Kwanini CCM hawashangilii Ushindi wa kesi dhidi ya Lema?

Elba

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
382
104
Wakuu, nimejaribu kufuatilia viongozi wa CCM na wafuasi wa CCM kwenye mitandao. Lakini sijaona hata mmoja akionyesha kufurahia Ushindi wa Kesi dhidi ya aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini Ndugu Godbless Lema. Hii inaashiria nini kisiasa? Ama ndiyo wameshakata tamaa na siasa za Arusha? Au tunaweza kuuita ushindi huu "ushindi wa machungu..."
 
Wanaelewa kinachofuata ni kuzudi kuumbuka bt kwa nape atakua anafanya sherehe cse anajua lazima atapata muda wa kuzungumza pumba
 
Wanajua hata wakatambike kwa mizimu ya kwao hawawezi kuipata arusha ndio mana unaona wamekosa furaha.


Hapa hata asiposimamishwa Lema, jimbo haliwezi kwenda ccm huo ndio ukweli halisi. Tena safari hii tutawatia aibu hawajawahi kuipata toka siasa za vyama vingi ianze Tz. CCM wamechokwa kuliko maelezo hapa arusha.

Walete mahela tule afu tukutane kwenye sanduku la kura kudadadeki...

Tutawaramba kuliko tulivyowaramba kule Arumeru, watajuta kufanya maamuzi ya kijinga.


Tunawasubiri kwa hamu kubwa.
 
Wanajua walichokifanya, nafsi zao zinawasuta, maana wananchi wa Arusha wametoa kilio kikubwa sana baada ya hukumu kuonyesha wanamhitaji mbunge wao Lema na si hukumu iliyotolewa na mahakama!
 
Wanajua walichokifanya, nafsi zao zinawasuta, maana wananchi wa Arusha wametoa kilio kikubwa sana baada ya hukumu kuonyesha wanamhitaji mbunge wao Lema na si hukumu iliyotolewa na mahakama!

Kwanza CCM haijui nani atagombea Arusha bila kuwaacha na makundi tena.

Ukitoka hapo wanajua kabisa wamejitekenya wenyewe kisha wanacheka wenyewe!!!!
 
CCM hadi kufikia 2015 watajuta kumpa uongozi JK. Hii decision ya leo imepoteza maelfu ya wafuasi wao kwani wameona kabisa nchi imekosa muelekeo kwa mahakama kutumiwa kisiasa. Kizazi kipya hakiitaki CCM, wamebaki wazee na Arusha mjini hakuna wazee wa kutosha kuipa ushindi so hakuna cha wao kushangilia au kusherehekea. Mwisho wa ubaya ni aibu
 
Wanajua walichokifanya, nafsi zao zinawasuta, maana wananchi wa Arusha wametoa kilio kikubwa sana baada ya hukumu kuonyesha wanamhitaji mbunge wao Lema na si hukumu iliyotolewa na mahakama!

Picha inakokwenda CCM inaonekana kama hawausiki na kuingia miundo mbinu ya kuhujumu ubunge wa Lema,bali kuna mkono wa baadhi ya wanaccm,matokeo yake yamefanya kwa namna ya kuwakomoa ccm,mchezo wa kuwa wewe umemwaga mboga [Arumeru] mimi namwaga ugali [Arusha].

Mchezo huo wa Ubunge wa Lema hauna baraka za wakuu wa ccm [Ndio maana Ikulu imewahi kutamka ikijua faul iliyochezwa kuwa itawaangukia watu kuspeculate na rumous zinazokuzwa kuwa issue ya Lema kuna mkono wa Ikulu.

Ila tunachoweza kusema kwa mchakato mzima wa kuunga dot kuna ishara fulani ya kuwa CCM kama ccm kwa ujumla wao hii issue ya Lema hata wao imewachanganya.Kama ilivyokuwa CDM nao walikuwa katika kuona jinsi sheria inavyofanya kazi lakini sio katika kiwango hichi ambacho kimeonyesha dhahili kuna faul imechezwa na ambayo kwa heshima ya IKULU kufikia kutoa waraka kukanusha kuwa HAIHUSIKI kwa wenye akili zao wanajua mchezo huo sio mdogo.Kwa kuwa hadhi ya IKULU ni kubwa kujua kuwa mahamuzi ya IKULU ni mhimili unaojitegemea hivyo haiwezi kuingilia na hata kama ikiingilia haipaswi kuonyeshwa wala hata kufikilika kwa raia wa kawaida kuhisi hata kuspeculate kuwa IKULU imehusika.

Kwa kujua kuwa MAHAKAMA ni muhimili binafsi lakini IKULU imetoa taarifa kukakanusha kitu au jambo inalojua kuwa MAHAKAMA imetimiza kazi yake kama ni sawa ama si sawa bado ni jukumu la mahakama japo IKULU inawezwa kupelekewa taarifa kama malalamiko.Lakini kwa tukio hili picha inayoonyesha IKULU kwa kujua umuhimu na unyeti wa hali ya KISIASA ya JIJI la Arusha imebidi kujitoa muhanga kujibu hisia na muona ambao umejijenga kwa watu tena kwa speed ya siku moja isiyozidi masaa kumi na mbili toka hukumu itoke,basi dhahiri shairi kuwa hali ya kisiasa baada ya maamuzi ya Mahakama yaweza kuwa tete na tata kwa jimbo Arusha ambalo katika siasa za Tanzania ndio jimbo ambalo limeleta utata wa kisiasa kwa picha ambayo Nchi nzima unalijua kuwa ni swala nyeti sana na kuwa CDM ndio wenye nguvu ya kisiasa jimboni humo.

Hivyo kama ilivyo picha ya IKULU ndivyo picha ilivyo kwa CCM,na hivyo nitendo ambalo kwa picha ya kawaida kuna watu ambao wako ndani ya CCM ndio wenye tukio zima hilo kwa nia ya mfumo unaonekana kushika kasi ndani ya CCM ya kukomoana kwa mahasimu wa kisiasa.Na nyuma ya hao wanasiasa kuna wasomi na wataalamu ambao sasa inavyoonyesha wanadhamira mbaya na Taifa.Kwa kuwa hukumu ya jimbo la Arusha ukweli halisi uliitajika umakini na busara kubwaa sana kutoa judgement ambayo ingezingatia hali ya Ukweli wa kisiasa wa jimbo zima la Arusha ambalo kwa sasa kwa muda mrefu limekuwa ni jimbo tata na nyeti kwa siasa za Tanzania.
 
Kwa muda sasa tumezoea kuona baadhi ya vyama vya upinzani kuacha kusimamisha wagombea katika baadhi ya majibo hasa wanapoona hakuna uwezekano wa kushinda. Lakini inawezekana kwa mara ya kwanza tukashuhudia CCM ikikacha kusimamisha mgombea jimbo la Arusha Mjini hasa kama Bw Lema atapitishwa tena na CDM kutetea jimbo lake!
 
Wanaelewa kinachofuata ni kuzudi kuumbuka bt kwa nape atakua anafanya sherehe cse anajua lazima atapata muda wa kuzungumza pumba
Kwa Nape sidhani kama ana cha kuzungumza hapa. Kwa kuwa ndani ya CCM. Arusha ni ngome ya wapinzani wake kundi la Lowasa. Nikimtazama Nape naona ni heri jimbo liende CDM kuliko ngome ya Lowasa. Na ndo maana hata Arumeru hakumsupport Sioi tangu mwanzo. Kinachonishangaza hapa, hata hao Kundi la Lowasa wameloa!! Au ndo bado uoga wa Arumeru? Madiwani wote CCM, mbunge Chadema... Shame of the year!!
 
Wanajua hata wakatambike kwa mizimu ya kwao hawawezi kuipata arusha ndio mana unaona wamekosa furaha.


Hapa hata asiposimamishwa Lema, jimbo haliwezi kwenda ccm huo ndio ukweli halisi. Tena safari hii tutawatia aibu hawajawahi kuipata toka siasa za vyama vingi ianze Tz. CCM wamechokwa kuliko maelezo hapa arusha.

Walete mahela tule afu tukutane kwenye sanduku la kura kudadadeki...

Tutawaramba kuliko tulivyowaramba kule Arumeru, watajuta kufanya maamuzi ya kijinga.


Tunawasubiri kwa hamu kubwa.

Uyasemayo ni kweli tupu mama.
 
poleni wana Chadema hukumu imewachanganya kweli mpaka mnaamua kuanzisha thread halafu mnajijibu wenyewe.
Maskini! Mpaka unatia huruma ulivyokuwa mpole. Rejao yuko wapi? Manake naona ww ndo kidogo umeanza kupata nguvu baada ya " msiba" Arumeru
 
Kwa tathmini niliyofanya, CCM hata ingemsimamisha Kikwete na CDM wakaweka bendera tu bado CDM wangeshinda kama ifuatavyo;
1. Bendera= 51%
vs
Kikwete= 49%

2. Dr. Slaa = 99%
vs
Kikwete = 1%

3. Lema = 99
vs
Kikwete= 1%
 
Back
Top Bottom