Kutengwa kwa wafuasi wa katoliki S/wanga, Ukweli umebaki pale pale

"Kilichotokea ni kwamba nilikuta baadhi ya wajumbe CCM ambao pia ni waumini wa kanisa hilo wakisema mapadri wanamkashifu mgombea wetu kuwa ana tabia mbaya wakati wao wana mapungufu mengi," alisema Kabanga akiwanukuu waumini wenzake.

"Ndipo nilipoanza kuwatetea mapadiri wangu na kuwaambia watu hao waache kuzungumza hayo kwa kuwa sote ni wakirstu swa Kanisa Katoliki na hao ni mapadiri wetu ambao hutupatia huduma za kiroho. Niliwaambia kuwa hata wakisema hivyo leo, padri ni padri na ataendelea kuwahudumia," alisema Kabanga.

Alisema katika mkutano huo aliwaomba waumini wenzake kuacha kuwakashifu mapadiri, badala yake kuendelea kufuata misingi ya imani ya kanisa hilo huku wakisikiliza mafundisho yao na kuacha kufauata matendo wanaoyofikiri yapo kinyume na mwenendo na maadili ya mapadri hao.

Kuhusu suala la mgombea wa CCM kukufuru utatu mtakatifu, yaani Mungu, mwana na roho, Kabanga alikanusha kuwepo na kitendo hicho na kueleza kuwa kauli zake zilitafsiriwa vibaya.

"Alichosema mgombea wetu ni kuhamasisha wanachama na wapenzi wake kuchagua mafiga matatu, mafiga matatu ambayo ni rais, mbunge na diwani na si vinginevyo," alisema Kabanga.

"Hata hivyo sisi kama chama tulimwita mgombea wetu na kumsihi kuacha kutumia maneno ambayo yanagusa imani kwenye kampeni zake," alisema Kabanga.

Kuhusu kutengwa kwake, Kabanga alisema uamuzi huo unamuuma na kumkosesha amani katika maisha yake ya sasa.


"Hata ninapokuwa njiani nikitembea, najisikia vibaya kwa jinsi waumini wenzangu wanavyoniangalia na jinsi wanavyozungumzia kuwa nimetengwa na kanisa," alisema.

Naye Chiritina Ninde, ambaye pia ametengwa na kanisa hilo, aliimbia Mwananchi kuwa mgombea wa chama hicho katika kampeni zake
aliwataka wapiga kura kuchagua mafiga matatu ambayo ni rais, mbunge na diwani akirejea maandiko ya kwenye kitabu kitakatifu cha Biblia kuwa kuna nafsi tatu ambazo ni Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu ambazo Kikristo hutafsiriwa kuwa ni kitu kimoja.

Ninde, ambaye haruhusiwi kushiriki ibada, kupokea sakaramenti na huduma nyingine za kiroho zinazotolewa na kanisa hilo kutokana na kutengwa, anasema adhabu hiyo inamuumiza sana.

"Inauma sana mtu kutengwa na jumuiya uliyokuwa ukishiriki nayo katika kila kitu leo siruhusiwa kushiriki ibada wala kuhudhuria mazishi ya ndugu wala jamaa yangu ambaye kanisa litahusika... kwakweli hadi sasa sielewi cha kufanya," alisema huku akionyesha barua aliyokabidhiwa na kanisa la hilo Parokia ya Kristu Mfalme Desemba 17.

"Mimi nimezaliwa na kudumu katika imani ya kanisa katoliki hadi sasa. Sijawahi kusikia tukio kama hilo tangu kuzaliwa kwangu na wala sikutegemea kama ingefikia siku nikatengwa na kanisa."

Baadhi ya waumini walilimbia gazeti hili kuwa chanzo cha mgogoro huo ni kitendo cha kanisa hilo kutoa elimu ya uraia wakati wa kampeni, likihamasisha waumini wake kuchagua viongozi bora.


Lakini elimu hiyo ilichukuliwa na wanachama wa CCM kuwa ililenga kumsaidia mgombea wa Chadema ambaye ni Mkristo.

"Kila mara mapadri walitumia muda mwingi kuhamasisha waumini kuchagua viongozi bora huku wakitoa sifa za mtu anayefaa kuwa kiongozi. Lakini sifa hizo zilionekana kumhusu mgombea wa Chadema
jambo lililowafanya waumini hao kutafisiri kuwa mapadiri wanaipendelea Chadema," alisema muumini mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Joseph.
Hili sakata ni uchakachuaji mtupu. Nashangaa hawa watu wanasilimishwa nao hawataki. Hili ndio tatizo la watu fulani kujiona kuwa wao wamekamilika na kuchukuwa nafasi ya UUngu. Nafikiri viongozi wa kanisa nao wanakufuru kwa kudhania kuwa wao ndio waamuzi kwa imani ya mtu.

Mimi sioni sababu ya waumini walitengwa kujisikia vibaya iwapo imani zao ziko kwa Mungu wao. Hawa viongozi hawaweshi wala kuzima naiwapo wanaogopa kukosa kuzikwa watapokufa basi hilo si tatizo kwani sijasikia maiti akashindwa kuzikwa. Ninavyosikia kuwa Ukiristo umejengwa na kusamehe makosa sasa hawa wenzetu wanaposhindwa kuwasamehe wenzao ndio tuseme wanangojea mpaka 2015?
 
Thread yenyewe kajichanganya tu ili uonekane udini upo!! Mbona mara mafiga matatu mara aliitwa na kukatazwa kugusa imani za watu tukueleweje??
 
Acha misikiti ieneze huo idini na wakristu wasibaki nyuma then tuone mwisho wa siku na huyo Mkwere aliyeanzisha hili jambo
 
Buchanan Uko nje ya maada kabisa, hebu rudi JF- Great thinkers. Wanazungumziwa Wapambe, wahamasishaji, viongozi na wagombea ambao wanapiga propaganda za kuchagua kutokana na dini.

Hapa hawazungumziwi wachaguaji ambao wao bado hawana udini na ndio maada ya thread hii. Soma between the lines utagundua kuwa huo ndio ujumbe mkuu.

Jamani sio utani, kwa mnaoshabikia udini hamuelewi madhara yake. TUACHANE NA UDINI, TUZINGATIE MAENDELEO YA NCHI YETU.

Ukweli ni huu: Nchi abayo ina asilimia 30 wakristo, 35 waislamu na 35 ni dini nyinginezo ikiwa pamoja na zile za asili huwezi kulitenga kundi lolote lile kati ya hayo. Utatuzi wake ni kuweka udini pembeni na kuishi wote kama ndugu kama tulivyoishi huko awali.


Hizi Data za idadi ya Waislamu, Wakristu na wafuasi wa dini za asili umezipata wapi na ni lini ilfanyika sensa ya kufahamu idadi yao katika nchi hii? Naona itapendeza sana sensa ijayo ikajumuisha kipengele hicho.
 
Haya makanisa kuingilia siasa ndio huishia kwenye mauaji kama ilivyotokea Rwanda, kanisa ndio lililosababisha mauaji ya kimbari huko.
 
Haya makanisa kuingilia siasa ndio huishia kwenye mauaji kama ilivyotokea Rwanda, kanisa ndio lililosababisha mauaji ya kimbari huko.

Acha kukurupuka

Kama hujui jambo ni vema ukanyamaza, naamini kama hawa waumini wangekuwa sio wakristu na wametenda hilo kosa MGEKUWA MNAANDAMANA SASA TANZANIA NZIMA MKIDAI MMEONEWA,,,

Hawa watu pamoja na mbunge wao walikufuru imani yao na adhabu waliyopewa ni halali hawahitajoi huruma yako ni wao wajirudi hakuna cha chadema wala CCM
 
Ukristo unaweza kutolewa na padre?

Anatoa nini hasa?

Ukristo unaondolewaje na mtu? mambo mengine kuchekeshana tu...s/wanga shule hakuna nini?

Kwani wameondolewa ukristo au uanachama wa kanisa? Chuki zako zinakufanya uwe mbumbumbu wa mambo mengi!
 
Tunajua kwa nini hamtaki kukiri udini upo kwa sababu unawanufaisha

CCM ndio waanzilishi wa karata ya udini, baada ya kuanzisha hoja za udini (rejea mambo ya oic na kadhi) kisha wakaona inakula kwao wakakimbilia kujificha mapema eti kuna udini! Kwa kuwa wao ndio waanzilishi watajua namna ya kuumaliza udini, wasilazimishe vyama vingine kuingilia mambo yao!
 
Buchanan Uko nje ya maada kabisa, hebu rudi JF- Great thinkers. Wanazungumziwa Wapambe, wahamasishaji, viongozi na wagombea ambao wanapiga propaganda za kuchagua kutokana na dini.

Hapa hawazungumziwi wachaguaji ambao wao bado hawana udini na ndio maada ya thread hii. Soma between the lines utagundua kuwa huo ndio ujumbe mkuu.

Jamani sio utani, kwa mnaoshabikia udini hamuelewi madhara yake. TUACHANE NA UDINI, TUZINGATIE MAENDELEO YA NCHI YETU.

Ukweli ni huu: Nchi abayo ina asilimia 30 wakristo, 35 waislamu na 35 ni dini nyinginezo ikiwa pamoja na zile za asili huwezi kulitenga kundi lolote lile kati ya hayo. Utatuzi wake ni kuweka udini pembeni na kuishi wote kama ndugu kama tulivyoishi huko awali.

Zawadi unapodai wanaoshabikia udini unamaanisha akina nani? CCM wamehubiri sana udini mpaka wakaweka mambo ya kishetani ya kadhi kwenye ilani yao walipoona inakula kwao wakakimbilia kuenwza propaganda eti kuna udini kwenye vyama vingine!

Kama utakuwa fair Zawadi elekeza lawama mahali kunakostahili, otherwise unakuwa unabomoa zaidi ya kujenga! Na hizo data za Wakristo/Waislamu kwa idadi sijui umezitoa wapi, National Bureau of Statistics au vipi?
 
Mtoa Topic aidha ana ajenda yake mfukoni au chuki binafsi kwa Kanisa katoliki ima amegeuka mpiga ramli kama si hivyo angepokea taarifa elekezi iliyo tolewa rasmi na Kanisa Katoliki kuhusu hatma ya waumini wao waliokufuru IMANI Katoliki Taarifa haina kificho iko wazi Na wahusika wamekiri kuikosea imani Katoliki Wewe unae sherehesha ni nani ndani ya UKATOLIKI? Acha unafiki wala hutendi jema hasa kwa taifa lako bali unafisadi na kesho utatoa hesabu mbele ya mwenyezi MUNGU kwa huo uchochezi uufanyao dhahiri omba toba kwa imani yako upesi MWENYEZI MUNGU NI MWINGI WA REHEMA NA KUSAMEHE!
 
Hili sakata ni uchakachuaji mtupu. Nashangaa hawa watu wanasilimishwa nao hawataki. Hili ndio tatizo la watu fulani kujiona kuwa wao wamekamilika na kuchukuwa nafasi ya UUngu. Nafikiri viongozi wa kanisa nao wanakufuru kwa kudhania kuwa wao ndio waamuzi kwa imani ya mtu.

Mimi sioni sababu ya waumini walitengwa kujisikia vibaya iwapo imani zao ziko kwa Mungu wao. Hawa viongozi hawaweshi wala kuzima naiwapo wanaogopa kukosa kuzikwa watapokufa basi hilo si tatizo kwani sijasikia maiti akashindwa kuzikwa. Ninavyosikia kuwa Ukiristo umejengwa na kusamehe makosa sasa hawa wenzetu wanaposhindwa kuwasamehe wenzao ndio tuseme wanangojea mpaka 2015?

Mwanangu ili uwe na haki ya kutoa mawazo fanya utafiti! Kama kanisa limepewa mamlaka kwamba WATAKALO LIFUNGIA/LIFUNGA DUNIANI BASI LIMEFUNGWA/LIMEFUNGULIWA MBINGUNI. Kumbe basi Kanisa katoliki haliwezi kumshinda MUNGU UJASIRI AMBAYE ALIWAADHIBU MALAIKA WALIO ASI Kama Hao makafir walioasi imani hawatotubu upesi na kupokea msamaha Basi Haraka njia nyeupe Waende kwenye uislamu wakakufuru imani hiyo kama walivyo fanya waone si kutengwa na kuwapa fursa ya kutubu bali fatwa yao ni kukatwa kichwa ili wende upesi jehennam habari ndiyo hiyo mwanangu!
 
Hili sakata ni uchakachuaji mtupu. Nashangaa hawa watu wanasilimishwa nao hawataki. Hili ndio tatizo la watu fulani kujiona kuwa wao wamekamilika na kuchukuwa nafasi ya UUngu. Nafikiri viongozi wa kanisa nao wanakufuru kwa kudhania kuwa wao ndio waamuzi kwa imani ya mtu.

Mimi sioni sababu ya waumini walitengwa kujisikia vibaya iwapo imani zao ziko kwa Mungu wao. Hawa viongozi hawaweshi wala kuzima naiwapo wanaogopa kukosa kuzikwa watapokufa basi hilo si tatizo kwani sijasikia maiti akashindwa kuzikwa. Ninavyosikia kuwa Ukiristo umejengwa na kusamehe makosa sasa hawa wenzetu wanaposhindwa kuwasamehe wenzao ndio tuseme wanangojea mpaka 2015?

Mwanangu ili uwe na haki ya kutoa mawazo fanya utafiti! Kama kanisa limepewa mamlaka kwamba WATAKALO LIFUNGIA/LIFUNGA DUNIANI BASI LIMEFUNGWA/LIMEFUNGULIWA MBINGUNI. Kumbe basi Kanisa katoliki haliwezi kumshinda MUNGU UJASIRI AMBAYE ALIWAADHIBU MALAIKA WALIO ASI kama hawatotubu upesi na kupokea msamaha Waende kwenye uislamu wakakufuru imani hiyo kama walivyo fanya waone si kutengwa na kuwapa fursa ya kutubu bali fatwa yao ni kukatwa kichwa ili wende upesi jehennam habari ndiyo hiyo mwanangu!
 
"Alichosema mgombea wetu ni kuhamasisha wanachama na wapenzi wake kuchagua mafiga matatu, mafiga matatu ambayo ni rais, mbunge na diwani na si vinginevyo," alisema Kabanga.

"Hata hivyo sisi kama chama tulimwita mgombea wetu na kumsihi kuacha kutumia maneno ambayo yanagusa imani kwenye kampeni zake," alisema Kabanga


Jamani hamuoni hapo kwenye red kama si kweli kwanini walimwita na kumsihi kwenye ukweli uwongo hujitenga
 
Hata hivyo sisi kama chama tulimwita mgombea wetu na kumsihi kuacha kutumia maneno ambayo yanagusa imani kwenye kampeni zake said:
Mbona mleta mada, Aikaotana, anakwepa hii nukuu? Kwani maneno ambayo mgombea alionywa kutoyatuamia kwa sababu yanaguza imani ni yapi? Huku ndiko kuchakachua story ili kutimiza malengo binafsi
 
Back
Top Bottom