Kukumbatia na kuenzi dhana ya utawala wa kifalme kumepitwa na wakati, Waingereza na wengine wamerogwa na nani?

dalalitz

JF-Expert Member
Sep 6, 2013
3,332
1,862
Kuna huu Uongozi wa Kifalme,

Inasemekana hata Afrika zilikuwepo Tawala lukuki zilizokuwa na nguvu za Himaya za Kifalme na kwingineko Ulimwenguni pia.

Kwa Afrika, Tawala za Kifalme ingawa unaaminika kuwa zilikuwa nzuri zikiishi kwa Utulivu na amani zilikuja kuvurugwa na kutokomezwa na 'Waliojivika' sifa ya ustaarabu na kutenda kila hila mwishowe tawala hizo zikadondoka wakaleta mapokopoko yao ya Demokrasia za kinafki.

Kwa Unafki na kwa sababu za wazi zilizokusudia kunyonya kila kilicho chema na kuacha visivyopendeza tu wanafki hawa (Waingereza) wakabakisha chembechembe tu za kuwa kulikuwepo na utawala huo Afrika lakini wakiwa wameshavuruga kila kilichokuwa kinaenda vyema awali.

Hata hivyo, huko Uingereza kabla yao kusambaza vibaraka wao Ulimwenguni kufanya hila. Utawala wa Kifalme ulikuwepo miaka mingi nyuma na bado unaendelea kuwepo. Ijapokuwa utawala huu upo Kisheria, Malkia au Mfalme ni cheo kinachoitwa 'Shereheshi'.

Viumbe hawa wachache (Kiongozi wa Familia ya Kifalme) ingawa yapo majukumu yake Kiserikali lakini kwa unafki mkubwa inasemwa kuwa wakifanya shughuli hizo za Kiserikali hawalipwi lakini kumbuka upo mfuko maalumu unaotokana na Pesa ya walipakodi unaoihudumia Familia hii inapata kila uchao. Na si Pesa ya kitoto.

Wakati huohuo Familia hii inaogelea katika ukwasi mkubwa na mpana na ambao umechumwa zama na zama.
Na waingereza raia wa kawaida wakibung'aa miaka yote.

Najiuliza, hawa jamaa (WAINGEREZA) si ndio wanaohubiri siku zote swala la Demokrasia?

Kwanini wasishinikize iwapo ni muhimu kuwepo kwa aina hiyo ya Mfumo kwao, kwanini Ufalme isitafutiwe namna nyingine ya kupatikana ili kuwepo na usawa badala ya watu wachache wale kurithishana?

Itakuwa Wamerogwa vibaya sana aisee.
 
Kumepitwa na wakati kivip? Huo ndio mfumo wa maisha yao au unakata uwizi wa FISIEMU..
 
Kuna huu Uongozi wa Kifalme,
Inasemekana hata Afrika zilikuwepo Tawala lukuki zilizokuwa na nguvu za Himaya za Kifalme na kwingineko Ulimwenguni pia...
Mfumo wa ufalume upo sanaa Ulaya nzima ndo njia peke ya kulinda utamaduni na Uzalendo wa nchi zao, sisi Africa baadhi ya nchi kama Tanzania zilipotoshwa na kuua asili yao na kukumbatia hata lugha zisio eleweka na sio asili zetu kama kiswahili kiingereza nk.
 
Je, unafahamu manufaa ya kiuchumi ambayo Uingereza inayapata kila mwaka kutokana tu na uwepo wa ufalme? Ama unatazama tu upande mmoja wa gharama zinazotumika kuhudumia ufalme?

Ni mfumo gani wa kiutawala ambao kiongozi ama viongozi wa nchi hawahudumiwi kwa kodi za raia?

By the way, Uingereza ilishawahi kuufuta ufalme miaka ya nyuma. Mfalme aliyekuwa madarakani kipindi hicho aliuawa.

Baada ya miaka kadhaa wakagundua kuwa mfumo mpya wa kiutawala waliouanzisha ni mbaya zaidi kuliko hata ule ufalme uliokuwepo awali. Matokeo yake wakarejesha mfumo wa kifalme ambao upo mpaka leo.
 
Je, unafahamu manufaa ya kiuchumi ambayo Uingereza inayapata kila mwaka kutokana tu na uwepo wa ufalme? Ama unatazama tu upande mmoja wa gharama zinazotumika kuhudumia ufalme?

Ni mfumo gani wa kiutawala ambao kiongozi ama viongozi wa nchi hawahudumiwi kwa kodi za raia?

By the way, Uingereza ilishawahi kuufuta ufalme miaka ya nyuma. Mfalme aliyekuwa madarakani kipindi hicho aliuawa.

Baada ya miaka kadhaa wakagundua kuwa mfumo mpya wa kiutawala waliouanzisha ni mbaya zaidi kuliko hata ule ufalme uliokuwepo awali. Matokeo yake wakarejesha mfumo wa kifalme ambao upo mpaka leo.

Hoja yangu kuu ipo katika namna huo Ufalme wenyewe kumilikiwa na ka-familia kamoja,
Niliwaza mawili, kwanza, haina Tija kuwepo (Kwa maoni yangu) lakini iwapo itaonekana pengine ni lazima,
Je, ni kwanini usiwekwe utaratibu wa tofauti na huo wa kupeana 'kaka to kaka au dada tu dada' nk.?
Zama tulizonazo si za kukukariri mambo.
Hao mabwana ni kama wanasiasa tu, wapo na wanajipanga kwa kila hali kuendelea kuwepo miaka na miaka.

Umegusia kuhusu mapato, yes nakubali 'washamba wapo' wanaofurika kuzagaa na kushangaa wanyonyaji hao wanaonakishiwa kwa lugha tamu kama watunza utamaduni nk.
Si kweli, utaniambia UK itadondoka kusipokuwepo na Ufalme?

Inayoendelea ni ni Biashara ya kuuma na kupuliza.
Hawa Mabwana wametega mizizi ya 'kula shushu' bila kupambana kiuhalali.
Na kujua ni ka-group ka dizaini hiyo walitamani kuwa na himaya kubwa zaidi toka enzi hizo sema mazingira yamebana.

Kukushika Sikio mwaka 1991 yupo mbunge mmoja anaitwa Tony Benn aliwahi kupeleka muswada Bungeni wa kushawishi Waingereza kuondokana na Ufamle ili kuwepo na utaratibu wa kumchagua Rais lakini huko Bungeni kura kwenye muswada huo hazitosha.

Narudia tena hawa jamaa ni WANYONYAJI fikiria hawalipi income tax, hawalipi capital-gain kweli na wanakubali kumbuka ni Kafamilia kote ujue, kweli?

UCHAWI UPO SI BURE. :D
 
Huo mfumo umeishi sababu wananchi wa uingereza wa kawaida wana maisha mazuri wanayoyapata kwa urahisi..

Ingekuwa wananchi wa uingereza wengi wana njaaa.. huo ufalme ungeshakufa zamani sana
 
Kuna huu Uongozi wa Kifalme,

Inasemekana hata Afrika zilikuwepo Tawala lukuki zilizokuwa na nguvu za Himaya za Kifalme na kwingineko Ulimwenguni pia.

Kwa Afrika, Tawala za Kifalme ingawa unaaminika kuwa zilikuwa nzuri zikiishi kwa Utulivu na amani zilikuja kuvurugwa na kutokomezwa na 'Waliojivika' sifa ya ustaarabu na kutenda kila hila mwishowe tawala hizo zikadondoka wakaleta mapokopoko yao ya Demokrasia za kinafki.

Kwa Unafki na kwa sababu za wazi zilizokusudia kunyonya kila kilicho chema na kuacha visivyopendeza tu wanafki hawa (Waingereza) wakabakisha chembechembe tu za kuwa kulikuwepo na utawala huo Afrika lakini wakiwa wameshavuruga kila kilichokuwa kinaenda vyema awali.

Hata hivyo, huko Uingereza kabla yao kusambaza vibaraka wao Ulimwenguni kufanya hila. Utawala wa Kifalme ulikuwepo miaka mingi nyuma na bado unaendelea kuwepo. Ijapokuwa utawala huu upo Kisheria, Malkia au Mfalme ni cheo kinachoitwa 'Shereheshi'.

Viumbe hawa wachache (Kiongozi wa Familia ya Kifalme) ingawa yapo majukumu yake Kiserikali lakini kwa unafki mkubwa inasemwa kuwa wakifanya shughuli hizo za Kiserikali hawalipwi lakini kumbuka upo mfuko maalumu unaotokana na Pesa ya walipakodi unaoihudumia Familia hii inapata kila uchao. Na si Pesa ya kitoto.

Wakati huohuo Familia hii inaogelea katika ukwasi mkubwa na mpana na ambao umechumwa zama na zama.
Na waingereza raia wa kawaida wakibung'aa miaka yote.

Najiuliza, hawa jamaa (WAINGEREZA) si ndio wanaohubiri siku zote swala la Demokrasia?

Kwanini wasishinikize iwapo ni muhimu kuwepo kwa aina hiyo ya Mfumo kwao, kwanini Ufalme isitafutiwe namna nyingine ya kupatikana ili kuwepo na usawa badala ya watu wachache wale kurithishana?

Itakuwa Wamerogwa vibaya sana aisee.
Mfalme au malkia yupo kiutamaduni tu, si sawa na wale wa zamani ambao waliongoza nchi, hawa hawaongozi chochote kwani hawana jeshi wala mamlaka ya aina yoyote ile.
 
Mfalme analelewa kujua jamii yake tokq utoto na uongoxi na kujali maskin.demokrasia inamleta magu na phd yake fake
 
Back
Top Bottom