Eng ibird
JF-Expert Member
- Nov 19, 2021
- 709
- 1,003
Ubwege ulifanya, ungechapa unatembeaHabari Wakuu
Kumekuwa na uzi nyingi kuhusu single maza wapo ambao wanawatetea na wengine wanawaponda. Mimi ni mmoja Kati ya waanga wa single maza kiukweli ni mtihani mgumu kudumu nao na hii imechangiwa na wao kuwa na akili fupi kwa asilimia kubwa labda mtu alizaa nae awe amekufa, ngoja niwape kilichonikuta.
Ndugu zangu nilimpenda mdada mmoja herufi yake inaanzia J Tena nilimkuta ana mimba ina miezi mi3 na niliona siku nimekutana nae kwenye meet tukaa chini ndio akanieleza na kuniambia huyo mtu aliyempa mimba ameikacha na ameamua kumove on ananionesha hadi message za mazungumzo yao yakionesha kweli mdadda kamove on, na sometimes aliniomba niongee na huyo aliyemzalisha baada ya kuona anamsumbua ili asimfuatilie kabisa.
Baada ya kunithibitishia wameachana nikaona niwe nae kwenye mahusiano na kiukweli nilimsaidia mpaka anajifungua na mahusiano yetu yalikuwa ya moto nikaona kabisa hapa nimepata mtu by the way mimi kwenye maisha yangu yote sijawahi kuwa na mahusiano mawili kwa wakati mmoja yeye alikuwa pekee ndugu nilitoa sana kwake kuanzia muda mpaka kifedha na yeye alinipa mapenzi yakutosha Sana.
Baada ya kupita muda kidogo hapo akiwa tayari ameshajifungua mtoto ana miezi mi4 manzi nikawa si muelewi kabisa na nikaona kuna mabadiliko nayaona kwanza akawa hanitafuti, nikimpigia simu zangu hapokei, na kuanza uswahili wa mambo mengine.
Siku moja nilimpigia simu nikashangaa kapokea mzazi mwenzake jibu alinipa ni kuwa nipo na mama watoto amelala acha kusumbua watu mkuu ilinikera Sana ile kauli nikakata simu wakati huyu manzi aliniambia ameenda kwenye msiba wa ndugu yake kumbe yupo ghetto la mzazi mwenzake. Imepita muda mchache nikakuta nimetumiwa picha mzazi mwenzake yupo na huyo manzi wangu wakipigana mabusu nilijua kabisa aliyotuma hivyo ni yule mzazi mwenzake nikama vile anatafuta bifu na mimi maana number ilikuwa ngeni kwangu na picha nyingine alimpiga akiwa uchi kalala kiupande nadhani ilipigwa bila yeye ( manzi ) kujua maana alikuwa amelala ndugu zangu sikuwahi kuwa kwenye maumivu kama yale kwenye mapenzi aisee kumbuka hapo sijafanya nae mapenzi maana nilimpa muda arecover hali yake ndio niombe mechi
NB: imagine demu nimemvumilia akiwa ana mimba na kipindi chote hicho sikuwa na manzi mwingine au kufanya mapenzi na mtu mwingine alafu the end of the day anakupiga na kitu kizito kiasi hicho