Kudanganya......

Mwenyewe anauliza uongo na kudanganya mapenzini hakuepukiki? .... na ni wakati gani haifai kudanganyana na kusema uwongo?

.....soulmate, nidanganye danganye tu, ukiniambia ukweli roho itauma...
Nami nikikudanganya danganya utanielewa?....Nakupenda tu..:D
 
Janjaweed.....si kichomi bana, ni jipu nimelikalia....maumivu yake, mwe! :what:
 
.....soulmate, nidanganye danganye tu, ukiniambia ukweli roho itauma...
Nami nikikudanganya danganya utanielewa?....Nakupenda tu..:D


Unajua nini kaka na swahiba wangu Mbu?

Akikudanganya hutajua. Ukijua basi huo si uongo tena hata kama yeye atadhani kwamba kakudanganya...Kwa ufupi atakuwa amejidanganya mwenyewe!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Mwali uko wapi wewe?

Njoo basi umsindikize babu....

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
BADILI TABIA Kasema vyema. ila me ninapodanganya huwa naumia iwapo ntaujua ukweli ama kugundua nimedanganywa ama ntaumia kama ule uongo cjawahi kusema km huo uongo nshawah kusema huwa nachukulia poa kwan "wat goes around comes around"
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Hii mbaya sana........ Ila ulivyoiongea ni lazima kuna kichomi cha kweli moyoni tena chanzo ki karibu

Hah Janjaweed bana, inaweza ikawa ni kidonda kilotoneshwa hahaha.........eti chanzo ki karibu hah

Soulmate hebu njoo ujibu kwa tuo hapa tusijeanzabebesha lawama kwa wasohusika bure!
 
Ah, mi sina la kusema, nasoma soma tu
Kwangu kudanganya ni alama ya dharau
iwe unadangaya wazi wazi au kiujanja...
Ila nimependa hiyo metaphore ya mtu
anae tulia kama ananyolewa vile. lol

....mnh, wenzetu humu hawataki! wanadai si maishani tu hata kwenye mapenzi, bila uwongo wa kudanganya maisha "eti" yatakuwa magumu sana.
 
Hah Janjaweed bana, inaweza ikawa ni kidonda kilotoneshwa hahaha.........eti chanzo ki karibu hah

Soulmate hebu njoo ujibu kwa tuo hapa tusijeanzabebesha lawama kwa wasohusika bure!

.....soulmate si nisha confess hapo juu siku ile ulonifumania bana...?
:sly:
 
Hahaha aisee hapa mmenikumbusha mbali sana aisee, mie nadhani glands zangu za hacra zimekufa aisee. Kuna mmoja wetu humu kazungumzia suala la low self esteem.... yaani unasema uwongo kwa kuwa unajua huwezisema ukweli mbele ya mwandani wako kwa kuwa hujiamini na ulilolifanya. Mmenikumbusha one of the vituko vya ex wangu ambaye aliniitroduce kwa mdada ambaye alisema walisoma wote (I trusted him na yule mdada nikamfanya one of my telephone buddies) only to find that hawajawahisoma wote pamoja na ni wapenzi kwa muda mrefu tu. Ilinichukua muda wa wiki tatu kuumeza uongo huo ikiwemo kumwuliza kila mara naye alikuja na jibu lake alokremu la kushikilia pale pale kuwa walisoma wote. Siku nilipomshukia na facts, bahati mbaya nilisema kwa tone ya dharau kiasi cha kumfanya asiamini kuwa ni mie kondoo wake.

Hii inaturudisha kwa Babu DC na Mbu. Babu DC nafikiri ni vema tukatofautisha kati ya uwongo/danganya wenye nia ya kunusuru, kuokoa au kuongeza dakika za mahusiano, ambao huwa unaruhusiwa mara moja tu yaani unausemea mara moja kisha huurudii tena (either kwa kutokifanya kile kilichokufanya udanganya au kukifanya kwa teknologia mpya ili usishikwe)

Ila uwongo ambao unajirudia, kwa mwenzi yule yule eh, ni bora mtendaji ukaanza kujiuliza uzito wa penzi lako kwa umpendaye kabla hujaanza kutengeneza uwongo mwingine kwa kosa linalojirudia aisee
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Ah, mi sina la kusema, nasoma soma tu
Kwangu kudanganya ni alama ya dharau
iwe unadangaya wazi wazi au kiujanja...
Ila nimependa hiyo metaphore ya mtu
anae tulia kama ananyolewa vile. lol

Mwali,

Sina hakika kama tunaelewana au la? Ila kuna issues ambazo kujidai kusema ukweli mtu anaonekana mjinga kabisa....

Ngoja nikutafutie mfano!

Babu DC!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
BADILI TABIA Kasema vyema. ila me ninapodanganya huwa naumia iwapo ntaujua ukweli ama kugundua nimedanganywa ama ntaumia kama ule uongo cjawahi kusema km huo uongo nshawah kusema huwa nachukulia poa kwan "wat goes around comes around"

:screwy:......kha? Unadanganya "live" hapa wewe. Eti?:confused:..ndio umeandika 'uwongo' gani huu wewe mrembo..lol
 
Hahaha aisee hapa mmenikumbusha mbali sana aisee, mie nadhani glands zangu za hacra zimekufa aisee. Kuna mmoja wetu humu kazungumzia suala la low self esteem.... yaani unasema uwongo kwa kuwa unajua huwezisema ukweli mbele ya mwandani wako kwa kuwa hujiamini na ulilolifanya. Mmenikumbusha one of the vituko vya ex wangu ambaye aliniitroduce kwa mdada ambaye alisema walisoma wote (I trusted him na yule mdada nikamfanya one of my telephone buddies) only to find that hawajawahisoma wote pamoja na ni wapenzi kwa muda mrefu tu. Ilinichukua muda wa wiki tatu kuumeza uongo huo ikiwemo kumwuliza kila mara naye alikuja na jibu lake alokremu la kushikilia pale pale kuwa walisoma wote. Siku nilipomshukia na facts, bahati mbaya nilisema kwa tone ya dharau kiasi cha kumfanya asiamini kuwa ni mie kondoo wake.

Hii inaturudisha kwa Babu DC na Mbu. Babu DC nafikiri ni vema tukatofautisha kati ya uwongo/danganya wenye nia ya kunusuru, kuokoa au kuongeza dakika za mahusiano, ambao huwa unaruhusiwa mara moja tu yaani unausemea mara moja kisha huurudii tena (either kwa kutokifanya kile kilichokufanya udanganya au kukifanya kwa teknologia mpya ili usishikwe)

Ila uwongo ambao unajirudia, kwa mwenzi yule yule eh, ni bora mtendaji ukaanza kujiuliza uzito wa penzi lako kwa umpendaye kabla hujaanza kutengeneza uwongo mwingine kwa kosa linalojirudia aisee

Ndugu yangu MwanajamiiOne,


Ni muhimu sana kutofautisha uongo wa mambo ya kawaida na yale ya msingi. katika mambo ambayo ndiyo nguzo ya uhusiano wenu, basi hapo hakuna utani wala uongo. Ila katika mambo ya kawaida ambayo nimeshasema hayana tija ila si busara kumweleza soulmate wako, mie sioni tabu kuweka uongo hapo. Na uongo huo, ndio niliwahi huko nyuma kuuita uongo mtakatifu. Huna sababu kwa mfano kumweleza BF au mume mambo ambayo yanaweza kumkera hata kama si hatari kwa uhusiano wenu. Una haja gani kumweleza kuwa classmate wako anapenda kuchuna waume za watu?

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Charminglady, iweje kusema uongo kunakuuma....ila, kusema uongo uliokwisha usema unauchukulia powa "what goes around comes around"

How possible bana :confused:
 
MwanajamiiOne, kingine ninachokupendea hata kama twaweza shinda kutwa nzima twabishana, usiku haupiti unakuwa ushanielewa arguments yangu...

Am sure unakumbuka vividly reaction yake (uso ukisawajika) siku ulipomwambia udanganyifu wake waujua kwa ukweli wako ulojitosheleza.
Thats why I brought this topic here.
Jitu linadanganya uwongo mweupee pee.....siku ukimwambia acha uwongo wa kijinga, linakutumbulia mimacho kama mjusi alobanwa na mlango :eek: mnxs! .....'hobby' nyingine hovyo kabisa.
 
MwanajamiiOne, kingine ninachokupendea hata kama twaweza shinda kutwa nzima twabishana, usiku haupiti unakuwa ushanielewa arguments yangu...

Am sure unakumbuka vividly reaction yake (uso ukisawajika) siku ulipomwambia udanganyifu wake waujua kwa ukweli wako ulojitosheleza.
Thats why I brought this topic here.
Jitu linadanganya uwongo mweupee pee.....siku ukimwambia acha uwongo wa kijinga, linakutumbulia mimacho kama mjusi alobanwa na mlango :eek: mnxs! .....'hobby' nyingine hovyo kabisa.


Nadhani hapa tunakubaliana sana tena sana ndugu yangu Mbu!

Hakuna sababu ya msingi kusema uongo kwenye mambo yanayogusa kiini cha muungano wenu. Otherwise mtazua mambo ya Tanganyika na Zanzibar!

Huyo jamaa yake MJ1 alikuwa na sababu gani ya kutoa introdn ya kipuuzi kama hiyo? Hivi alidhani kuwagonganisha wanawake zake 2 ni ufahari?

Mie sifagilii uongo wa kupuuzi...Ila pia sifagilii confession zisizokuwa na tija!!

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom