Kwa wasiomjua mh. Hamad rashid (mb)

Tuondolee upupu wako hapa haya mambo yake binafsi na biashara zake yanahusu nini, hii ni sawa na ujinga wa kusema mbowe na biasharazake mara hivi mara vile au kumsema slaa na uliokuwa upadri wake na ccbrt.
Lete hoja acha majungu ndungu yangu

Nyoka katolewa pangoni au siyo? anazungumziwa Hamad kama mtu mwenye tabia anayoiendeleza ya ubinafsi na ubishi usio na maslahi kwa taifa.

Hivi anakomalia nini mambo ya bara wakati kwa mdomo wake Zanzibar ni nchi huru. Au ndiyo kutaka ukewenza ukiwa kwa mume mwingine. Huo ni Umalaya kwa maana halisi
 
Kaka nadhani uko nyuma sana na issue inavyokwenda hawa nccr,tlp na udp walishaambiwa waachane na cuf wakagoma so ulitaka walazimishwe??? Go to hell all vibaraka wa ccm
Mkuu,
Mwanzoni, CDM walitaka kushirikiana na CUF tu bila ya hao NCCR,UDP,TLP
sasa, CDM inataka nccr,tlp na udp waachane na CUF ili iwashirikishe.
Mkuu, hapa sielewi kitu..tafadhali fafanua kidogo.

kwa ulivyoandika hapa ni kuwa uko updated na issue hii.
 
Haya malumbano yanatia hasira tu.

Nimeyavumilia toka jana, ni vile tu naheshimu Forum Rules.

Ni muumini wa Muungano lakini sasa kuna chuki inajengeka ndani yangu dhidi ya Muungano.

Nataka katiba MPYA, nataka Tanganyika ya Baba na Babu yangu. I want her back!!!!!!!!!!!

Huu uhayawani wa kwenda nchi ya watu (Tanganyika) na ukapewa cheo ili ule hela ya wanatanganyika wakati wao fursa hiyo hawana ni Ushenzi wa kiwango cha juu!

Na mimi naseme katika mambo ya kijinga kabisa ambayo Nyerere alitufanyia na kutuingiza ni kutuunganisha na hawa watu. These are very difficult people to deal with yaani wagumuu haswa, watu wenye roho zilizojaa unafiki basi, hivi tufanye je kuachana na huu muungano? aah!
 
Hamad huyu ndie yule ambae viongozi wa CDM walimaliza mbinu za kumpigia magoti ili ajiunge na Chadema hapohapo awe ndie mgombea mwenza wa Slaa , Yaani Chadema mlitaka kutuwekea mtu ambae amejaa matatizo ,sasa naamini Chadema sio chama makini.

Leo amewakomalia na kuwashinda mbinu pale bungeni ,mnamuona si mtu mwema na hafai ,nafikiri mtakuwa mko au mmeachwa solemba na hamfai kabisa kuwemo kwenye siasa na mliambiwa zamani kuwa CUF ni kigogo wa siasa za upinzani hadi CCM imesalimu amri kule Zenji ,mtaiweza wapi ?
 
Kaka mimi si anti Chadema na sishabikii vyama kwani wao wanatutumia sisi kujinufaisha wao, nina mifano mingi tu hili vuguvugu unaloliona leo la chadema lilishawahi kutokea Kenya kina Mwai Kibaki wakashika madaraka wakati wao walipokuwa wapinzani kama Chadema agenda yao kuu ilikuwa katiba yaani same as here lakini walivyoingia madarakani kilichotokea twakijua kama hujui muulize koffi annan atakuambia na acampo.

Nimesema sisi ndio tunaowatuma wanasiasa wakatuwakilishe kwa maana nyepesi sisi ndio waajiri wao, inabidi kwanza tujitambue nini tunawatuwa ili wafanye yale yenye matakwa yetu na manufaa yetu na si kinyume na hapo.

Angalia vizuri post zangu utaona kuna sehemu nyingi sana nakubaliana na CDM na kiheshimu kama chama cha siasa na nawaheshimu sana viongozi wake na naamini mchango wao utasaidia kuelekea kule tunapotaka Tanzania ifike. Lakini siwezi kunyamaza na kusifia kijinga nikiona kitu ambacho kinaitoa CDM kwenye mstari kwani wakipoteza mwelekeo ile safari yetu itakuja kugeuka ndoto.

Turudi kwenye suala la NCCR, TLP na UDP kuto kuwa vyama vya upinzani, mimi naamini ni vyama vya upinzani ikiwa kosa lao kupeana bashasha na wanaccm na viongozi wa ccm bungeni basi wanakuwa wao ni wasaliti sioni mantiki ya siasa hapa. Hivi unataka kuniambia CDM watakuwa wanawanunia wenzao wa ccm eti tu wao ndio wapinzani wa kweli? Siamini watu makini kama kina Mbowe wanaweza wakawa na mawazo kama yako! Kumbuka kuwa siasa si kununiana ndio maana uliona hata ile picha ya Slaa na Pinda Slaa kakauka kucheka huku akigonga! Ndugu yangu vitendo vingine vinasababisha maneno ya kejili na kuna wengine wana upeo mdogo wa kufikiri wakachukulia zile kejeli ni kweli. Mfano kuna baadhi ya wabunge walisikika wakiwaa mbia wacdm wakati wanatoka naomba ni nukuu "Tumewazoea kukimbia, kwisha, uchoyo, weak politicians, na kwenye posho msije, mnadaiwa na mabenki,"walisikika wabunge wakisema kwa kupiga kelele" wapo watu wataanza kufikiria pengine hizi hoja zinaweza zikawa na ukweli ndani yake


Naomba niishie hapa ila ifike wakati tuvichambue hivi vyama na kuangalia je vinatekeleza malengo yetu au wanatekeleza malengo yao kama wanasiasa?

Kwa kukusaidia seriously sijui una umri gani lakini I am now 62 nimestahafu baada ya kutumikia serikali chini ya utawala (siyo uongozi) wa CCM miaka 37.

Ukiondoa Chadema huku bara vyama hivi vimeundwa na CCM kukidhi matakwa ya watoa misaada katika democrasia ya kuigiza ya vyama vingi. Na nashuhudia; Mungu shahidi pesa za walipa kodi zimetumika kuvisimika hivi vyama. Kwa hiyo uwe mwangalifu, mchunguzi, jiridhishe bila kuegemea hiari ya moyo kuwa mchakato wa CCM wa kung'ang'ania madaraka unafanikiwa kupitia vibaraka akina Mrema, Cheyo, Hamadi the list is long.

Wanachokifanya kwenye hii hoja ni kuwa na proxy control ya upinzani kupitia wapinzani mamluki. Kama una idea ya mbinu za kushinda vita lazima umjue adui yako kwa kuwa karibu naye (access) ili utumie mikakati ya kumzidi.

Nakukumbusha JK alisema watatumia platuni, ikishindwa itatumika kombania, ikishindikana bataliani ..... nk. Kwa CCM ni suicide kuwa na upinzani makini. Na sasa hivi tayari wewesoma umakini wa CDM kwa hiyo wananchi potelea mbali wana kazi moja ya kuwadhoofisha CDM from any kona kwa gharama yo yote (Ndiyo maana pesa ya Dowans italipwa tu kugharimia upuuzi huu).

ISSUE: Unasema umewachagua CDM??, na wengine wamewachgua CCM!!! ambao ni watawala; waliahidi nini wana sera, mikakati na rasilimali gani zinazotekelezeka?

Maoni yangu ni kuwa CDM wanapigania haki kwanza ambayo mtaji wake ni watu mimi na wewe. Haki hyo ieleweke (ifahamike na kila mtu) na ionekane inatendeka kutokana na Katiba ya watu, sheria nzuri kanuni na taratibu zenye kueleweka na kuwekeka moyoni na akilini. Siyo za kupandikizwa wakati ukweli (Ufisadi) umefichwa na kuendeshwa chini ya uvungu.
 
Hamad huyu ndie yule ambae viongozi wa CDM walimaliza mbinu za kumpigia magoti ili ajiunge na Chadema hapohapo awe ndie mgombea mwenza wa Slaa , Yaani Chadema mlitaka kutuwekea mtu ambae amejaa matatizo ,sasa naamini Chadema sio chama makini.

Leo amewakomalia na kuwashinda mbinu pale bungeni ,mnamuona si mtu mwema na hafai ,nafikiri mtakuwa mko au mmeachwa solemba na hamfai kabisa kuwemo kwenye siasa na mliambiwa zamani kuwa CUF ni kigogo wa siasa za upinzani hadi CCM imesalimu amri kule Zenji ,mtaiweza wapi ?

Wewe hujapata somo ni kigego
 
Hoja ya Mohamed ni kuwa vyama vya tlp,nccr,udp na cuf vimesajiliwa kama vyama vya siasa vimegombea uongozi nakupata nafasi walizopata, kifupi waligombea kama vyama vya siasa na kwa kuwa ktk uchaguzi walishinda ccm (bila kujali wamechakachua au la, uhalisia unabaki kuwa wameshinda) vyama vilivyoshindwa vinakuwa vya upinzani. Wananchi ndio waliowachagua wabunge wa cdm, cuf, nccr, udp na tlp na wakati wanawachagua walikuwa wanajua vyama vyao hivyo kwa kuwa vyama vyao vimeshindwa na ccm wote wamekuwa wapinzani. Je kwa nini cdm inajipambanua kuwa wao ndio wapinzani wa ukweli wenzao ni wa uongo (wanafiki)?

Kiukweli vyama vyote vyenye wabunge isipokuwa ccm ni vyama vya upinzani kimuonekana lakini kimtazamo na kiuhalisia wapinzani wanaweza kuwa ni cdm tu. japokuwa wabunge wa baadhi ya vyama kimsimamo ni wapinzani mf kafulila na wenzake wa nccr na baadhi ya wabunge wa cuf kifikra na kimtazamo hata kiitikadi ni wapinzani lakini wote hao wapo chini ya muamvuli wa vyama, vyama vyao vinajibainisha kuwa si vya upinzani hapo ndio utata wa muungano/ushirikiano wa wapinzani unapo jitokeza

kwa upande wangu chama hakiwezi kuwa na ushirikiano na chama wanachotofautiana KIITIKADI na kimtazamo hapo itakuwa ni USANII na si ushirikiano wenye manufaa. NDIO MAANA TUJIULIZE INAKUWAJE CCM WASHABIKIE USHIRIKIANO WA WAPINZANI WAKE? IKIWA UMOJA WAO NI MAAFA KWAO JE KWA NINI WANATAKA HAWA WAPINZANI WAWE WAMOJA TAFAKARI KISHA CHUKUA HATUA

Mkuu,
Hiyo red, kwa mantiki hii CDM ilikubali kushirikiana na CUF katika bunge lililopita ili kufanya usanii?

Kuna member mmoja alitoa mfano wa mikwaruzano,wa Obama na Hillary wakati wa kugombea kuchaguliwa kuwa mgombea urais kupitia chama chao. Uchaguzi ulipokwisha walifanya mkutano wa "heal the wounds" za campain zao. hata sasa Republicans na Democrats baada ya change of guard ya House of representatives wanaonekana wanakaa na kutenda kazi pamoja lakini pia misuguano ya kiitikadi ikiendelea.

Sasa hili enyi wachangiaji hapa hamuoni kuwa uchaguzi umeisha ,si wakati wa kampeni sasa, kwa nini chama cha "upinzani wa kweli" au chama "pekee" cha upinzani hakitumii busara hii ya kufanya kazi na vyama vyengine ili kuweza kuwa na sauti kubwa zaidi? Au CDM hawataki kuponesha makovu ya Uchaguzi?
 
Nyoka katolewa pangoni au siyo? anazungumziwa Hamad kama mtu mwenye tabia anayoiendeleza ya ubinafsi na ubishi usio na maslahi kwa taifa.

Hivi anakomalia nini mambo ya bara wakati kwa mdomo wake Zanzibar ni nchi huru. Au ndiyo kutaka ukewenza ukiwa kwa mume mwingine. Huo ni Umalaya kwa maana halisi

Mwanangu huyu kaonja asali sasa anachonga mzinga.
Amefikia sasa amejiona Gavana toka Zenj kaja kuiwakilisha zenj kwenye koloni lao la Tanganyika.huyu anatakiwa kuMmalawi ajambe huko aone kama hakunyea debe!
kichefu chefu!
 
Haya malumbano yanatia hasira tu.

Ni muumini wa Muungano lakini sasa kuna chuki inajengeka ndani yangu dhidi ya Muungano.

Nataka katiba MPYA, nataka Tanganyika ya Baba na Babu yangu. I want her back!!!!!!!!!!!

Huu uhayawani wa kwenda nchi ya watu (Tanganyika) na ukapewa cheo ili ule hela ya wanatanganyika wakati wao fursa hiyo hawana ni Ushenzi wa kiwango cha juu!

Na mimi naseme katika mambo ya kijinga kabisa ambayo Nyerere alitufanyia na kutuingiza ni kutuunganisha na hawa watu. These are very difficult people to deal with yaani wagumuu haswa, watu wenye roho zilizojaa unafiki basi, hivi tufanye je kuachana na huu muungano? aah!

Wakuu,
Bunge letu, wabunge wetu na watawala wetu wakilitaka hili la kuirejesha Tanganyika yetu basi ni kama kufumba na kufumbua.
Ajabu kubwa 2011 Rais amesema tutafanya sherehe za kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara!!???
Yaani hili neno Tanganyika hata hawataki kulisikia.Hata sisi wananchi hatuko serious kudai Tanganyika yetu. Tunapenda kufurahisha JF tu!
JokaKuu anasema Bunge la Tanzania ni "de facto" bunge la Tanganyika lakini Bunge hili linashindwa kuirejesha Tanganyika kama nchi moja iliyounda muungano.
G55 walipotea..lakini tunao wengine wenye uchungu na Tanganyika.Hawa wanamuogopa nani na Mwalimu hayupo tena?
Hata hivyo nimefurahi kusikia wanaJF tunalitaja mara kwa mara Tanganyika..tupaze sauti zetu ili CDM isikie ili ipeleke hoja ya kuirudisha Tanganyika....au Katiba mpya itatatua tatizo hili?
Tusikate tamaa...tuna mfano wa kuiga Sudan ya kusini.
 
Na mimi naseme katika mambo ya kijinga kabisa ambayo Nyerere alitufanyia na kutuingiza ni kutuunganisha na hawa watu. These are very difficult people to deal with yaani wagumuu haswa, watu wenye roho zilizojaa unafiki basi, hivi tufanye je kuachana na huu muungano? aah!

Asante sana mwanangu nilipopataka ndio hapo kweli kabisa umenigusa hawa jamaa sio same spirit na watanganyika hasa hata Mungu aliwatenga na kuwaweka visiwani kivyao
Tusipoutoa huu mwiba mguu utaota cancer let time say!
 
Mohamed Rashid kaonyesha udhaifu mkubwa, hata kama zamani wa-Tanzania hawakumfahamu, sasa hivi watamjua kuwa alikuwa ni mtu aliyebeba maslahi binafsi. jana Bungeni ndo kajimaliza kabisa ki-SIASA, hana maana ni watu wanaotumiwa kuibaka demokrasia. Historia Itawasuta.
 
MBOWE NA HAMADI RASHIDI NANI MBINAFSI ? Hamadi anapendelea watu wa kabila gani ? Mtu kuwa mkurugenzi wa kampuni kunatatizo gani ? hiyo ni sifa ya uchapakazi ! Hata wewe unaweza fungua kampuni yako umekatazwa ? au wewe ni sawa na nyoka wa mdimu ambaye hali ndimu lakini yeyote anayetaka kuja kuchuma ndimu anamn'gata ! nafasi zipo kwa watu wote isipokuwa tatizo ni uwezo wako mdogo na finyu ndy umekupeleka kusema na kutafuta habari za watu nakutuletea ukinzani tunapenda majungu na uzushi ! Badilika Dada !
 
Nyoka katolewa pangoni au siyo? anazungumziwa Hamad kama mtu mwenye tabia anayoiendeleza ya ubinafsi na ubishi usio na maslahi kwa taifa.

Hivi anakomalia nini mambo ya bara wakati kwa mdomo wake Zanzibar ni nchi huru. Au ndiyo kutaka ukewenza ukiwa kwa mume mwingine. Huo ni Umalaya kwa maana halisi

Mwanangu huyu kaonja asali sasa anachonga mzinga.
Amefikia sasa amejiona Gavana toka Zenj kaja kuiwakilisha zenj kwenye koloni lao la Tanganyika.huyu anatakiwa kuMmalawi ajambe huko aone kama hakunyea debe!
kichefu chefu!
 
Pamoja na wananchi kukaa kimya kwa muda mrefu na kumwacha Mh Hamad Rashid kujitia kuwa yeye ndiyo msafi kuliko wengine wote asifikiri kuwa watu hawamjui tamaa yake inayomshinda Fisi, Bwana Hamad amekuwa na tabia ya ubinafsi wa kutisha kuliko ule anao usema kwa wenzake na hata hufikia kudhuru na kuumiza watu anapotaka jambo lake litimie, Bwana Hamad uroho wake hauwezi lingaanishwa na yoyote hapa nchini kwa sisi tunaomjua narudia hufikia kudhuru hadi kuumiza iwapo anataka matakwa yake yakamilike, wananchi wanafahamu wakati akiwa yeye na wabunge majority hakukumbuka kubadilisha kanunu za bunge sababu alipenda uheshimiwa na marupurupu ya mkuu wa kambi ya upinzani choyo chake hataki kuona mwingine yupo juu yake, lakini hii leo siyo issue.
nilitaka mumuelewa Hamadi kama afuatavyo Hamadi leo hii ni mkurugenzi wa kampuni ya TALKTEL COMMUNICATIONS LTD lakini mnajua aliipataje nafasi ya ukurugenzi wakati yeye si mwasisi wa kampuni hii , Mpwa wa Hamadi aliingia talktel kama partner through local partners kwa mapenzi ya undugu alimwita Hamadi kuingia mule ndani kwa ajili ya influence ya kiserikali na kusaidia mambo fulani fulani ya PR na wakubwa lakini ilikuwa wameingiza jini baada ya hamadi kupewa kiti mle ndani alianza kuwashawishi local partner waasi ili waweze kupora hiyo kampuni kwani share alizokuwa nazo mpwa wake aliona hazitoshi alitaka zaidi nataka kuelezea ni jinsi gani asivyolidhika aliwashawishi local partner wagomee shares walizonazo lakini wale wamarekani walikataa walipokataa Bwana hamadi alianza kuwatesa na kuwafungulia kesi kila siku na kuwapeleka immigration na kuwasiliana na polisi ili wakimbie nchi mbinu za kizamani kabisa hakuangalia hata heshima ya nchi kwa wageni yeye aliona masilahi yake tu mbele ni mtu hatari kwelikweli alivuruga kampuni na mipango yake yote hadi watu wenye idea ya mradi wakasambaratika na kubakia ombaomba hapa mjini lakini yeye akiwa amebakia na kampuni hapa mjini kampuni hii hivi sasa ina operate kutokea ofisini kwake kule maeneo ya lugalo golf club ambapo mheshimiwa anaishi humohumo huyu ndiyo MH .Hamad Rashidi Aanewaambia wenzake wabinafsi wakati wakiwa wamesimama mbele ya haki, na jua huyu bwana ni mbishi lakini akibisha haya tutaweka ushahidi mwingi wa kutosha na jinsi alivyohusika uporaji wa kampuni bwana huyu hakuishia kuwafukuza investors tu, leo hii katika kundi lao la local shareholders wapatao 8 waliopora kampuni ameishakorofishana na wote wamebaki wachache nasikia hata mpwawe aliemkaribisha naye katimka leo hii yeye ndiyo mwenyekiti wa Talktel communication ltd shame on you Hamadi. Aibu zako ni kubwa kitaifa na kimataifa unaweza kupora kampuni lakini siyo haki ya watanzania wote iliyopo kihalali kwa ajili ya kutimiza matakwa yako wenye nchi hii hawatakukubalia wewe ni chui ndani ya ngozi ya kondoo .
NAOMBA KUWAKILISHA


Wewe kajifunze kwanza kuandika. Hata hivyo huna mashiko katika hoja yako. Hebu kuwa critical.
 
Mkuu kuwa na posts nyingi sio kukubalika au wewe ndio uaminiwe la hasha nilichotaka kuweka hapa hakihusiani na itikadi yoyote ila nilitaka watu wamuelewe mtu huyu anapodhamilia jambo kwa faida yake huwa haangalli wengine watadhulika vipi hivyo tabia yake hii haipo tu katika siasa bali hata huko mtaani anapoendesha maisha yake ya kila siku. Hivyo ni mtu wa kunganganiza jambo hata kama halina tija kwa watu bora yeye amelitaka, siandiki ili kushindana kwa wingi wa post ila nitaandika nikapoona nahitaji kuandika au kufahamisha jambo lisilojulikana.
 
Tuondolee upupu wako hapa haya mambo yake binafsi na biashara zake yanahusu nini, hii ni sawa na ujinga wa kusema mbowe na biasharazake mara hivi mara vile au kumsema slaa na uliokuwa upadri wake na ccbrt.
Lete hoja acha majungu ndungu yangu

Vipi? Huoni?
 
Back
Top Bottom