Kuruhusiwa kwa mikutano ya kisiasa nchini nani kufaidika zaidi kati ya CCM na vyama vya upinzani?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Kumekuwa na mijadala mirefu inayoendelea nchini, Kwa wananchi kujiuliza, hivi kuruhusiwa Kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa, ni nani watakaofaidika zaidi, je ni CCM au vyama vya upinzani?

Kwanza, kabla ya kutafakari ni nani atafaidika zaidi, tujiulize kwanza, nini chimbuko la kufungiwa Kwa mikutano ya kisiasa?

Tunajua wazi kuwa utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake Hayati Magufuli, ulivunja Sheria ya vyama vya siasa pale alipopiga marufuku mikutano yote ya kisiasa mwaka 2016, wakati anaelewa fika kuwa alikuwa akivunja Sheria.

Kwa kuwa tokea mwaka 1992, wakati nchi yetu iliporejea kwenye mfumo wa vyama vingi, moja ya misingi mikubwa ya mfumo huo ni kuruhusu mikutano ya hadhara Kwa vyama vyote vya kisiasa nchini, kutangaza sera zao kupitia kwenye mikutano hiyo ya hadhara.

Vile vile tutambue wazi kuwa mikutano hiyo ya kisiasa ilizuiwa Kwa vyama vya upinzani pekee, wakati chama tawala, kilikuwa kikiendelea kama "Kawa" na mikutano yake ya kisiasa nchi nzima, Kwa kisingizio kuwa ni chama tawala, kilichounda Serikali, Kwa hiyo wao pekee ndiyo wanaopaswa kuzunguka nchi nzima, kuwaeleza wananchi, maendeleo yao!

Sasa tujiulize ni sababu zipi, zilizofanya mtawaka wa wakati huo, "akurupuke" tu na kuzuia mikutano hiyo ambayo alikuwa akijua ni kuwa ni kuvunja Sheria za nchi?

Hakuna sababu nyingine iliyomfanya mtawala huyo azuie mikutano hiyo, zaidi ya woga wake kuwa kwenye uwanja sawa wa kisiasa, chama Cha CCM, kisingeweza ushindani na vyama vya upinzani.

Kwanza, watanzania watakuwa na shauku kubwa ya kuwasikiliza vyama vya upinzani, Ili kujua ni kitu gani, watawala wetu walipata "mchecheto" Hadi CCM waliamua kuvipiga marufuku vyama hivyo kufanya mikutano ya kisiasa, ambayo ni haki yao kisheria.

Pili, wananchi watakuwa na shauku kubwa kwenda kwenye mikutano hiyo, Ili kujua, ni kwanini Jeshi la Polisi, lilikuwa linazuia mikutano hiyo, wakati wao jukumu lao, Kwa mujibu wa PGO yao, ambayo ndiyo mwongozo wa utendaji wa kazi yao, siyo kuruhusu mikutano hiyo, Bali ni kupokea taarifa tu kutoka kwenye vyama hivyo na wao wanachotakiwa kufanya ni kuilinda mikutano hiyo Ili iweze kufanyika Kwa amani na utulivu. Full Stop

Kwa hiyo Kwa maoni yangu, wananchi hawatakuwa na shauku ya kwenda kwenye mikutano ya CCM, Kwa kuwa wanajua hawatakuwa na jipya, Kwa kuwa katika kipindi chote Cha tokea mwaka 2016, walikuwa "wamependelewa" wao pekee kufanya mikutano hiyo ya hadhara ya kisiasa.
 
Kwa hofu hiyo ya mikutano ya kisiasa nchini, CCM badala kujiandaa kunadi sera, maono na mipango yake wao wanachosubiri ni kujibu hoja za CHADEMA tena kupitia kikundi cha watu wanaojiita chawa wa mama!
Hao CCM kweli wameishiwa na sera!

Ni Bora basi hicho kikundi kipya Cha CHAWA WA MAMA, nacho wakakiundia jumuiya mpya ya CCM, kama zilivyo jumuiya ya vijana na jumuiya ya kinamama😀
 
Kwa hofu hiyo ya mikutano ya kisiasa nchini, CCM badala kujiandaa kunadi sera, maono na mipango yake wao wanachosubiri ni kujibu hoja za CHADEMA tena kupitia kikundi cha watu wanaojiita chawa wa mama!
Ni bahati mbaya sana this time hatuna upinzani IMARA wangeifumua CCM vibaya.
1. Kutoroshwa rasilimali za Taifa kwenda Arabuni.
2. Inflation na gharama za maisha kuwa juu.
3. Deni la Taifa kupaa bila maelezo ya kujitosheleza.
4. Kifo cha Mwendazake (Hili japo ingeonekana ni kula matapishi yao ila lingewanufaisha sana)
Ni rahisi mno kuipasua TAWALA sasa hivi kulikoni kipindi chochote.
 
Kumekuwa na mijadala mirefu inayoendelea nchini, Kwa wananchi kujiuliza, hivi kuruhusiwa Kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa, ni nani watakaofaidika zaidi, je ni CCM au vyama vya upinzani...
Watakaofaidika ni vibaka wengi waliokuwa hawapati fursa ya kwenda kukwapua maeneo tofauti kwa kisingizio cha mikutano ya kisiasa!
 
Ni bahati mbaya sana this time hatuna upinzani IMARA wangeifumua CCM vibaya.
1. Kutoroshwa rasilimali za Taifa kwenda Arabuni.
2. Inflation na gharama za maisha kuwa juu.
3. Deni la Taifa kupaa bila maelezo ya kujitosheleza.
4. Kifo cha Mwendazake (Hili japo ingeonekana ni kula matapishi yao ila lingewanufaisha sana)
Ni rahisi mno kuipasua TAWALA sasa hivi kulikoni kipindi chochote.
Nyamemba
Je una uhakika na ulisemalo?!

Kama hatuna upinzani imara, Mwendazake angewazaje kuingia "mcheketo" Hadi kuzuia mikutano ya hadhara, Hadi ya ndani ya vyama vya kisiasa vya upinzani nchini?!
 
Kumekuwa na mijadala mirefu inayoendelea nchini, Kwa wananchi kujiuliza, hivi kuruhusiwa Kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa, ni nani watakaofaidika zaidi, je ni CCM au vyama vya upinzani...
Upuuzi mtupu.
Siyo kila sheria iko sahihi na imejazwa haki.
Mfano.
Sheria za environmental zina piga marufuku Nyerere damu, Lakini zinayaacha mabwawa ya Owen yakiharibu mazingira.

Sheria zinaruhusu uwepo wa wauaji ili police wakalinde. Wasipolinda sheria inawatia hatiani.

Kwanini usivunje sheria kuondoa wauaji (Chadema) ili police na RAIA waishi kwa amani?

Amani hii tumeisherekea kwa hakuna mauaji ya mabomu na maandamano ( RIP -mwanachuo wetu) karibu mauaji chini ya SAMIA regime.
 
Ni bahati mbaya sana this time hatuna upinzani IMARA wangeifumua CCM vibaya.
1. Kutoroshwa rasilimali za Taifa kwenda Arabuni.
2. Inflation na gharama za maisha kuwa juu.
3. Deni la Taifa kupaa bila maelezo ya kujitosheleza.
4. Kifo cha Mwendazake (Hili japo ingeonekana ni kula matapishi yao ila lingewanufaisha sana)
Ni rahisi mno kuipasua TAWALA sasa hivi kulikoni kipindi chochote.
Weee nawe acha uongo bhana... magufuri asingezuia mikutano ya hadhara kama kuna upinzani dhaifu .. huo udhaifu umeupima kwa kutumia kipimo kipi ??
 
Kumekuwa na mijadala mirefu inayoendelea nchini, Kwa wananchi kujiuliza, hivi kuruhusiwa Kwa mikutano ya hadhara ya kisiasa, ni nani watakaofaidika zaidi, je ni CCM au vyama vya upinzani...
Wananchi watafaidika zaidi.
 
Rais kuruhusu hii mikutano ya hadhara mwaka huu 2022/2023 ni nzuri sana kwa CCM kwa sababu mpaka kufika 2025 Wapinzani na agenda zao za kukosoa zitakuwa zimezoeleka kwa wananchi kwa hiyo CCM haitapata wakati mugumu 2025 na kasori nyingi watakuwa wamesolve ndani ya kipindi hikiii hii ni CAG ya pili kwa mama. Heko kwa mama.

CCM akili nyingi sana.
 
Hao CCM kweli wameishiwa na sera!

Ni Bora basi hicho kikundi kipya Cha CHAWA WA MAMA, nacho wakakiundia jumuiya mpya ya CCM, kama zilivyo jumuiya ya vijana na jumuiya ya kinamama
Ni jumuia mpya ndani ya chama, kwani haukuwa ukilifahamu hilo.
JUMUIA YA CHAWA WA MAMA.
 
Ni bahati mbaya sana this time hatuna upinzani IMARA wangeifumua CCM vibaya.
1. Kutoroshwa rasilimali za Taifa kwenda Arabuni.
2. Inflation na gharama za maisha kuwa juu.
3. Deni la Taifa kupaa bila maelezo ya kujitosheleza.
4. Kifo cha Mwendazake (Hili japo ingeonekana ni kula matapishi yao ila lingewanufaisha sana)
Ni rahisi mno kuipasua TAWALA sasa hivi kulikoni kipindi chochote.
Hiyo number 4 waliofurahia kifo cha Jiwe ni wengi mno, sasa ulitaka lizungumzweje?

Issue ya kwamba hakuna upinzani imara ni mpumbavu na zuzu tu anayeweza kuamini hivyo, kipindi cha Jiwe upinza ulikuwa imara sana na CCM ilikufa kabisa lakini kilichokuwa kikiendelea ni vyombo vya ulinzi na usalama kudhibiti upinzani huku kukishamiri nguvu za mungu-mtu ambaye alitawala kwa mkono wa chuma yaani hata chama chake hakukipa nafasi bali ilikuwepo one man show huku akipambwa na chawa wake akina Musiba, Bashiru, Polepole, Makonda, Sabaya, Jerry Muro, Ali Hapi, tumu yote ya wasiojulikana pamoja na Sukuma gang wote kwa ujumla wao.
 
kamango
Wewe kweli Bado una "hangover" ya Mwendazake!

Hivi unawezaje kutetea kuzuiliwa Kwa mikutano ya kisiasa, Kwa vyama vya upinzani, wakati huo huo chama tawala Cha CCM, kikiendelea na mikutano hiyo bila kubughuziwa na Jeshi la Polisi?😎
Pambaneni sasa, mikutano kila uchao na maandamano usiku kucha, tuone kama mtalima na kupanda kabla ya mvua hazijakata Feb.
Kama una hoja njoo uonyeshe hekari za mpunga utakazo panda na kuvuna kwa mikutano ya kisiasa
 
Ni bahati mbaya sana this time hatuna upinzani IMARA wangeifumua CCM vibaya.
1. Kutoroshwa rasilimali za Taifa kwenda Arabuni.
2. Inflation na gharama za maisha kuwa juu.
3. Deni la Taifa kupaa bila maelezo ya kujitosheleza.
4. Kifo cha Mwendazake (Hili japo ingeonekana ni kula matapishi yao ila lingewanufaisha sana)
Ni rahisi mno kuipasua TAWALA sasa hivi kulikoni kipindi chochote.
Upe muda wakati
_115176141_gettyimages-1228239935.jpg
 
Back
Top Bottom