Kulikoni CHADEMA baadhi ya wagombea majmboni kutorudisha fomu?!

Kilichotokea jimboni Chunya kwa mfano:Mwanachama mmoja wa CHADEMA alienda kuchukua form ya ubunge kwa tiketi ya CHADEMA,Uongozi wa mkoa wa CHADEMA ukamuwekea pingamizi kwamba sio chaguo lao na watasimamisha mgombea mwingie... TIA MAJI,TIA MAJI SIKU YA KURUDISHA FORM HII HAPA... CHADEMA haikupeleka mbadala wa yule waliyemuwekea pingamizi!

Mmm Kama hiki ndo kilichotokea basi shughuli ipo.......tena kubwa!
 
Lakini kwa upande mwingine huenda ni mahesabu tu ya Chadema -- ya ku-concentrate kwenye majimbo ambako yana angalau uhakika wa kushinda -- siyo mradi tu kugombea kila jimbo. Sababu kubwa ni fedha. Hii iliwasaidia kupata angalau viti 5 mwaka 2005, ukilinganisha na CUF (walipata zero) kwani ili mradi tu kuweka wagombea kila jimbo.

Pili, kama walivyosema wengine, huenda wagombea wa CCM wamewahonga baadhi ya wagombea wasirudishe fomu -- kwani hizi ndizo nyendo zao. Tunaanza kuona unafiki wa Takukuru -- huwa wanakuwa vipofu kuona na kushughulikia rushwa za namna hii. Upofu huu tutauona sana wakati wa uchaguzi -- wagombea wa CCM kuhonga wapiga kura na sidhani kama chombo hicho kitaingilia kwa hofu ya chama wanachokishabikia - CCM -- kupoteza Wabunge wengi.
 
Mnyamahodzo,

Sema nikupe facts zingine au unaenda na wewe kukusanya data? Kama umeridhika, nitake radhi kwa kunisema vibaya kwenye post yako ya kwanza kny thread hii......!

Tafadhali usiwe munkari. Nimekujibu kwa kukueleza ukweli.
facts gani ambazo unataka kunipa; zile kugawa vyerehani 60 kwa wakinamama wa vijiji tofauti wanaambiwa wavitumie kujiongezea kipato (that 60 being distribited, not placed at one centre), ama zile za kuorodhesha majina kwa ajili ya mbolea ya rudhuku halafu hampati mlichokihitaji na mbolea nyingine kwenda kuuzwa Songea? Ama facts za kuzigeuza ofisi za serikali ya mitaa na kujenga majengo ambayo yamefanywa zahanati ambazo Mkuu wa kituo ni Nurse Glade B, ambaye ndiye tabibu, nurse, mgawa dawa vyote yeye ili tu aonekane amewaletea wananchi huduma za hospitali karibu? No No Noooo ! Siwezi kuzikubali.

Sifahamu unamfahamu makinda toka lini namna alivyojiingiza katika siasa za Njombe.
 
Tafadhari naomba usiwe na Munkari kiasi hicho kuwa mtaratibu. Sijakusema vibaya. nimesema ukweli. Kama nawe umo ndani, utang'aka. Kitu kizuri ni kuwa facts za kuniambia barabara zinatengenezwa kila baada ya miezi mitatu, au kuanzisha MAKINDA CUP, au kuwapatia vyerehani 60 wale wakinamama wa vijiji kadhaa(kijiji kimojawapo walipewa 2) ziwaendeleze wakinamama hawa wakitanzania. Facts za namna mwalivyojiandikisha majina kwa ajili ya mbolea ya ruzuku halafu wasiopate walichoomba na mbolea kuuzwa mkoa mwingine?
Facts ya kuwataka wanachi wajenge dispensary halafu nurse Glade B (sawa na wa RED Cross) ndiyo mkuu wa kituo, tabibu, nurse, na mgawa dawa vyote yeye? nikubaliane nazo hizo.

Sijui uko Njombe kweli au uko Pwani? Unajua wewe ulipo. Kikubwa ielzee ukweli hali ya Njombe na kitu kile huyu mama alichofanya kwa watu wa Njombe; ametumia ukimya wao na uoga wao kuwakandamiza.

Jivunie; Anna makinda amewafanyia nini watu wa Njombe Kusini for 15 years? ainisha kinagaubaga.

We mwenye mawazo? Hivi umeipata hoja yangu sawa sawa lakini?

Sikiliza thread hii inajiuliza kwa nini Chadema hawajaweka candidates in some areas...then mimi nimejaribu kutoa jibu kwa Njombe kusini.....kwamba pengine kutoka na haya:
  1. Wananchi wamekuwa wakipewa mbolea za ruzuku na madawa
  2. Barabara kuu..Njombe -Ludewa imekuwa ikishindiliwa kila baada ya miezi mitatu au Sita hivi
  3. Issue ya Lumbesa sasa hivi kule ni ndoto....
  4. etc etc
Nikasema kutokana na haya, basi wapinzani wanakosa agenda mbadala (pengine)......!yaani wamekosa confidence, wamemgwaya mama.....sasa kumbe wangekuja na hoja mbdala kama yako (ya ufisadi) ambayo mimi sikuipata before wangeweza ingia kule vifua mbele......sawa?

Mimi hata siku moja sijawahi muendorse mama Makinda kama right Candidate kwa Njombe kusini hata hapo juu hakuna sehemu nimesema Makinda ni right candidate kwa Njombe kusini.....! upo hapo papaaa?
 
Nadhani ni matatizo ya kiutendaji ndiyo yalowafanya wakashindwa kurejesha hizo forms. Kwa kawaida CHADEMA mwaka huu nategemea itatisha kuliko chaguzi zake zote zilizotangulia, na kuliko chama chochote cha siasa kwa upande wa upinzani. Kikubwa ni mambo ya kusubiri na kuona.

:welcome:

Thanks
 
Tafadhali usiwe munkari. Nimekujibu kwa kukueleza ukweli.
facts gani ambazo unataka kunipa; zile kugawa vyerehani 60 kwa wakinamama wa vijiji tofauti wanaambiwa wavitumie kujiongezea kipato (that 60 being distribited, not placed at one centre), ama zile za kuorodhesha majina kwa ajili ya mbolea ya rudhuku halafu hampati mlichokihitaji na mbolea nyingine kwenda kuuzwa Songea? Ama facts za kuzigeuza ofisi za serikali ya mitaa na kujenga majengo ambayo yamefanywa zahanati ambazo Mkuu wa kituo ni Nurse Glade B, ambaye ndiye tabibu, nurse, mgawa dawa vyote yeye ili tu aonekane amewaletea wananchi huduma za hospitali karibu? No No Noooo ! Siwezi kuzikubali.

Sifahamu unamfahamu makinda toka lini namna alivyojiingiza katika siasa za Njombe.


....Sikiliza mkuu, wewe naona unazungumzia zaidi mambo ya hearsay.....! mimi nimekwambia nimeona mama yangu ana mifuko mitatu ya Mbolea ndani kwake, ana dawa ya ukungu na si yeye tu amepata hivi vitu....na ndivyo anavitaka sasa wewe unaniambiaje watu wemeandikisha then mbolea ikachengeshwa? hapo ndipo tunatofautiana na wewe....nakwambia mimi nimeona kwa macho yangu mbolea imegawiwa kijiji kizima....hadithi gani unaleta ndugu yangu?
 
....Sikiliza mkuu, wewe naona unazungumzia zaidi mambo ya hearsay.....! mimi nimekwambia nimeona mama yangu ana mifuko mitatu ya Mbolea ndani kwake, ana dawa ya ukungu na si yeye tu amepata hivi vitu....na ndivyo anavitaka sasa wewe unaniambiaje watu wemeandikisha then mbolea ikachengeshwa? hapo ndipo tunatofautiana na wewe....nakwambia mimi nimeona kwa macho yangu mbolea imegawiwa kijiji kizima....hadithi gani unaleta ndugu yangu?

Sikiliza NL, kwanza naomba nikijulishe lipo tatizo ambalo MODS wanaweza kutueleza ni kwanini NINALIPATA.Ninapojibu post narudi kwenye page niliyokuwepo as if I was refreshing na kile nilichoandika sikioni. Ndiyo maana unakuta kitu kile kile kinajirudia.

Sasa naomba kaisome ile post yako vizuri uliyonifanya nikujibu.

Ulisema miezi 3 sasa unabadilisha miezi 3 ama 6.

Unapokuja kwenye suala la shule mtu ambaye kwa Njombe hawata msahau japo kuwa vibaraka wa Makinda wanataka asahaulike ni Dr Hilman Ndembwela Ngunangwa. Ndiye aliyefanya makubwa kwa shule zote za Serikali na za NDDT. Hizi za kata ni upuuzi kujivunia kwa mtu unayeeelewa shule ni nini.

Kaisome thread yangu nilipomjibu mtoa mada nimetoa sababu kwanini huenda Makinda akawa yuko mgombea pekee.

Si kwamba hawa watu wa Njombe hawajui kitu, tatizo hawana alternative. Msemwa aliingilia huko huko kwa mafisadi, tena hakujua kumwaga fedha kama Jah People alivyomfanyia Makweta; diyo maana alishindwa.

Jifunze Alatanga akiwa TLP 2005 alivyomkimbiza Makweta japo unajua ukweli Alatanga hana elimu ya kumshinda Makweta.

Wanachi hawana mbadala. Lakini si ubora wa Makinda. Nina mashaka huenda MAkinda kawapa mlungula. zingatia HUENDA.
 
Wakuu zangu,
Mimi ningependa sana kufahamu kilichotokea!..
Kama viongozi wa Chadema kweli walichagua kutosimamisha wagombea ktk baadhi ya majimbo, nafikiri ipo kila sababu wananchi hasa sisi tunaoshabikia tupewe maelezo ya kina.
Huyo mwandalizi wa kampeni hizi sijui nani, na anayo maelezo gani maanake huu ni uzembe wa hali ya juu kabisa ikiwa kweli Chadema wameamua wao kutosimamisha wagombea majimbo 10.
Na waamini maneno yangu, gharama ya makosa kama haya itakuwa kubwa sana..
 
watakuja na maelezo ya ccm ndio wachawi.....mimi binafsi ningependa kuona demokrasia inakuwa na wapinzani wanapata nafasi hasa katika kata na majimbo (haimaanishi sitaki wapate rais). lakini naona baado. Binafsi siwasanifu kwa janga hili ila naona ambavyo bado tuna safari katika mageuzi ya siasa za tz. naamini si kosa la kiutendaji hili...hapa kuna shida ya mgombea mwenyewe sijajua though ni ipi..kuna shida ya baadhi (si lazima hawa ambao hawakurudisha fomu) ya wachumia tumbo kukubali kununuliwa ili kuuza jimbo...bado tuna njaaa bado tunataka demokrasi kidogo ina challenge sana. Nimewahi kusikia mgombea fulani alikuwa anauza ushindi wake kila uchaguzi kwa kukubali kusaini matokeo ya kushindwa ilhali anajua ameshinda...big shame! watu bado hawajajua wanataka nini lol
mix with yours
Nyie mavuvuzela mbona nyie mko hapa na hamkuchukua fomu kokote? Tupishe bwana msitutaabishe bure. Twajua tufanyalo.
 
Nyie mavuvuzela mbona nyie mko hapa na hamkuchukua fomu kokote? Tupishe bwana msitutaabishe bure. Twajua tufanyalo.
Mkuu sawa wee tukana tu lakini kumbuka ni kura zao hawa unaowasema ndizo zitakazo kupa ushindi.
Maadam unaomba kura zao , wana kila haki na sababu ya kuuliza!
 
Wakuu leo nimesikia asubuhi katika radio Wapo kuwa kuna baadhi ya majimbo wagombea ubunge wa CHADEMA hawakurejesha fomu zao hadi ilipofika jana kwa muda waliotakiwa.

Majimbo hayo ni pamoja na lile la Isimani kwa mh. Lukuvi na la Anna Makinda. Pia mengine sikuweza kuyapata maana nilipatwa na mshangao.

CHADEMA jitokezeni hapa mtueleweshe yaliyowasibu wanachama wenu hawa tena viongozi huko waliko na hawakurejesha fomu??!!

Je hii inaashiria nini?

Naamini mmeanza vizuri na ni vema mmalize vizuri. Msitoe nafasi ya changamoto kwa wagombea wengine. Kinachotakiwa ni kuongeza idadi ya wabunge mjengoni!!

Wanawaogopa wagombea wa CCM.
 
Ndugu mwenye mawazo nimekubaliana na mawazo yako hapo juu.....! Sasa hapo nilipohiglight ndicho kilichotokea Njombe kusini kwa Makinda sawa.....?

Hehehe hommie bana naona unampigie kampeni huyu bibi kiaina.... nina ushahidi kashindwa kujenga daraja tu kwenda kwa mama yake mzazi ndo alete maendeleo ya kushindilia barabara kila baada ya miezi 3 wapi na wapi? Kadaraja tu kwenda kijiji cha mama ake anashindwa kukaboresha hapo changa la macho asome alama za nyakati mwaka huu hata unaibu atausikia kwenye bomba.
 
Hehehe hommie bana naona unampigie kampeni huyu bibi kiaina.... nina ushahidi kashindwa kujenga daraja tu kwenda kwa mama yake mzazi ndo alete maendeleo ya kushindilia barabara kila baada ya miezi 3 wapi na wapi? Kadaraja tu kwenda kijiji cha mama ake anashindwa kukaboresha hapo changa la macho asome alama za nyakati mwaka huu hata unaibu atausikia kwenye bomba.

Fidel, nimefurahi kujitokeza. habari za kuvuna fiasi na mahindi?

Unajua NL kasahau ni9 kwanini Makinda hataki kwenda Kihesa. watu wale wanamchukukia jinsi alivyobadolisha position ya tank la maji. Toka pale alipo-plan Dr Ngunangwa. Matokeo ule mtaa wajuu wote wanaliona tank chini yao na maji kuyakosa. ukutaka ukachote na ndoo kisha pandisha nayo mlima hadi nyumbani kwako. wote huu
 
Back
Top Bottom