Abdul Nondo
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 515
- 2,875
Mimi, viongozi na wanachama kadhaa Jimbo la Kigoma Mjini ambao ni mgombea wetu udiwani kata ya Kasingirima ndug. Alumbula Khalidi, Alhaji Mzee Selemani Simba, Ntakije Ntanena na Khamis Mzungu tuliokamatwa na polisi siku ya uchaguzi wa kata ya Kasingirima-Jimbo la Kigoma Mjini tarehe 20/03/2024 baada ya kumzuia kijana wa CCM aliyekuwa na kura bandia.
Tumefunguliwa kesi na muda wowote kuanzia sasa tunaweza pelekwa mahakamani wakitutuhumu kufanya fujo kituo cha kupigia kura cha Mtaa wa Livingston-Kasingirima na pia tuhuma nyingine ni kumshambulia kijana wa CCM, tuhuma ambazo sio za kweli. Tumetakiwa wote kurejea Central Police Kigoma siku ya Jumanne, tarehe 25/3/2024.
Ila mbali na kufunguliwa kesi hizo na mimi nimewasilisha malalamiko yangu kwa OCD Kigoma Mjini na kufungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya polisi kituo kikuu aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO No. 15 na 16 tarehe 20/03/2024 katika uchaguzi wa Kasingirima baada ya kubaini na kutaka kijana aliyekuwa na kura bandia akamatwe. Nitafuata taratibu zote hadi hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya askari huyu.
Abdul Omary Nondo.
Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa - ACT Wazalendo.
==============
Machi 26, 2024
Mimi, viongozi na Wanachama kadhaa Jimbo la Kigoma Mjini ambao ni Mgombea wetu Udiwani kata ya Kasingirima ndugu, Alumbula Khalidi, Alhaji Mzee Selemani Simba, Ntakije Ntanena na Khamis Mzungu tuliokamatwa na Polisi siku ya Uchaguzi wa Kata ya Kasingirima -Jimbo la Kigoma Mjini tarehe 20/03/2024 baada ya kumzuia kijana wa CCM aliyekuwa na kura bandia.
Tulikamatwa na kufunguliwa kesi na muda wowote kuanzia sasa tunaweza pelekwa Mahakamani wakitutuhumu kufanya fujo kituo cha kupigia kura cha Mtaa wa Livingston -Kasingirima na pia tuhuma nyingine ni Kumshambulia kijana wa CCM tuhuma ambazo sio za kweli.
Ila mbali na kufunguliwa kesi hizo na mimi niliwasilisha malalamiko yangu kwa OCD Kigoma Mjini na kufungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya Polisi kituo cha kati aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO kifungu cha 15 na 16 mnamo tarehe 20/03/2024 katika uchaguzi wa Kasingirima baada ya kubaini na kutaka kijana aliyekuwa na kura bandia akamatwe.
Tayari jalada la uchunguzi limeshafunguliwa na kesi tayari amekabidhiwa Mpelelezi Afande Elias wa Kituo cha Kata Kigoma. Na leo tayari nimeleta Mashahidi 6 ili kuchukuliwa maelezo.
Abdul Omary Nondo
Mwenyekiti wa Ngome ya vijana Taifa -ACT Wazalendo.
-=============
KIGOMA: Viongozi kadhaa wa Chama cha #ACTWazalendo akiwemo Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa, Abdul Nondo wanatarajiwa kupandishwa Mahakamani muda wowote kuanzia Machi 27, 2024 wakidaiwa kufanya fujo katika uchaguzi dhidi ya Mwanachama wa CCM waliyedai ana kura bandia, Kata ya Kasingirima, Jimbo la Kigoma Mjini (Machi 20, 2024).
Naibu Katibu wa Habari na Uenezi wa ACT, Shangwe Ayo amesema watuhumiwa wengine ni Alumbula Khalidi, Alhaji Selemani Simba, Ntakije Ntanena na Khamis Mzungu
Kamanda wa Polisi Mkoa, Philemon Makungu amesema “Sio ACT tu waliokamatwa hata wa #CCM tuliwashikilia, walifanya fujo, upelelezi unaendelea ukikamilika watafikishwa Mahakamani.”
Upande wa Nondo amesema “Licha ya kufunguliwa Mashtaka, mimi pia nilifungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya Polisi Kituo cha Kati aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO kifungu cha 15 na 16.”
Tumefunguliwa kesi na muda wowote kuanzia sasa tunaweza pelekwa mahakamani wakitutuhumu kufanya fujo kituo cha kupigia kura cha Mtaa wa Livingston-Kasingirima na pia tuhuma nyingine ni kumshambulia kijana wa CCM, tuhuma ambazo sio za kweli. Tumetakiwa wote kurejea Central Police Kigoma siku ya Jumanne, tarehe 25/3/2024.
Ila mbali na kufunguliwa kesi hizo na mimi nimewasilisha malalamiko yangu kwa OCD Kigoma Mjini na kufungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya polisi kituo kikuu aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO No. 15 na 16 tarehe 20/03/2024 katika uchaguzi wa Kasingirima baada ya kubaini na kutaka kijana aliyekuwa na kura bandia akamatwe. Nitafuata taratibu zote hadi hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya askari huyu.
Abdul Omary Nondo.
Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa - ACT Wazalendo.
==============
Machi 26, 2024
Mimi, viongozi na Wanachama kadhaa Jimbo la Kigoma Mjini ambao ni Mgombea wetu Udiwani kata ya Kasingirima ndugu, Alumbula Khalidi, Alhaji Mzee Selemani Simba, Ntakije Ntanena na Khamis Mzungu tuliokamatwa na Polisi siku ya Uchaguzi wa Kata ya Kasingirima -Jimbo la Kigoma Mjini tarehe 20/03/2024 baada ya kumzuia kijana wa CCM aliyekuwa na kura bandia.
Tulikamatwa na kufunguliwa kesi na muda wowote kuanzia sasa tunaweza pelekwa Mahakamani wakitutuhumu kufanya fujo kituo cha kupigia kura cha Mtaa wa Livingston -Kasingirima na pia tuhuma nyingine ni Kumshambulia kijana wa CCM tuhuma ambazo sio za kweli.
Ila mbali na kufunguliwa kesi hizo na mimi niliwasilisha malalamiko yangu kwa OCD Kigoma Mjini na kufungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya Polisi kituo cha kati aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO kifungu cha 15 na 16 mnamo tarehe 20/03/2024 katika uchaguzi wa Kasingirima baada ya kubaini na kutaka kijana aliyekuwa na kura bandia akamatwe.
Tayari jalada la uchunguzi limeshafunguliwa na kesi tayari amekabidhiwa Mpelelezi Afande Elias wa Kituo cha Kata Kigoma. Na leo tayari nimeleta Mashahidi 6 ili kuchukuliwa maelezo.
Abdul Omary Nondo
Mwenyekiti wa Ngome ya vijana Taifa -ACT Wazalendo.
-=============
KIGOMA: Viongozi kadhaa wa Chama cha #ACTWazalendo akiwemo Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa, Abdul Nondo wanatarajiwa kupandishwa Mahakamani muda wowote kuanzia Machi 27, 2024 wakidaiwa kufanya fujo katika uchaguzi dhidi ya Mwanachama wa CCM waliyedai ana kura bandia, Kata ya Kasingirima, Jimbo la Kigoma Mjini (Machi 20, 2024).
Naibu Katibu wa Habari na Uenezi wa ACT, Shangwe Ayo amesema watuhumiwa wengine ni Alumbula Khalidi, Alhaji Selemani Simba, Ntakije Ntanena na Khamis Mzungu
Kamanda wa Polisi Mkoa, Philemon Makungu amesema “Sio ACT tu waliokamatwa hata wa #CCM tuliwashikilia, walifanya fujo, upelelezi unaendelea ukikamilika watafikishwa Mahakamani.”
Upande wa Nondo amesema “Licha ya kufunguliwa Mashtaka, mimi pia nilifungua jalada la kesi kwa OCCID dhidi ya Polisi Kituo cha Kati aliyetumia "Unreasonable Force" dhidi yangu kwa kunipiga kinyume na PGO kifungu cha 15 na 16.”