Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,554
Imepita miaka kama mitatu hivi niko katika urafiki na bibie lakini hatujawahi kuwa wote kwenye 6 x 6. Mara ya kwanza nilipanga naye lakini baada ya kupata kilaji sawasawa mi mwenyewe niliondoka pasipo kumuaga akabaki kwenye room peke yake. Mara ya pili akaniita yeye, kama kawaida tukaongea kwa nini niliondoka, sikuwa na sababu ya msingi - tukapanga siku ya kutimiza ahadi. Ilipofika siku nikamkuta kwenye eneo tayari ameishachukua na chumba - akapigiwa simu akaondoka na kuniacha na mafunguo ya hotel. Imekuwa ikitokea hivyo mara kwa mara, jana mapumziko ya 8/8 tukakubaliana kuonana tukaonana, imefika mida ya usiku tukatoka wote kwenda ku-do; historia imejirudia vilevile, nashindwa kujua ni kwa nini.... kuna ambaye iliwahi kumtokea?