Elimu kuhusu Padre na Upadre wa kanisa Katoliki

KAWETELE

JF-Expert Member
Dec 11, 2015
682
1,612
FB_IMG_1693145038878.jpg


ELIMU YA PADRE WA KANISA KATOLIKI

(Sehemu ya Kwanza)

Na. John-Baptist Ngatunga
___________________________
Padre wa Kanisa Katoliki kwa kawaida amesoma na kulelewa kwa katika Mfumo ufuatao kwa hapa Tanzania:

Ieleweke toka mwanzoni kabisa kwamba Mapadre tuliona hapa Tanzania wamegawanyika katika sehemu au Makundi mawili kulingana na Mfumo wao wa Kimalezi:

1. Madre wa Jimbo
2. Mapadre wa Mashirika ya Kimisionari na Kitawa.

Mgawanyo huu wa Mapadre unaenda moja kwa moja pia kwa Maaskofu wetu. Ukiona Maaskofu wameandikwa Majina yao na mbele ya Majina yao ya Pili kuna vifupisho, basi ujue huyo ni Askofu na ni Mtawa au Mmisionari wa Shirika la Kitawa au Kimisionari ndani ya Kanisa. Na hicho kifupisho ni Kifupisho cha Jina la shirika lake. Hapa tunawaona Maaskofu wafuatao:

1. Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya OFMCap - Askofu Mkuu wa Dodoma

2. Askofu Mkuu Yuda Thadei Ruwa'ichi OFMCap - Askofu Mkuu wa Dar es Salaam

3. Askofu Augustine Shao CSSp - Askofu wa Zanzibar

4. Askofu Ludovick Minde ALCP/OSS - Askofu wa Moshi

5. Askofu Joseph Mlola ALCP/OSS - Askofu wa Kigoma

6. Askofu Rogath Kimaryo CSSp - Askofu wa Same

7. Askofu Beatus Urassa ALCP/OSS - Askofu wa Sumbawanga

8. Askofu Lazarus Msimbe SDS - Askofu wa Morogoro

9. Askofu Stephano Musomba OSA - Askofu Msaidizi wa Dar es Salaam

10. Askofu Wolfgang Pisa OFMCap - Askofu wa Lindi

Maaskofu wengine ambao sijawataja ni Maaskofu wa Majimbo. Rejea Orodha ya Maaskofu kama yalivyoandikwa kwenye TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC).

Turudi kwenye Mfumo wa Malezi ya Mapadre.

Ili kurahisisha uelewa wa hiki ninachotaka kukisema ni naomba nijikite zaidi kwa Mapadre wa Majimbo ambao ndio wengi zaidi kwa hapa Tanzania. Naongelea Mfumo ambao Mapadre wetu wengi wameupitia.

Baada ya Mvulana kuonesha nia ya kutaka kuwa Padre na kufuata taratibu zinazotakiwa kwaajili ya wito huo wa Upadre; Kijana huyo akishamaliza kufanya Mtihani Darasa la Saba anafanya Mitihani Miwili ya Mchujo ya Seminari. Mtihani wa kwanza unakuwa na Mahojiano ya Mdomo (Oral Examination).

Ikifaulu Mtihani huo anafanya Mtihani mwingine wa pili ambao wote waliofaulu Mtihani wa kwanza wanakusanywa pamoja. Mtihani huu wa pili unakuwa ni Mtihani wa kuandika (Written Examination). Masomo yanayoulizwa hapo ni Hisabati, Kiingereza na Dini.

Katika Mitihani hiyo, yanaulizwa Maswali ambayo lengo lake ni kupata Watoto wenye uwezo mkubwa wa uelewa. Maswali yanahitaji Fikra Sahihi. Na hapo hakuna rushwa, Michongo au connection. Anachukuliwa Mtoto aliyekidhi vigezo muhimu vya ufaulu na sio kwa kujuana au kupeana 'shavu'.

Baada ya kufaulu na kupita katika vigezo hivo, anaenda kuanza Rasmi Masomo na Maisha ya Seminari ya Mwaka wa Maandalizi (Preparatory Year) Maarufu kama Pre- Form One. Hapo atasoma kwa muda wa Mwaka 1 akifundishwa Masomo yote ya sekondari na Msisitizo mkubwa ukiwa katika Lugha ya Kiingereza.

Katika Mwaka huo Rekodi za Mitihani, Mazoezi na Majaribio yote ya Mwaka mzima zinatunzwa ili kupata Wastani wa Ufaulu ambao mara nyingi huwa kati ya 50% au 60%. Mwishoni mwa Mwaka huo wa Masomo, hufanya Mtihani wa mwisho ambao Matokeo yake pamoja na Rekodi zake zilizotunzwa zinatafutiwa Wastani.

Kama atafaulu hapo, ataanza Kidato cha Kwanza katika Seminari Ndogo yaani Minor au Junior Seminariy ambayo ni kwaajili ya Kidato I - VI kama ilivyo kwa Mwaka ule wa Pre-Form One.

Katika Masomo yake tangu anapoingia Seminari kuanzia Pre-Form One hadi Form Six Mtindo wa ni mmoja wa kumpima Mseminari huyo. Yaani kinachomfanya Mseminari huyo aendelee kubaki kwenye Mfumo huo wa Malezi yake ili awe Padre ni kuzingatia kwa ukamilifu yote muhimu katika Malezi.

Hapa naomba niseme Nyanja Kuu Tatu zinayozingatiwa sana katika Malezi ya Waseminari ili wawe Mapadre:

1. MALEZI YA KIROHO (Spiritual Formation)

Hapa Mseminari atatakiwa kulelewa katika Misingi ya Kidini yaani Maisha ya Kiroho ya kuwa karibu na Mungu kwa kuishi Maisha ya kiroho, kuwa na hofu ya Mungu, kupokea sakramenti, kushiriki katika Misa Takatifu kila siku, kushiriki katika Ibada na Majitolewa mbalimbali, kuwa katika Uchaji na kujipatia muda wa kutosha kwa Sala binafsi, Mafundisho na Mafungo ya Kiroho.

Atatakiwa alijue, alisome, alitafakari na kuliishi Neno la Mungu (Kila Mseminari ni lazima awe na Biblia Takatifu), kuzishika Amri za Mungu na Amri za Kanisa. Kuishi fadhira za Kimungu yaani Imani, Matumaini na Mapendo. Asome Vitabu mbalimbali vyenye Mafundisho sahihi ya Kiimani. Pamoja na Mambo mengine mengi sana yanayohusu Dini, Imani Katoliki na Maisha ya Kiroho kwa Ujumla wake.

2. MALEZI YA KIELIMU (Intellectual Formation)

Hapa ndio shule yenyewe ilipo. Mseminari atatakiwa kusoma kwa bidii na Maarifa ili aweze kujichotea Maarifa kwa kiwango cha juu sana. Mseminari atafundishwa vizuri na atatakiwa afaulu Mitihani yake vizuri na kukidhi kigezo vyote vya Kitaaluma kwa kufaulu vizuri sana. Atatakiwa ashirikiane na wenzake kimasomo.

Suala la Uaminifu na Uadilifu wakati wa kufanya Mitihani ni Jambo nyeti sana linalozingatiwa katika Usimamizi wake. Mseminari anayeshindwa kufikisha Wastani wa Ufaulu hawezi kuendelea na Masomo yake. Na hapo ndipo utakapokuwa mwisho wa Safari yake ya Malezi ya Upadre.

Licha ya kufaulu Mitihani, Mseminari anatakiwa kuwa na Upeo na uwezo mkubwa wa kufikiri, kuhoji, kidadisi, kuchambua, kuchanganua, kugundua na kuyahusianisha masuala na mambo mbalimbali. Hiki ni kipengele kinachohusu Maendeleo ya Akili na Fikra kwa Ujumla.

Na katika kudhihirisha Mapaji ya Roho Mtakatifu ya AKILI na ELIMU, Kanisa Katoliki linasisitiza sana umuhimu wa Elimu. Ndio maana hata Wamisionari walioleta Ukristo walikuja na kujenga 'Mafiga matatu': KANISA, SHULE na HOSPITALI ili kumkomboa Mwanadamu Kiroho, Kiakili na Kimwili.

Kipimo cha Mtihani kwa Seminari kwa kawaida hakitegemei sana Mitihani ya Kitaifa. Maana mifumo na viwango vya Ufaulu vya Seminari kiko juu kidogo zaidi ya vile vya Sekondari nyingi za hapa nchini. Lengo ni kumwandaa Padre Mtarajiwa kuwa na Upeo wa juu wa ufahamu wa Mambo zaidi ya Waamini wake atakaowaongoza kama KUHANI, NABII na MFALME.

3. MALEZI YA KIBINADAMU (Human Formation)

Katika kipengele hiki Mseminari analelewa katika Maisha ya Kijamii, nidhamu, Heshima kwa watu wote, utii kwa Sheria, kanuni na taratibu za Seminari na Mahali popote atakapokuwa. Anatakiwa kuwa Mkomavu wa Kimwili, Kiakili na Kiroho Mwenye uwezo wa kujizuia na kutunza Siri.

Atatakiwa ajitambue yeye binafsi na awatambue wengine pia na kuishi nao Maisha ya Kijamii (Social life). Atatakiwa ashirikiane na wengine katika Shida na Raha, Michezo, utamaduni, utambuzi, ukuzi na uendelezaji wa vipaji.

Ajibidishe katika Kazi mbalimbali za mikono ili kumjenga katika uwezo wa kujitegemea. Ni kosa kwa Mseminari kuwa Mvivu, Mwizi, kujihusisha na Mahusiano ya aina yoyote ya Kimapenzi, kutumia vilevi au aina yoyote ya Madawa ya kulevya.

ITAENDELEA....... Sehemu ya Pili.
 
FB_IMG_1693146125044.jpg


ELIMU YA PADRE WA KANISA KATOLIKI

(Sehemu ya Pili)

Na. John-Baptist Ngatunga
___________________________
Baada ya kumaliza Malezi ya Seminari Ndogo yaani Pre-Form One hadi Kidato cha Sita na kupata Ufaulu wa Division I au II; Mseminari ataendelea na Masomo yake katika Seminari Kuu ambako atasoma Masomo ya Falsafa (Philosophy) kwa Miaka 3 na Miaka 4 Tauhidi (Theology) na Mwaka 1 wa Uchungaji (Pastoral Year) yaani Mwaka wa kupata Uzoefu wa Kichungaji (Field). Baada ya hapo atapata Ushemasi na kuwa Padre.

Mapadre wengi wa Majimbo husoma katika Seminari Kuu zifuatazo zilizopo chini ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC):

Philosophy (Falsafa):
1. St. Antony of Padua Ntungamo Senior Seminary (Bukoba)
2. Our Lady of the Angels Kibosho Senior Seminary (Moshi)

Theology (Tauhidi):
3. St. Paul the Apostle Kipalapala Senior Seminary (Tabora)
4. St. Karoli Lwanga Segerea Senior Seminary (Dar es Salaam)

Pia kuna Seminari Kuu ambayo hapo awali ilikuwa chini ya Watawa wa Mtakatifu Benedicto (OSB) wa Abasia ya Peramiho iliyoko Jimbo Kuu la Songea Mkoani Ruvuma anayopokea kwa kiwango kikubwa ana Waseminari wa Majimbo yaliyo chini ya Majimbo Makuu ya Songea na Mbeya:

5. St. Augustine Peramiho Major Seminary:
Philosophy (Falsafa) na Theology (Tauhidi)

Mseminari yeyote anayetaka kuendelea na Masomo yake ya Upadre katika Seminari Kuu ni lazima awe na sifa za Kitaaluma sawa na yule Mwenye sifa za kwenda kusoma chuo kikuu popote duniani. Ndio maana nimesema ni lazima Kidato cha Sita afaulu kwa kupata Division I au II.

Nje ya hapo, atatakiwa akasome kwanza Diploma ya Fani yoyote ile ili apate sifa sawa na yule anayeweza kusoma Shahada ya kwanza katika chuo kikuu au Taasisi yoyote ya Elimu ya Juu.

Kama ilivyo desturi ya Masomo ya Theology ambayo ili uwe na sifa ya kusoma Theology kwa kiwango cha kutaka kupata Shahada ni lazima kwanza usome na kumaliza Kozi za Falsafa basi. Kwa mantiki hii ieleweke pia kuwa hakuna Padre wa Kanisa Katoliki ambaye hajasoma Falsafa. Na maana rahisi ya FALSAFA ni "Elimu ya Elimu zote."

Na katika Miaka ya Falsafa, atawasoma Historia ya Falsafa (Ancient, Medieval, Modern na Contemporary). Atawasoma Wanafalsa mbalimbali kuanzia Wayunani wa Kale (Ancient Greek Philosophers) na wengine wote hadi Wanafalsafa wa Karne hii ya 21.

Atasoma Kozi zote za Falsafa unazozifahamu na usizozifahamu na kufaulu kwa kiwango kisichotiliwa Mashaka. Akishindwa kukidhi vigezo vya Ufaulu hawezi kuendelea na Masomo yake ya Upadre.

Akimaliza Falsafa kwa Miaka 3 na kupata Degree, ataendelea na Masomo ya Theology ambako atasoma Maandiko Matakatifu (Biblia) kwa undani, Sakramenti, Maisha ya Kiroho, Maadili ya Kanisa, Imani ya Kikristo na Imani za Dini nyingine, Uchungaji, Liturujia, Historia ya Kanisa, Sheria za Kanisa, Katekesi na mengine.

Licha ya Masomo hayo ya Darasani, Mseminari atajifunza mambo mengine mengi tu kama vile: Lugha mbalimbali, Muziki, Kompyuta, Sheria, Ujasiliamali, Ualimu, Ushauri na Unasihi, Michezo, Sanaa na Utamaduni, Ufundi na mengine mengi yatakayomsaidia katika Utume wake katika Maisha ya Kichungaji.

Baada ya kumaliza Masomo yake ya Upadre katika Seminari Kuu, kunakuwa na utaratibu tofauti tofauti kutegemeana na Jimbo au Shirika la Kitawa. Lakini kikubwa ni kwamba wapo wanaomaliza Seminari Miaka yote 7 ya kukaa Darasani (Miaka 3 Falsafa na Miaka 4 Tauhidi) wakimaliza wanarudi Majimboni kupata Daraja ya Ushemasi ambao wanautumikia kwa Miezi isiyopungua 6 na kisha Kupadrishwa.

Lakini wengine wakimaliza Masomo yao ya Mwaka 3 wa Tauhidi sawa na Mwaka wa 6 (yaani Miaka 3 ya Falsafa Miaka 3 ya Tauhidi) wanaenda Mwaka wa Uchungaji ambao ni Mwaka 7.

Baada ya kumaliza Mwaka huo wa 7 hurudi Seminarini kumaliza Mwaka 4 wa Tauhidi ambao watasoma Miezi 6 watarudi kupata Daraja ya Ushemasi, kisha wanarudi tena Seminarini kuendelea na Masomo yao wakiwa Mashemasi. Baada ya hapo hurudi Majimboni kwao tayari kuipokea Sakramenti Takatifu ya Upadre.

Ndugu zangu; kuwa Padre sio mwisho wa kusoma kwa Padre wa Kanisa Katoliki. Baada ya Kupadrishwa, Padre anaweza kupelekwa tena Masomoni muda na wakati wowote kutegemeana na hitaji la Jimbo. Hapo atapelekwa kusomea chochote kile ambacho Mhashamu Baba Askofu wa Jimbo husika ataona inafaa kwa kushauriana na Waandamizi wake.

Padre husika atapelekwa kwenye Chuo Kikuu chochote. Kumbuka mpaka hapa tayari anakuwa ana Degrees 2 (Falsafa na Tauhidi). Lakini ataendelea na Masomo hukoChuo Kikuu ili kuendelea kujipatia Maarifa. Elimu ni Moja ya Mapaji Saba ya Roho Mtakatifu pamoja na Akili. Hivo, Mapadre wanasoma soma kwa kiwango cha juu sana.

Na kama sikosei, nadhani kuanzia Mwaka 2012 kuna utaratibu hapa Tanzania kwamba kila Padre anayetakiwa kuteuliwa kwa nafasi ya Uaskofu ni lazima awe na Shahada ya Uzamivu yaani Shahada ya Juu kabisa ya Udaktari (Philosophiae Doctor-PhD) ya Fani au Taaluma yoyote.

Hapa tuelewe kuwa Udaktari ninaouzungumzia hapa sio Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) bali Udaktari wa Kitaaluma wa kukaa Darasani: kusoma na kufanya Tafiti.

Hapa naomba sana ieleweke vizuri sana kuwa zaidi ya 90% ya Maaskofu wa Kanisa Katoliki hapa nchini ni Madaktari wa Falsafa katika Taaluma mbalimbali (They are Doctors of Philosophy in different Specializations).

Japo mara nyingi sana huwa wanatambuliwa tu kwa Cheo cha MHASHAMU ASKOFU MKUU.....au MHASHAMU ASKOFU....Laiti kama wangekuwa ni Watu wa kujikweza kama wafanyavyo baadhi ya walioheshimishwa kwa Udaktari wa Heshima pengine ilitakiwa tuwe tunawatambua kwa MHASHAMU ASKOFU DOKTA...........(PhD).

Ni Wasomi hawa watu lakini basi tu huwa hawaringi na hawajikwezi. Ila kiukweli kule 'ghorofani' kwao huwa kunafikiri ipasavyo. Wako vizuri sana hawa Mababa Maaskofu, Mapadre na Mashemasi. Kielimu Viongozi hawa wako mbali sana kuliko hata wanavyojionesha na tunavyowachukulia wengi wetu.

ITAENDELEA....... Sehemu ya Tatu
 
ELIMU YA PADRE WA KANISA KATOLIKI

(Sehemu ya Tatu)

Na. John-Baptist Ngatunga
___________________________

Sifa za Kipee za Viongozi wa Kanisa Katoliki:

1. Baadhi ya Sifa hizo ni kwamba, Viongozi hawa kwa kawaida huwa hawahangaiki na Vioja; wanahangaika na Hoja. Ukija na Hoja watakujibu kwa Hoja; ukija na Vioja wala hawakuhoji. Wanajibu Hoja kwa Hoja sio Hoja kwa Vioja.

2. Mfumo wao wa kutatua changamoto daima huwa ni Majadiliano zaidi kuliko Mabishano. Hawawezi na hawapendi kubishana, ila wanapenda kujadiliana. Hii ni kwasababu wanajua kuwa kubishana ni kutaka kujua nani yuko sahihi ila kujadiliana ni kutaka kujua nini kipo sahihi.

3. Wanapenda kucheza na Masuala (Issues) sio watu. Wanajadili Masuala hawajadili sana Matukio au watu. Ndio maana hata linapotokea jambo la Kitaifa kama hili suala la Mkataba wa Bandari kati Tanzania na DP World waliongelea suala lenyewe yaani MKATABA na wakajikita katika Hoja hiyo. Hawajamlenga Mtu au Watu. Wamezungumzia Mkataba (Issue) sio Watu na Dini zao au Makabila yao.

4. Hawana desturi ya kukurupuka katika Maamuzi yenye maslahi mapana kwa Jamii. Wanajipa muda wa kutosha kulitafakari jambo, kusali na kuliombea Taifa au Jamii, kufanya Tafiti juu ya jambo kabla ya kutoka hadharani na matakamko. Ndio maana wakitoa WARAKA au TAMKO unakuwa Mjadala wa Kitaifa. Na ndiyo desturi ya Wanafalsafa (They don't rush to conclusion without premisses).

Tofauti na baadhi ya Taasis ambazo hukurupuka tu kama chafya na kutoa matamko bila kufanya Tafiti. Wakati mwingine badala ya kujikita katika NINI, wao wanajikita katika NANI. Badala ya kujibu Hoja kwa Hoja wenyewe wanawashambulia watoa Hoja. But it's not to the Catholic Church.

5. Kwa kuzingatia historia ya Maisha yao ya Kitaaluma, usomi, akili, upeo na uelewa mkubwa walio nao; itoshe tu kusema kuwa Kanisa Katoliki ni moja ya Taasisi zinazoongozwa na Viongozi wenye Matumizi mazuri sana Akili. Na kwamba 'Intelijensia' ya Kanisa Katoliki huwa haibabaishi, haibahatishi, haikisii, haikurupuki, haionei, haidanganyi. Ipo objective na inatenda haki.

6. Na kutokana na hilo sitakuwa nimekosea nikisema, "The Catholic Church is the Big Brain Institution; Full of Competent, Confident and Confidential Intellectuals led by the Power of the Holy Spirit to lead God's people bodily and Spiritually" (Kanisa Katoliki ni Taasisi yenye Akili kubwa; iliyojaa Wasomi Mahiri, wanaojiamini na wasiri wanaoongozwa na Nguvu ya Roho Mtakatifu kuwaongoza watu wa Mungu Kimwili na Kiroho).

7. Viongozi hawa ni Watu wenye Moyo wa kusaidia sana Jamii kwa kutoa Huduma mbalimbali za Kijamii ili kuiinua Jamii kutoka Lindi na Tupe la Umasikini. Angalia Huduma za Kijamii zitolewazo na Kanisa: Elimu, Afya, Maji, Nishati ya Umeme, Ajira, na nyingine nyingi.

8. Hawa Viongozi wakiliamua jambo lao, ni lazima tu litafanikiwa kutokana na umakini, umahiri, uchapakazi, kujitoa, uadilifu, Imani. Angalia Jinsi Taasis za Elimu na Afya wanazozianzisha, kuzisimamia na kuziendeleza zinavyofanya vizuri: Angalia Vyuo Vikuu kama:
(i) St. Augustine University of Tanzania (SAUT)
Pamoja na Vyuo vyake Vishiriki vyote

(ii) Ruaha Catholic University (RUCU)

(iii) Catholic University of Health and Aliened Sciences (CUHAS -BUGANDO)

(iv) Mwenge Catholic University (MWECAU)

Sijavitaja Vyuo vya Kati, Seminari Ndogo na Shule za Sekondari ambazo zinafanya vizuri sana Kitaifa na Shule za Msingi.

Angalia pia Hospitali mbalimbali:
(i) Hospitali ya Rufaa Bugando (Mwanza)
(ii) Hospitali ya Peramiho (Ruvuma)
(iii) Hospitali ya Ndanda (Mtwara)
(iv) Hospitali ya Ifakara (Morogoro)
(v) Hospitali ya Lugarawa (Njombe)

Zijavitaja Vituo vya Afya na Zahanati.

Na kwa hapa Tanzania ukiiondoa Serikali katika suala la utoaji wa Huduma za Jamii, Taasis inayofuata ni Taasis inayoongozwa na Viongozi hawa: Maaskofu, Mapadre, Watawa (Mabrother na Masista) yaani Kanisa Katoliki. Na usipolitaja Kanisa Katoliki kwa hilo utakuwa aidha haujui au unachuki binafsi.

9. Viongozi wa Kanisa Katoliki wanaupenda UKWELI. Na Mtumishi wa Mungu Father John Hardon, SJ aliwahi kusema, "Our Duty as Catholics is to know the Truth; to live the Truth; yo defend the Truth; to share the Truth with others; to suffer for the Truth" (Kazi yetu kama Wakatoliki ni kuujua Ukweli; kuuishi Ukweli; kuulinda Ukweli; kuutetea Ukweli; kuwashirikisha wengine Ukweli; kuteseka kwaajili ya Ukweli).

Na kimsingi huyo UKWELI ni YESU KRISTO. "Yesu akawaambia, 'Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba; ila kwa njia ya Mimi'" (Yohane 14:6)

10. Kutokana na ukweli huo, Viongozi hao wa Kanisa Katoliki huheshimiwa sana na Waamini wao. Na hapa nikuambie tu ukweli kwamba kwa Muamini Mkatoliki, anawaheshimu Viongozi hawa pengine kuliko Kiongozi wa aina yoyote ile unayoijua wewe.

Na linapotokea jambo lenye ukinzani kati ya Viongozi wao na Mtu au kundi fulani la watu, ni rahisi sana kwa Mkatoliki kuufuata upande wa Viongozi wao. Ukitaka kuamini hiki ninachokuambia, fuatilia suala zima la TAMKO LA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA (TEC) KUHUSU MKATABA WA BANDARI.

Sio kwamba Waamini hawa Wakatoliki wanafuata tu mkumbo la hasha. Hii ni kwasababu wanawajua vizuri sana Viongozi wao kuwa wako serious (makini) sana na mambo yao. Ni Viongozi ambao wanaongea wanachokimaanisha na wanakimaanisha wanachokiongea.

Sio kama walivyo baadhi ya Viongozi wengi wanaoleta Propaganda za kishamba na Siasa za kitoto ambazo zina athari kwa Jamii wanayoiongoza halafu wenyewe hawajali, wabinafsi na wanaoyajali matumbo yao tu bila kuwa na jicho la huruma kwa raia wengi wanaotaabika kwenye wimbi la ufukara ulipitiliza.

Viongozi ambao wakati mwingine unaweza ukadhani labda Akili zao zina makengeza. Wanatamani kukiona hiki ila macho hayana ushirikiano na mshikamano na uso wao. Ni Viongozi ambao wanajua Ukweli lakini hawako tayari kukusema ukweli au wanaogopa kumshauri Boss wao kisa tu Boss ameshaonesha mwelekeo fulani wanaoujua kwahiyo wanaogopa kumshauri tofauti na ukweli kwa kuogopa kuvipoteza Vyeo vyao.
Very hopeless Leaders!!

11. Viongozi wa Kanisa Katoliki wana BUSARA. Na ninaposema Busara namaanisha, "Matumizi sahihi ya Maarifa". Ni wasomi walioelimika. Yaani ni wasomi wanaojua kuitumia Elimu yao kwa manufaa yao na manufaa ya Jamii inayowazunguka.

Unajua, hapa Tanzania tuna Wasomi wengi sana na tuna Viongozi wengi sana Wasomi ambao hawajafanikiwa kuelimika. Waliosoma ni wengi ila walioelimika wako wachache sana. Wengi wamesoma ila wachache wameelimika.

Ndio maana tuna baadhi ya Viongozi ambao jinsi wanavyotumia Elimu na Akili zao katika baadhi ya Maamuzi huwezi kuamini kama kweli walifundishwa na Walimu wenye Vyeti halali au ni wale wa Vyeti Feki. Ukiwasikiliza jinsi wanavyotengeneza Logic zao katika maongezi unaweza ukadhani labda ni watoto wanaojifunza kuongea.

12. Viongozi wa Kanisa Katoliki ni mfano halisi wa MCHUNGAJI MWEMA ambaye Yesu Kristo Mwenyewe kwa kinywa chake alimsema, "Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema hutoa nafsi yake kwa ajili ya kondoo...... Mimi ndimi mchungaji mwema, nawajua walio wangu, nao walio wangu wanijua Mimi" (Yohane 10:11,14)

Mchungaji Mwema ana sifa kuu Tatu:
1. Mwema
2. Huitoa nafsi yake kwaajili ya kondoo wake
3. Huwajua kondoa wake nao walio wake wanamjua

Hawa Viongozi ni WEMA kwa kuwa wana NIA NJEMA na Wakatoliki na hata wale wasiokuwa Wakatoliki yaani ambao hawamo katika 'Zizi' la Ukatoliki (Yohane 10:16). Maana yake Mapadre na Maaskofu wetu ni WEMA kwa Watanzania wote.

Viongozi hawa WANAZITOA NAFSI ZAO kwaajili ya Taifa la Mungu. Ndio maana wanapambana kuzitetea Rasilimali za Taifa hili kwa manufaa ya Watanzania wote japo wasiojua wanawatukana badala ya kuzijibu Hoja zao kwa Hoja.

Wanawajua Waamini wao wanataka nini na Waamini wao nao wanawajua Viongozi wao na wanawaheshimu. Ndio maana nilisema kwa Mkatoliki kindakindaki, huwezi kumwambia chochote kinyume na Wachungaji wao akakuelewa. Hii ni kwasababu Maaskofu na Mapadre wanajuana na Waamini wao.

Hapa nimejaribu kugusia tu kwa uchache kuhusu namna Padre wa Kanisa Katoliki anavyopitia Maisha ya Kimalezi ya Kiroho, Kielimu na Kijamii kwa wale wenye Wito wa Upadre. Lakini kama ulikuwa umenifuatilia toka mwanzo nimeelezea kuhusu upatikanaji wa Viongozi hawa na Elimu zao. Sasa kazi ni kwako kupima kati ya Elimu ya Viongozi wa Kanisa Katoliki na Elimu ya hao Viongozi wanaokuongoza Kidini au Kisiasa nani wanatumia vizuri Elimu na Maarifa yao?
 
Kumbe na ww unachuki na uislam sawa wanajitahidi kusoma lakini hawana raha na maisha wala elimu zao Maana ile habari ya mwanaume kamili haiwahusu hata akifa hawezi acha nembo yake maana phd yake haibaki lakini angeacha utumwa wa kizungu angeacha familia kwahiyo ukiwa padri ni hasara kwa familia yako na taifa
 
mapadri wana soma miaka mingapi?

je, mapadri wa vijijini wanapewa posho ya kufanya kazi kwenye mazingira magumu?

Formation of Priests​

6 years Minor seminary or secondary school English system is comprised of 4 years Ordinary level and 2 years Advanced level. The Moshi Diocese minor seminary is St. James Minor Seminary in Kilema, Moshi.
The journey toward the priesthood is long and difficult, requiring many years of training. If we take the educational journey of one boy to priesthood in Tanzania today, this is how his journey will be:

1-2 years kindergarten
7 years primary education (grade school)
DSCN1330.JPG

One year spiritual formation prior to entering the major seminary:St. Charles Lwanga-Karanga Formation Center.
3 years studying philosophy, psychology, scriptures, spirituality, and liturgy Our Lady of the Angels Major Seminary - Kibosho, Moshi Diocese St. Anthony Major Seminary - Ntungamo, Bukoba Diocese
all Philosophy.jpg

4 years studying TheologySt. Paul Major Seminary - Kipalapala, Tabora RegionSt. Charles Lwanga Major Seminary - Segerea, Dar Es Salaam ArchdioceseSt. Augustine of HIppo Major Seminary - Songea Region
all Theology.jpg

One year pastoral internship or field work which includes Ordination as Deacon six months prior to the end of seminary training
IMG-20190110-WA0009.jpg

Ordination to the Roman Catholic Priesthood
 
Kumbe na ww unachuki na uislam sawa wanajitahidi kusoma lakini hawana raha na maisha wala elimu zao Maana ile habari ya mwanaume kamili haiwahusu hata akifa hawezi acha nembo yake maana phd yake haibaki lakini angeacha utumwa wa kizungu angeacha familia kwahiyo ukiwa padri ni hasara kwa familia yako na taifa

Hapana mkuu.. Padre yeyote ni Kuhani, hata Katika Biblia kuna makuhani walikuwa matowashi.. ile kuto kuoa ni kama Sadaka.. kuhusu familia .. wao familia yao ni waumini wao.
 
Viongozi wa dini wa Katoliki wote ni wasomi wa juu tangu Uhuru kwa mifumo yao jinsi walivyojiwekea.

Tena sio usomi wa kuungaunga bali ni ule wa hali ya juu sana.

Sio kama hawa jamaa wa mwendokasi na wale wa dini nyingine.

Ndio maana wako imara siku zote hawakurupukagi kwenye mambo kimhemko.
 
View attachment 2730513

ELIMU YA PADRE WA KANISA KATOLIKI

(Sehemu ya Pili)

Na. John-Baptist Ngatunga
___________________________
Baada ya kumaliza Malezi ya Seminari Ndogo yaani Pre-Form One hadi Kidato cha Sita na kupata Ufaulu wa Division I au II; Mseminari ataendelea na Masomo yake katika Seminari Kuu ambako atasoma Masomo ya Falsafa (Philosophy) kwa Miaka 3 na Miaka 4 Tauhidi (Theology) na Mwaka 1 wa Uchungaji (Pastoral Year) yaani Mwaka wa kupata Uzoefu wa Kichungaji (Field). Baada ya hapo atapata Ushemasi na kuwa Padre.

Mapadre wengi wa Majimbo husoma katika Seminari Kuu zifuatazo zilizopo chini ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC):

Philosophy (Falsafa):
1. St. Antony of Padua Ntungamo Senior Seminary (Bukoba)
2. Our Lady of the Angels Kibosho Senior Seminary (Moshi)

Theology (Tauhidi):
3. St. Paul the Apostle Kipalapala Senior Seminary (Tabora)
4. St. Karoli Lwanga Segerea Senior Seminary (Dar es Salaam)

Pia kuna Seminari Kuu ambayo hapo awali ilikuwa chini ya Watawa wa Mtakatifu Benedicto (OSB) wa Abasia ya Peramiho iliyoko Jimbo Kuu la Songea Mkoani Ruvuma anayopokea kwa kiwango kikubwa ana Waseminari wa Majimbo yaliyo chini ya Majimbo Makuu ya Songea na Mbeya:

5. St. Augustine Peramiho Major Seminary:
Philosophy (Falsafa) na Theology (Tauhidi)

Mseminari yeyote anayetaka kuendelea na Masomo yake ya Upadre katika Seminari Kuu ni lazima awe na sifa za Kitaaluma sawa na yule Mwenye sifa za kwenda kusoma chuo kikuu popote duniani. Ndio maana nimesema ni lazima Kidato cha Sita afaulu kwa kupata Division I au II.

Nje ya hapo, atatakiwa akasome kwanza Diploma ya Fani yoyote ile ili apate sifa sawa na yule anayeweza kusoma Shahada ya kwanza katika chuo kikuu au Taasisi yoyote ya Elimu ya Juu.

Kama ilivyo desturi ya Masomo ya Theology ambayo ili uwe na sifa ya kusoma Theology kwa kiwango cha kutaka kupata Shahada ni lazima kwanza usome na kumaliza Kozi za Falsafa basi. Kwa mantiki hii ieleweke pia kuwa hakuna Padre wa Kanisa Katoliki ambaye hajasoma Falsafa. Na maana rahisi ya FALSAFA ni "Elimu ya Elimu zote."

Na katika Miaka ya Falsafa, atawasoma Historia ya Falsafa (Ancient, Medieval, Modern na Contemporary). Atawasoma Wanafalsa mbalimbali kuanzia Wayunani wa Kale (Ancient Greek Philosophers) na wengine wote hadi Wanafalsafa wa Karne hii ya 21.

Atasoma Kozi zote za Falsafa unazozifahamu na usizozifahamu na kufaulu kwa kiwango kisichotiliwa Mashaka. Akishindwa kukidhi vigezo vya Ufaulu hawezi kuendelea na Masomo yake ya Upadre.

Akimaliza Falsafa kwa Miaka 3 na kupata Degree, ataendelea na Masomo ya Theology ambako atasoma Maandiko Matakatifu (Biblia) kwa undani, Sakramenti, Maisha ya Kiroho, Maadili ya Kanisa, Imani ya Kikristo na Imani za Dini nyingine, Uchungaji, Liturujia, Historia ya Kanisa, Sheria za Kanisa, Katekesi na mengine.

Licha ya Masomo hayo ya Darasani, Mseminari atajifunza mambo mengine mengi tu kama vile: Lugha mbalimbali, Muziki, Kompyuta, Sheria, Ujasiliamali, Ualimu, Ushauri na Unasihi, Michezo, Sanaa na Utamaduni, Ufundi na mengine mengi yatakayomsaidia katika Utume wake katika Maisha ya Kichungaji.

Baada ya kumaliza Masomo yake ya Upadre katika Seminari Kuu, kunakuwa na utaratibu tofauti tofauti kutegemeana na Jimbo au Shirika la Kitawa. Lakini kikubwa ni kwamba wapo wanaomaliza Seminari Miaka yote 7 ya kukaa Darasani (Miaka 3 Falsafa na Miaka 4 Tauhidi) wakimaliza wanarudi Majimboni kupata Daraja ya Ushemasi ambao wanautumikia kwa Miezi isiyopungua 6 na kisha Kupadrishwa.

Lakini wengine wakimaliza Masomo yao ya Mwaka 3 wa Tauhidi sawa na Mwaka wa 6 (yaani Miaka 3 ya Falsafa Miaka 3 ya Tauhidi) wanaenda Mwaka wa Uchungaji ambao ni Mwaka 7.

Baada ya kumaliza Mwaka huo wa 7 hurudi Seminarini kumaliza Mwaka 4 wa Tauhidi ambao watasoma Miezi 6 watarudi kupata Daraja ya Ushemasi, kisha wanarudi tena Seminarini kuendelea na Masomo yao wakiwa Mashemasi. Baada ya hapo hurudi Majimboni kwao tayari kuipokea Sakramenti Takatifu ya Upadre.

Ndugu zangu; kuwa Padre sio mwisho wa kusoma kwa Padre wa Kanisa Katoliki. Baada ya Kupadrishwa, Padre anaweza kupelekwa tena Masomoni muda na wakati wowote kutegemeana na hitaji la Jimbo. Hapo atapelekwa kusomea chochote kile ambacho Mhashamu Baba Askofu wa Jimbo husika ataona inafaa kwa kushauriana na Waandamizi wake.

Padre husika atapelekwa kwenye Chuo Kikuu chochote. Kumbuka mpaka hapa tayari anakuwa ana Degrees 2 (Falsafa na Tauhidi). Lakini ataendelea na Masomo hukoChuo Kikuu ili kuendelea kujipatia Maarifa. Elimu ni Moja ya Mapaji Saba ya Roho Mtakatifu pamoja na Akili. Hivo, Mapadre wanasoma soma kwa kiwango cha juu sana.

Na kama sikosei, nadhani kuanzia Mwaka 2012 kuna utaratibu hapa Tanzania kwamba kila Padre anayetakiwa kuteuliwa kwa nafasi ya Uaskofu ni lazima awe na Shahada ya Uzamivu yaani Shahada ya Juu kabisa ya Udaktari (Philosophiae Doctor-PhD) ya Fani au Taaluma yoyote.

Hapa tuelewe kuwa Udaktari ninaouzungumzia hapa sio Udaktari wa Heshima (Honoris Causa) bali Udaktari wa Kitaaluma wa kukaa Darasani: kusoma na kufanya Tafiti.

Hapa naomba sana ieleweke vizuri sana kuwa zaidi ya 90% ya Maaskofu wa Kanisa Katoliki hapa nchini ni Madaktari wa Falsafa katika Taaluma mbalimbali (They are Doctors of Philosophy in different Specializations).

Japo mara nyingi sana huwa wanatambuliwa tu kwa Cheo cha MHASHAMU ASKOFU MKUU.....au MHASHAMU ASKOFU....Laiti kama wangekuwa ni Watu wa kujikweza kama wafanyavyo baadhi ya walioheshimishwa kwa Udaktari wa Heshima pengine ilitakiwa tuwe tunawatambua kwa MHASHAMU ASKOFU DOKTA...........(PhD).

Ni Wasomi hawa watu lakini basi tu huwa hawaringi na hawajikwezi. Ila kiukweli kule 'ghorofani' kwao huwa kunafikiri ipasavyo. Wako vizuri sana hawa Mababa Maaskofu, Mapadre na Mashemasi. Kielimu Viongozi hawa wako mbali sana kuliko hata wanavyojionesha na tunavyowachukulia wengi wetu.

ITAENDELEA....... Sehemu ya Tatu
Hongera sana daaa, nilikosa hii chance ningekuwa paroko sifar
 
Back
Top Bottom