Mkuu haya maneno yako nishawahi kumweleza huyu shossi. Hatamie nilimwambia wewe ni cuf,ila unaogopa kujionyesha.Mohamed,
issue hapa si kafulila au cheyo kuchekeana na wabunge wa ccm ama wabunge wa cdm kununiana na wabunge wa ccm.
issue hapa ni ushirika uliopo miongoni mwa viongozi wa vyama hivyo.
1.Augustine lyatonga mrema siku zote amekuwa akimfanyia kampeni kikwete huku akiwapondea cdm, naye utasema ni mpinzani wa kweli?wabunge wa cdm watakuwa wanaongea naye kama mtanzania mwenzao lakini hawawezi kumuaminikatika masuala muhimu ya kisiasa.
2John cheyo alikuwa akimfanyia kampeni kikwete, tena huyu mwaka jana kwenye bunge lililopita kambi ya upinzani ilimtimua uenyekiti wa kamati baada ya kwenda kinyume na msimamo wa kambi, naye utamuita mpinzani wa kweli?lakini wabunge wa cdm wanaongea naye na kuishi naye kama mtanzania mwenzao sio mtu serious katika opposition politics.
3.James mbatia wa nccr mageuzi amekuwa na uhusiano mbaya sana na cdm, kampeni zake za ubunge kwa tuliokuwa dsm tunajua hujuma laiyoiendesha dhidi ya mh.halima mdee na cdm lakini wananchi waliamua kumchagua halima mdee, na kwa kuzingatia mazingira ya akina kafulila, moses machali, mkosamali na bi.zaituni wote hawa ni wabunge kupitia nccr mageuzi waliondoka cdm kwa matatizo mbalimbali.Kwahiyo wanaongea na kujumuika na wabunge wenzao wa cdm lakini katika hali halisi hawawezi kushirikiana seriously na cdm unless ututhibitishie kwamba mbatia maeacha bifu na cdm.
Kwahiyo ndugu yangu pamoja na kujaribu kuwa advocate wa cuf na ni haki yako na muda huo huo kujaribu kutudanganya kwamba wewe si anti cdm, unakuwa unatuongopea.kila mara tunakusoma kiongozi msimamo wako yunaeleweka huna sababu ya kuwakana cuf wakati kila uchao unawatetea.Kitu cha msingi ni kusimama na facts, upenzi wa chama ama ufuasi wa chama ni jambo la kawaida sana-hizi siasa unazotuletea kwamba wewe sio mwanasiasa si zenyewe, wewe ni mwanasiasa inawezekana hujitambui ama unataka kutughilibu.
Wewe kajifunze kwanza kuandika. Hata hivyo huna mashiko katika hoja yako. Hebu kuwa critical.
Mkuu katavi yaani baada ya kutumia nguvu nyingi sana za kujaribu kuelewesha watu wanachokipost ni cha kusikia na si kuthibitika tu kurudisha macho juu naona mleta mada ana post 3 yaani nimechoka ile mbaya inaonyesha huyu ameingia humu JF kwa dhumuni moja tu. Mimi sidhani kama siasa ni kuchukiana, kugombana kunakoambatana na kuchafuana. Naamini siasa ni kuwatumikia wananchi ili kuwaletea maendeleo basi sisi kama waajiri wa hao wanasiasa tujue tunayoyataka tusiamuliwe na wanasiasa! Lazima ifike mahali wanasiasa watuheshimu na waache mambo ya kuchafuana na kutukanana binafsi sikufurahiwa na kejeli za jana bungeni! na sitapenda kejeli zile ziendelezwe hapa JF kwani sisi na wale watoa kejeli hatutakuwa na tofauti yoyote.