani hawakupewa?

Sijui ni ardhi gani ambayo waiongelea ambayo inawazuia wakenya wasiipate.........................kila kitu kina thamani yake kwenye soko....................tutoke kwenye hizi ghiliba za wanansiasa za suala la ardhi kuwa halina uhusiano na shirikisho halafu tuangalie ni jinsi ipi shirikisho la EAC litasaidia kutokomeza umasikini hapa nchini........................huhitaji kumiliki ardhi kuondoakana na umasikini................soko la ajira tukiweza kulipanua na hili haliwezekani kufanikiwa ndani ya TZ pekee...........we have to look beyond the tiny box called TZ...............

Acha hoja za kitoto, sasa Nakumatt ya Kenya na hoja ya ARDHI vina uhusiano gani? mbona mtanzania Bakhresa ana shughuli zake Kenya, Rwanda, Uganda, Malawi, Burundi, Congo DRC lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao...au mbona Ali Mfuruki ndio mwenye kumiliki Franchise ya WoolWorth Afrika Mashariki lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao? Mbona wasauzi wameweka Shoprite sehemu mablimbali za bongo lakini hawajasema sasa raia wao wana haki sawa kwenye ARDHI yetu:tongue:

Kama wewe ni mwekezaji seroius toka Kenya, Uganda, US, UK, etc, etc unakaribishwa kuja kuwekeza bongo kwa mikono miwili. Lakini kama wewe ni Mungiki wa Kibera sahau kupewa haki sawa ya ARDHI yetu...Tutaendelea kuwa-Screen hivi hivi kwa sababu hatutaki kufikia hapo mlipo sasa ambapo wananchi wenuwa kawaida hawana hata mahala pa kulala!:tongue:

Ushauri wangu kwako kuanza kudai ARDHI yenu ambayo babu zenu wali-dhulumiwa na familia ya Kenyatta:lol:
 
tatizo kwako huelewi ya kuwa uhuru maana yake ni kufuta urithi wa mkoloni ikiwemo mipaka aliyotuwekea.....................mkoloni alitugawa ili atutawale...............................hivi yawaje akija kaburu kutoka sauzi anapewa ardhi ambayo wewe unadai ni lulu...............................ululu huo uko wapi wakati umasikini wazidi kushamiri.....................sana sana watetea ubinafswi ambao hautupeleki popote.....................yawaje inap[okuja EAC tujione ni lulu lakini kwa wazenji tujione hatuna maana hata kuona aibu kujiita jina stahili la watanganyika?????????????
Du! huyu jamaa anahitaji kupepewa ili akili zake za udadisi wa kimantiki zimrejee japo kwa dakika chache wakati anadadavua mada hii....Aliyekuambia uhuru ni kufuta mipaka ni kilaza. Ardhi ndiyo msingi wa uhai wetu na kinachohitajika ni kuhakikisha kuwa kila mtanzania anamilikishwa sehemu ya ardhi ili aitumie kwa ajili ya mustakabali wake ili kuondokana na dhana ya rais kuwa mmiliki wa ardhi yote kwa niaba yetu. Kwa hiyo usitegemee kupendwa km unawatilia ngumu raia wa nchi nyingine uhuru na fursa za kumiliki ardhi yetu kwa kisingizio cha shirikisho la afrika mashariki, wakati tukijua kuwa katika nchi hizo nyingine hakuna kipande cha ardhi kilicho wazi km ilivyo Tanzania.
 
Ubaya wa kikwete ni kwamba sio mnafiki na anapenda kusema ukweli.kama nchi za jirani hawajahudhuria sherehe za miaka 50 za uhuru wa Tanganyika eti kwa kuwa wamenyimwa ardhi niko upande wa Jk.wewe endelea kulalamika na kunung'unika kwa ukale wa mawazo kuwabembeleza na kuwafurahisha kina Mwai na museveni....Mwache Kikwete atutetee sisi wanyonge.wew ungewahi kuzaliwa let say wakati wa ukoloni bila shaka ungekuwa MNYAPARA ie mkoloni mweusi.
 
Hakuna wa kuniajiri mie ninaishi Marekani nina guarantee ya maisha yangu na wanangu pia nina miradi yangu ya kulima mashamba mkoani Rukwa na Morogoro labda wakuajiri wewe, ile wanangu kuzaliwa hapa na kuwa na social security numbe wnaweza kufanikiwa katika maisha sihitaji kuwaibia watanzania ili wafanikiwe kazi ni kwao sky is the limit

tatizo la hoja yako ni kushindwa kuelewa ya kuwa uwe mtanzania au la hakuna ardhi ya bwerere.............................aje mgeni au mwenyeji ardhi ni yakununua........................kuwachukia wawekezaji wa EAC ambao watapewa hadhi sawa na wazawa au raia wa TZ ni kufilisika kifikra...........................uwe marekani au kwingineko haisaiidii kama hutambui soko la ajira la nchi hii linakwama kwa ukosefu wa ajira ambao chanzo chake ni mapungufu ya sera bora za uwekezaji zinazojali raia.............
 
Ubaya wa kikwete ni kwamba sio mnafiki na anapenda kusema ukweli.kama nchi za jirani hawajahudhuria sherehe za miaka 50 za uhuru wa Tanganyika eti kwa kuwa wamenyimwa ardhi niko upande wa Jk.wewe endelea kulalamika na kunung'unika kwa ukale wa mawazo kuwabembeleza na kuwafurahisha kina Mwai na museveni....Mwache Kikwete atutetee sisi wanyonge.wew ungewahi kuzaliwa let say wakati wa ukoloni bila shaka ungekuwa MNYAPARA ie mkoloni mweusi.

upende usipende.........................shirikisho la EAC linakuja sasa huyo JK sijui atakusaidaje kama hata sasa hana majibu ya ukosefu wa ajira..............................Raisi ambaye amekiri kuwa hajui kwanini TZ ni masikini...........................hivi atakutetea kivipi na umasikini ndiyo unazidi kushamiri.................................chungulia majibu ya umasikini huu nje ya mipaka ya TZ au utabakia na mawazo yako mgando uliyonayo
 
Acha hoja za kitoto, sasa Nakumatt ya Kenya na hoja ya ARDHI vina uhusiano gani? mbona mtanzania Bakhresa ana shughuli zake Kenya, Rwanda, Uganda, Malawi, Burundi, Congo DRC lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao...au mbona Ali Mfuruki ndio mwenye kumiliki Franchise ya WoolWorth Afrika Mashariki lakini hatujadai haki sawa kwenye ARDHI yao? Mbona wasauzi wameweka Shoprite sehemu mablimbali za bongo lakini hawajasema sasa raia wao wana haki sawa kwenye ARDHI yetu:tongue:

Kama wewe ni mwekezaji seroius toka Kenya, Uganda, US, UK, etc, etc unakaribishwa kuja kuwekeza bongo kwa mikono miwili. Lakini kama wewe ni Mungiki wa Kibera sahau kupewa haki sawa ya ARDHI yetu...Tutaendelea kuwa-Screen hivi hivi kwa sababu hatutaki kufikia hapo mlipo sasa ambapo wananchi wenuwa kawaida hawana hata mahala pa kulala!:tongue:

Ushauri wangu kwako kuanza kudai ARDHI yenu ambayo babu zenu wali-dhulumiwa na familia ya Kenyatta:lol:

hiyo Super Market unafikiri imejengwa hewani?
 
Back
Top Bottom