Kutuma salamu za pongezi kwenye mkutano wa AU kwa miaka saba mfululizo, ni mambo gani anayojali Xi Jinping?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,036
VCG111342442678.jpg


Hivi karibuni, Rais Xi Jinping wa China alituma salamu za pongezi kwenye Mkutano wa 37 wa Wakuu wa Nchi za Umoja wa Afrika. Huu ni mwaka wa saba mfululizo akiendelea kutuma salamu kwenye mkutano huo. Huu ni mkutano wa kwanza wa kilele kufanywa na Umoja wa Afrika tangu ulipojiunga rasmi na G20, na mwaka huu China na Afrika pia zitafanya mkutano mpya wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika FOCAC.Je, ni mambo gani anayojali Xi Jinping kuhusu maendeleo ya Afrika na uhusiano kati ya China na Afrika miaka hii?



Kwanza, China inathamini na kuunga mkono Afrika kujiendeleza kisasa kwa mbinu za kujiamulia. Katika miaka ya hivi karibuni, ikisukumwa na Ajenda ya 2063 ya Umoja wa Afrika, kutambua Afrika mpya ya utangamano, amani na ustawi ni njia ya kisasa iliyochaguliwa na nchi na watu wa Afrika. Katika Mazungumzo ya Viongozi wa China na Afrika yaliyofanyika mwaka jana nchini Afrika Kusini, rais Xi Jinping aliahidi kuwa China itakuwa mwenzi wa Afrika inapojiendeleza kisasa na kupendekeza hatua tatu za kusaidia maendeleo ya Afrika katika sekta za viwanda, kilimo cha kisasa na uandaaji wa watu wenye ujuzi, ambazo zinaendana sana na mahitaji ya maendeleo ya kisasa ya Afrika. Hivi sasa, China inatafuta maendeleo ya kisasa ya kichina na inakaribisha nchi za Afrika kunufaika na maendeleo yake. Mwaka jana, kiwango cha biashara kati ya China na Afrika kiliweka rekodi mpya ya kihistoria ya dola za Marekani bilioni 282.1, na China imekuwa mwenzi mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika kwa miaka 15 mfululizo. Wakati huo huo, uzoefu wa mbinu za China za kujiendeleza kisasa pia umevutia ufuatiliaji na utafiti kutoka kwa Waafrika.



Pili, China inashuhudia na kuhimiza kuongezeka kwa hadhi na ushawishi wa kimataifa wa Afrika. Miaka kumi iliyopita, wakati Afrika ilipochukuliwa na nchi za Magharibi kama "bara lililokata tamaa", Xi Jinping, ambaye alitembelea nchi za Afrika kwa mara ya kwanza kama rais wa China, aliliita "bara lenye matumaini" na akaongoza ushirikiano kati ya China na Afrika katika miaka inayofuata mpaka ukafikia kiwango cha juu zaidi kisicho na kifani na kukuza kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Afrika. Hii imepelekea mataifa yenye nguvu za jadi kama vile Marekani, Ulaya, na Japani kuiangalia kwa jicho lingine na kuizingatia tena Afrika. Mwaka jana, Ethiopia ilialikwa kujiunga na kundi la BRICS na Umoja wa Afrika ukawa mwanachama rasmi wa G20. China imetoa uungaji mkono mkubwa katika masuala husika. Hivi sasa, "Dunia ya Kusini" inayowakilishwa na China na Afrika inashamiri na kuchukua nafasi kubwa katika masuala ya kimataifa. Ushirikiano kati ya China na Afrika unajumuisha dhana mpya ya uhusiano wa kimataifa unaotafuta ushirikiano wa kunufaishana na kuleta msukumo na fursa mpya kwa maendeleo ya dunia.



Tatu, China inatarajia kujenga jumuiya ya karibu ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja. Kama nchi kubwa zaidi inayoendelea na bara lenye nchi nyingi zaidi zinazoendelea, China na Afrika zilishuhudia historia zinazofanana na pia zina dhamira moja iliyo sawa. Rais Xi Jinping alitangaza katika salamu zake za pongezi kwamba mkutano mpya wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika utafanyika mwaka 2024. Kwa zaidi ya miongo miwili, Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika likiwa jukwaa muhimu la mazungumzo ya pamoja kati ya China na Afrika na mfumo madhubuti wa ushirikiano wa kivitendo, limekuwa na jukumu muhimu katika kukuza ushirikiano kati ya Afrika na China na kati ya nchi za Kusini. Inaaminika kuwa mkutano wa mwaka huu utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza mchakato wa maendeleo ya kisasa ya Afrika, na utaendelea kujenga daraja la ushirikiano kati ya China na Afrika katika nyanja mbalimbali, ili matokeo ya ushirikiano yanufaishe watu wa pande zote mbili.



Wachina husema, umbali hauwezi kuzuia watu kufahamiana ". Inaaminika kuwa chini ya uongozi wa pamoja wa wakuu wa China na nchi za Afrika, uhusiano kati ya China na Afrika kwa hakika utahimili mikiki ya kuongezeka kwa migogoro ya siasa za kijiografia na sintofahamu za kiuchumi, na kufikia kiwango cha juu zaidi.
 
Pretending that he so much cares about A-F-R-I-C-A, and not after any exploitation !!
 
Back
Top Bottom