Kuelekea uchaguzi 2020, CCM inazidi kuimarika, CHADEMA inakufa,CUF inafutika, ACT inajikongoja

T2015CCM

JF-Expert Member
Sep 13, 2012
7,931
987
Utafiti unaonyesha kuwa kwa kipindi cha miaka miwili na ushee tangu CCM iingie madarakani na kuunda serikali, chama hicho kimezidi kuimarika mara dufu zaidi tofauti na ilivyokuwa 2015.

Utekelezaji wa ilani unaofanywa na Serikali yake, utatuaji wa kero za wananchi, ukaribu wa chama hicho na wananchi wake waliokiweka madarakani unazidi kukipaisha huku vyama vya upinzani vikizidi kudorora.

Chama kinachodorora zaidi ni CUF kikitafunwa na mgogoro wa ndani baina ya viongozi wake wakuu wa kitaifa. CHADEMA inazidi kupukutika na kufanya kuwa chama cha pili kwa kudorora kunakosababishwa na kukimbiwa na viongozi wake kwa kasi kubwa hususani madiwani zaidi ya 55 kujiuzulu nafasi zao na wenyeviti wa mitaa na vijiji 300 hali kadhalika pamoja na mbunge mmoja.

CHADEMA pia kinatafunwa na mgogoro wa kimya kimya wa uongozi wa chama hicho ambapo kundi kubwa la viongozi hawamkubali mwenyekiti wao lakini yeye anajisimika kwa mabavu na kwa kutumia fedha.

ACT cha ZITTO kinapambana na hali yake kuchukua nafasi ya upinzani lakini nacho kina hali mbaya sana ambapo viongozi wake kadhaa wa kitaifa wamejivua uanachama na kuhamia vyama vingine ikiwamo CCM. Amebaki ZITTO peke yake akipiga kelele huku na kule.

Upinzani ujitathmini!
 
Bila ushindani kupitia upizani wa dhati CCM itajifia kiutendaji kama huko nyuma enzi za chama dola yaani chama kimmoja.
KPI yaani Key Perfomance Indicator ya CCM kwa sasa sio ya kuridhidha lakini kuna angalau ushindani wa kuikosoa CCM.Je vikifa vyama vikubwa Chadema na CUF ya Maalim Seif ndio tutarudi enzi za ujima hadi tukavaa marapu rapu wakati huo huo tulikuwa na viwanda vikubwa vya nguo visivyopungua 6.
Endeleeni kuchezea demokrasi kwa madhumuni binafsi.Time will tell.
 
Bila ushindani kupitia upizani wa dhati CCM itajifia kiutendaji kama huko nyuma enzi za chama dola yaani chama kimmoja.
KPI yaani Key Perfomance Indicator ya CCM kwa sasa sio ya kuridhidha lakini kuna angalau ushindani wa kuikosoa CCM.Je vikifa vyama vikubwa Chadema na CUF ya Maalim Seif ndio tutarudi enzi za ujima hadi tukavaa marapu rapu wakati huo huo tulikuwa na viwanda vikubwa vya nguo visivyopungua 6.
Endeleeni kuchezea demokrasi kwa madhumuni binafsi.Time will tell.
Hutoeleweka hata kidogo elewa tu jinsi tulivyo watanzania,Ni Mbowe na wenziwe wabishi tu.Ila ilikuwa haina sababu ya kuhangaika kushindana na Chama tawala.Sema kwa kuwa tunahitaji pesa saaawa.Mwanzo wa mapinduzi wa demokrasia ni mwananchi mwenyewe,kama anafanyiwa na haoni ya nini kumpigania? Maisha yetu ndio yanaenda hivyo tu.Kiachwe kijiendeshe kupunguza gharama za uchaguzi,...wapeni nchi waongeze mpaka pale wananchi waamue sasa hapana imetosha.Kikombe tunywacho bado hakijaisha ni vigumu kujua mahitaji yetu makuu kwa sasa.
Asili ya binadamu ni pale tu kwa pamoja tukiona hapana sasa,ndio unaanza kuona risasi,visu ndio ujue hapo ni point ya matukio hayo kuwa tumeelewa.Kufiikia walikofikia wengine....angalia tu historia inasema nini?Watu wamekufa sana kuzifanya nchi kuubwa Duniani kusimama zilipo sasa.Kuna mengi sana ya kujifunza huku Afrika kwetu.
 
Ni kwa wale wachache wanaojipa matumaini kuwa CHADEMA bado imara, japo wanatambua kuwa hali ni mbaya ndani ya chama chao. Sisi tulio nje ya chadema wenye akili timamu tunaona kuwa chama hiki kinakufa kwani siku zote dalili ya mvua ni mawingu.

1. Nani asiyeona kujiondoa kwa baadhi ya watu wenye dhamana ndani ya chama hiki kuwa ni dalili za kufa kwake? wawe wamepewa fedha au la kubwa zaidi ni matokeo ya kuwepo kwa chama siku zijazo halina ubishi kuwa ni dalili tosha kina dhoofika na hatimaye kitakufa.

2. Nani asiyeona kung'ang'ania kwa mtu mmoja ndani ya chama mwenye maono dhaifu kama mwenyekiti kwa miaka zaidi ya 15 kama vile hakuna mwenye uwezo wa uongozi ndani ya chama chenye maprofesa kuwa ni sababu ya chama/jumui inayoenda kufa?

3. Nani anayebisha kuwa chama hiki ni kampuni ya familia inayojineemesha kupitia mfumo wa siasa na uwepo wa vyama vingi katika nchi yetu?

CHADEMA INAKUFA. Mwenye macho haambiwi tazama, na mwenye akili timamu ya utambuzi hatobisha bali atakaa kimya na kusikitikia wasiojitambua na wenye maslahi binafsi na chama husika.
 
Back
Top Bottom